Wanabodi,
Asubuhi hii FFU wamewatawanya wamachinga katika maeneo ya Ubungo mataa, Ubungo maji, stendi ya mkoa na wale wanaofanya biashara katika maeneo ya gridi ya taifa.
Mojawapo ya maeneo ambayo yameathirika ambayo nimeyashuhudia ni ile baa ya Standard ambayo ipo karibu na stendi ya mkoa. Baa hiyo imevunjwa katika eneo lake la mbele ikiwa ni hatua za utekelezwaji wa oparesheni hiyo.
Kuna magari ya FFU na askari kanzu yasiyopungua 30 ambayo yametanda maeneo hayo ya Ubungo. Pamoja nayo yapo mawashawasha mawili ambayo yanasubiri kufanya kazi pale itakapohitajika.
Kwa ujumla hali bado ni shwari na machinga wengi wameingia mitini kwa sasa japo kuna kajikundi kadogo ambacho bado kanajibizana na askari pale maeneo ya mataa. Kajikundi hako kana mabango mawili ambayo yanasomeka:
"Haya ndiyo maisha bora kwa kila mtanzania?"
"Nyie mnasaini posho mnakula, siye tunakufa na njaa".
Oparesheni hii inafuatia matangazo yaliyokuwa yanatolewa na Tanesco, Tanroads na Manispaa ya Kinondoni ya kuwaondoa watu wanaofanya shughuli katika maeneo ya gridi ya taifa, chini ya njia za umeme na katika hifadhi ya barabara.
Kwa mujibu wa Tanesco, Tanroads na Manispaa ya Kinondoni ilitakiwa wafanyabiashara hao wawe wameondoka katika maeneo hayo kufikia tarehe 01.04.2012 la sivyo wangeondolewa kwa nguvu.
NB:
Kwa wale akina Tomaso: Sikuweza kupata picha kwa sababu kamchina kangu hakana uwezo wa kuchukua picha.
Asubuhi hii FFU wamewatawanya wamachinga katika maeneo ya Ubungo mataa, Ubungo maji, stendi ya mkoa na wale wanaofanya biashara katika maeneo ya gridi ya taifa.
Mojawapo ya maeneo ambayo yameathirika ambayo nimeyashuhudia ni ile baa ya Standard ambayo ipo karibu na stendi ya mkoa. Baa hiyo imevunjwa katika eneo lake la mbele ikiwa ni hatua za utekelezwaji wa oparesheni hiyo.
Kuna magari ya FFU na askari kanzu yasiyopungua 30 ambayo yametanda maeneo hayo ya Ubungo. Pamoja nayo yapo mawashawasha mawili ambayo yanasubiri kufanya kazi pale itakapohitajika.
Kwa ujumla hali bado ni shwari na machinga wengi wameingia mitini kwa sasa japo kuna kajikundi kadogo ambacho bado kanajibizana na askari pale maeneo ya mataa. Kajikundi hako kana mabango mawili ambayo yanasomeka:
"Haya ndiyo maisha bora kwa kila mtanzania?"
"Nyie mnasaini posho mnakula, siye tunakufa na njaa".
Oparesheni hii inafuatia matangazo yaliyokuwa yanatolewa na Tanesco, Tanroads na Manispaa ya Kinondoni ya kuwaondoa watu wanaofanya shughuli katika maeneo ya gridi ya taifa, chini ya njia za umeme na katika hifadhi ya barabara.
Kwa mujibu wa Tanesco, Tanroads na Manispaa ya Kinondoni ilitakiwa wafanyabiashara hao wawe wameondoka katika maeneo hayo kufikia tarehe 01.04.2012 la sivyo wangeondolewa kwa nguvu.
NB:
Kwa wale akina Tomaso: Sikuweza kupata picha kwa sababu kamchina kangu hakana uwezo wa kuchukua picha.