Mimi sio mkatoliki lakini ukweli ni kwamba kanisa katoliki ni miongoni mwa taasisi za kidini zilizo imara sana pamoja na uwezo wa kujua kinachoendelea katika nchi. Na mtu makini hawezi kulichukulia kirahisi hili tamko la kadinali Pengo.
Pamoja na kwamba sina uhakika kwamba Kadinali Pengo anauza madawa ama hauzi, nilicho na uhakika ni kwamba kutokana na uimara wa kanisa katoliki baada ya kauli hii hata kama serikali ilikuwa na mpango wa kumchunguza itabidi isitishe mpango huo.
Pia ikumbukwe kwamba kumekuwa na tuhuma toka upande mmoja wa imani kwamba serikali inaendeshwa kwa mfumo kristo na siku za hivi karibuni juhudi hizo zimepamba moto. Sasa hii inaweza kuwa ni mkakati wa kutaka kulitoa kanisa katoliki katika ''kumiliki'' siasa za nchi hii, na kuna waumini wake wawili wanaonekana kupania kuchukua uraisi wa nchi 2015. Imani yangu ni kwamba haitakuwa kazi rahisi kiasi hicho.
tuliache hili tusiharibu thread hii
nikishapata ushahidi nitalifungulia thread na kuku notify
sawa?
Mkuu ingawa mie sipo katika dini hizo lakini naukubali usemi wako na hata historia inaonyesha hivyo kuwa limejengwa juu ya mwamba na kupitia mambo mengi lakini limebaki imara kutokana na msingi huo, kumbe hata hili ingawa hatuzuiliwi kutoa maoni kama tunavyoshirikishana, nadhani uimara wake unabaki tu na kwa kujadiliana hapa tunalipaisha zaidi, mie naona umaarufu wa mtu ndio unafanya ajadiliwe, vinginevyo mbona kuna wengi ambao wapo kama hawapo vile.kanisa katoliki limejengwa juu ya mwamba, haliwezi kutikiswa na milango ya kuzimu kama hii ninayoiona humu jf
Muda uliotumia kuandika hicho kitu hapo juu ungeutumia kuandika japo kidogo kitu halisi alichokisema Pengo ingetusaidia sana. Hivi hakuna kijana wa kikatoliki humu JF aliyekwenda ufukweni jana a clarify hii kitu?Naomba tu niharakishe kusema huu ni upuuzi na upumbavu wa viwango visivyopimika.
Serikali haina list yenye jina la Pengo, na wala Pengo hakutamka maneno hayo.
Ninachojiuliza ni nini dhamira ya Habari leo hata waandike habari ya kichochezi kiasi hiki?
Natamani kama ningekuwa na uwezo wa kuandika ilivyokuwa lakini bahati mbaya nipo maporini, laptop imekorofisha so natumia simu na haina memory card so ipo too slow when I type that I have to wait some seconds.
Right source but wrong contents.
pengo aache kudanganya wasiomjua na wasiojua taarifa zake.pengo si mwadilifu hata kidogo,ni mdau mkubwa sana wa madawa ya kulevya.ni vyema atulie kwa kuwa hajaumbuliwa.
Inanikumbusha kule Marekani ya kusini ambako inasadikika kuwa kuna waamuni wengi wa dini ya katoliki.Pope alipofanya ziara yake miaka ya 1990-2010.Pope alikumbana na mabango yaliyoandikwa " Iweje munatuhubiria kuhusu maisha mazuru ya peponi hapo baadae wakati ninyi huko Vatcan mnaishi maisha mazuri ya peponi sasa?" . Watanzani/Waafrika tuamke tumefumbwa macho na hizi dini na tumeshindwa kujua hata mbivu na mbichi. D. Morgan aliwahi kusema " Kama kungekuwa na uchaguzi kati ya dini na siasa ningechagua siasa,kwa sababu nchi nyingi dunia huwezi kuta kuna vyama zaidi ya vitatu vya siasa .Hivyo mgawanyiko kutokana na siasa ni mdogo ukilinganisha na mgawanyiko unaotokana na madhehebu ya dini". Siwezi kumtetea am kumshambulia/kumshutumu Pengo ila yeye ni binadamu.Hizi dini zimetugeuza geuza hata hatutafakari tunapozichambua .Tumeaminishwa kuwa mtu akiwa kiongozi mkubwa wa dini basi yeye ni mtakatifu na ameondoka kwenye kundi la wanadamu-Tafakari.Ndio maana leo hii wadhalimu wanawatumia viongozi wa dini.
Sasa kama hamko pathetic; na kama siyo mhalifu anabwabwaji nini??
Anaweweseke, na wewe hapa unatoka mapofu kumtetea aaargh
Masabuda, vita sio kitu cha kukitamani hata kidogo. Najua amani ikidumu ianakuwa kama pombe watu hulewa, lakini wenye akili hulewa na kuendelea mbele bila kuleta uharibifu.
Nadhani kwasababu alikuwa kinara wa kutaka majina yatajwe, sasa jina lake kuwemo hata kama hakuna uthibitisho kuna wanaotizama kwamba ni namna ya kuchamfua ama kumyamazisha asizidi kuulizia kuhusu hao madealer, ndivyo nilivyoona.busara za kadinali Pengo zinashangaza....sana....
kazi ya polisi ni kutodharau taarifa yeyote wanayopewa
sasa kama polisi wamepewa jina lake wafanyaje?
si lazima waliweke kwenye uchunguzi mpaka watakapothibitisha vinginevyo??
yeye ana wasiwasi gani ?
kwani wamemtaja hadharani au kwenda kum arrest?????
Soma vizuri, haakuna mahali pengo kasema yuko kwenye list ya polisi!
Waislam hawatetei waovu; only maaskofu ndio huwa hawakosi watetezi ambao hawataki kutumia akili all over the world; watoto wengi scotland na ulaya wameharibiwa wakristo na pope kimya
Naomba tu niharakishe kusema huu ni upuuzi na upumbavu wa viwango visivyopimika.
Serikali haina list yenye jina la Pengo, na wala Pengo hakutamka maneno hayo.
Ninachojiuliza ni nini dhamira ya Habari leo hata waandike habari ya kichochezi kiasi hiki?
Natamani kama ningekuwa na uwezo wa kuandika ilivyokuwa lakini bahati mbaya nipo maporini, laptop imekorofisha so natumia simu na haina memory card so ipo too slow when I type that I have to wait some seconds.
Right source but wrong contents.