Mtuhumiwa ma mauaji ya Mwangosi afikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali

Napata wasi wasi kama kweli mtu aliyeshtakiwa ndiye muuaji !!! Jina gani hili "PACIFICUS CLEOPHACE SIMON"full Eurocentric, kama la kutengezwa vile, halina ubini wa kibantu. Labda ndio maana hakuwa na roho ya utu !!! Lakini kwa kuwa atakuwa amesoma shule yo yote Taanzania na kuishi naye mtaani, atakuwa anafahamika. Kwa kuwa JF ni mwisho wa yote, naomba yeyote ambaye anakumbuka kukutana na jina la namna hiyo katika maisha yake aniondoe wasi wasi.

Sawabho, pengine hili limekupiga chenga kidogo ama hufatilii dynamics za utamaduni wa Bongoland. Wazazi walio wengi wa zama hizi za sasa wameibuka na mtindo mpya wa kutopenda kuwapa watoto wao utambulisho wa ubini wa kibantu. Ni mtindo unaozidi kushika kasi. Ni aibu na ni bahati mbaya. Sababu za uhakika hazijulikani lakini ninahisi ni kuwakwepesha wasihusishwe na makabila (unajua ubini wa kibantu unatambulisha kabila la mhusika) wakati tulipaswa kujivunia urithi huo ambao ndio nguvu ya taifa. Hata hivyo kitu ambacho hakitakwepeka na ninatabiri kitaendelea kulisumbua taifa ni utambulisho wa udini kupitia majina hayo hayo. Kumbe kama tungechukua mkondo wa kutumia utambulisho wa ukabila badala ya udini, ingekuwa neema zaidi yanayokuja!! Hii ndio Bongoland - tumechanganyikiwa!!
 
wasitudanganye. Hii ni conspiracy. Wahusika wakuu ni waziri IGP, RPC na mwenyewe aliyetenda.
 
Bila tume huru ya uchunguzi ya kimahakama, yote yanayofanza sasa ni maigizo ya MZEE JANGALA.
 
Vipi kuhusu wale nane wengine aliokuwa nao?

Kwanini ashitakiwe huyu corporal pke yake wakati picha zinaonyesha zaidi ya askari 8 walikuwa wamemzunguka marehemu???Hii yaweza kuwa ni danganya toto.
Huyu Kamnda wa Polisi wa Mkoa yuko wapi??? Huyu ni mtuhumiwa Namba 1 maana yeye ndiye aliyeenda kuamrisha hao polisi waanze kurusha na kupiga mabomu.

Tunataka kusikia Kamanda Kamuhanda akifikishwa kwa pilato haraka sana kabla Watanzania hawajachukua sheria mkononi. Kamuhanda alimwambia Marehemu Mwangosi kuwa yeye anataka kustahafu vizuri kwa hiyo asingeweza kuruhusu maandamano na mikutano ya CDM mkoani Iringa!

Sasa tunamwuliza Kamuhanda kwa kesi hii ambayo imeanza kuunguruma ndiyo atastahafu vizuri??? Hii kesi haitamwacha salama. Lazima itakula kwake lazima tu! Ni mambo 3 ayatarajie: Kushtakiwa kwa mauaji,Kustaafishwa kwa lazima au Kufukuzwa kazi! One of the 3 gonna happen to this hopeless and helpless RPC!
 
Shahidi wa kwanza ni RPC wa Iringa!

Huo ndio utani, Haraka ya nini? si isubiriwe kamati imalize kazi wote waliohusika waburuzwe mahakamani bila RPC Kamuhanda na yule aliyekumbatibiwa na marehemu Mwangosi akiwa hai na wote saba waliomzunguka kufikishwa mahakamani haki bado, kafara ya constable Pacifcus ni changa la macho sawa na sinema ya kihindi Aandha Kanoon.
 
Baada ya wiki mbili watanzania watakuwa wameshasahau hili swala na Kijana atakuwa huru na atahamishiwa Mwanza.

Matukio yanaishaga kiaina aina. Ulimboka kesi imeishia hewani. Mauaji ya morogoro watanzania wameshapoa. Ya Mwangosi yatasahaulika na yatakuja mengine kutupumbaza kuyasahau yaliyopita kama ilivyo kwa wapigakura wengi kufuta kumbukumbu na kudumbukiza kura zao kwa kuwachagua wezi wale wale:kev: na wauaji:laser:wale wale na vihiyo wale wale na wapiga mabenci wale wale na wasema ndiyooooooo wale wale. Kifupi tunachagua wafu
 
How u feel sorry to the one among those killers!!??

I bet Ndahani is an excellent parent to his/her child/children. The parental instincts/love to the young kid overcame the fact that this is an accussed killer.
 
Ona sasa kijana miaka 23 anateketea kwa kutolewa kafara ya jela na hao Polisi, Kamuhanda nae achukuliwe hatua!

Mimi mnaniudhi kumuonea huruma huyu nguchiro aliyekosa haya!Yaani natamani anyongwe kwanza yeye halafu hao wengine ndiyo wafunguliwe mashitaka mahakamani.
 
Mkubwa! Nimepitiwa tu! Ila hakika nilikuwa na hili la kusema ya kwmb MTUHUMIWA NAMBA MOJA ni huyu RPC kama haki ingetendeka na siyo SHAHIDI nimepitiwa tu!

Inaoekana unataka kuchanganya mambo, kwa mtazamo wangu RPC ni mshitakiwa 2 ila yule askari aliyevunjwa mguu ndiye shahidi namba 1 ,wanasheria tuwekeni sawa .naomba kuwakilisha
 
Huyu dogo ametolewa kafara tu. Kwa kuangalia kwa haraka haraka, ni bwana mdogo tu wa miaka 23 ambaye hana uzoefu. Alikuwa anatekeleza amri za wakubwa wake tu za kumshughulikia Mwangosi and maybe he was just too overzealous or the gun openned fire by mistake kwani huenda alisahau kutoa kidole chake kwenye trigger.

Bado RPC wa Iringa na wote waliohusika kumpiga Mwangosi wanatakiwa wafikishwe mahakamani, hata kama si kwa murder bali kwa conspiracy to commit a crime. Walimjua fika kwa sura kuwa Mwangosi ni mwandishi wa habari, alipiga mayowe kuwa yeye ni mwandishi hata wasiomjua walisikia, lakini RPC aliachia polisi wampige huku akiangalia tu.

Wote waliohusika kumpiga Mwangosi, pamoja na RPC wa Iringa aliyeangalia tu wafikishwe mahakamani. Si huyo askari bwana mdogo wa miaka 23 peke yake.
 
RPC nae ni mshaitakiwa,apelekwe na yule alikuwa na nguo za kiraioa na kibastola chake hewani!!!!!!!!!!!!!!tehe teheee
 
23yrs!!!!!!!!!!!!!!! So young OMG!!!!!!!!!!!!!
Tunataka picha isije ikawa kama sinema ya Kova na Joshua Mulundi wa Ulimboka
 
Vipi kuhusu wale nane wengine aliokuwa nao?

The Hague huwa inalamba kuanzia MKUBWA ALIYEKUWAPO ENEO LA TUKIO ambaye kutokana na nafasi/cheo chake angeweza kuzuia ujambazi huo, halafu kamanda wa kikundi husika anawajibika kwa matendo ya askari wake, kisha askari walioshiriki unyama huo kwa namna moja au nyingine, why? Kwa sababu Ushahidi upo wazi kabisa kwamba marehemu Mwangosi aliteswa kinyama sana kabla ya kuuawa. Je, askari aliyefikishwa mahakamani ndiye pekee aliyemdhibiti marehemu na kumpiga kipigo ambacho huenda kingemwacha mlemavu kama angenusurika? Mbona ushahidi wa picha unaonesha kulikuwa na kundi kuubwa la askari waliokuwa wanatoa kipigo hicho? Au hao wengine walitenda kwa mujibu wa sheria? Na kama haitoshi, mwandishi huyu alinyakuliwa mikononi mwa RPC kwenda kuteswa na kuuawa, mtuhu iwa nambari moja ni nani hapo?

Kichwa kinauma, wacha nitafute ushauri wa doc...!
 
Baada ya wiki mbili watanzania watakuwa wameshasahau hili swala na Kijana atakuwa huru na atahamishiwa Mwanza.

Matukio yanaishaga kiaina aina. Ulimboka kesi imeishia hewani. Mauaji ya morogoro watanzania wameshapoa. Ya Mwangosi yatasahaulika na yatakuja mengine kutupumbaza kuyasahau yaliyopita kama ilivyo kwa wapigakura wengi kufuta kumbukumbu na kudumbukiza kura zao kwa kuwachagua wezi wale wale:kev: na wauaji:laser:wale wale na vihiyo wale wale na wapiga mabenci wale wale na wasema ndiyooooooo wale wale. Kifupi tunachagua wafu

Dogo kuna mshiko mzuri tu unamsubiri kama atacheza vizuri scene yake!
 
hapana mkuu, kama picha za tukio zisingepatikana wangesema kuwa cdm ndio wameua na viongozi wote wa cdm bila shaka wangepanda kizimbani kasoro wale ambao hawkuwa pale ikiwa ni pamoja na kufuta chama.
Sasa kama ni polisi basi polisi wote waliokuwa kwenye tukio wanahusika ili angalau hata yule aliyeumia akijaribu kumkinga marehemu angekuja kusamehewa mahakamani kwa kitendo hicho alichojaribu uungwana bila mafanikio. Maana sheria za majeshi zinafuata amri na kawaida amri hutoka juu kwenda chini. RPC alikuwepo na hukuna shaka ndiye alitoa amri.
Acha sheria iwe sheri na tuachane na hizi siasa za double standards!!

Kwa ufahamu wangu kidogo nilioupata nilipokuwa katika mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, tulifundishwa kuwa askari unatakiwa kupokea amri ya mwisho na kuitekeleza bila maswali. Ninachoweza kusema hapa baada ya kuangalia ile picha ya Marehemu Mwangosi akisulubiwa na wale askari huku akiwa amemkumbatia yule afande ni dhahiri kuwa Marehemu alikuwa akiomba hifadhi kwa yule kamanda. Ukiangalia vizuri ile picha yule kamanda aliyekumbatiwa na marehemu alikuwa na cheo kikubwa kuliko askari wengine wote katika ule mduara. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na jitihada zake zote za kuwatuliza wenzake kutokutoa kipondo kwa marehemu inadhihirisha wazi kuwa askari wale wote walikataa kutii amri yake,bila shaka yupo askari mwingine aliyekuwa na cheo kikubwa kumzidi na alitoa amri yenye kuashiria wale polisi kuipuuza amri ya yule aliyekumbatiwa na marehemu na ndio maana yule Pc. Cleophus Pasificus alitii amri ya mkuu kuliko yule afande na kufyatua lile bomu lililofanya maangamizi kwa Mwangosi.
Jambo la pili ni kuwa mara zote Polisi wamekuwa wakiwaasa raia kutokuchukua sheria mikononi mara wanapokuwa wamewakamata watuhumiwa, sasa inakuwaje polisi walewale wanatenda kinyume na wanachokihubiri siku zote Mwangosi hakutoa upinzani wowote kwao ilikuwaje waendelee kucharaza kwa virungu kiasi kile? Hapa lengo tokea awali linadhihirisha wazi ilikuwa ni lazima auwawe tu. Funzo kwa raia: Ukimkamata mtuhumiwa chukua sheria mikoni maana Polisi hawana maana tena.
 
Hakuna kitu hapa, hizi ni fiksi tu za kutulainisha watanzania, lakini hatushawishiki wala hatudanganyiki
 
Back
Top Bottom