Mabomu ya Polisi yatanda Ubungo

Mkuu.. Machinga Complex ni kipimo kizuri cha upungufu wa akili wa viongozi wetu.. Nilisema toka wakati wanaanza matayarisho kwamba kama nia ni hiyo wanayoisema basi itakuwa ni hasara.. Nadhani kulikuwa na personal interests ndo maana wakalazimisha..
Hili la ubungo kwangu mie naona Serikali kabla ya kutoa deadline wangewatafutia eneo mbadala ambalo liko ndani ya biashara.. Au wangeweza hata kununua eneo toka kwa raia na kulitenga kwa ajili ya wamachinga.. Kuwafukuza bila ya kujua wataenda wapi ni kuwaonea na kuwalazimisha kuingia katika vitendo vya uhalifu.. Serikali makini icingewaacha wajazane pale ndo waje kuwaondoa..

Nakubaliana na mdau hapa!
 
Tatizo la kukariri kwamba dola ni matumiza ya nguvu, kwani wakiwaambia wateue uongozi wa wamachinga then wajadiliane nao baada ya hapo wafikiee sulhisho kwa manufaa ya pande zote mbli hao watu wangeondoka tena bila gharama kubwa kiasi hiki. Sasa hao FFU watalinda hapo milele? hAO CHINGA Leo kesho na keshokutwa hawatakuwepo lakini polisi wakitoka watarudi tena. lk hide n seek game
Hakika watarudi tu, labda wawe wanawavizia ghafla ghafla.
Nchi hii shida kweli serikali ya ccm inamaamuzi ya kuangalia upande mmoja tu sijui hii namna wamekopi wapi?
 
Sioni tatizo kuwaondoa ila sasa wangeweka mipango wawapeleke sehemu ambayo watafanyia hizo kazi ili wawe wanalipa hata ushuru...tatizo wanawafukuza lakini waende wapi? na hii ni shida ya hii nchi hakuna mipango kila mtu anajiwazia yeye tu...

Lile eneo litakua na usalama zaidi hao machinga wakiondolewa mana kwanza asilimia kubwa ni vibaka wanaiba wanajichanganya pale.

Nakubaliana nawe lakini Watanzania wabishi, hata ukuwapatia nafasi nzuri ya kufanyia biashara hawatakwenda huko; tatizo letu atuheshimu sheria. Nawapa pole lakini wafuate sheria siyo kila mahali unafanya biashara tu hii siyo sawa.
 
Sheria mbona haitekelezwi kwa jengo la Tanesco ambalo liko ndani ya hifadhi ya barabara?
 
Msitegemee ccm kuungwa mkono, kila kukicha wanatengeneza uadui na raia, hawayaoni makosa yao, kwa mfano, serikali ya ccm kuiweka gridi ya taifa pale ilipo ni location mbaya, ni rahisi sana kuhujumiwa akitokea mhujumu, kwa mujibu wa master plan ya mipango miji, stand ya mabasi inasomeka ilipaswa kuwa maeneo ya tabata, kuna eneo kubwa sana lilitengwa kwa ajili hiyo, wamemegeana maeneo na kiua plan hiyo, wakajibana pale ubungo terminal iliyokuwa ya uda, hostel za chuo kikuu kuzijenga mabibo ni kosa jingine la wazi kwa serikali ya ccm, wangezijenga kwenye eneo la chuo kikuu mlimani kwani pana eneo kubwa sana, badala yake kuna biashara ya kiuwekezaji, mlimani city. location ilipo upcountry bus terminal ukijumlisha movement ya wanachuo kwenda na kurudi main campus kunafanya kuwepo watu wengi eneo la grid ya taifa na ndipo wamachinga kwa nature ya biashara zao inawavuta kuwatega wateja wapitao ama kwenda hostel, majumbani ama bus terminal. serikali haiyaoni makosa yake, inayaona makosa iliyoyazalisha na kuyashughulikia kikatili sana. waondoe pale bus terminal ili kuepusha kizaaza siku grid ama mtambo wa kufua umeme kwa gesi ukipata hitilafu kubwa.
Serikali ya ccm ni adui wa wananchi.

Jogi, ni serikali gani ambayo ingeingia madarakani na kuwaacha wamachinga wafanye biashara kwa style ile wanayofanya kama ile ya ubungo, ambapo hata pa kupita panakosekana? Hata ingekuwa ni serikali ya CHADEMA bado ingefanya hivyohivyo? Kuhusu hostel za mabibo kujengwa zilikojengwa hili jambo tulilihoji sana wakati ule tunatia mgomo Mlimani city isijengwe badala yake zijengwe hostel.
Ukweli ni kwamba mabibo hostel isingeweza kujengwa chuoni kwa kuwa ile ni investment binafsi ya NSSF. Kama NSSF wakiamua kubadili matumizi ya zile hostel, udsm watatakiwa kuondoa wanafunzi wao. So isingewezekana kuruhusu shirika binafsi lijenge kwenye eneo la chuo kama makubaliano si kuzikabidhi hizo hostell chuoni in the future kama ilivyo kwa mlimani city.
Kuhusu kugawana eneo la basi terminal sina idea yoyote, but naambiwa ile basi terminal inahamishiwa kibamba, sijui hili lina ukweli gani.
 
watarudi na kuruhusiwa kufanya biashara zao utakapokaribia uchaguzi mkuu mkuu 2015...!
 
Kuwaondoa ni sawa, kwa usalama wao wenyewe na raia wengine.
Lakini wazingatie kuwa hawa ni Machinga (Marching-Guys).

Ugomvi wangu ni mbinu za kuwatoa hapo, wanawatisha na mabaki ya mabomu ya Arumeru
 
Polisi wa Tanzania katika kazi wanazopenda kuzifanya, na huzifanya kwa ufanisi mkubwa sana ni hii ya kuwapiga wamachinga.

Utashangaa wamejaza mabomu ya machozi, risasi za moto na magari ya washawasha kama vile wanakwenda vitani. Pamoja na hasira za kugaragazwa Arumeru, serikali ina hasira za wanaubungo kuikataa ccm na wanatambua kwamba vijana wanazidi kuikataa.

Well, ni wazo zuri kuwaondoa katika hayo maeneo hatarishi lakini wamewaandalia maeneo ya kuwahamishia? kwani magufuli na tanesco hawajui kwamba hao watu wako hapo ili kujitafutia rizki zao!? kwanini wasiwaandalie mahali muafaka pa kufanyia biashara kabla ya kutumia maguvu kuwahamisha?

pumba ulizochangia ni bora ungewapa kuku wakutagie mayai.
 
Iache ipigwe hiyo mijitu ya dar isiyopenda mabadiliko wao kutwa wameshikilia ccm kama vle walichanjwa chale za matak.oni na mwalimu nyerere au kawawa.
Badilikeni ndugu zangu wa dar saa ya ukombozi ndio sasa jamani.!
 
Nipo maeneo ya ubungo hali si nzuri hata kidogo
Kuna machinga wenye uchu wa maisha Dar? Machinga wako mikoani, wanaojua thamani ya kila senti wanayoipata. Hao ndio hata polisi hualika majeshi mengine kuwasaidia. Maana wanajua wanachokipigania. Sio hawa watoto wavivu waliokimbia shamba na kuingia Dar es Salaam.
 
hatimaye serikali imewaondoa wafanyabiashara wanaofanya biashara zao katika eneo la ubungo songas pembezon mwa barabara ya mandela.
 
Eti hamuondoki kwa kuwa kuna stand ya daladala,kota za tanesco n.k pia eti muonyeshwe pa kwenda! Kwani nani aliwaonyesha mje hapo Ubungo? Huo ni ubishi wa kizamani,umeme utakapolipuka mtageuza kibao na kulaumu serikali! Acheni hizo!
 
Hz ni njama maaskari wanaongozwa na Serikali ya CCM wanamalizia hasira zao kwa kuona kuwa CDM wanakuja moto juu c mmeona wenyewe huko Arumeru Mashariki na majimbo mengine wajiandae na waache kuwaharibia wananchi wa kipato cha chini au kwa sbb wao wana sehemu za kudaia posho hy kazi isiwape kiburi wananchi tukiamua tunaweza ohoooo.
 
Jogi, ni serikali gani ambayo ingeingia madarakani na kuwaacha wamachinga wafanye biashara kwa style ile wanayofanya kama ile ya ubungo, ambapo hata pa kupita panakosekana? Hata ingekuwa ni serikali ya CHADEMA bado ingefanya hivyohivyo? Kuhusu hostel za mabibo kujengwa zilikojengwa hili jambo tulilihoji sana wakati ule tunatia mgomo Mlimani city isijengwe badala yake zijengwe hostel.
Ukweli ni kwamba mabibo hostel isingeweza kujengwa chuoni kwa kuwa ile ni investment binafsi ya NSSF. Kama NSSF wakiamua kubadili matumizi ya zile hostel, udsm watatakiwa kuondoa wanafunzi wao. So isingewezekana kuruhusu shirika binafsi lijenge kwenye eneo la chuo kama makubaliano si kuzikabidhi hizo hostell chuoni in the future kama ilivyo kwa mlimani city.
Kuhusu kugawana eneo la basi terminal sina idea yoyote, but naambiwa ile basi terminal inahamishiwa kibamba, sijui hili lina ukweli gani.

Mkuu kuwahamisha wamachinga katika eneo lenye biashara ni KUKOSA AKILI YA BIASHARA..

Nilipiga kelele sana (hawa vichwa ngumu wa serikalini) wakati wanawaondoa wamachinga manzenze, mahakama ya ndizi na hata ubungo si support kabisa huu ujinga nitaeleza kwanini

a. Umajinga unatoa ajira isiyo rasmi kwa vijana wengi sana Tanzania dawa si kuwaondoa bali kuondoa zile nyumba, taasisi etc zilizokaribu na centres za wamachinga mfano. mazense serikali ilitakiwa inunue na kuhamaisha makazi ya watu pale na kuweka soko kubwa pale vilevile ubungo jengo la tanesco na maujinga yao waondoke wamachinga watengenezewe utaratibu wa kuwa na soko lao pale..

b. Turnover, in terms of cash transaction and services provided per day maeneo ya machinga ni kubwa sana ni uhai kwa taifa na kwa wananchi wake hasa kodi kwakuwa mazao na huduma zinauzwa maeneo hayo..

Serikalini tatizo lao hawajawahi kufanya kazi za biashara mtu amekuwa officer wa kufukuzia allowances hawezi kujua business preposition na faida itokanayo ndio maana wanaweza kuja na amri za kijinga kama hizo..ndio maana tunataka rais mmachinga sio professional politicians ..soma signature yangu
 
Back
Top Bottom