Kama huna bando ni hivi, Ndugai aliupata Uspika kwa fitna dhidi ya Mama Anne Makinda, Ndugai alitibiwa kwa mamilioni ya fedha ughaibuni na hajapona Bado, Ndugai ana tabia ya kuwachapa bakora wapinzani wake...
Na Kali kuliko zote, Ndugai anawashikilia Wabunge 19 wasio na vyama kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano....

Video Iko chini
View attachment 2064271
Hii ndio aina ya watetezi wa Rais Samia?
 
Spika Ndugai ndie ameanzisha moto,lakini si hivi hivi nadhani kajipanga kwa lolote.
Hakosi volunteers wabunge ,akiamua kuiwekea kauzibe serikali ya Mama SSH,lazima itayumba kwa kiasi fulani kupitisha miswaada bungeni.Tatizo wabunge wengi wanamuogopa Ndugai.
Kwa upande wa Mama yetu yeye anao vigogo wenye ushawishi mkubwa ndani ya chama na nje ya chama.Ila hatutegemei kuona Speaker anaendelea kukwaluzana na Mkuu wa nchi siyo ishara nzuri kwa CCM.
 
Yaani hiki kinachoendelea kwa kweli sio ishara nzuri kwa Rais Samia ila ni ishara kwa UKOMBOZI wa nchi hii.Yaani hii nchi inavichekesho sana na sielewi kwa nini mama anapigwa fitna,hebu angali mpuuzi aliyemuandalia hotuba Rais ya desemba 31/12/2021 yaani ni Ugolo mtupu.Badala ya kuzungumzia hali tete ya ugumu wa maisha ya watu wanamuandalia Rais vitu vya hovyo visivyogusa maisha yao tena kwa wakati muafaka.
 
Aiseee kwasasa nchini hii inashida, huyo dogo inawezekana anahoja ila anavyoifikisha sasa,nayeye anakuwa muharifu kabisa.......halafu huyu unakuta siku anateuliwa kuwa DC kwaakili hizi tunasafari ndefu.....Ndugai inawezekana katoa ya kweli ila sasa nani atamsikiliza kwasababu ya unafiki wake?
 
JOBO ANA HOJA LAKINI NAE NI WALEWALE!

Mtu ambaye amehusika katika ongezeko kubwa la deni la matibabu nje ya nchi ni pamoja na JOBO, anaweza kuwa na hoja sasa ya msingi (kuhusu mama yenu kukopa sana, mikopo yenye masharti), hoja hiyo tutaisikiliza lakini watu timamu tutakumbuka masuala kadhaa na tutahoji. Hivi!

Kwa mujibu wa Sheria ya Uendeshaji wa Bunge ya mwaka 2008, katika kifungu cha 24(1), “matibabu ya mbunge yatagharamiwa na Bunge ndani na nje ya nchi.” Bunge la Jobo limekuwa linatumia kifungu hiki kuidhinisha malipo ya matibabu ya Jobo na baadhi ya wabunge, wa CCM.

Deni la matibabu nje ya nchi, liliongezeka kwa kasi isiyo ya kawaida katika kipindi ambacho watumishi wa serikali wanaotibiwa nje ya nchi wanadhibitiwa na Rais, na Jobo mwenyewe amekuwa “mgonjwa (mkuu) mashuhuri” aliyetibiwa nje katika kipindi hicho.

Na hoja zake za jana, tunaweza kuzijadili kwa mtazamo tofauti wa kizalendo zaidi kwa kupitia kwa umakini zaidi taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG), ya mwaka 2017/2018, ongezeko hili ni la kati ya tarehe 30 Juni 2017 na tarehe 31 Desemba 2017.

Na muhimu zaidi, deni hilo lilongezeka katika kipindi ambacho wagonjwa wanaokwenda nje lazima waruhusiwe na Rais, na “mgonjwa mkuu” aliyetibiwa nje ni Jobo, ongezeko la deni la matibabu linahusu pia Jobo na sikuwahi kusikia wakati wa mwendazake, Jobo akihoji lolote!

Kwa mujibu wa takwimu za CAG, jamaa alikaa India kwa takriban miezi 5, akiwa na wasaidizi wake na familia yake. Posho ya mbunge anapokuwa nje ya nchi kwa siku 1 ni US$500; mtumishi wa bunge ni US$450; mwenzi wa ndoa ni US$300. Ni vile sisi ni mazuzu, huyu mtu hafai kuwa alipo!

Kwa uchambuzi wa ripoti ya CAG, Jobo alikaa India kwa miezi 5, ambayo ni siku 150. Kama kwa siku moja alilipwa US$500, miezi 5 alilipwa US$75,000. Kwa TZS, kwa viwango vya ubadilishaji fedha vya Sh. 2,170 kwa dola moja, jamaa alitumia Shs. 162,750,000 kama posho ya kuishi India.

Akiwa India, ‘kaperanaumu’ alikuwa na wasaidizi wawili – maana alihamishia ofisi yake huko huko hotelini. Kwa gharama ya US$450 kwa siku, mara mbili, watumishi hawa walilipwa US$900 kwa siku. Kwa siku 150 walizokaa India, maana yake walilipwa US$135,000, sawa na Sh. 292,950,000.

Wakati ofisi ya Jobo inatoa gharama zote hizi kwa ajili ya matibabu ya Jobo, kuna orodha ndefu ya wabunge wa upinzani (wakati huo) ambao walinyimwa huduma kama hiyo ambayo ni haki yao kisheria. Lakini ikawa halali kabisa kwa Jobo na aliona sawa tu kuishi India miezi 5.
C$P
Katika suala la msingi ambalo afrika tunachelewa Safari ya maendeleo ni Kwenye matumizi ya ela.

Ndio maana hata Hii mikopo ni bora ukope sana lakini uone matokeo yake na kuwe na uwazi Katika matumizi kuliko kukopa kidogo na matokeo yawe sifuri watu wajigawie siku zipite
 
Katika suala la msingi ambalo afrika tunachelewa Safari ya maendeleo ni Kwenye matumizi ya ela.

Ndio maana hata Hii mikopo ni bora ukope sana lakini uone matokeo yake na kuwe na uwazi Katika matumizi kuliko kukopa kidogo na matokeo yawe sifuri watu wajigawie siku zipite

..wakati wa Mkapa tulikuwa tunalilia tusamehewe madeni.

..leo wanaibuka viongozi wanataka nchi ikope bila kuonyesha mikakati ya kulipa madeni yetu.
 
K gang wamepoteana, hamna anayewaunga mkono, sio CCM sio UPINZANI, na wasukuma halisi hawawataki pia, 2030 for January njia nyeupee
 
Huyu mwenezi inawezekana elimu yake siyo zaidi ya darasa la nne...hoja inawezekana anayo lakini uwasilishaji wake ni wa kiwango Cha chini kabisa...yasni kutaja mpaka kabila la Ndugai??! Maana yake Nini hads?! Yaani wagogo hawafai?!?! Dah...CCM ipo hatarini kabisa....CCM huwa inawaokota wali viongozi Kama Hawa?! Pengine alitoa kauli hi baada ya kunywa ulanzi...hovyo kabisa...
 
Spika Ndugai ndie ameanzisha moto,lakini si hivi hivi nadhani kajipanga kwa lolote.
Hakosi volunteers wabunge ,akiamua kuiwekea kauzibe serikali ya Mama SSH,lazima itayumba kwa kiasi fulani kupitisha miswaada bungeni.Tatizo wabunge wengi wanamuogopa Ndugai.
Kwa upande wa Mama yetu yeye anao vigogo wenye ushawishi mkubwa ndani ya chama na nje ya chama.Ila hatutegemei kuona Speaker anaendelea kukwaluzana na Mkuu wa nchi siyo ishara nzuri kwa CCM.
Huuu ni mwanzo tu, hii ni rasharasha Sheikh mzigo mzima uko njiani
 
Huyu mwenezi inawezekana elimu yake siyo zaidi ya darasa la nne...hoja inawezekana anayo lakini uwasilishaji wake ni wa kiwango Cha chini kabisa...yasni kutaja mpaka kabila la Ndugai??! Maana yake Nini hads?! Yaani wagogo hawafai?!?! Dah...CCM ipo hatarini kabisa....CCM huwa inawaokota wali viongozi Kama Hawa?! Pengine alitoa kauli hi baada ya kunywa ulanzi...hovyo kabisa...
Hahaha vipi kuhusu kibajaji na msukuma??
 
Kama huna bando ni hivi, Ndugai aliupata Uspika kwa fitna dhidi ya Mama Anne Makinda, Ndugai alitibiwa kwa mamilioni ya fedha ughaibuni na hajapona Bado, Ndugai ana tabia ya kuwachapa bakora wapinzani wake...
wakati ndugai anapata uspika anna makinda alishastaafu. Anna makinda alipata uspika ili kumpunguza kasi sitta.
 
We una roho na nafsi ya kichawi kabisa, ulitaka aende kwa sangoma au mganga wa kienyeji au ulitaka afe???
Ila hili swala la Ndugai kutibiwa kwa Tsh. 2B ni moja ya matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.
 
Kama huna bando ni hivi, Ndugai aliupata Uspika kwa fitna dhidi ya Mama Anne Makinda, Ndugai alitibiwa kwa mamilioni ya fedha ughaibuni na hajapona Bado, Ndugai ana tabia ya kuwachapa bakora wapinzani wake...
Na Kali kuliko zote, Ndugai anawashikilia Wabunge 19 wasio na vyama kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano....

Video Iko chini
View attachment 2064271
KIGOGO ANAASEMA ANADANGANYWA NA KINA OILCOM KWAMBA WATAMLIPIA ADA KUPIGANIA URAIS 2025,NDIO MAANA UFAHAMU UNAONDOKA
#SSH_2021-#2030.
*AMESHAPITA BADO KUAPISHWA TU.
 
Back
Top Bottom