Moto wa Katiba Mpya CHADEMA kutinga Ikulu; KAMATI Kuu yateua kamati ndogo ya muafaka

hiyo timu ni hatari!! Dk slaa, mbowe, lissu, prof safari, prof baregu... Lazima jk, pinda, lukuvi, luhanjo wakubali matokeo
 
chadema waende kwa nia nzuri wala wasiweke masharti vinginevyo waendelee na chaguo lao la kwanza la kuandamana nchi nzima. hakuna atakayewapokea kwa masharti kwani hilo liliwashinda bungeni wakatoka nje.
 
Naona mmejipanga kuchangia thread yenu.
Fine, ila najua kimewauma kwa kuwa mnajua fika kwamba jamaa yenu hawezi kushindana kwa hoja na vichwa kama Baregu na Safari. Msiwe na hofu jamaa sio mjinaga kiasi hicho mpaka aruhusu kuaibishwa ofisini kwake, atakataa tu.

By the way, nawaachia thread yenu. Nasign off.

Kama milivyofikiri atakataa kuhusu Katiba mpya?

Kikwete atawaona mkifata taratibu za kumuona na si kupitia magazetini na vyombo vya habari.

Ushauri wa bure, muulizeni Shibuda awape ujanja. Na nnadhani huu utakuwa ni ushauri wake baada ya kukutana na Kikwete Dodoma. Nna uhakika Shibuda ndio mwenye mawazo kama haya ya kisiasa.
 
Anaenda kukuonana na Dikteta tena mfalme...lol
TL hakumwita JK dikteta. KATIBA yetu ndio inaweza kumfanya Rais wetu akawa dikteta. Wakibahatika kumwona wamstue Rais wetu kuwa Muungano sio kati ya Tanzania na Zanzibar bali Tanganyika na Zanzibar.
 
Waliopangwa kumwona Rais baadhi yao hawana rekodi nzuri na CCM mathalan, Prof safari alikimbia CCM kwa fujo na kwenda CUF na baadaye chadema, Prof Baregu akiwa chuoni aligombana na serikali kuhusu mkataba wake
 
kundi kubwa linalokwenda kumuona Rais lina hasira na serikali na mvutano wa kutupiana maneno kwa muda mrefu. Hivi kweli meza ya mazungumzo itakalika?
 
If I were JK I would have rejected Chadema's request to meet him keeping in mind that the same group of people voted with their feet during his parliament inaugural speech alleging him to tamper with the ballots. Chadema are clearly exhibiting double standard by seeking to talk to a man whom they accuse of sweeping election by fraudulent means.

Chadema's move explains as to why African politics will never prosper at all owing to the presence of ambivalent leaders who can not live up to their stance for at one point pretend to be so firm about their commitments and at the following point they easily succumb and do so mindless decisions.
 
Wameshaona jinsi gani waliwakosea wananchi wanaowawakilisha kwa kuwanyima uwakilishi katika suala nyeti la mabadiliko ya katiba hivyo wameamua kwenda kuonana naye ili wajenge credibility waliyoipoteza kwa wanchi. Tusubiri watakayoyazungumza.
YOU are not serious, they did sent a message. Ndiyo maana CCM waliacha kuchangia mjadala, wakamjadili TL badala ya kujadili sheria kusudiwa, usisahau wengine walienda mbali na kusema TL hujasoma hivyo wakashauri aende shule, do u think this is a gd point to include in that bill. assignment nakupa: kasome CV za hao waliotoa maoni ya aina hiyo pale mjengoni utashangaa.

Kumbuka maoni ya kambi ya upinzani. Read btn lines usiwe unaruka mistari soma yote tena uielewe. Hivi ww unadhani Jaji Mkuu mstaafu, Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Warioba, Katibu Mkuu mstaafu wa AU Dr.Salim na wazee wengine maarufu ktk nchi hii waliopinga utaratibu huo, nao ni CDM. Au kwa maoni yako TZ ni DSM ZENJ and DOM maana ndiko walikofika kukusanya maoni. THINK
 
Rais na chadema mkitaka kufanikiwa kukaa meza moja wote wekeni silaha zenu chini kila mmoja wenu abebe kalamu tu ya kuandikia hoja za mwenzake na kuzifanyia kazi. nawapongeza sanaaaaaaaaaaaaaaaa
 
itakalika kwani wakifika mbele ya rais wote mikono iko nyuma na kujishaua shaua,kukaa na rais ujiko acha bana
kundi kubwa linalokwenda kumuona Rais lina hasira na serikali na mvutano wa kutupiana maneno kwa muda mrefu. Hivi kweli meza ya mazungumzo itakalika?
 
Hivi ni Tundu ndo aliesema juu ya udikteta wa raisi wa Tanzania? Lisu alichofanya ni kutoa tafsiri ya katiba yetu tuliyonayo kwamba unampa fursa raisi kuwa dikteta, ni katiba inayotoa mwanya wa kuwa na uraisi wa kifalme.

Hapa si Kikwete tu hata kesho akiwa Lipumba au hata Dr Slaa, kwa katiba yetu tuliyo nayo ina toa mwanya kuwa dikteta au kuwa na uraisi wa kifalme, na hii tafsiri siyo ya Lisu tu hata mstaafu Jaji Samata ambae amewahi kuwa jaji mkuu, ni juzi tu kalisema hili mbele ya makam wa raisi-Dr Bilal, waziri mkuu mstaafu Dr Salim.

Mbona kauli hiyo hiyo imetolewa na jaji Samata hakuna anaemjadili? Au kuna ushabiki hapa ndio unaotawala? Hilo la udikteta si la mtu bali ni la katiba yetu. Na kuhusu kwenda kumuona kwa mnaozungumzia ushabiki hamlioni hili kuwa ni mtego mkubwa sana, wengi mnadhani ni ujinga unaofanyika subirini matokeo yake mtayaona.

Hilo jambo limebeba sura ya kimataifa katika matokeo yake, na nimeshasema kuna sura mbili za matokeo hapo ambazo zote zina faida kwa Chadema na wapenda haki.

Kaeni mtafakari sio kuleta ushabiki wa kwenye taarabu, eti wataenda halafu watarudi, hapo kuna jambo.
 
waliochaguliwa kwenye kamati ya kumuona Rais wamechaguliwa na nani maana wananchi hawajashilishwa kuwachagua. tunataka wananchi washirikishwe si kamati kuu ya chadema tu wanatunyima uhuru wetu

acha unafiki kwani wewe cdm mpaka wakushirikishe?
 
Mwita 25,absolutely true,IF YOU WERE JK,But you are not and you will not till the end of this global world,unless you change your perspective against the truth for the general populace regarding the consititution of the wananchi and not for CCM leaders.
 
kikwete wapokee kondoo wako chadema wewe ndiye mchungaji wetu wasikilize kwa makini na wajibu hoja zao. Usiwaache na dukuduku nchi yetu italipuka baba watasingizia hukuwasilikiza kumbe walishindwa kujenga hoja
 
Back
Top Bottom