Pengo: Wananipakazia madawa ya kulevya!

kanisa katoliki limejengwa juu ya mwamba, haliwezi kutikiswa na milango ya kuzimu kama hii ninayoiona humu jf
 
Mimi sio mkatoliki lakini ukweli ni kwamba kanisa katoliki ni miongoni mwa taasisi za kidini zilizo imara sana pamoja na uwezo wa kujua kinachoendelea katika nchi. Na mtu makini hawezi kulichukulia kirahisi hili tamko la kadinali Pengo.

Pamoja na kwamba sina uhakika kwamba Kadinali Pengo anauza madawa ama hauzi, nilicho na uhakika ni kwamba kutokana na uimara wa kanisa katoliki baada ya kauli hii hata kama serikali ilikuwa na mpango wa kumchunguza itabidi isitishe mpango huo.

Pia ikumbukwe kwamba kumekuwa na tuhuma toka upande mmoja wa imani kwamba serikali inaendeshwa kwa mfumo kristo na siku za hivi karibuni juhudi hizo zimepamba moto. Sasa hii inaweza kuwa ni mkakati wa kutaka kulitoa kanisa katoliki katika ''kumiliki'' siasa za nchi hii, na kuna waumini wake wawili wanaonekana kupania kuchukua uraisi wa nchi 2015. Imani yangu ni kwamba haitakuwa kazi rahisi kiasi hicho.

Nimekukubali mkuu, you are critical thinker
 
tuliache hili tusiharibu thread hii
nikishapata ushahidi nitalifungulia thread na kuku notify
sawa?

Kaldinali (siyo pengo tu) akitabiri utasikia mara moja huitaji kupoteza muda wako kutafuta ushahidi. Huoni jambo zito kama hilo lilivyokufikia na kukuchukulia muda kiasi cha kutosha?
 
kanisa katoliki limejengwa juu ya mwamba, haliwezi kutikiswa na milango ya kuzimu kama hii ninayoiona humu jf
Mkuu ingawa mie sipo katika dini hizo lakini naukubali usemi wako na hata historia inaonyesha hivyo kuwa limejengwa juu ya mwamba na kupitia mambo mengi lakini limebaki imara kutokana na msingi huo, kumbe hata hili ingawa hatuzuiliwi kutoa maoni kama tunavyoshirikishana, nadhani uimara wake unabaki tu na kwa kujadiliana hapa tunalipaisha zaidi, mie naona umaarufu wa mtu ndio unafanya ajadiliwe, vinginevyo mbona kuna wengi ambao wapo kama hawapo vile.
 
Naomba tu niharakishe kusema huu ni upuuzi na upumbavu wa viwango visivyopimika.
Serikali haina list yenye jina la Pengo, na wala Pengo hakutamka maneno hayo.
Ninachojiuliza ni nini dhamira ya Habari leo hata waandike habari ya kichochezi kiasi hiki?
Natamani kama ningekuwa na uwezo wa kuandika ilivyokuwa lakini bahati mbaya nipo maporini, laptop imekorofisha so natumia simu na haina memory card so ipo too slow when I type that I have to wait some seconds.
Right source but wrong contents.
Muda uliotumia kuandika hicho kitu hapo juu ungeutumia kuandika japo kidogo kitu halisi alichokisema Pengo ingetusaidia sana. Hivi hakuna kijana wa kikatoliki humu JF aliyekwenda ufukweni jana a clarify hii kitu?
 
Inanikumbusha kule Marekani ya kusini ambako inasadikika kuwa kuna waamuni wengi wa dini ya katoliki.Pope alipofanya ziara yake miaka ya 1990-2010.Pope alikumbana na mabango yaliyoandikwa " Iweje munatuhubiria kuhusu maisha mazuru ya peponi hapo baadae wakati ninyi huko Vatcan mnaishi maisha mazuri ya peponi sasa?" . Watanzani/Waafrika tuamke tumefumbwa macho na hizi dini na tumeshindwa kujua hata mbivu na mbichi. D. Morgan aliwahi kusema " Kama kungekuwa na uchaguzi kati ya dini na siasa ningechagua siasa,kwa sababu nchi nyingi dunia huwezi kuta kuna vyama zaidi ya vitatu vya siasa .Hivyo mgawanyiko kutokana na siasa ni mdogo ukilinganisha na mgawanyiko unaotokana na madhehebu ya dini". Siwezi kumtetea am kumshambulia/kumshutumu Pengo ila yeye ni binadamu.Hizi dini zimetugeuza geuza hata hatutafakari tunapozichambua .Tumeaminishwa kuwa mtu akiwa kiongozi mkubwa wa dini basi yeye ni mtakatifu na ameondoka kwenye kundi la wanadamu-Tafakari.Ndio maana leo hii wadhalimu wanawatumia viongozi wa dini.

Hapo kwenye bluu hapo? Ni dini gani imekuaminisha hivyo? Kwa mfano, kama wewe ni Mkristu; ukitazama maisha ya Mitume ( Petro, Filipo na Yuda-Iskariote) kwa uchache tu. Utabaini ulichokisema ni ujinga fulani hivi.
 
Just because you read it in a magazine
Or see it on the TV screen
Don't make it factual
Though everybody wants to read all about it
Just because you read it in a magazine
Or see it on the TV screen
Don't make it factual, actual............... by MJ
 
suala la biashara ya madawa ya kulevya au kulawiti watoto au kunajisi au jinai yoyote ila kamwe sio swala la kidini ni purely swala la kisheria, so Mwadhama Pengo ametajwa kuhusika na biashara hiyo haramu kwa mujibu wa sheria zetu, haitoshi tu kumtaja au kumtuhumu hapana, vyombo vinavohusika pamoja na waliomtaja wafanye uchunguzi wa kina wapate ushahidi wa kutosha then afikushwe mahakamani kujibu tuhuma hizo akishindwa ahukumiwe kwa mujibu wa sheria zilizopo, yeye kuwa kardinali hana kinga ya kutokufikishwa mahakamani na kamwe kanisa katoliki kalikuwahi kuhubiri watu watumie au waswambaze madawa ya kulevya wala maovu mengine yoyote. Kwa upande wa pili Mwadhama ni kiongozi wa kanisa katoliki Tanzania ambayo ni dhamana kubwa sana, kuhusishwa na madawa ya kulevya sii tuhuma ndogo, anatakiwa adhibitishe beyond doubt kuwa hahusiki, lakini hiyo haitoshi waliomchafua anatakiwa awatafute kwa kushirikiana na vyombo vinavohusika wafikishwe mbele ya sheria ili kumsafisha lakini pia kulisafisha kanisa ambalo kwa karibuni limekuwa kwenye kashfa nyingi sana.Niliwahi kumsikia Rais akisema viongozi wa dini wanajihusisha na madawa ya kulevya, hivi rais huyu aliapa kulinda na kutetea katiba yetu?? kama ndio mbona haitetei kwa kushindwa kuwafikisha watuhumiwa wa madawa kwenye vyombo vya sheria maana anawajua??
 
Sasa kama hamko pathetic; na kama siyo mhalifu anabwabwaji nini??

Anaweweseke, na wewe hapa unatoka mapofu kumtetea aaargh


In blue i can see all the signs of somebody stressed! I only Hope hautoki mapovu not mapofu as you said rather!
 
Masabuda, vita sio kitu cha kukitamani hata kidogo. Najua amani ikidumu ianakuwa kama pombe watu hulewa, lakini wenye akili hulewa na kuendelea mbele bila kuleta uharibifu.

amani ya kise...ge hii tuliyonayo ni ya nini? zulma, wizi, ufisadi
hivi ww utamani nchi yako iwe kama rwanda, no or minimal rushwa, ujanja kama wenu bongo hapa hamana, sheria inafuata mkondo hata kwa kigogo

bora tuzichape tutaheshimiana na esp soon southern tz will independent
 
busara za kadinali Pengo zinashangaza....sana....

kazi ya polisi ni kutodharau taarifa yeyote wanayopewa

sasa kama polisi wamepewa jina lake wafanyaje?
si lazima waliweke kwenye uchunguzi mpaka watakapothibitisha vinginevyo??

yeye ana wasiwasi gani ?

kwani wamemtaja hadharani au kwenda kum arrest?????
Nadhani kwasababu alikuwa kinara wa kutaka majina yatajwe, sasa jina lake kuwemo hata kama hakuna uthibitisho kuna wanaotizama kwamba ni namna ya kuchamfua ama kumyamazisha asizidi kuulizia kuhusu hao madealer, ndivyo nilivyoona.

Kwanza haya mambo ya kupeana majina toka mwaka 2006, hiyo listi hata mimi nakubaliana inawezekana imegeuzwa for blackmailing purposes!

Tuhuma ni tuhuma tu! Polisi wakishaanza kukufuata fuata bila hata kuwa na ushahidi unajuwa wanakukeep busy tu lol
 
Tunakoelekea ni Mungu anajua.....!Sihitaji kuwa na akili ya ziada ya kujua nikimaliza k.un.ya lazima nitawaze,ili kujua ujinga,upuuzi au ujuha wa hiyo kashfa.Let us wait and see!
 
Waislam hawatetei waovu; only maaskofu ndio huwa hawakosi watetezi ambao hawataki kutumia akili all over the world; watoto wengi scotland na ulaya wameharibiwa wakristo na pope kimya

Wewe mjahidina tumia akili yako. Swala la kubakwa halipo makanisani tu. Waulize wenzako wa Pakistan jinsi walimu wa Madrassa wanavyowatendea watoto. Ni vile tu jambo likitokea kanisani linakuwa na uhuru wa kusemwa. Nimwekwambia tusiingie kwenye imani za watu utaniita mbaya sasa hivi. Huu uhalifu unaousema ni wa kufikirika, lkn wa Boko Haram na Muslim Brotherhood ni dhahiri na dunia inajua. Unaanzisha upuuzi wako wa kidini hapa sijui kwa manufaa ya nani aliyekunyima elimu. Nimekwambia kama ushahidi upo, ashtakiwe sio kusema sema kama vilaza.
 
Naomba tu niharakishe kusema huu ni upuuzi na upumbavu wa viwango visivyopimika.
Serikali haina list yenye jina la Pengo, na wala Pengo hakutamka maneno hayo.
Ninachojiuliza ni nini dhamira ya Habari leo hata waandike habari ya kichochezi kiasi hiki?
Natamani kama ningekuwa na uwezo wa kuandika ilivyokuwa lakini bahati mbaya nipo maporini, laptop imekorofisha so natumia simu na haina memory card so ipo too slow when I type that I have to wait some seconds.
Right source but wrong contents.

thank u,nashukuru kwa ufafanuzi,mi nilitaka kuhoji busara ya pengo ilikojificha na kumuacha uchi bila busara!
 
kwa wanaofahamu nafasi ya Pengo na mamlaka aliyopewa na kanisa,hawatosema kitu bali wanatambua thamani ya maneno aliyoyasema! Tusiandikie mate,mtajua kadinali kama mshauri wa pope ni mtu wa namna gani.
 
wakinyamazishwa viongozi wa dini kuhubiri ukweli mawe yatapiga kelele
kanisa haliwezi kunyamazia maovu,litadharaulika mbele za watu lkn machoni
pa bwana ni takatifu.Shetani mwenyewe yupo kazini kuwatumia magamba
na magazeti yao kuwazulia maovu ili kuzuia kazi ya Mungu lakini
mshindi siku zote ni Mungu.mengi yatajidhihirisha mwaka huu
cardinal pengo amekosa nn haji ajihusishe na madawa? mnajua mapato ya jimbo la DSM kwa mwaka pekee?mnajua mapato ya
KKKT,angliacan morvian nk?
kila parokia inajitegemea na ruzuku wanapewa kutoka jimboni,wana vyanzo vingi vya mapato,miradi mingi shule hospitali
nk halihitaji hela za madawa kujiendesha linajitosheleza.huo ni uzuzshi wa kijinga,n
habari leo nao wazushi wanaandika habari bila hata kuhoji upande wa upili ujue hata waandishi wake makanjanja
hawana elimu ya kiuandishi habari ya upande mmoja siku zote sio habari.wanajiharibia sifa na soko lao
hilo gazeti ukitoa maoni yako kuipinga CCM au habari walizoandika huwa hawachapishi maoni yako,see how they are ignorant.
 
hii ni move ya kanisa ndani ya siasa(note plz:siyo siasa ndani ya kanisa!).
 
Back
Top Bottom