Mtuhumiwa ma mauaji ya Mwangosi afikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,542
93,149
September 12, 2012

BREAKING NEWssssssssMTUHUMIWA WA MAUAJI YA MWANGOSI AFIKISHWAMAHAKAMANI LEO IRINGA




Baadhi ya wanahabari wakitoka mahakamani


Askari anayetuhumiwa kumuua Daudi Mwangosi leo amefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya mkoa wa Iringa na kusomewa mashitakata yake. Huku akiwa chini ya ulinzi mkali ambao ulifanya wanahabari waliofika mahakamani kujitahid kupata picha kwa ugumu.

Akisoma mashtaka mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya Daines lymo mwendesha mashtaka ameeleza kuwa mtuhumiwa Pacificus Cleophase Simon (23

HABARI KAMILI ITAKUJIA HIVI PUNDE

Yule asikari aliyemuua David mwangosi kafikishwa mahakamani Iringa chini ya ulinzi mkali.
Mshitakiwa huyo katambulika kwa jina la PACIFICUS CLEOPHACE SIMON miaka 23.
MY TAKE.
Inatakiwa wote walikuwepo sehemu ya tukio wafikishwe mahakamani. kwa huyu mmoja kaonewa sababu walikuwa wengi akiwemo aliye mwamulisha. mia


na Mwandishi wetu

ASKARI polisi aliyefyatu bomu lililomlipua na kumuua kinyama mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, David Mwangosi (40), amefikishwa katika mahakama ya kijeshi na kuvuliwa uaskari.

Vile vile, askari huyo mwenye cheo cha PC anatarajiwa kufikishwa
katika mahakama za kiraia kujibu mashitaka yanayomkabili.

Habari kutoka ndani ya jeshi hilo mkoani Iringa zilimtaja askari huyo kuwa ni PC Pacificus Cleophace Simon (23), mwenye namba G2372. Ni askari wa FFU Iringa, na hajafikisha miaka mitatu kazini.

Inaelezwa kuwa askari huyo ambaye anadaiwa kukiri kuua bila kukusudia, ameshakula kiapo cha ungamo mbele ya mlinzi wa amani.

Kufikishwa katika mahakama ya kijeshi kwa askari huyo, kumekuja baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa awali ambao umebaini kuwa bomu alilofyatua ndilo lililosababisha kifo cha Mwangosi.

Kwa mujibu wa habari hizo, askari huyo kwa sasa anashikiliwa na polisi mkoani Iringa na anatarajiwa kufikishwa katika mahakama ya kiraia wakati wowote.

Hata hivyo, habari zaidi zinasema kuwa askari huyo huenda akapanda kizimbani baada ya tume iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema na Kamati iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, kukamilisha kazi zao ndani ya siku 30.

Hadi tunakwenda mitamboni, Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, Michael Kamhanda na IGP Mwema hawakupatikana kuthibitisha taarifa hizo.

Picha zilizopigwa kwenye tukio la mauaji ya Mwangosi, zilionyesha askari wakiwa wamemzingira na kumpiga, baadhi yao wakiwa na virungu, na wengine bastola. Mmoja miongoni mwao, ameshikilia bunduki na kuielekeza tumboni.

Vile vile, baadhi ya askari wamemtaja mwenzao aliyemlipua Mwangosi, wakataja na mahali anakoishi mjini Iringa.

Askari waliokuwepo siku ya tukio, walilieleza gazeti hili kwa sharti la kutotaja majina yao kwamba aliyemlipua Mwangosi na kumuua papo hapo yuko chini ya ulinzi tangu siku ya tukio akiwa na askari wengine walioonekana wakimpiga mwandishi huyo.

Mwangosi aliuawa Jumapili iliyopita katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi, mkoani Iringa wakati akiripoti habari za ufunguzi wa tawi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), huku polisi wakiwazuia kufanya kazi yao ya kisiasa.

Bomu lililomlipua Mwangosi lilimjeruhi askari polisi aliyetambulika kwa jina la Aceli Mwampamba, aliyekuwa amekumbatiwa na mwandishi huyo wakati akishambuliwa na kundi la polisi.

 
Walioko Iringa tunaomba picha kwa sababu picha za wauwaji wote tunazo, hatukubaliani na mazingaombwe haya, halafu naomba tu kuuliza sasa ile kamati ya harusi ya Nchimbi kazi yake ni nini sasa? changa la macho hili.
 
Yule asikari aliyemuua David mwangosi kafikishwa mahakamani Iringa chini ya ulinzi mkali.
Mshitakiwa huyo katambulika kwa jina la PACIFICUS CLEOPHACE SIMON miaka 23.
MY TAKE.
Inatakiwa wote walikuwepo sehemu ya tukio wafikishwe mahakamani. kwa huyu mmoja kaonewa sababu walikuwa wengi akiwemo aliye mwamulisha. mia

Ni mahakama gani? walisema mahakama ya kijeshi, is this true?
 
Shahidi wa kwanza ni RPC wa Iringa!

Bila RPC na wale makamanda wengine waliokuwepo pale wakati Mwangosi anauawa kuvuliwa u-polisi pia na kufikishwa mahakamani na kushitakiwa kama washitakiwa namba 2 kwa kuchochea mauaji kwangu nasema HUU NI USANIII TU..

Si askari wote walikuwa wanampiga,unawezaje kunithibitishia kwamba wale wengine hawakutaka kumuua? lengo lao lilikuwa moja na walimchochea mwenzao kumaliza kazi kwani aliona wanachelewa. Kwani kazi ya Polisi mtu akivunja sheria ni kumpiga?
 
Yule asikari aliyemuua David mwangosi kafikishwa mahakamani Iringa chini ya ulinzi mkali.
Mshitakiwa huyo katambulika kwa jina la PACIFICUS CLEOPHACE SIMON miaka 23.
MY TAKE.
Inatakiwa wote walikuwepo sehemu ya tukio wafikishwe mahakamani. kwa huyu mmoja kaonewa sababu walikuwa wengi akiwemo aliye mwamulisha. mia
kelele zilizopigwa na hasa hapa jf kijitahidi kuweka picha za matukio zimesaidia sana kuizuia serikali isilete repoti ya uongo kwa watanzania kama ilivyozoeleka.
Kwa hiyo chamsingi sasa ni kuwa angalau katika hatua 100 za kwenda tumepunguza mbili basi iwe kama ndio tuaanza kuwasha moto.
Tuongeze msukumo na hasa kwa wale wanaoelewa masuala ya kisheria waweke wazi ufafanuzi ili na hao wengine weletwe mbele ya sheria ambapo itasaidia huko mbeleni hawa jamaa zetu wa polisi kupunguza au hata kuacha ukatili na manyanyaso yao.

 
Kwa nini apelekwe kwa ulinzi mkali? Si wao walimwambia lipua? Wale wote walioko kwenye ule mduara wanahusika akiwemo Rpc.
 
Shahidi wa kwanza ni RPC wa Iringa!

No please...
Mshitakiwa wa kwanza alitakiwa kuwa RPC Kamuhanda, akifuatiwa na RCO na huyo muuaji pamoja na wale wengine sita kama wanavyoonekana kwenye picha mbalimbali zilizopigwa wakati wakimtesa Mwangosi.

Kutomshitaki Kamuhanda katika tukio hili la mauaji ya Mwangosi ni sawa na kuiminya haki ya marehemu na kuwatukana watanzania kwa ujumla wao.
 
Shahidi wa kwanza ingependeza awe RPC wa Iringa!

Ingependeza sana!
hapana mkuu, kama picha za tukio zisingepatikana wangesema kuwa cdm ndio wameua na viongozi wote wa cdm bila shaka wangepanda kizimbani kasoro wale ambao hawkuwa pale ikiwa ni pamoja na kufuta chama.
Sasa kama ni polisi basi polisi wote waliokuwa kwenye tukio wanahusika ili angalau hata yule aliyeumia akijaribu kumkinga marehemu angekuja kusamehewa mahakamani kwa kitendo hicho alichojaribu uungwana bila mafanikio. Maana sheria za majeshi zinafuata amri na kawaida amri hutoka juu kwenda chini. RPC alikuwepo na hukuna shaka ndiye alitoa amri.
Acha sheria iwe sheri na tuachane na hizi siasa za double standards!!

 
Afisa wa polisi Mwenye namba G2573 Bwana Pacificus Cleophace Simon anayetuhumiwa kumlipua kwa bomu marehemu Daudi Mwangosi amefikishwa mahakani leo na kusomewa mashitaka ya mauaji(mudder case).

Askari huyo mwenye umri wa miaka 23 alifika mahakamani na gari aina ya Toyota Landcruiser GX T320ARC huku maafisa usalama wakimzonga kijana huyo kuwazuia waandishi wa habari kupigapicha.

Afisa huyo amerudishwa rumande kutoka na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Kesi itatajwa tena tarehe 26 mwezi huu.
 
Afisa wa polisi Mwenye namba G2573 Bwana Pacificus Cleophace Simon anayetuhumiwa kumlipua kwa bomu marehemu Daudi Mwangosi amefikishwa mahakani leo na kusomewa mashitaka ya mauaji(mudder case).

Askari huyo mwenye umri wa miaka 23 alifika mahakamani na gari aina ya Toyota Landcruiser GX T320ARC huku maafisa usalama wakimzonga kijana huyo kuwazuia waandishi wa habari kupigapicha.

Afisa huyo amerudishwa rumande kutoka na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Kesi itatajwa tena tarehe 26 mwezi huu.

Tears in my eyes! I feel sorry for the young boy!
 
Sikubaliani kabisa na kesi hii ni batili, Wanaharakati wote wanapaswa kuipinga hii kesi maana ni kuwafanya Watanzania ni wapumbavu kuliko maelezo.

Daudi-Mwangosi.jpg
 
Back
Top Bottom