Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Habari ambazo nimezipata (toka kwa ka-nzi) zinadokeza kuwa Mkurugenzi wa NSSF Dr. Ramadhani Dau amevamiwa usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Kinondoni na majambazi na kuporwa vitu mbalimbali vikiwemo fedha na nyaraka mbalimbali. Tunashukuru Mungu kuwa yeye mwenyewe hakudhurika. Uchunguzi wa Polisi unaendelea...
Habari kutoka Tanzania Daima
Mkurugenzi NSSF avamiwa
na Irene Mark
KIASI kikubwa cha fedha ambacho idadi yake haijajulikana pamoja na nyaraka mbalimbali zimeibwa kutoka kwenye nyumba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ramadhan Dau. Akithibitisha kutokea kwa wizi huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Elias Kalinga, aliliambia Tanzania Daima Jumapili kwamba tukio hilo limetokea majira ya saa tisa usiku wa kuamkia jana.
Kamanda huyo alisema nyumba iliyovunjwa ni mali ya Dau, iliyoko jirani na viwanja vya Leaders Kinondoni, ambayo hata hivyo hakuna anayeishi humo baada ya mmiliki wake kuhamia sehemu nyingine.
Mwenye mali yake amesema hawezi kwa haraka haraka kukumbuka ni kiasi gani cha fedha ingawa anasema kulikua na pesa nyingi pamoja na nyaraka zake mbalimbali. Hakuna mali zaidi zilizoibwa.
Hiyo nyumba iko jirani na viwanja vya Leaders pale Kinondoni awali Dau alikuwa akiishi humo, lakini mpaka wizi unatokea yeye na familia yake walikuwa wanaishi kwenye nyumba nyingine, alisema.
Akielezea namna wizi huo ulivyofanyika, kamanda Kalinga, alisema ukuta mkubwa unaozunguka nyumba hiyo ulitobolewa kwa kitu kizito ambacho kilitoa sauti na kwamba wahalifu hao waliingia na kuwafunga kamba walinzi.
Alisema jeshi la polisi linawashikilia walinzi hao ambao ni wafanyakazi wa NSSF kwa tuhuma za kuhusika kwenye tukio hilo na kuwataja kuwa ni Deus Mtatiro (52) mkazi wa Kinondoni na Yusuf Bakari (56), mkazi wa Ubungo.
Tunawahusisha hawa walinzi na wizi huo ni vigumu mwizi kuvunja ukuta na kuingia ndani bila walinzi kushtuka na kutumia silaha zao mpaka wanafungwa kamba hakuna juhudi zozote za kuzuia wizi huo walizofanya.
Ndiyo maana tunawahoji ili kujua kama walihusika ama laa tukimaliza tutawapeleka mahakamani lakini juhudi za kuwapata wengine zinaendelea, alisema kamanda Kalinga.
Habari kutoka Tanzania Daima
Mkurugenzi NSSF avamiwa
na Irene Mark
Kamanda huyo alisema nyumba iliyovunjwa ni mali ya Dau, iliyoko jirani na viwanja vya Leaders Kinondoni, ambayo hata hivyo hakuna anayeishi humo baada ya mmiliki wake kuhamia sehemu nyingine.
Mwenye mali yake amesema hawezi kwa haraka haraka kukumbuka ni kiasi gani cha fedha ingawa anasema kulikua na pesa nyingi pamoja na nyaraka zake mbalimbali. Hakuna mali zaidi zilizoibwa.
Hiyo nyumba iko jirani na viwanja vya Leaders pale Kinondoni awali Dau alikuwa akiishi humo, lakini mpaka wizi unatokea yeye na familia yake walikuwa wanaishi kwenye nyumba nyingine, alisema.
Akielezea namna wizi huo ulivyofanyika, kamanda Kalinga, alisema ukuta mkubwa unaozunguka nyumba hiyo ulitobolewa kwa kitu kizito ambacho kilitoa sauti na kwamba wahalifu hao waliingia na kuwafunga kamba walinzi.
Alisema jeshi la polisi linawashikilia walinzi hao ambao ni wafanyakazi wa NSSF kwa tuhuma za kuhusika kwenye tukio hilo na kuwataja kuwa ni Deus Mtatiro (52) mkazi wa Kinondoni na Yusuf Bakari (56), mkazi wa Ubungo.
Tunawahusisha hawa walinzi na wizi huo ni vigumu mwizi kuvunja ukuta na kuingia ndani bila walinzi kushtuka na kutumia silaha zao mpaka wanafungwa kamba hakuna juhudi zozote za kuzuia wizi huo walizofanya.
Ndiyo maana tunawahoji ili kujua kama walihusika ama laa tukimaliza tutawapeleka mahakamani lakini juhudi za kuwapata wengine zinaendelea, alisema kamanda Kalinga.