Freeman Mbowe atua Mahakamani kunusuru nyumba ya mtoto wake

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
dudley-2.jpg
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kuinusuru nyumba iliyokamatwa kwa amri ya Mahakama ili kulipa Sh. Milioni 62.7 za mishahara ya Waandishi wa Habari 10 wanaomdai mtoto wake, Dudley Mbowe ambaye ni Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima. Pia soma: Nyumba ya Dudley Mbowe kupigwa mnada kwa kushindwa kulipa Sh milioni 62.7 za waandishi

Mbowe, jana Machi 6, 2024 kupitia Wakili wake John Mallya aliwasilisha shauri hilo chini ya Hati ya Dharura mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Mary Mrio.

Amefungua shauri dhidi ya Maregesi Paul, Fidelis Felix, Christina Mwakangale, Janeth Josiah, Exuperius Kachenje, Hellen Sisya, Kulwa Mzee, Nora Damian, Makuburi Ally, Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania na Kampuni ya Udalali ya JJ Auctioneers& Debt Collectors.

Wakili Mallya alidai wajibu maombi tayari wamepewa madai yao pamoja na hati ya kiapo iliyopwa na Mbowe Februari 26, 2024.

“Mheshimiwa wajibu maombi tumeshawapa nakala hivi karibuni tusikilize kama wamekuja na majibu,” alidai Mallya.
Screenshot 2024-03-07 164815.png

Dudley Mbowe
Akijibu hoja hizo, mmoja wa wajibu maombi, Kulwa Mzee, alidai ni kweli wamepokea nyaraka hizo, zikiwa zimeambatanishwa na hati ya kiapo iliyoapwa na Mbowe, akiomba nyumba iachiliwe na Mahakama itoe amri wajibu maombi wamlipe gharama kutokana na utekelezaji wa amri hiyo ya Mahakama.

“Mheshimiwa tumepitia nyaraka wenzetu wametupa siku 15 tujibu, tunaihakikishia Mahakama kwamba tutajibu ndani ya muda tuliopewa,” alidai Kulwa.

Wakili Mallya aliomba kujibu hoja hiyo, alidai shauri lao wameliwasilisha chini ya hati ya dharura, maombi yao ni kuiondoa nyumba hiyo kwani tayari ilishabandikwa matangazo kwa ajili ya kupigwa mnada.

Alidai ikiendelea kuwa kama ilivyo inaweza kupigwa mnada kwa sababu suala hilo lina muda wa utekelezaji.

Akijibu Kulwa alidai ni kweli maombi yako katika hati ya dharura lakini lazima wasome vizuri ili wajibu kwa kuwasilisha hati ya kiapo kinzani kwa sababu katika maombi hayo kuna suala la kumlipa mwombaji gharama .

Aliomba kama siku 15 nyingi watajibu ndani ya siku saba, Mahakama ilikubali majibu yawasilishwe mapema, shauri hilo litasikilizwa Machi 12, 2024.

Mbowe katika madai yake anadai nyumba hiyo iliyokamatwa si mali ya Dudley na kwa kuthibitisha hilo amembatanisha na hati ya nyumba hiyo yenye jina la Freeman Mbowe.

Mahakama hiyo pia imepanga kuendelea na shauri la madai ya waandishi hao kwa Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Machi 12, 2024.

Februari 13, 2024, Mahakama ilikubali maombi ya wadai na kumteua dalali wa Mahakama kukamata nyumba kwa ajili ya kuipiga mnada.

Februari 28, 2024 dalali wa Mahakama, Jesca Massawe alifanikiwa kubandika matangazo ya kukamata nyumba ya Mkurugenzi tayari kupigwa mnada kufidia deni la malimbikizo ya mishahara wafanyakazi.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Mary Mrio alitoa amri hiyo baada ya kupitia hoja za washinda tuzo katika Tume ya Usuluhishi na Uamuzi(CMA) Julai 2023.

Shauri hilo namba 28461 la mwaka 2023, wadai Maregesi Paul na wenzake tisa dhidi ya Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe.

Baada ya mdaiwa kukaidi kulipa, wadai walikubaliana njia sahihi kukamata nyumba yake namba 9 iliyopo Mtaa wa Feza, Mikocheni B barabara ya Chipaka na Mahakama ilikubali.

Walalamikaji hao walipata tuzo Julai 17, 2023 mbele ya Msuluhidhi wa CMA Ilala, Bonasia Mollel.

Madai ya awali yalikuwa jumla ya Sh milioni 114 baada ya kukaa mezani kwenye majadiliano kwa pamoja kiwango hicho cha fedha kilishuka na kufikia Sh milioni 62.7.

Dudley alikubali kulipa fedha hizo kwa awamu tatu, Oktoba 30, Desemba 30, 2023 na awamu ya mwisho ilikuwa mwishoni Februari 2024 lakini hakulipa.

Vilevile anadai yeye si sehemu ya wadaawa katika shauri hilo la maombi ya utekelezaji baina ya wanahabari hao na mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima.

Hivyo anaiomba mahakama hiyo ifanye uchunguzi kubaini usahihi wa ukamataji wa nyumba hiyo kwa ajili ya utekezaji wa shauri la maombi ya utekezaji (tuzo ya CMA) na ichunguze kama yeye alikuwa ni mdaawa katika shauri hilo.

Kisha anaiomba Mahakama hiyo baada ya uchunguzi huo itamke kuwa kukamatwa kwa nyumba hiyo si halali na ni batili na iwaamuru wajibu maombi walipe gharama halisi alizozitumia mpaka tarehe ya kuachiliwa kwa nyumba hiyo na nafuu nyingine kadri Mahakama itakavyoona inafaa.

Katika shauri la maombi ya utekelezaji lililofunguliwa na wanahabari hao, wakati lilipoitwa leo, mjibu maombi yaani mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima/ Dudley hakuwepo mahakamani yeye mwenyewe wala mwakilishi wake.

Hivyo, Mahakama hiyo imeahirisha na kupanga kuendelea nalo katika hatua ya usikilizwaji Machi 12, 2024.

Mwanzo wa sakata hilo
Awali, wanahabari hao walifungua shauri hilo la mgogoro wa kikazi namba 28461 la mwaka 2023, CMA Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, baada mwajiri wao huyo kuvunja mikataba yao ya ajira, wakiomba kulipwa malimbizo ya mishahara yao jumla ya Sh114 milioni.

UPDATES
- Waandishi wambwaga Freeman Mbowe Mahakamani. Nyumba yaachiwa

Chanzo: Bestmedia
 
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amekimbilia mahakamani kunusuru kupigwa mnada nyumba anayodai kuwa ni mali yake iliyokamatwa kwa amri ya Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, akiweka pingamizi dhidi ya amri hiyo.

Nyumba hiyo ya ghorofa moja iliyoko katika kiwanja namba 9, Mtaa wa Feza, Mikocheni B, jijini Dar es Salaam ilikamatwa Februari 28, 2024 na dalali wa Mahakama, kampuni ya udalali ya MM Auctioneer & Debt Collectors, kwa amri ya Mahakama.

Mahakama hiyo iliamuru kukamatwa na kupigwa mnada nyumba hiyo kutokana na maombi ya wadai katika shauri la maombi ya utekelezaji wa tuzo ya Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) iliyotolewa kwa waliokuwa waandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Paul Maregesi na wenzake tisa.

Maregesi na wenzake walifungua shauri hilo mahakamani hapo dhidi ya mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima, Dudley Mbowe, baada ya kushindwa kutekeleza tuzo hiyo ya CMA, kuwalipa deni la malimbikizo ya mishahara yao Sh62.7 milioni.

Baada ya mdaiwa huyo Dudley kushindwa kufika mahakamani mara tatu, ndipo wanahabari hao waliiomba Mahakama, ikaamuru wakakamate nyumba hiyo waliyoiainisha kama mali ya mdaiwa wao, mtoto huyo wa Mbowe, (Dudley), ili ipigwe mnada.

Hata hivyo, Mbowe naye amefungua shauri la maombi mahakamani hapo dhidi ya wanahabari hao, mkurugenzi huyo wa gazeti la Tanzania Daima (mwanaye Dudley) na dalali huyo wa Mahakama akipinga kukamatwa na kupigwa mnada kwa nyumba hiyo.

Shauri hilo la maombi la Mbowe limetajwa mahakamani hapo mbele ya Naibu Msajili Mary Mrio, leo Alhamis, Machi 7, 2024 na Mbowe amewakilishwa na wakili wake, John Mallya huku wajibu maombi (wanahabari hao) wakijiwakilisha wenyewe.

Wakili Mallya ameieleza Mahakama hiyo kuwa msingi wa shauri hilo ni kuomba kuachiliwa kwa nyumba hiyo kwa kuwa si mali ya mdaiwa katika shauri hilo la maombi ya utekelezaji (mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima – Dudley), bali ni mali ya mteja wake Mbowe.

Amesema katika hati ya maombi iliyoambatana na kiapo, pia wameambatanisha na hatimiliki ya nyumba hiyo inayoonesha nyumba hiyo inamilikiwa na mteja wake, Mbowe.

Kwa niaba ya wajibu maombi, Maregesi ameieleza Mahakama kweli wamepata nyaraka za shauri hilo na kwamba walizipata jana, hivyo akaomba wapewe muda wa kuzipitia, huku akiungwa mkono na mwenzake, Kulwa Mzee ambaye ameomba muda wa siku 15.

“Katika nyaraka walizotuletea kuna kiapo na vielelezo vingi, kwa hiyo tunaomba muda wa kutosha kuzipitia ili nasi tulete counter affidavit (kiapo kinzani) na tunaomba kuleta majibu yetu ndani ya siku 15,” amesema Mzee.

Hata hivyo, baada ya majadiliano na maelekezo ya mahakama pande zote zimekubaliana na Mahakama imeamuru wajibu maombi hao kuwasilisha mahakamani hapo majibu yao dhidi ya maombi hayo ya Mbowe, kabla ya Machi 12 na imepanga kusikiliza shauri hilo Machi 12, 2024.

[https://www]

Dudley Mbowe

Katika hati kiapo chake, Mbowe kinachounga mkono maombi yake hayo anadai alisajiliwa kuwa mmiliki halali wa nyumba hiyo Februari 4, 2010 na kwamba tangu wakati huo amekuwa akiitumia nyumba hiyo kwa makazi.

Anadai alipata taarifa za kukamatwa kwa nyumba hiyo Februari 15, 2024 kupitia mitandao ya kijamii, hivyo akamuandikia barua Wakili Mallya kwenda kudurusu mahakamani jalada hilo la maombi ya utekelezaji wa tuzo ya CMA, kujua hasa nini kilichotokea mahakamani.

Mbowe anadai hana uhusiano wowote wa kikazi na wajibu maombi (wanahabari hao) na kwamba yeye hajashtakiwa nao katika mahakama yoyote ya kisheria nchini kwa madai yoyote ya jinai au ya madai.

Vilevile anadai yeye si sehemu ya wadaawa katika shauri hilo la maombi ya utekelezaji baina ya wanahabari hao na mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima.

Hivyo anaiomba mahakama hiyo ifanye uchunguzi kubaini usahihi wa ukamataji wa nyumba hiyo kwa ajili ya utekezaji wa shauri la maombi ya utekezaji (tuzo ya CMA) na ichunguze kama yeye alikuwa ni mdaawa katika shauri hilo.

Kisha anaiomba Mahakama hiyo baada ya uchunguzi huo itamke kuwa kukamatwa kwa nyumba hiyo si halali na ni batili na iwaamuru wajibu maombi walipe gharama halisi alizozitumia mpaka tarehe ya kuachiliwa kwa nyumba hiyo na nafuu nyingine kadri Mahakama itakavyoona inafaa.

Katika shauri la maombi ya utekelezaji lililofunguliwa na wanahabari hao, wakati lilipoitwa leo, mjibu maombi yaani mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima/ Dudley hakuwepo mahakamani yeye mwenyewe wala mwakilishi wake.

Hivyo, Mahakama hiyo imeahirisha na kupanga kuendelea nalo katika hatua ya usikilizwaji Machi 12, 2024.

Mwanzo wa sakata hilo

Awali, wanahabari hao walifungua shauri hilo la mgogoro wa kikazi namba 28461 la mwaka 2023, CMA Mkurugenzi wa Gazeti la Tanzania Daima, baada mwajiri wao huyo kuvunja mikataba yao ya ajira, wakiomba kulipwa malimbizo ya mishahara yao jumla ya Sh114 milioni.

Hata hivyo, CMA katika uamuzi wake uliotolewa na Mwenyekiti, Bonasia Mollel Julai 17 mwaka 2023, iliamuru wadai walipwe Sh62.7 milioni baada ya pande zote kukaa pamoja na kujadiliana na kufikia makubaliano ya pamoja.

Dudley alikubali kulipa fedha hizo kwa awamu tatu kila mwisho wa mwezi wa Oktoba, Desemba 30, 2023 na awamu ya mwisho ilikuwa Februari, 2024, lakini hakutekeleza ahadi hiyo ndipo wakafungua shauri la maombi ya utekelezaji.

Dudley hajawahi kufika mahakamani mara zote ambazo shauri hilo lilipangwa kusikilizwa yaani Februari 9, 13 na 14, 2024 ndipo wanahabari hao wakaomba Mahakama iamuru nyumba hiyo waliyitaja kama yake ikamatwe na Mahakama ikatoa amri hiyo.
 
Mtoto wake mhuni na msanii kama baba yake tu. Yaani TZ tuna bahati mbaya, hakuna chama mbadala wa CCM, japo ndani ya vyama kuna baadhi ya watu wazuri.
 
Back
Top Bottom