Itategemea na atakavyojieleza. Kama vipi unalea hicho kitambi chake.
<br />Ni maelezo yepi ambayo kwako yanakubalika?
sijui kwa sasaHebu tuchukulie kwamba umekwenda kusoma nje ya nchi, au umekwenda mbali sana na nyumbani kwako kikazi. Umekaa huko kwa miaka miwili . unaporudi, unakuta mkeo ni mjamzito! Hebu niambie ungefanya kitu gani?
<br />
<br />
alibakwa.
<br />Kwa hiyo akisema tu "alibakwa" basi...wewe utakubali na kujiandaa kulea mtoto wenu, sio?
NN hawa wanajisemea tuu ila sidhani kama atakuwa na la kujieleza.
Kama huko nje nilichakachua ila sijaleta kiumbe bana yeye inakuwaje achakachue mpaka abebe na mimba
Aende huko huko alikojanzwa huo ujauzito wake
<br />Mwanaume akizaa nje ya ndoa inakuwaje hapo?ila mwanamke ndo hasameheki?
<br />
<br />
nitachunguza kama kuna ukweli.
anaweza kusamehe lakini vipi kuhusu mtoto wa nje?Msamehe tu,kwani wewe huko hukumega?tofauti tu ni kwamba yeye kapata mimba.Msamehe msonge mbele
<br />Mhhh kubakwa mhhh sijui kama nitaamini hiyo story<br />
Kuna kesi ilifunguliwa <br />
Je ndugu zangu wana taarifa<br />
Je mbakaji walikutana wapi mpaka afikie kumbaka
<br /><br /><br />
<br /><br />
Mwanaume nikizaa nje ya ndoa nitajitetea kwamba nataka kumuoa awe mke wa pili.Sasa wewe mwanamke utajiteteaje!!!!!!!!!!!!!!!???????????
<br />Hiyo ya kubakwa na kupata mimba ni very unlikely. Licha ya hivyo, wewe ni mke wa mtu na supposedly eti umebakwa. Sasa kwa nini unaihifadhi hiyo mimba? <br />
<br />
Ni mtu mzima wewe. Unapobakwa unajua nini cha kufanya. Kuna morning after pills ambazo ungeweza kutumia lakini ukaamua vinginevyo. Hata kama ni kweli ulibakwa bado nadhani utakuwa na wakati mgumu sana wa kuaminika. Binafsi sitakuamini.
kwahiyo unataka niue kiumbe? Mambo yashaharibika na kwa vyovyote wewe ndio utabaki kuwa mwamuzi mimi nitaomba huruma yako tu.
Ikitokea hvyo mwanamke anakuwa kashajipanga nyani. Anajua kabisa lolote laweza tokea.
Ila wanaume msikimbilie kuacha kisa umemkuta na mimba. Mi naamini kosa kubwa kama hilo ukimsamehe sidhani kama atakuja kukukosea tena.
<br />Msamehe tu,kwani wewe huko hukumega?tofauti tu ni kwamba yeye kapata mimba.Msamehe msonge mbele
Ukiamua kulea mimba ya mbakaji wako mimi siwezi kuishi na wewe tena kama mume na mke. Nitakuacha niendelee na maisha yangu.
Ooh kama ni hivyo basi mbona atakuwa karahisisha kazi. Nitakachofanya ni kusepa na kusonga mbele na maisha yangu. Yeye hanipi uhai wangu. Nilikuwepo kabla yake na nitakuwepo baada yake.
Hudhani kama atakuja kukukosea tena? Kama hakushindwa kujizuia kukosea mara ya kwanza ni nini kitakachomfanya asikosee safari zijazo? Na kwenye kuchiti hakuna cha eti ulikosea mara moja maana hilo tendo la ngono ukiondoa kubakwa huwaga ni la kupangwa.
Kuna mchakato mzima unaolitangulia. Kuna kupapasana, kuna kuvua au kuvuana nguo, kuna kujiweka sawa katika mtindo mtakaotumia na kadhalika na kadhalika. Sasa hilo mtu unaweza ukaliita ni kosa la bahati mbaya? Abadani asilani, hilo ni kosa la kupangwa.
Ila mwisho wa siku, kilicho muhimu na cha msingi ni uamuzi wa mtu husika. Kama mtu akiamua kumsamehe mwenzake baada ya kutendwa hivyo basi huo ni uamuzi wake na ana haki ya kuamua alivyoamua. Binafsi siwezi kusamehe. Nitakuacha papo hapo pasipo hata na majadiliano. Wanawake wako wengi mno kuendelea kung'ang'ania kubakia na wewe kama vile sina options zingine maishani.