Ushauri wa Bure Kwa Rais Samia Kuhusu Uwezekano wa Maandamano Kupinga Mkataba wa Bandari/DP World

Mchanya

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
976
1,525
Nakuombea Mungu akupe hekima wewe na wasaidizi wako muweze kulitatua sakala hili vema na kwa wakati. Inahitajika HEKIMA KUBWA kuliweka sawa jambo hili, kwani sioni matumizi ya nguvu, mabavu, vitisho kama itasaidia zaidi ya HEKIMA. Sana sana yataenda kuongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulipunguza kama sio kuliondoa.
Wiki hii, Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya kuyazuia maandamano yenye lengo la kupinga wazo la mkataba huu - hili ni kosa kubwa la kiufundi. Ushauri ni kwamba yaruhusu maandano ambayo sote tunajua kwamba ni ya amani, yapewe ulinzi, ukiwa na muda yapokee, pokea salam za maandamano hayo, au ukiwa umetingwa na kazi basi mwagize hata Makamu wako, au Waziri Mbarawa au hata Mkuu wa Mkoa ayapokee. Hii itatuma ujumbe kwamba unasikiliza kilio cha wengi, uko tayari kuondoa wasiwasi walio nao watanzania wengi kuhusu sakala hili. Athari za kuzuiwa maandamano ni mbaya zaidi kuliko faida za kuyaruhusu na kuyapokea. Hii ni fursa nzuri kwako ya kujipambanua na utawala uliopita uliotumia nguvu, vitisho katika kukabiliana na masuala mazito yenye kuathiri wenye nchi - Watanzania. Hii ni fursa nzuri sana ya kudhihirisha falsafa yako ya Maridhiano, Ustahamilivu, Mabadiliko, na Kujenga Upya (Reconciliation, Resiliency; Reforms; and rebuilding)

Hata Waziri Mbarawa wakati anahitimisha mjadala kuhusu suala hili Bungeni alisema anakaribisha maoni ya wadau mbalimbali kuhusu suala hili lililolalamikiwa sana. Kuruhusu maandamano ni kwenda sambamba na kauli ya Waziri Mbarawa Bungeni kwamba anapokea na kusikiliza maoni ya watu wote.

Sio siri tena kwamba suala la mkataba wa Bandari (Yetu/zetu?) na DP World (Dubai) kwa hapa ilipofikia, limegeuka kuwa kero kubwa kwa wote, kwa aliyelileta (Serikali) na walioletewa, yaani wananchi. Kero kwa sababu serikali imejaribu, inahangaika na inatumia nguvu nyingi kuwaelimisha Watanzania juu ya manufaa ya mkataba huu, lakini bahati mbaya Watanzania walio wengi aidha hawaelewi au hawajakubaliana na wazo hili. Kero kwa Watanzania kwasababu maswali mengi wanayouliza hayapati majibu, au hata majibu yakipatikana hayawaridhishi na yanawaacha wakiwa na mashaka - ni kero. Kwa kweli ni haki yao kuwa mashaka kutokana na historia ya mikataba ya huko nyuma, lakini hii ni nchi yao, hivyo wanapaswa kuhoji kila kitu kwani atakayeathirika zaidi ni mwananchi huyu wa kawaida.

Uzoefu unaonesha kwamba, ukiwa na tatizo na ukashindwa kulitatua vizuri kwa wakati, ni wazi kwamba tatizo hilo litazaa tatizo lingine, na huenda tatizo la pili litakalozaliwa likawa kubwa zaidi na lenye athari nyingi kwa wote kuliko tatizo la msingi.

Hekima ikuongoze ikikupendeza ufikirie namna ya kuusitisha mkataba huu, kwani serikali ikiendelea na mkataba huu kwa kulazimisha, ni wazi kwamba wananchi wengi watapoteza imani na wewe na serikali yako kwa ujumla.

Ni ushauri tu, unaweza kuchukuliwa ama kuachwa.

Nawasilisha.



 
Waziri anakaribisha vipi maoni ya wadau wakati mkataba haujawekwa wazi na serikali?

Polisi kwa nini wanakataza watu kuandamana kwa amani na kutimiza haki zao za kikatiba?
 
Nakuombea Mungu akupe hekima wewe na wasaidizi wako muweze kulitatua sakala hili vema na kwa wakati. Inahitajika HEKIMA KUBWA kuliweka sawa jambo hili, kwani sioni matumizi ya nguvu, mabavu, vitisho kama itasaidia zaidi ya HEKIMA. Sana sana yataenda kuongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulipunguza kama sio kuliondoa.
Wiki hii, Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya kuyazuia maandamano yenye lengo la kupinga wazo la mkataba huu - hili ni kosa kubwa la kiufundi. Ushauri ni kwamba yaruhusu maandano ambayo sote tunajua kwamba ni ya amani, yapewe ulinzi, ukiwa na muda yapokee, pokea salam za maandamano hayo, au ukiwa umetingwa na kazi basi mwagize hata Makamu wako, au Waziri Mbarawa au hata Mkuu wa Mkoa ayapokee. Hii itatuma ujumbe kwamba unasikiliza kilio cha wengi, uko tayari kuondoa wasiwasi walio nao watanzania wengi kuhusu sakala hili. Athari za kuzuiwa maandamano ni mbaya zaidi kuliko faida za kuyaruhusu na kuyapokea. Hii ni fursa nzuri kwako ya kujipambanua na utawala uliopita uliotumia nguvu, vitisho katika kukabiliana na masuala mazito yenye kuathiri wenye nchi - Watanzania. Hii ni fursa nzuri sana ya kudhihirisha falsafa yako ya Maridhiano, Ustahamilivu, Mabadiliko, na Kujenga Upya (Reconciliation, Resiliency; Reforms; and rebuilding)

Hata Waziri Mbarawa wakati anahitimisha mjadala kuhusu suala hili Bungeni alisema anakaribisha maoni ya wadau mbalimbali kuhusu suala hili lililolalamikiwa sana. Kuruhusu maandamano ni kwenda sambamba na kauli ya Waziri Mbarawa Bungeni kwamba anapokea na kusikiliza maoni ya watu wote.

Sio siri tena kwamba suala la mkataba wa Bandari (Yetu/zetu?) na DP World (Dubai) kwa hapa ilipofikia, limegeuka kuwa kero kubwa kwa wote, kwa aliyelileta (Serikali) na walioletewa, yaani wananchi. Kero kwa sababu serikali imejaribu, inahangaika na inatumia nguvu nyingi kuwaelimisha Watanzania juu ya manufaa ya mkataba huu, lakini bahati mbaya Watanzania walio wengi aidha hawaelewi au hawajakubaliana na wazo hili. Kero kwa Watanzania kwasababu maswali mengi wanayouliza hayapati majibu, au hata majibu yakipatikana hayawaridhishi na yanawaacha wakiwa na mashaka - ni kero. Kwa kweli ni haki yao kuwa mashaka kutokana na historia ya mikataba ya huko nyuma, lakini hii ni nchi yao, hivyo wanapaswa kuhoji kila kitu kwani atakayeathirika zaidi ni mwananchi huyu wa kawaida.

Uzoefu unaonesha kwamba, ukiwa na tatizo na ukashindwa kulitatua vizuri kwa wakati, ni wazi kwamba tatizo hilo litazaa tatizo lingine, na huenda tatizo la pili litakalozaliwa likawa kubwa zaidi na lenye athari nyingi kwa wote kuliko tatizo la msingi.

Hekima ikuongoze ikikupendeza ufikirie namna ya kuusitisha mkataba huu, kwani serikali ikiendelea na mkataba huu kwa kulazimisha, ni wazi kwamba wananchi wengi watapoteza imani na wewe na serikali yako kwa ujumla.

Ni ushauri tu, unaweza kuchukuliwa ama kuachwa.

Nawasilisha.



 

Attachments

  • 895F1FEE-C6CD-4927-9595-C0BE7FB26AD4.jpeg
    895F1FEE-C6CD-4927-9595-C0BE7FB26AD4.jpeg
    116.8 KB · Views: 2
Wale watu wanakaa, wanapanga yao, wanapitisha wanavyotaka, then mnaletea eti mjadili. This is nonsense!
 
Hao wanaoandamana huo muda wangeutumia kutafuta pesa, watapigwa na kuumizwa afu hakuna kitachotokea zaidi.
 
Nakuombea Mungu akupe hekima wewe na wasaidizi wako muweze kulitatua sakala hili vema na kwa wakati. Inahitajika HEKIMA KUBWA kuliweka sawa jambo hili, kwani sioni matumizi ya nguvu, mabavu, vitisho kama itasaidia zaidi ya HEKIMA. Sana sana yataenda kuongeza ukubwa wa tatizo badala ya kulipunguza kama sio kuliondoa.
Wiki hii, Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya kuyazuia maandamano yenye lengo la kupinga wazo la mkataba huu - hili ni kosa kubwa la kiufundi. Ushauri ni kwamba yaruhusu maandano ambayo sote tunajua kwamba ni ya amani, yapewe ulinzi, ukiwa na muda yapokee, pokea salam za maandamano hayo, au ukiwa umetingwa na kazi basi mwagize hata Makamu wako, au Waziri Mbarawa au hata Mkuu wa Mkoa ayapokee. Hii itatuma ujumbe kwamba unasikiliza kilio cha wengi, uko tayari kuondoa wasiwasi walio nao watanzania wengi kuhusu sakala hili. Athari za kuzuiwa maandamano ni mbaya zaidi kuliko faida za kuyaruhusu na kuyapokea. Hii ni fursa nzuri kwako ya kujipambanua na utawala uliopita uliotumia nguvu, vitisho katika kukabiliana na masuala mazito yenye kuathiri wenye nchi - Watanzania. Hii ni fursa nzuri sana ya kudhihirisha falsafa yako ya Maridhiano, Ustahamilivu, Mabadiliko, na Kujenga Upya (Reconciliation, Resiliency; Reforms; and rebuilding)

Hata Waziri Mbarawa wakati anahitimisha mjadala kuhusu suala hili Bungeni alisema anakaribisha maoni ya wadau mbalimbali kuhusu suala hili lililolalamikiwa sana. Kuruhusu maandamano ni kwenda sambamba na kauli ya Waziri Mbarawa Bungeni kwamba anapokea na kusikiliza maoni ya watu wote.

Sio siri tena kwamba suala la mkataba wa Bandari (Yetu/zetu?) na DP World (Dubai) kwa hapa ilipofikia, limegeuka kuwa kero kubwa kwa wote, kwa aliyelileta (Serikali) na walioletewa, yaani wananchi. Kero kwa sababu serikali imejaribu, inahangaika na inatumia nguvu nyingi kuwaelimisha Watanzania juu ya manufaa ya mkataba huu, lakini bahati mbaya Watanzania walio wengi aidha hawaelewi au hawajakubaliana na wazo hili. Kero kwa Watanzania kwasababu maswali mengi wanayouliza hayapati majibu, au hata majibu yakipatikana hayawaridhishi na yanawaacha wakiwa na mashaka - ni kero. Kwa kweli ni haki yao kuwa mashaka kutokana na historia ya mikataba ya huko nyuma, lakini hii ni nchi yao, hivyo wanapaswa kuhoji kila kitu kwani atakayeathirika zaidi ni mwananchi huyu wa kawaida.

Uzoefu unaonesha kwamba, ukiwa na tatizo na ukashindwa kulitatua vizuri kwa wakati, ni wazi kwamba tatizo hilo litazaa tatizo lingine, na huenda tatizo la pili litakalozaliwa likawa kubwa zaidi na lenye athari nyingi kwa wote kuliko tatizo la msingi.

Hekima ikuongoze ikikupendeza ufikirie namna ya kuusitisha mkataba huu, kwani serikali ikiendelea na mkataba huu kwa kulazimisha, ni wazi kwamba wananchi wengi watapoteza imani na wewe na serikali yako kwa ujumla.

Ni ushauri tu, unaweza kuchukuliwa ama kuachwa.

Nawasilisha.
Hapana, siyo wengi kama unavyotaka kuaminisha watu.


Hakuna aliyenyimwa kuandamana, wameambiwa waeleze route yao ili uwekwe ulinzi wstapopopita na uli ijulukane wapokelewe wapi, waeleze viongozi wa maandamano ni nani ili ijulikane wasemaji wao na ujumbe wanamfikishia nani ili ataarifuwe kuwalokea. Yote hayo hawataki.


Sasa jiulize, ikiwa yote hayo hawataki, wanataka maandamano (demonstration)? Au wanataka riots (machafuko)?


Kama haitoshi, wakaambiwa wakaanze kwa kujipanga kwa kupeleka mlalamiko yao kwa kufata ngazi za kiserikali. Nalo pia hawataki, tujiulize wanataka nini?


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
 
Hata Waziri Mbarawa wakati anahitimisha mjadala kuhusu suala hili Bungeni alisema anakaribisha maoni ya wadau mbalimbali kuhusu suala hili lililolalamikiwa sana. Kuruhusu maandamano ni kwenda sambamba na kauli ya Waziri Mbarawa Bungeni kwamba anapokea na kusikiliza maoni ya watu wote.
Kwanza huyu waziri alitakiwa kudondoka kitini kwa kuliingiza taifa kwenye taharuki, sambamba na hilo tunahitaji mikataba 17 waliyosaini gizani huko Dubai iwekwe wazi kwasababu wao ni sehemu ndogo sana ya sisi
 
Ni ngumu kupokea maandamano hayo kama hajajiandaa kujibu hoja zake. Anyway anaweza kuyapokea tu akawaambia atajibu, inatosha hata katibu kata ayapoke ili mradi ujumbe ufike kwa amani. Kuna ndugu zetu fulani waliwahi kufanya maandamano kwenda mambo ya ndani waliruhusiwa na hakukutokea rabsha yoyote. Hata hao waandamanaji wakiruhusiwa kuandamana mpaka huko wanakotaka kwenda hawataleta madhara ulinzi ukiwekwa
 
Samahani kidogo, yatahusu pia mikataba ya madini na gesi au ni kwa ajili ya bandari tu basi? Naomba majibu kwa mlio karibu na waandaaji ili nami nione tija ya kushiriki au la?
 
Back
Top Bottom