Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Jeshi la Polisi Mkoani Iringa limemkamata Jacob Mhanga (54) Mkazi wa kijiji cha Utiga Mkoani Njombe akiwa na meno saba ya Tembo katika nyumba ya kulala wageni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Allan Bukumbi amesema Mtuhumiwa huyo alikutwa katika nyumba ya kulala wageni katika kijiji cha Mbalamaziwa Kara ya Kisanga Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa na atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Vilevile Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Uhifadhi na kupitia taarifa fiche kutoka kwa raia wema lilimkamata Mathias Malenga (37) Mkazi wa Kijiji cha Image Kata ya Image Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa akiwa na silaha mbili moja shotgun ambayo haina namba na nyingine ni gobore ndani ya nyumba yake a Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani upelelezi ukikamilika.
Chanzo: Millard Ayo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Allan Bukumbi amesema Mtuhumiwa huyo alikutwa katika nyumba ya kulala wageni katika kijiji cha Mbalamaziwa Kara ya Kisanga Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa na atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Vilevile Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Uhifadhi na kupitia taarifa fiche kutoka kwa raia wema lilimkamata Mathias Malenga (37) Mkazi wa Kijiji cha Image Kata ya Image Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa akiwa na silaha mbili moja shotgun ambayo haina namba na nyingine ni gobore ndani ya nyumba yake a Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani upelelezi ukikamilika.
Chanzo: Millard Ayo