Serikali ya CCM wanaua elimu; wanabadili mfumo wa elimu bila walimu

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,847
18,254
Sitaki salamu nimevurugwa, naingia kwenye mada moja kwa moja. Nchi hii ina maamuzi ya ovyo na ya kipumbavu sana. Kila kitu kinafanyika ovyo ovyo! Ni juzi tu serikali imeuza nchi kwa warabu wa DP World. Na ni jana tu Rais Samia ameenda India kuwaomba wahindi waje kununua kipande cha nchi kilichobaki baada kuwauzia warabu.

Bado vumbi la uuzaji wa nchi halijatua, serikali ya CCM imegeukia kuua elimu ya watoto wa walalahoi. Wanataka kuua elimu kwa makusudi kwa sababu watoto wao wanasoma Ulaya na Marekani. Vizazi vyao havitahusika na uharibifu huu. Lengo kubwa ni kutengeneza kizazi cha mbumbumbu wanaotawalika kirahisi ili watoto wao wakirudi kutoka masomoni ughaibuni waendelee kuwatawala watoto wa makabwela bila kutumia nguvu kubwa. Inauma sana.

Hivi ni lini serikali ya CCM itajifunza kutokana na makosa? Kipindi cha nyuma serikali ilifanya mabadiliko katika mitaala bila kuwafundisha walimu. Kuna somo ambalo hadi sasa linafundishwa shuleni linaitwa Stadi za Kazi lenye mada za kitaalamu kama vile ufundi seremala, uashi, utengenezaji wa redio, ufugaji, ushonaji, nk lakini hakuna mwalimu hata mmoja aliyepata mafunzo ya useremala, uashi, ufundi, ufugaji au ushonaji na kuandaliwa mahsusi kwa ajili ya kufundisha masomo kama hayo.

Tazama sasa serikali hii hii ya CCM inataka kubadili mitaala bila kuwapa mafunzo walimu. Nimetembelea tovuti ya taassi ya elimu ili kuona jinsi mitaala itakavyobadilika nimeshikwa na butwaa! Mitaala imebadilika kwa 99% kama unavyoona lakini serikali haijafanya jitihada zozote za kusomesha walimu licha ya kusisitiza kuwa miezi michache ijayo mitaala hii mipya itaanza kutumika hapa nchini. Hivi hawa viumbe ni nani aliyewaroga? Hebu ingia wewe mwenyewe kwenye tovuli ya taasisi ya elimu ujisomee usije ukadhani labda nawaonea kwa sababu ya chuki zangu binafsi. Kwa kweli serikali hii ina mipango ya ovyo sijapata kuona.
1697605826762.png

Niilitegemea serikali kwanza iwekeze kwenye mafunzo ya walimu kwa miaka takribani nitano hadi walimu waive ndipo ianze utekelezaji mitaala mipya. Cha ajabu serikali imetoa miaka 3 ya kuelimisha wananchi kuhusu katiba mpya licha ya kwamba maoni yalishakusanywa na Tume ya Warioba na kuandika rasimu lakini inashindwa kutoa miaka 5 ya kuwaandaa walimu watakaofundisha mitaala mipya kwa watoto wa wakulima! Kumbe huwa wanaangalia yale mambo tu ambayo yana manufaa kwao kisiasa. Hawana uchungu na maendeleo ya wananchi wa kawaida. Hawa jamaa ni wabinfasi kuliko fisi wa mwituni. Serikali ya kihuni siku zote hufanya mambo kihuni ilmradi matumbo yao yanashiba na kusaza. Nchi ya ajabu sana hii.
 
Mkuu,Mama anatimiza maelekezo aliyopewa wakati anashika hatamu!

Yaani "Badili mfumo wa elimu uendane na wakati uliopo"yaani kujiajiri!

Sisi walimu tuna paradigm shift seminar elekezi zinatosha kabisa kwa kuanzia!!

Scientists kama sisi tuna uwezo wa kusimamia stadi za KAZI mbalimbali na wanafunzi wakaelewa!!

Tumuunge mkono!!
 
Mkuu,Mama anatimiza maelekezo aliyopewa wakati anashika hatamu!

Yaani "Badili mfumo wa elimu uendane na wakati uliopo"yaani kujiajiri!

Sisi walimu tuna paradigm shift seminar elekezi zinatosha kabisa kwa kuanzia!!

Scientists kama sisi tuna uwezo wa kusimamia stadi za KAZI mbalimbali na wanafunzi wakaelewa!!

Tumuunge mkono!!
Semina elekezi zitakutosha usome arabic, chinese, na textile production uje kuwafundisha wanafunzi wakuelewe? You cant be serious mkuu.
 
Kufuga sungura,nguruwe,kilimo Cha titkiti plus simple skills nyingine!ni kuvaa ovaroli tu mkuu!!

In this modern times hatuhitaji simple skills. Hiyo ni 60s mentality
Modern erra inahitaji modern skill ili uweze ku survive.
Ww mpaka leo unakomalia kufuga sungura na nguruwr in modern times? Seriously
 
In this modern times hatuhitaji simple skills. Hiyo ni 60s mentality
Modern erra inahitaji modern skill ili uweze ku survive.
Ww mpaka leo unakomalia kufuga sungura na nguruwr in modern times? Seriously
Hapo ndipo serikali sikivu ya CCM ilipoifikisha nchi hii. Na kibaya zaidi wanabadili mitaala bila kuwapa walimu mafunzo ya aina yoyote. Kwa namna hii tutafika kweli mkuu?
 
Hapo ndipo serikali sikivu ya CCM ilipoifikisha nchi hii. Na kibaya zaidi wanabadili mitaala bila kuwapa walimu mafunzo ya aina yoyote. Kwa namna hii tutafika kweli mkuu?
Usijali wasipotoa ELIMU kwa Walimu basi wabadilishe TGTS ili walimu waweze kusoma online vinginevyo mitaala itafeli kama ilivyofeli BRN na CBC maana walileta competence based culcurum ( CBC ) bila kutoa mafunzo kwa Walimu.

Experience is a better teacher.
 
Umeandika mengi mazur ila wewe na ukoo wako mmechukua hatua gani mpaka Sasa kuistopisha CHUKUA CHAKO mapemaaaa!??"
 
Umeandika mengi mazur ila wewe na ukoo wako mmechukua hatua gani mpaka Sasa kuistopisha CHUKUA CHAKO mapemaaaa!??"
Mimi na ukoo wangu tulikuwa na mpango maalumu wa kuwaondoa chawa kwenye miili yetu lakini Magufuli akaharibu deal. Huko kaburini aliko Mungu anamuona
 
Sijawahi kuona nchi yenye maamuzi na mipango ya ovyo kama hii. Hivi ninavyoandika mada hii nipo gizani. Nchi imeuzwa kwa wahindi, hawataki umeme uwake ili wauze majenereta.
 
Mkuu,Mama anatimiza maelekezo aliyopewa wakati anashika hatamu!

Yaani "Badili mfumo wa elimu uendane na wakati uliopo"yaani kujiajiri!

Sisi walimu tuna paradigm shift seminar elekezi zinatosha kabisa kwa kuanzia!!

Scientists kama sisi tuna uwezo wa kusimamia stadi za KAZI mbalimbali na wanafunzi wakaelewa!!

Tumuunge mkono!!
Mkuu wangu 'semina elekezi' hazijawahi kuwa mbadala wa teacher training ili waendane na mitaala mipya. Acha kuleta masikhara kwenye suala serious kama hili. Wanaoumia ni watanzania wote, including your relatives and children. So, stop joking when people are discussing burning issues like this.
 
Mkuu ata mitaala iliyopo ni majangaa nahisi kwenye elimu tuna watu ambao sio sahihi wanakula per diem.nenda uangalie Vitabu vya kiswahili na English vimejaa Hadith za pwagu na pwaguzi.
 
Mkuu ata mitaala iliyopo ni majangaa nahisi kwenye elimu tuna watu ambao sio sahihi wanakula per diem.nenda uangalie Vitabu vya kiswahili na English vimejaa Hadith za pwagu na pwaguzi.
Kwenye hili la mitaala mipya, nina wasiwasi kwenye upatikanaji wa vitendea kazi kama vile computer, mazingira bora ya kujifunzia pamoja na mafunzo kwa nguvukazi (walimu). Shule tayari zimeishafunguliwa kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mtaala mpya lakini bado walimu hawajapatiwa mafunzo, na vitendea kazi wala vitabu vya kufundishia. Hakukuwa na ulazima wa kuanza utekelezaji wa mtaala mpya kwa haraka hivyo bila kufanya maandalizi ya kutosha.

Pia katika michepuo iliyotajwa nashangaa eti mtu atakayesoma mchepuo wa sayansi atachagua asome ama somo la biology au physics. Hili limefanyika kwa bahati mbaya au kuna kitu kimekosewa? Wanafunzi watakaoenda kusomea udaktari huko MUHAS ina maana hawana haja ya kusoma masomo ya physics na biology? Tutawapataje madaktari kwa namna hii?

Kumbuka ili usome udaktari lazima uwe umesoma masomo ya PHYSICS, CHEMISTRY na BIOLOGY. Ndio maana wanafunzi waliosoma tahasusi ya CBG hawasomei udaktari kwa kuwa hawakusoma PHYSICS ambalo ni somo la lazima kama unataka kusomea udaktari. Kwa hii mitaala mipya naona wanafunzi wote watakaohitimu hawataweza kusomea udaktari. Sasa madaktari tutakuwa tunaagiza kutoka China au Marekani? Inasikitisha sana.

Kwa maoni yangu, utekelezaji wa mtaala mpya ulipaswa kusubiri kwanza. Bajeti ya Wizara ya Elimu iliyosomwa mwaka jana haikuikujaziwa fedha za ziada kwa ajili ya ununuzi wa vitendea kazi (vitabu, kompiuta,nk), mafunzo kwa walimu na uboreshwaji wa miundombinu (madawati, umeme, madarasa, maabara, stoo, nk) itakayowezesha utekelezaji wa mtaala mpya.

Fikiria darasa moja la shule za kata linakuwa na wanafunzi 300 na wote wanakaa chini (hakuna madawati) na pia shule nyingi (90%) hata zilizop mjini, hazina umeme. Hizo compiuta zitatumiwaje na watoto 300 kwenye darasa moja wakati wanakaa wakiwa wamebanana hata nafasi ya kuweka kompiuta hakuna (hata kama zingekuwepo). Na wakati huo huo shule haina umeme wa kuchajia kompiuta wala stoo ya kuzitunza baada ya matumizi. Je, serikali hamuoni kuwa huu mtaala mpya mnaouharakisha hautekelezeki kivitendo?

Haya ndiyo madhara ya kuchanganya siasa na utaalamu. Kinachozungumzwa kwenye majukwaa ya siasa ni taofauti na kile kinachotekelezwa. Kwanza, kwa maelezo yako Dr Komba umesema walimu wanapewa semina kama maandalizi ya kuwaandaa kutekeleza mtaala mpya. Lakini hadi sasa yawezekana ni 1% ya walimu waliopata hiyo semina elekezi. Je, hawa 99% waliobaki watafundishaje bila semina?

Hata hivyo, sidhani kama unaweza kumfundisha mwalimu somo la Elimu ya Biashara (Business Education) akaelewa kwa siku 2 tu na kwenda kufundisha kwa umahiri. Huu ni uongo. Ilitakiwa hawa walimu waende kusoma sio chini ya mwaka mmoja ndipo waje wakafundishe. Tunarudia makosa yaleyale ya miaka iliyopita. Kulikuwa na somo la Stadi za Kazi lililoanzishwa na kuwaagiza walimu kufundisha bila kuwapa mafunzo. Kwa mfano, kwenye hilo somo la stadi za kazi kuna mada za ufundi redio, ufundi umeme, ushonaji, nk. Sasa mwalimu hujamfundisha mambo ya ufundi umeme na redio na ushonaji wa nguo unategemea afundishe kwa kutumia miujiza gani?

Nionavyo mimi ni kwamba serikali, ikiongozwa na wanasiasa, imeamua kuharibu mfumo wa elimu kwa makusudi na kwa kisingizio cha kujiajiri wakati bado haijajiandaa ipasavyo kutekeleza mtaala mpya. Na kwa kuwa serikali ndiyo imeshika mpini wa kisu na wananchi wameshika makali, lazima tu wananchi wakubali kuburuzwa, hasa ukizingatia wengi wao ni mbumbumbu.

Mwisho wa siku tutatengeneza taifa la wasomi wajinga ambao hawawezi kushindana na wasomi kutoka nchi nyingine zenye eilimu bora na zinazojali maisha ya wananchi wao. Hii nchi ngumu sana.
 
Kuna shule moja nilienda jijini mwanza nakwambia watoto ni kama wapo vitani.darasa limejaa mpaka ubaoni na mlangoni hakuna njia.aisee CCM nao watakuwa wanakaa wanatushangaa saaana wanavyotufanyia tunakaa kimya.
 
Back
Top Bottom