Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Ni kweli mkuu nashukuru kwa haya uliyouliza maana ni maswali ya msingi sana. Hata hivo, who is Dr who keeps large sum of money at homeVladmir Semilong,
Ni bahati mbaya nyumba yake kuvamiwa na maisha yake kuwa hatarini. Lakini kuna haya ya msingi ya kujiuliza.
Huyu ni mtu ambaye tuliambiwa alipaswa kuwa Gavana wa Benki Kuu na anaweka fedha nyingi sana nyumbani!
Je hizi fedha nyingi ni kiasi gani? au tafsiri ya fedha nyingi ni nini?
Kwa nini aweke fedha nyingi nyumbani? Ningeelewa japo angekuwa na shilingi Milioni moja na kusema hizi ni kipu chenji za dharura pale nyumbani, lakini akisema kaibiwa milioni kumi nyumbani tumhoji milioni kumi zinafanya nini nyumbani?
Yeye kama mchumi na mtaalamu wa masuala ya fedha aliyebobea, anausaidiaje uchumi wa Tanzania kudhibiti thamani na mzunguko wa shilingi ya Tanzania ikiwa anahifadhi fedha nyingi nyumbani na si Benki?
Hata kama angedai ilikuwa ni kuwalipa vibarua, je vibarua ujira wao ni kiasi gani mpaka awe na "fedha nyingi" nyumbani? Je nyaraka hizi ni zake binafsi na mali zake binafsi au kuna nyaraka za shirika?
Inasikitisha sana unapoona Wasomi wanashindwa kuwa mstari wa mbele kufundisha umma wa Tanzania mambo endelevu. Kila siku tunapiga kelele Ujima wa Tanzania na Watanzania kuficha fedha kwenye godoro na nyaraka uvunguni badala ya kupeleka Benki hata kuweka kwenye sefu la vitu ambavyo ni fedha.
Wenzetu huweka nyaraka na vitu vya muhimu mahali pa salama panapolindwa na nyaraka na vitu hivi vya thamani huwekewa bima, kwa kuwa vyote vina thamani.
Sijui ni lini tutaanza kuyaleta Tanzania yafanyike kwa kweli na si kuendelea kuhubiri "wenzetu ulaya wameendelea" huku wewe ndio wa kwanza kuweka fedha kwenye chungu ukakichimbia kwenye udongo wenye mchwa!
? Ni hela tu au na mambo mengine ya muhimu anayatunza ndani ya nyumba yake?