Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,620
- 46,264
Ukifuatilia Historia za vyama vikuu vya upinzani Tanzania vingi huwa vinaibuka na kupotea kama mvua za msimu, havidumu.
Vyama vikubwa vingi vya upinzani Tanzania viliundwa mwaka 1992. NCCR ilikuwa ya kwanza kuwa chama kikuu cha upinzani ikaipa tabu sana CCM katika uchaguzi wa mwaka 1995, mwaka 2000 NCCR ikaenda katika kaburi la kisiasa na haijafufuka mpaka leo.
CUF wao walikuwa na ushawashi Tanzania mwaka 2000 na 2005, baada ya hapo kikabaki kama chama cha Zanzibar zaidi. ACT nao inaonekana wanafuata mkondo huo .
CHADEMA pekee yake ndio chama cha upinzani ambacho kilianzishwa mwaka 1992 kinachoonekana kuendelea kukua na kuwa ushawashi katika siasa za Tanzania, hata baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 CHADEMA kinaonekana bado kimebakiwa na nguvu za kupambana na kurejesha heshima yake kama chama serious cha siasa cha kitaifa.
Uchaguzi wa mwaka 2025 ni mtihani mkubwa sana kwa uhai wa CHADEMA na demokrasia ya nchi hii.
Vyama vikubwa vingi vya upinzani Tanzania viliundwa mwaka 1992. NCCR ilikuwa ya kwanza kuwa chama kikuu cha upinzani ikaipa tabu sana CCM katika uchaguzi wa mwaka 1995, mwaka 2000 NCCR ikaenda katika kaburi la kisiasa na haijafufuka mpaka leo.
CUF wao walikuwa na ushawashi Tanzania mwaka 2000 na 2005, baada ya hapo kikabaki kama chama cha Zanzibar zaidi. ACT nao inaonekana wanafuata mkondo huo .
CHADEMA pekee yake ndio chama cha upinzani ambacho kilianzishwa mwaka 1992 kinachoonekana kuendelea kukua na kuwa ushawashi katika siasa za Tanzania, hata baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 CHADEMA kinaonekana bado kimebakiwa na nguvu za kupambana na kurejesha heshima yake kama chama serious cha siasa cha kitaifa.
Uchaguzi wa mwaka 2025 ni mtihani mkubwa sana kwa uhai wa CHADEMA na demokrasia ya nchi hii.