Freeland
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 14,481
- 10,217
Wana jamvi'
Napiga hodi Jukwaani'
Nina tatizo la kimapenzi la mda mrefu ambalo naamini humu JF ndo mahala naweza kupata ufumbuzi wa tatizo langu.
Inahusu maisha yangu ya kimapenzi, Miaka minne iliyopita (2009) niliingia kwa mara ya kwanza katika ulimwengu wa mapenzi,Nikakutana na Leah akiwa mwaka wa kwanza chuoni mimi nikiwa mwaka wa pili.Huyu binti nilimpenda sana naye alionesha kuwa ananipenda,tukakubaliana kwa pamoja kuwa wapenzi,tukaweka misingi ya kutofanya mapenzi hadi tukioana,tukafanya mambo mengi pamoja,tukawa pamoja mda mwingi,fedha kidogo niliyokuwa nayo nilijibana kwa ajili ya kumtimizia mahitaji yake madogo madogo.Tulitambulishana kwa ndugu zetu wa karibu,kweli tukawa wawili.Mimi binafsi nilimpenda sana kuliko mnavyoweza kudhani.
Nikiwa mwaka wa tatu na yeye akiwa mwaka wa pili nikaanza kuona mabadiliko kidogo,lakini siku namaliza mtihani wa mwisho chuoni na kumaliza degree ya kwanza akaniacha rasmi bila sababu ya msingi.Aliniathiri sana mambo yangu mengi wakati huo nilikua na scholarship ya masters UK nikashindwa kwenda kwa sababu nilimiss deadline kwa sababu nililazwa hospitali kwa muda wa mwezi mzima na ushee.
Nilikua na bahati kwani mara tu baada ya kumaliza shule nilipata na ajira wakati huo nikiwa nimelazwa.Nikaanza kazi lakini nikiwa bado siwezi kukaa bila kumfikiria Leah,efficiency yangu kazini ikawa sio nzuri.Bosi wangu akaniita akanisihi nimwambie nini kinanisibu,ilinibidi nimweleze.Kwa busara zake akaamua kunipa likizo ya mwezi mzima na leave allowance hapo nikiwa na miezi miwili tu kazini.
Nikarelax kidogo.Baada ya miezi mitano nikapata msichana mwingine,huyu ndiye alikuwa msichana wangu wa kwanza kufanya nae mapenzi.Lakini nikawa bado simpendi kutoka moyoni.Hakuna siku wala saa inapita bila kumuwaza Leah.Nikawa nashindwa kum care huyu msichana kwa sababu moyo wangu hauko kwake.Tukaamua kuvunja uhusiano.
Mwaka 2011 Februari nikawa na msichana mwingine ambae niko nae hadi sasa,huyu ananipenda kwelikweli hadi mimi hua naogopa.Lakini moyoni mwangu nalazimisha kumpenda.Ukweli nampenda Leah.Bado siwezi bila yeye.
Naomba mnisaidie;
1.Huyu wa sasa ananipenda sana lakini moyo wangu haupo kwake,nifanyeje?
2.Leah anaonesha kutonipenda kabisa kwa sababu hata nikimpigia simu hapokei,lakini nampenda kulikoni,nifanyeje?
3.Naogopa kuja kuwa mume msumbufu kwa familia pale nitakapooa nisiyempenda kwa dhati,nifanyeje?
Napiga hodi Jukwaani'
Nina tatizo la kimapenzi la mda mrefu ambalo naamini humu JF ndo mahala naweza kupata ufumbuzi wa tatizo langu.
Inahusu maisha yangu ya kimapenzi, Miaka minne iliyopita (2009) niliingia kwa mara ya kwanza katika ulimwengu wa mapenzi,Nikakutana na Leah akiwa mwaka wa kwanza chuoni mimi nikiwa mwaka wa pili.Huyu binti nilimpenda sana naye alionesha kuwa ananipenda,tukakubaliana kwa pamoja kuwa wapenzi,tukaweka misingi ya kutofanya mapenzi hadi tukioana,tukafanya mambo mengi pamoja,tukawa pamoja mda mwingi,fedha kidogo niliyokuwa nayo nilijibana kwa ajili ya kumtimizia mahitaji yake madogo madogo.Tulitambulishana kwa ndugu zetu wa karibu,kweli tukawa wawili.Mimi binafsi nilimpenda sana kuliko mnavyoweza kudhani.
Nikiwa mwaka wa tatu na yeye akiwa mwaka wa pili nikaanza kuona mabadiliko kidogo,lakini siku namaliza mtihani wa mwisho chuoni na kumaliza degree ya kwanza akaniacha rasmi bila sababu ya msingi.Aliniathiri sana mambo yangu mengi wakati huo nilikua na scholarship ya masters UK nikashindwa kwenda kwa sababu nilimiss deadline kwa sababu nililazwa hospitali kwa muda wa mwezi mzima na ushee.
Nilikua na bahati kwani mara tu baada ya kumaliza shule nilipata na ajira wakati huo nikiwa nimelazwa.Nikaanza kazi lakini nikiwa bado siwezi kukaa bila kumfikiria Leah,efficiency yangu kazini ikawa sio nzuri.Bosi wangu akaniita akanisihi nimwambie nini kinanisibu,ilinibidi nimweleze.Kwa busara zake akaamua kunipa likizo ya mwezi mzima na leave allowance hapo nikiwa na miezi miwili tu kazini.
Nikarelax kidogo.Baada ya miezi mitano nikapata msichana mwingine,huyu ndiye alikuwa msichana wangu wa kwanza kufanya nae mapenzi.Lakini nikawa bado simpendi kutoka moyoni.Hakuna siku wala saa inapita bila kumuwaza Leah.Nikawa nashindwa kum care huyu msichana kwa sababu moyo wangu hauko kwake.Tukaamua kuvunja uhusiano.
Mwaka 2011 Februari nikawa na msichana mwingine ambae niko nae hadi sasa,huyu ananipenda kwelikweli hadi mimi hua naogopa.Lakini moyoni mwangu nalazimisha kumpenda.Ukweli nampenda Leah.Bado siwezi bila yeye.
Naomba mnisaidie;
1.Huyu wa sasa ananipenda sana lakini moyo wangu haupo kwake,nifanyeje?
2.Leah anaonesha kutonipenda kabisa kwa sababu hata nikimpigia simu hapokei,lakini nampenda kulikoni,nifanyeje?
3.Naogopa kuja kuwa mume msumbufu kwa familia pale nitakapooa nisiyempenda kwa dhati,nifanyeje?