Serikali: Huu ndio ushauri wa mwisho kwa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF)

Mimi binafsi nikiugua mafua hakuna dawa inayoweza niponesha kama promethazine, sasa nitalazimishwaje kutumia cetrizen ambayo by nature hainisaidii kitu?
Sasa ukienda kutibiwa ukaandikiwa cetrizen utaitupa ukanunue hiyo inayokutibu au utafanyaje? Mimi sijawahi kwenda hospitali yoyote naumwa mafua nikaandikiwa dawa tofauti na cetrizen. Ukiwauliza watoa huduma kwanini wanataka kutuua kwa usugu wa vimelea wanasema wameelekezwa na NHIF watoe dawa hiyo tu.

Nikishaona hivyo inabidi niingie gharama nikanunue dawa ya coldril au dr cold syrup nijitibu. Kwa maana hii sasa bima inakuwa haina maana yoyote zaidi ya michosho isiyokuwa na mwisho na kutiana hasara zisokuwa na msingi wowote. Inasikitisha mno.
 
Mkuu, Hiyo ya kikokotoo ni PSSF, pia kama serikali isingefanya ulazima wa kumuunga mtumishi katika mfuko wa bima ya afya wengi wasingechukulia umuhimu wa kujiunga kama alivyo mwananchi wa kawaida
Sawa lakini serikali ya CCM ndiyo chanzo cha hizi shida zote zinazowakabili wananchi kwa kuwa wao serikali ndio wanaolazmisha watu kuingia kwenye matatizo watake wasitake. Serikali ya kipuuzi sana hii aisee!
 
Sasa ukienda kutibiwa ukaandikiwa cetrizen utaitupa ukanunue hiyo inayokutibu au utafanyaje? Mimi sijawahi kwenda hospitali yoyote naumwa mafua nikaandikiwa dawa tofauti na cetrizen. Ukiwauliza watoa huduma kwanini wanataka kutuua kwa usugu wa vimelea wanasema wameelekezwa na NHIF watoe dawa hiyo tu.

Nikishaona hivyo inabidi niingie gharama nikanunue dawa ya coldril au dr cold syrup nijitibu. Kwa maana hii sasa bima inakuwa haina maana yoyote zaidi ya michosho isiyokuwa na mwisho na kutiana hasara zisokuwa na msingi wowote. Inasikitisha mno.
Hapana, NHIF hawajawahi kumwelekeza mtoa huduma kutoa aina fulani ya dawa , HAPANA

huo ni mwamvuli ama kichaka cha kajificha cha watoa huduma hivyo huwatupia lawama NHIF
 
Tutajie basi ni jubilee insurance??
Insurance za matibabu ziko nyingi nchi hii lakini serikali wanalazimisha watumishi wote waingie NHIF ili wapate fedha za kuchota kipindi cha kampeni kuwahonga wapiga kura. Hii nchi ngumu sana mkuu.
 
Sawa lakini serikali ya CCM ndiyo chanzo cha hizi shida zote zinazowakabili wananchi kwa kuwa wao serikali ndio wanaolazmisha watu kuingia kwenye matatizo watake wasitake. Serikali ya kipuuzi sana hii aisee!
Hapana mkuu, kuilaumu serikali moja kwa moja is unfair, Serikali inapowapa taasisi watu waisimamie maanake imewapa dhamana kubwa, wakifail haimaanishi serikali imefail ila watu hao, cha msingi ni reformation tu
 
Hapana, NHIF hawajawahi kumwelekeza mtoa huduma kutoa aina fulani ya dawa , HAPANA

huo ni mwamvuli ama kichaka cha kajificha cha watoa huduma hivyo huwatupia lawama NHIF
Mkuu kuna siku mimi mwenyewe niliwahi kwenda ku-complain NHIF wakanijibu wao ndio wamewazuia watoa huduma wasitoe dawa nje ya maelekezo kutoka NHIF kwa kisingizio kuwa wakiandika dawa nzuri zinazotibu vizuri mfuko utaishiwa fedha. Yaani hawa wapuuzi wanajali mfuko zaidi ya uhai wa wananachama. Wapuuzi sana aisee!
 
Hapana mkuu, kuilaumu serikali moja kwa moja is unfair, Serikali inapowapa taasisi watu waisimamie maanake imewapa dhamana kubwa, wakifail haimaanishi serikali imefail ila watu hao, cha msingi ni reformation tu
Mkuu mbona wewe unawatetea sana hawa wezi? Kwanini lakini?
 
Mkuu kuna siku mimi mwenyewe niliwahi kwenda ku-complain NHIF wakanijibu wao ndio wamewazuia watoa huduma wasitoe dawa nje ya maelekezo kutoka NHIF kwa kisingizio kuwa wakiandika dawa nzuri zinazotibu vizuri mfuko utaishiwa fedha. Yaani hawa wapuuzi wanajali mfuko zaidi ya uhai wa wananachama. Wapuuzi sana aisee!
Iko hivi , kimsingi matibabu yote yanatakiwa yafate STG, ukitoka nje ya hapo , hii hasara ni yako, Binafsi nawajua vyema NHIF, Strategy ( strategic doctor), AAR nk maana tulishavurugana mahali

Changamoto ni watoa huduma, Hawako makini kabisa, ukiwa makini hakuna wa kukuyumbisha, waulize Wamiliki wa vituo vya kutolea huduma za afya watakwambia, huwa wanaingizwa loss mpaka wengine wana palalyse na kufa kabisa kwa sababu ya kutokuwa makini kwa watoa huduma wao
 
Tatizo watatumia kila wapatacho. Mishahara ya NHIF na marupurupu yao sio mchezo. Kuna mdau tulisomaga wote huko sec kwa sasa ndio mfadhili wetu. Wanalipa mabulingutu hawa si kama walimu.
 
Hii mifuko mingine ni kama nilivyoeleza kwenye uzi. Haijali gharama anazotumia mteja na hawana limitation kwa dawa. Dawa yoyote unapata tofauti na NHIF wanaobagua dawa nzuri na kuruhusu dawa hafifu tu ndio zitolewe kwa wanachama wao.
Je gharama zao za uchangiaji ni sawa na za nhif? Tuanzie hapo
 
Hapana, NHIF hawajawahi kumwelekeza mtoa huduma kutoa aina fulani ya dawa , HAPANA
Watoa huduma wanakuwa na kitabu cha amaelekezo kutoka NHIF kinachoelekeza aina ya dawa za kuwapa wanachama na nyingi ya hizi dawa hazina ubora. Kama hujawahi kukiona kitabu hicho nenda hospitali yoyote inayotoa huduma za NHIF ukiombe utapewa. Kina orodha ya dawa za NHIF. Wale wanaolipia cash wanapata aina yoyote ya dawa nzuri lakini wa NHIF wanabaguliwa.
 
Tatizo watatumia kila wapatacho. Mishahara ya NHIF na marupurupu yao sio mchezo. Kuna mdau tulisomaga wote huko sec kwa sasa ndio mfadhili wetu. Wanalipa mabulingutu hawa si kama walimu.
Hapa ndipo tatizo linapoanzia. Mifuko mingi ya bima na hifadhi ya jamii inatafunwa na wajanja wachache huku wanachama wakiishi maisha ya taabu. Hata PSSSF wanajilipa mabilioni ya hela kwa jasho la wanachama na wanatapanya mno fedha za wananchama. Ndio maana mtu ukiwagusa wanakuwa wakali kama pilipili. Wanatetea matumbo yao makubwa yasiyoshiba kamwe.
 
Hivi swali la gharama za bima nyengine limejibiwa? Na kuhusu ukomo wa umri kumekaaje huko. Na uwezo wa kuwabeba wazazi na wakwe?
 
Back
Top Bottom