Maoni juu ya fiber internet

Mdani

Member
Sep 17, 2011
28
44
Wadau wa JF, kabla ya yote nikili jf kuwa chuo kwangu kwani napata madini mengi kupitia komenti za wanajf.

Leo nimeonelea nije na mada chokozi; ni kwa nini mtandao wa fiber internet na air fiber umekuwa mgumu kusambazwa mikoani na maeneo ya vijijini.

Kampuni nyingi zinajielekeza kutoa huduma maeneo ya mjini tu (city center na 5G zone).

-Kwa nini hali iko hivyo?

-Changamoto ni zepi haya makampuni yanakabiliwa nazo kusambaza fiber?

-Je mtoa huduma mkuu ni mmoja kiasi kwamba kila 2nd ISP lazima achukue kwenye miundombinu hiyo hiyo?

-Je mkongo wa taifa uliosambazwa wakati wa Rais J.K Kikwete nchi nzima hauhusiani na hii intaneti ya fiber?

-Je utaalamu wa usambazaji wa fiber upoje? Kuna kitu cha kuzingatiwa kwa ma-isp?

-Je mimi kama mjasiriamali mdogo nawezaje kuwa ISP hata eneo dogo hapa wilayani?

-Je upande wa sera za nchi umekaeje mpaka hatupati ma-isp wadogo wadogo?

Kama mdau wa JF una utaalamu gani au mawazo gani kuhusu hizo hoja hapo juu?

Ila binafsi naweza kukiri kwamba hata viongozi wetu wa kisiasa hawana utashi kushinikiza digital life katika maisha yetu ya kila siku. Wenyewe macho yao yako kwenye maji, barabara na umeme.

Wenzetu wakenya wako mbali sana kwenye masuala ya intaneti na teknolojia ya habari. Makala nyingi nikitafuta mtandaoni ni za wakenya, Malaysia, Indonesia, Pakistan na nchi za hivyo.

Ila sio kwa Tanzania hawapo, wapo ila ni kama waganga wa kienyeji kujificha na ujuzi.

Nashukuru JF nimeweza kupata wataalam hapa na pale wa kibongo wanaoyajua na kuyaishi maisha ya dijitali; internet, electronics, connectivity na mambo kama hayo

Ahsanteni, karibuni kwa ujuzi

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
1. Biashara
2. Biashara

Wanataka wateja, kama kuna uhakika wa wateja wataleta huduma, ndivyo ilivyo hata wewe huwezi kwenda kijijini ukaporomosha lodge kisa tu hamna lodge kwa kijiji utaangalia je kuna wateja, ela unayo invest itarudi.

Upande wa pili Ttcl wanasambaza ila kumbuka hawawezi kisambaza vizuri na maeneo yote kwasabab kuu moja, zinahitajika fedha hivyo itatengwa ruzuku kama ilivyofanyika kwa sasa ila sio pesa nyingi sana kwasababu serikali ina vipaumbele vingi, hivyo basi watajitahidi kusambaza ila sio kwa ufanisi ni kama huduma zingine zitolewazo na serikali.

Jibu ni moja
Fiber zipo city centers kwasababu ndipo kuna wateja wengi na reliable wenye kipato cha kulipia tofauti na maeneo mengine.
 
Ukitaka kusambaza unaweza kusambaza vizuri tu, utaenda kuuziwa nawewe utaweka miundombinu yako na vibali vyote ufanye biashara kadri itakavyo kupendeza.

Kampuni nyingi hazijaingia huko kwasababu ya changamoto za uendeshaji na kuhitajika kwa mitaji mikubwa, na kumbuka hii ni subscription service kuna mambo mengi ya kuchanganua kabla ya mtu au kampuni kujitosa.
 
1. Biashara
2. Biashara

Wanataka wateja, kama kuna uhakika wa wateja wataleta huduma, ndivyo ilivyo hata wewe huwezi kwenda kijijini ukaporomosha lodge kisa tu hamna lodge kwa kijiji utaangalia je kuna wateja, ela unayo invest itarudi.

Upande wa pili Ttcl wanasambaza ila kumbuka hawawezi kisambaza vizuri na maeneo yote kwasabab kuu moja, zinahitajika fedha hivyo itatengwa ruzuku kama ilivyofanyika kwa sasa ila sio pesa nyingi sana kwasababu serikali ina vipaumbele vingi, hivyo basi watajitahidi kusambaza ila sio kwa ufanisi ni kama huduma zingine zitolewazo na serikali.

Jibu ni moja
Fiber zipo city centers kwasababu ndipo kuna wateja wengi na reliable wenye kipato cha kulipia tofauti na maeneo mengine.
Sasa hata kwenye majiji kama Arusha, Mwanza ISP ni wachache kama kigezo ni biashara. Wote wamejaa Upanga

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Ukitaka kusambaza unaweza kusambaza vizuri tu, utaenda kuuziwa nawewe utaweka miundombinu yako na vibali vyote ufanye biashara kadri itakavyo kupendeza.

Kampuni nyingi hazijaingia huko kwasababu ya changamoto za uendeshaji na kuhitajika kwa mitaji mikubwa, na kumbuka hii ni subscription service kuna mambo mengi ya kuchanganua kabla ya mtu au kampuni kujitosa.
Vipi ule mkongo wa taifa au ilikuwa kanjanja??

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Sasa hata kwenye majiji kama Arusha, Mwanza ISP ni wachache kama kigezo ni biashara. Wote wamejaa Upanga

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Hapo sasa ni suala la wawekezaji kuchangamkia fursa, leseni zipo TCRA za kutoa hizo huduma, mkongo upo hata leo ukienda TTCL utaunganishwa kwa hiyo hichi unacholalamikia ni sawa na mtu alalamike kwanini kigoma hamna maghorofa mengi kama yalivyojazana kariakoo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom