Nduka
JF-Expert Member
- Dec 3, 2008
- 8,552
- 2,360
Hivi kupitisha miswaada na sheria za Ruzuku na Madini Bungeni ndiyo ajenda waliyokupa Wapiga kura wa Kigoma Kaskazini hadi uchukulie kama mafaniko makubwa ya ubunge wako hailiwiadi sasa? Siyo tu Miswaada na Sheria haviliwi, kwa Tanzania ni kama kazi bure kwani hakuna anayefuata au kuheshimu haswa vikiwa kwenye "abstract level" kwa mtu wa kawaida kama ishu za Madini na Ruzuku. Watu tungekuelewa kama ungetaja kliniki ngapi, madarasa mangapi, mabomba ya maji na visima vingapi, barabara kilomita ngapi, nk umefanikisha tangu uwe Mbunge.
Ibara ya 63 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inataja kazi za mbunge na hizo ulizozitaja hazimo kabisa. Kama wewe ni mmoja wa watu wanaotaka mbunge kuja kuchimba visima, kujenga barabara, kujenga madarasa, na vitu vingine mnajua kazi za mihimili mitatu?