JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Nini kinaendelea Mbeya kuhusu Maandaano? Watu wa Mbeya tuambieni kinachoendelea kama hizi picha ni za kweli
photo_2023-11-09_09-41-19.jpg

photo_2023-11-09_09-41-18.jpg
===============

UPDATES...
Hofu na wasiwasi vimetanda kwa wananchi jijini Mbeya kufuatia askari polisi kuzagaa kwa makundi maeneo mbalimbali tofauti na siku nyingine.

Hata hivyo hakuna mamlaka yoyote iliyoeleza zaidi sababu za maaskari hao kutanda katika maeneo mbalimbali ikiwamo kwenye shughuli za wananchi.

Mwananchi ilipita maeneo mbalimbali ikiwamo mitaa ya Kadege, Mahakama Kuu na kituo cha daladala cha Kabwe na kushuhuhudia askari wakiwa katika makundi wakiwa na vifaa vyao vya kazi.

Baadhi ya wananchi wamesema bado hawajaelewa lengo la askari hao kusambaa katika maeneo mbalimbali huku wengine wakihusisha na maandamano yaliyokuwa yamepangwa kufanywa na wanaojiita wanaharakati.

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi mkoani humo, Benjamini Kuzaga simu yake haikupokelewa, huku Mkuu wa Mkoa huo, Juma Homera akieleza kuwa hana taarifa zozote za kuwapo askari katika maeneo hayo.

Chanzo: Mwananchi
 
Jiji la Mbeya ni tulivu na watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida huku wahuni na vibaka kama akina Mdude haieleweki leo wamekwenda kuvutia wapi mibangi yao. Labda tumuulize Erythrocyte labda anaweza kutupatia majibu stahiki.
 
Back
Top Bottom