wanafunzi wengi vyuoni wana watu wao,ukiwa nae ujue hipo siku atamrudia mtu wa toka enzi
kinachoniuma hapo ni kwanini ulikubali kutofanya nae mapenzi kabla ya ndoa
tena unaweza kuwa wewe uliyeanzisha ilo wazo..usirudie tena mambo ya tusiburi ndoa mkiacha utajutia,yaani umempa vijipesa vyako yeye hukumuona ata alama yoyote kwenye mwili wake ni hatari.
Vumilia tu ni kwasababu ulikua hujawai kupendwa/kupenda kwahiyo ulimuona huyo ndie kila kitu..huyo uliyenae endelea nae utakuja kumpenda hadi utashngaa
mimi nilishawai kuanzisha huusiano lakini sikuwa siliasi kwasababu nilikuwa naye mpenzi tunaependana sana ila yuko mbali..lakini huyu mtoto akawa haniamini,kilichotokea baada ya mwaka sasa tunapendana kuliko huyo mpenzi wangu,yaani yeye muislamu mi mkristo lakini kasema nitapenda kumuoa yuko tiyari kubadili dini.. Wakati ukweli ni kwamba siwezi kumuoa huyu ata kama ninampenda sana.
Ukweli ni kwamba utakuja kumsaau kwani ulimuona ndiye mwanzo na mwisho.
shukuru umempata wingine ambaye anakupenda sana.kumpata anayekupenda ni msaada mkubwa katika kumsahau huyo aliyekutosa.kuna watu wanatoswa na hawapati watu wakuapnda kwa dhati kama ww? can u imagine?
kinachokusumbua na kukuumiza ni kule kuachwa na mtu ambaye ulimpenda, kumthamini na kumsaidia,bado unamaumivu ya kudharauliwa,lkn si dhani kama bado unampenda kama mwanzo. na hata kama akirudi uwe nae tena unaweza ukaishia kulipiza kisasi kwa kumsaliti ili upunguze maumivu.
Mpotezee tu,
yalishawakuta wengi nami pia nna experience na jambo kama lako lakini nilifunguka bro' nikafuta fikra hizo nikaanzisha mawazo mapya kwenye kichwa changu, nakutengeneza hisia kuwa ni mtu hatari na ni adui mbaya kwangu kwani athamini chcote kile mlichofanya au kutafakari mkiwa pamoja.
nikajenga mawazo mapya kwani ilikuwa the same unampata akupendaye lakini unang'ang'na na uyo ni mateso makubwa njia yangu ilikuwa ni kusali sana kumwomba mungu akusaidie kumtoa moyoni mwako na kufunga karoom kaliko ndani ya moyo wako kalikojaa yeye na kukufungulia chumba kipya ndani ya moyo na ubongo wako ili uingize vipya wallahh! tena utashangaa nakujiona ulikuwa mbumbumbu wakati huo. funguka sasa achana na kuwaza ya zamani jenga uhusiano mpya mpende akupendae na mkubali kuwa ni zaidi ya yule kwa kila jambo haswa kwa upendo wake fikiri jinsi anavyojituma kukupenda je naye akikuacha utafanyaje? achana nae uyo leah ni mtu hatari kwako kwakuwa ameweza kutwist mind yako atakavyo hilo ni pepo ama la ni jinamizi. pole sana
Loh me mwaya sina cha kukuambia zaid ya pole weeee.
kama leah hana hata dalili yan hakupendii kbs ya nn kujiumiza ivyo jaman.
mpende akupendae asiyekupenda achana nae, acha mapenzi ya movie na tamthilia kijan grow up and move on!! kwa maneno mengine maisha lazima yaendelee alaah.
Mimi ushauri wangu kidogo ni weird
Bila kujali wala kuathiri mahusiano yako ya sasa.....akikupigia simu huyo Leah hebu onana naye, msikilize anasema nini, kisha mmombe mkamalizie pale mlipoishia. Ninaamini kabisa mkimalizie pale hutakuwa unajisikia maumivu kiviile. Hadithi hapa ni kwamba umelipia 'mzigo' kisha haujawa delivered. baas
Dah!! wewe mwanaume wewe!!!!!
Yani nimeishiwa cha kukwambia km hujamuelewa Mr Rock na wengine mambo waliyokuambia,
Nakushauri hivi,
Ili uweze kumsahahu huo lea wako kwanza achana na huyo dada wa watu aliyejitoa kukupenda kwa moyo wake wote,
Then nenda kalie lie kwa huyo lea mrudiane,
Alfu utakapokuta usichokitarajia kwa lea na ukaonja manyanyaso ya kimapnz kutoka kwa mwanamke,
Siku nyingine ukibahatika kumpata binti akakupenda km ulienae sasa utakuwa na adabu ya kuheshimu na kujali hisia za wenzio na kuachana na huo upupu unaouwaza sasa.(in short unachokifanya kwa ulienae sasa kimenidhi sana)
Huyo uliyenaye ndiye wako wa kweli. Lea si wako na ungekuwa kuwa naye huenda angekuharibia maisha. Hakupendi na hatakama atasema anakupenda atakuwa anakudanganya. Anayekupenda hawezi kukupiga kibuti hivyo. Mheshimu huyo uliyekuwa naye na mungu atawabariki. Yupo msichana mmoja alinifanyia hivyo, toka nimuache nimebarikiwa sana kimaisha. Hivi sasa ananitamani niendelee naye huku akiwa na mumewe. Nimekataa, nimeweka msimamo siwezi kurudisha matapishi. Hayo hayajakukuta peke yako jihadhari tafadhari utaharibikiwa maisha usipokuwa na msimamo katika maisha yako ya ndoa/mapenzi.
By Midavudavu
kinachokutesa ww ni ile hali ya kukaa nae ktk mahusiano bila kufanya nae mapenzi na mwishoe akakuacha hicho ndo kinachokutesa,sikiliza mkuu hilo jambo hata mi lilishawahi kunitokea na nlikuwa nadhani kama wewe kwamba sitaweza kumsahau huyo binti lakini mwisho nilimsahau,na mara nyingi wana kawaida ya kurudi pindi mambo yakiwaendea kombo kama huyo LEAH afanyavyo kwako kwasasa,FUNGUKA mkuu.Wana jamvi'
Napiga hodi Jukwaani'
Nina tatizo la kimapenzi la mda mrefu ambalo naamini humu JF ndo mahala naweza kupata ufumbuzi wa tatizo langu.
Inahusu maisha yangu ya kimapenzi, Miaka minne iliyopita (2009) niliingia kwa mara ya kwanza katika ulimwengu wa mapenzi,Nikakutana na Leah akiwa mwaka wa kwanza chuoni mimi nikiwa mwaka wa pili.Huyu binti nilimpenda sana naye alionesha kuwa ananipenda,tukakubaliana kwa pamoja kuwa wapenzi,tukaweka misingi ya kutofanya mapenzi hadi tukioana,tukafanya mambo mengi pamoja,tukawa pamoja mda mwingi,fedha kidogo niliyokuwa nayo nilijibana kwa ajili ya kumtimizia mahitaji yake madogo madogo.Tulitambulishana kwa ndugu zetu wa karibu,kweli tukawa wawili.Mimi binafsi nilimpenda sana kuliko mnavyoweza kudhani.
Nikiwa mwaka wa tatu na yeye akiwa mwaka wa pili nikaanza kuona mabadiliko kidogo,lakini siku namaliza mtihani wa mwisho chuoni na kumaliza degree ya kwanza akaniacha rasmi bila sababu ya msingi.Aliniathiri sana mambo yangu mengi wakati huo nilikua na scholarship ya masters UK nikashindwa kwenda kwa sababu nilimiss deadline kwa sababu nililazwa hospitali kwa muda wa mwezi mzima na ushee.
Nilikua na bahati kwani mara tu baada ya kumaliza shule nilipata na ajira wakati huo nikiwa nimelazwa.Nikaanza kazi lakini nikiwa bado siwezi kukaa bila kumfikiria Leah,efficiency yangu kazini ikawa sio nzuri.Bosi wangu akaniita akanisihi nimwambie nini kinanisibu,ilinibidi nimweleze.Kwa busara zake akaamua kunipa likizo ya mwezi mzima na leave allowance hapo nikiwa na miezi miwili tu kazini.
Nikarelax kidogo.Baada ya miezi mitano nikapata msichana mwingine,huyu ndiye alikuwa msichana wangu wa kwanza kufanya nae mapenzi.Lakini nikawa bado simpendi kutoka moyoni.Hakuna siku wala saa inapita bila kumuwaza Leah.Nikawa nashindwa kum care huyu msichana kwa sababu moyo wangu hauko kwake.Tukaamua kuvunja uhusiano.
Mwaka 2011 Februari nikawa na msichana mwingine ambae niko nae hadi sasa,huyu ananipenda kwelikweli hadi mimi hua naogopa.Lakini moyoni mwangu nalazimisha kumpenda.Ukweli nampenda Leah.Bado siwezi bila yeye.
Naomba mnisaidie;
1.Huyu wa sasa ananipenda sana lakini moyo wangu haupo kwake,nifanyeje?
2.Leah anaonesha kutonipenda kabisa kwa sababu hata nikimpigia simu hapokei,lakini nampenda kulikoni,nifanyeje?
3.Naogopa kuja kuwa mume msumbufu kwa familia pale nitakapooa nisiyempenda kwa dhati,nifanyeje?
Weeee usikute ni Leah M!!
Pole bwana. Ningekushauri ujiweke mbali na mahusiano kwa muda maana kila unapojaribu kwingine mambo yanakua mabaya zaidi kwasababu unacompare na Leah. Chukua muda, fanya mambo yako mwenyewe mpaka atakapoanza kukutoka kichwani. Otherwise utajikuta kila unapoingia unaishia kuhuzunika badala ya kufurahi, na unaoingia nao huwatendei haki vile vile.
evam pole sana kwa matatizo yaliokupata,najua inaumiza sana na ni ngume kuexpress, cha msingi kwanza kama ni mkiristo omba msaada wa Roho mtakatifu akupe faraja ya na kumsahau lea! pili usiijiamulie mapema na kujilazimisha kumchukua mtu usiye mpenda cozy utamuumiza na yeye.tatu lea hakupendi tena kama angekuwa anakupenda lazima angekutafuta hata mara mojamoja. kaa chini na uombe msaada wa mungu zaidi!