Mama Kilango v/s Sophia Simba ndani ya uchaguzi wa UWT...

Anna k yy ni kelele tu alitegemea kuwa F L akakosa sasa anataka uenyekiti ataweza yy huwa anadandia hoja
 
hawa wote wataalam wa mipasho ila simba ni zaidi aliwai kuwaambia wanawake wawanyime unyumba mabwana zao.!
 
mabwege tu wote hao,mama kilango mnafiki anapinga ufisadi kwa kuangalia machoni,kuna anaowakubali wawe mafisadi,bora kiduchu hata s. simba anastaha!
 
Kwanza hii si "UWT" ni "UWCCM".....Haiwakilishi wanawake wote wa Tanzania,inawakilisha wanawake wachache wa CCM ambao wana interests ktk "Status Quo"...hii si kama ile ya Bibi Titi,Mama Kaselabantu,Ntimizi,Sophia Kawawa na wengine!UWT ya leo haiwasemei Wanawake wa Tanzania waliopo vijijini..wenye shida na dhiki,imeundwa na kina Mama wasiojua kuwa Nanjilinji,Nakapanya,Itelambogo,Isukamahela,Utemini,Mwigumbi,Pawaga,Chipogolo,Veyula na Nyamikoma kuna wanawake wanaosafili kilometa ishirini kutafuta maji,tena maji yasiyo safi wala salama. "UWT" Imepoteza dhima ya kuwa sauti ya Malezi kwa mabinti wa Kitanzania,haina nidhamu,imejaa wanawake mashangingi wanaojali mipasho zaidi ya hoja!!Angalia wanawake viti maalumu kwa tiketi ya "UWT" bungeni,umesikia wamepiga kelele kumtetea Mwanamke halisi wa Tanzania?ndo kwanza wanapokea posho za kununulia "vikuku" na kuhonga vijana kukidhi haja zao. Imefikia kipindi tudai mambo yetu tulioyaimairisha wote wakati wa mfumo wa chama kimoja!majengo ya UVCCM yaliyojengwa enzi hzo tukichangishwa mashuleni na vyuoni,Mali za "UWT" walizochangia Mama na Bibi zetu kwa hela za kwenye pindo za kanga!.."UWT" ni ya Wanawake wa mjini,ndo mana hata Bank yao wameianzsha D'sm na haijulikani hata kwa Wanawake wa vijijini,wakopaji ni haohao wa mjinimjini...UWT ya Leo si ya kina Mama wanyonge,haitaki kuwakomboa Mama zetu toka kutunza fedha ktk pindo za kanga mpaka kutunza Bank...inaona fahari kuwa na wapiga kula masikini wanaowadanganya kwa khanga na vilemba nyakati za Uchaguzi.....SI KILANGO MKE WA MALECELA WALA SOPHIA SIMBA MTALAKA WA KITWANA KONDO!!
 
kwa nini mtu akishapewa madaraka hataki kutoka kuachia na wengine....nadhani ni wakati wa sophia kumpa mtu mwingine nae tuone ataongoza vipi hii jumuiya
 
sofia Simba ni janga!
Sijui hata kama anaweza andaa kitchen party peke yake.
 
Hawa wanasiasa walioingia kwenye siasa kwa mlango wa uani hawana lolote la kuchangia zaidi ya siasa zao za taarabu.
 
Uchaguzi uliopita aligombea mke wa Jaji Warioba na inasemekana hakutoa hata senti moja kwa wapiga kura, ikala kwake......
 
Hivi ni nani anayefaa CCM...? kila mtu ni kichekesho tu...Kuanzia Rais hadi tarishi!

Waache watupiane mawe...wote wako katika jumba la vioo
 
[h=2]Sunday, July 29, 2012[/h] [h=3]JK mapumzikoni nyumbani kwao Msoga[/h]

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Bibi Antonia Mbagalla (85) katika kijiji cha Msoga, kata ya Chalinze Wilayani Bagamoyo wakati wa mapumziko ya mwisho wa wiki leo(Jumapili).
Source Freddy Maro.
 
Huyo anna kilango asingekua malecela asingekua hapa alipo lakini pia hata huyo simba nae hafai... Wanahitaji mtu mpya na mtu safi na asiwe mke wa kigogo wa chama..
 
JUMAMOSI, AGOSTI 04, 2012 05:33 NA MWANDISHI WETU, DODOMA

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), Sofia Simba, amesema jumuiya hiyo haihitaji vurugu na mabadiliko zaidi, kwa kuwa iko imara kutokana na uongozi wake.

Alisema kama kuna mgombea wa nafasi ya mwenyekiti anayetaka kuleta mabadiliko, huyo anataka kuleta vurugu, kwa kuwa jumuiya iko imara kutokana na misingi imara aliyoiweka.

Sofia aliyasema hayo jana makao makuu ya CCM mjini hapa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kurudisha fomu ya kutetea nafasi yake wakati wa uchaguzi wa jumuiya hiyo, utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Pamoja na mambo mengine, Sofia alikuwa akimjibu mgombea mwenzake, Anne Kilango, ambaye juzi alichukua fomu na kusema ameamua kugombea nafasi hiyo kwa kuwa anataka kuleta mabadiliko ndani ya UWT.

“Kuna mwenzangu mmoja amechukua fomu hapa jana (juzi) na kujigamba kuwa anataka kuleta mabadiliko eti kwa sababu ana uwezo wa kufanya hivyo.

“Pia mtu huyo alisema yeye ndiye anayefaa kwa sababu aliingia UWT akitokea ngazi ya wilaya na kwamba mimi niliingia UWT nikitokea ngazi ya kata.

“Sasa ngoja niwaambie, mimi ndiye ninayeijua UWT kwa sababu nimeanzia chini hadi kufika hapa nilipo, kwani niliwahi kuwa Katibu wa UWT katika Tawi la NDC, kisha nikawa Mwenyekiti wa UWT Kata ya Upanga Magharibi pale Dar es Salaam mwaka 1993.

“Pia niliwahi kuwa Diwani wa Kata ya Upanga Magharibi mwaka 2000 na nikawa Mbunge mwaka 1995, na kikubwa zaidi kinachonifanya nitofautiane na huyo mtu ni kwamba, tangu mwaka 1998 nimekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT.

“Sasa angalieni wenyewe mimi na yeye ni nani anayeijua jumuiya, ni yeye aliyeingia akitokea wilayani au mimi niliyeingia nikitokea chini kabisa kwa wanajumuiya?

“Pamoja na hayo, nawaambia UWT iko imara, haihitaji mabadiliko makubwa kama anavyosema, kama anataka kuleta mabadiliko basi anataka kutuletea ugomvi ambao siyo sera yetu.

Kwa mujibu wa Sofia, wakati yeye akishika nafasi hizo, Anne Kilango alikuwa hajaingia katika siasa na kwamba wanachama wa UWT wanatakiwa kuwachagua viongozi wanaoifahamu vizuri jumuiya kuliko wasiofahamu.

Kwa muda mrefu tumekua kimya na tumesahau kuhusu hii jumuiya ya wanawake Tanzania yaani UWT.Hii ilikua inapashwa kubadili jina na kujulikana kama UWCCM na sivyo ilivyo hivi sasa kama ilivyofanyika kwa umoja wa vijana UVCCM HIVYO UMOJA HUO UWT HAUWAKIRISHI INTREST ZA WANAWAKE WA TANZANIA BALI WANAWAKE WANACHAMA WA CCM HIVYO UWEPO WAKE CHINI YA BENDERA YA WANAWAKE TANZANIA NI BATILI.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Back
Top Bottom