Sijakuelewa kuhusu Manzese, mbona wemejengewa paple pale karibu? Labda wewe ulitaka wajengewe pale darajani na si mita hamsini kutoka darajani kuelekea urafiki. Ok, tugeukie kwenye suala hilo la ubungo. Strategically, ubungo si mahali salama kabisa kwa mikusanyiko ya watu. Pale yale majenerator ni kama mabomu, na matransformer yaliyopo pale yanatumia mafuta ambayo yanaweza kusababisha milipuko. Kukusanya watu pale ubungo ni hatari sana kwa namna palivyo. Na kwa kifupi tu, wateja wa ubungo wanatokana na uwepo wa stendi ya daladala pamoja na mabasi ya mikoani. soon kituo cha mabasi ya mikoani kitahamia kibamba. Na kwa sababu za kiusalama kituo cha dala dala pia chaweza kuhama. But suala la kuwaondoa wamachinga pale naliunga mkono sana tu kutokana na mazingira ya pale yalivyo.Mkuu kuwahamisha wamachinga katika eneo lenye biashara ni KUKOSA AKILI YA BIASHARA..
Nilipiga kelele sana (hawa vichwa ngumu wa serikalini) wakati wanawaondoa wamachinga manzenze, mahakama ya ndizi na hata ubungo si support kabisa huu ujinga nitaeleza kwanini
a. Umajinga unatoa ajira isiyo rasmi kwa vijana wengi sana Tanzania dawa si kuwaondoa bali kuondoa zile nyumba, taasisi etc zilizokaribu na centres za wamachinga mfano. mazense serikali ilitakiwa inunue na kuhamaisha makazi ya watu pale na kuweka soko kubwa pale vilevile ubungo jengo la tanesco na maujinga yao waondoke wamachinga watengenezewe utaratibu wa kuwa na soko lao pale..
b. Turnover, in terms of cash transaction and services provided per day maeneo ya machinga ni kubwa sana ni uhai kwa taifa na kwa wananchi wake hasa kodi kwakuwa mazao na huduma zinauzwa maeneo hayo..
Serikalini tatizo lao hawajawahi kufanya kazi za biashara mtu amekuwa officer wa kufukuzia allowances hawezi kujua business preposition na faida itokanayo ndio maana wanaweza kuja na amri za kijinga kama hizo..ndio maana tunataka rais mmachinga sio professional politicians ..soma signature yangu
Sijakuelewa kuhusu Manzese, mbona wemejengewa paple pale karibu? Labda wewe ulitaka wajengewe pale darajani na si mita hamsini kutoka darajani kuelekea urafiki. Ok, tugeukie kwenye suala hilo la ubungo. Strategically, ubungo si mahali salama kabisa kwa mikusanyiko ya watu. Pale yale majenerator ni kama mabomu, na matransformer yaliyopo pale yanatumia mafuta ambayo yanaweza kusababisha milipuko. Kukusanya watu pale ubungo ni hatari sana kwa namna palivyo. Na kwa kifupi tu, wateja wa ubungo wanatokana na uwepo wa stendi ya daladala pamoja na mabasi ya mikoani. soon kituo cha mabasi ya mikoani kitahamia kibamba. Na kwa sababu za kiusalama kituo cha dala dala pia chaweza kuhama. But suala la kuwaondoa wamachinga pale naliunga mkono sana tu kutokana na mazingira ya pale yalivyo.
Duh, haya bwana. Hivi pale ubungo wale wamachinga wakiweka zile meza wanalipia bei gani? Hivi unajua ni hasara kiasi gani ambayo serikali inapata kutokana na hizi biashara zisizo rasimi? Kwa mfumo wa biashara ya namna ile inakuwa vigumu sana kukusanya kodi. Hata hivyo, sidhani kama gharama za kuhamisha ile miundombinu ya tanesco pale inafanana na returns ambazo serikali itapata kutoka kwa wamachinga. Kuhusu manzese, suala la usalama umeliangalia? Ukizingatia ile ni barabara kuu?Kwanini majereta yasihame badala ya watu wenye kuleta fedha wahame; manzenze yale makazi ya watu karibu na daraja ya kazi gani pale; pale panatakiwa pawe soko pande zote mbili; serikali iwaondoe wale wazee wenye makazi pale..
Biashara inalipa kwa serikali kuliko nyumba zao hizo hali kadhalika biashara ubungo inalipa kuliko majerata ya mgao.
Duh, haya bwana. Hivi pale ubungo wale wamachinga wakiweka zile meza wanalipia bei gani? Hivi unajua ni hasara kiasi gani ambayo serikali inapata kutokana na hizi biashara zisizo rasimi? Kwa mfumo wa biashara ya namna ile inakuwa vigumu sana kukusanya kodi. Hata hivyo, sidhani kama gharama za kuhamisha ile miundombinu ya tanesco pale inafanana na returns ambazo serikali itapata kutoka kwa wamachinga. Kuhusu manzese, suala la usalama umeliangalia? Ukizingatia ile ni barabara kuu?
Kwa hili naipongeza halmashauri ya jiji pamoja na polisi ila nawakumbusha kuwa isiwe kama kazi ya zimamoto wametumia nguvu Nyingi na wakati wao mwingi kuwatoa kwa leo basi wasijisahau wakajiondokea na kesho tukawapata Hawa machinga wamerudi kwenye hayo maeneo tena,jamani swala la watu kujitafutia riziki ni sawa kabisa lakini ni lazima tufuate sheria na taratibu za nchi kanuni za biashara zifuatwe bila kuathiri mazingira biashara zifanyike sehemu rasimi.siyo uweke meza ama kibanda cha kuuza suruwali barabarani kisa eti serikali haijakujengea soko hii isiwe sababu ya wewe kuvunja sheria na taratibu za nchi,tafuta chumba jirani na eneo husika panga weka mali ndani uzia ndani ya chumba kwa ustaarabu na jiji ama miji,barabara zetu ziwe safi kwa matumizi husika
Kwa kweli mpango huu ni mzuri kwa usalama wa hawa wafanyabiashara, matumiaji na taasisi zinazomiliki maeneo hayo na maendeleo yetu. Mpango huu pia utatusaidia ktk zoezi la mipango miji.
Lakin tatizo langu ni nguvu na mbinu inayotumika. Hv serikali haijui kuwa wafanyabiashara hawa wanategemea biashara hizi kuishi wao na familia zao? Hivi haijui kuwa kwa kufanya hivi ni sawa na kukiuka haki zao za kuishi? Kwa nini wasingeandaa mpango wa kuwahamishia sehemu nyingine au kuwawekea mazingira bora zaidi ya kufanya biashara?
Mkuu nimekusoma vizuri comment zako.Mkuu usalama si tatizo mkuu barabara kuu ndio hasa sehemu ya kufanya biashara sijaona mantiki yako labda uwe hujawahi kufanya business, barabara kuu nyumba za kuishi wapi na wapi pale panatakiwa maduka na biashara na soko la kisasa kabisa (manzense) kwasababu tuna maofficer wamesoma degree za biashara bila kufanya biashara kila siku kazi yao kuua masoko badala ya kuyaenzi hawajui masoko (au sehemu kuwa soko) ni kazi kubwa sana mkuu..
Ile miundo mbinu ya tanesco pale haifai kabisa kwanza ziko karibu na high way na makazi ya watu wanatakiwa wayapeleke hata katika kambi ya jeshi wakitaka..huko makongo juu kusiko na makazi na watu wengi kama ubungo ambako biashara inalipa
Mkuu returns ni kubwa sana kutoka kwa wamachinga a. ajira b. bidhaa zinazouzwa pale zote zinanunuliwa na vat inalipwa c. wengi wetu tuna leseni za biashara ndogondogo d. services huduma na idadi ya watu wanaotegemea huduma zetu kuanzia chakula cheap, nguo etc huwezi kulinganisha na mjengo wa tanesco na transfoma zake..
Maofisa wengi serikalini ni vilaza wa biashara wamekariri usafi, security etc. wanawaona wale vijana kama vile uchafu kwa vile wao walipomaliza shule waliingia ofsini hawajawahi kufanya biashara, wanatembea kwenye magari wanaona wale vijana ni bughudha etc..
MASOKO hayavunjwi yanaendelezwa; only in Tanzania MASOKO yanavunjwa sijawahi kuona ujinga kama huu.
aha ha aha ah duh eti kama eapoti...BIg up maghufuli , sema hawa jamaa wartarudi ..sasaq ndio muda muafaka wa kuwatafutia sehemu nyingien