sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,034
Niliweza kupata ajira nikiwa na miaka 23 miezi michache baada ya kuhitimu chuo, mambo yalikuwa mazuri si haba kwa umri huo, niliweza kutembelea gari, sim nzuri, geto limepambika + muziki munene.
Katika pita pita zangu nikamnasa binti kwa gia ya lifti, nilimpenda sana yule binti na nilikuwa namuhudumia vingi sana nguo, vocha mpaka chupi yaani mahitaji yake mengi sana ela ilitoka mfukoni kwangu.
Aliniomba ahamie ghetto kwangu, kiukweli sikufikiria mara mbili hasa kwa umri niliokuwa nao nikaona hapa ndio penyewe, game zitakuwa za kutosha.
Kazi ilikuwa ni ya mwaka moja tu japo kwenye mkataba walificha ficha, nilifukuzwa kwa surprise nikiwa hata sijajipanga, uwezo wangu wa kumhudumia ukapungua, hakuna rangi sikuiona, na maneno aliyatamka siwezi kuja kuyasahau.
Gari niliirudisha, pesa zilianza kukata, mambo ya out yaliisha, alinimwaga kama mtu ambaye hatujawahi kujuana maishani.
Baada ya mwaka nili nesa upya kwa kishindo zaidi, itoshe kusema kuna wanawake ni mashetani, alianza kujigonga upya ila nilimtolea nje kama vile simjui.
Katika pita pita zangu nikamnasa binti kwa gia ya lifti, nilimpenda sana yule binti na nilikuwa namuhudumia vingi sana nguo, vocha mpaka chupi yaani mahitaji yake mengi sana ela ilitoka mfukoni kwangu.
Aliniomba ahamie ghetto kwangu, kiukweli sikufikiria mara mbili hasa kwa umri niliokuwa nao nikaona hapa ndio penyewe, game zitakuwa za kutosha.
Kazi ilikuwa ni ya mwaka moja tu japo kwenye mkataba walificha ficha, nilifukuzwa kwa surprise nikiwa hata sijajipanga, uwezo wangu wa kumhudumia ukapungua, hakuna rangi sikuiona, na maneno aliyatamka siwezi kuja kuyasahau.
Gari niliirudisha, pesa zilianza kukata, mambo ya out yaliisha, alinimwaga kama mtu ambaye hatujawahi kujuana maishani.
Baada ya mwaka nili nesa upya kwa kishindo zaidi, itoshe kusema kuna wanawake ni mashetani, alianza kujigonga upya ila nilimtolea nje kama vile simjui.