Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Hivi tuna Amiri Jeshi wangapi katika nchi hii kiasi cha kila mwanasiasa kutangaza mambo ya vita???? Uelewa wangu tuna Amiri jeshi mmoja tu wanasiasa acheni kutumia majukwaa kuongea pumba zenu mko tayari na nani wewe umeambiwa na nani hasa
 
Vita ikitokea sasa napata wasiwasi huenda majeshi yetu yakapokea amri zinazokinzana maana Membe katangaza, sasa Lowassa, kesho sijui ni nani atatuambia tuko tayari, na mahanga yetu silaha yalishachomwa
 
Mimi nashangaa chain of command yetu iko wapi. Lowassa yeye ni nani kuzungumza kwa niaba ya JWTZ? Kamanda in Chief yuko wapi? Yaani Tanzania yetu imeshaparaganyika kiasi kwamba yeyote tu anaweza kuzungumza kwa niaba yake? Suala la vita au kuwa tayari kwa jeshi letu ni kamanda in chief peke yake anayeweza kulizungumzia. When was the last time you saw Lowassa inspecting a guard of honour?

Mkuu, kumbukumbu zangu zinanionesha,serikali ya dhaifu ilianza kulalamikiwa kuwa kuna ombwe la uongozi mara tu baada ya Low watch kung'olewa na bunge, yeye ndo alikuwa mtendaji mkuu wa mambo yote na mwasisi wa vyote including shule zile za Yebo yebo na wale walimu wa Voda fasta ilikuwa ni vision yake, alipoondoka kila kitu kikawa chini, huwa anayo maamuzi though ni fisadi, hapa amethibitisha lile neno alilowahi kutamka kwenye bunge la bajeti mwaka jana kwamba serikali imekuwa na ugonjwa wa kutokuchukua maamuzi, yeye kaona afanye kitu, sio mzee wa kupinda pinda, i mean yule mzee wa kule Katavi.
 
Kwahili na mkubali JK always subira uleta heli! Hakuna aja ya kukurupuka mara wanapeleka vifaa na wanajeshi nini km sio ukosefu wa fikra? Malawi juzi walituma delegation tena mpaka Bungeni hiyo yote ni kzungumza na sio vinginevyo..LEO TUMEONA KAULI TATA ZA CHEAP POLITICIANS WENYE NIA YA KUINGIA IKULU..SITTA.... MEMBE....LOWASSA.. Hawa wote kwa mtizamo wangu ni wakurupukaji and gullible leaders yani ni wafuata upepo...viongozi bora ni watulivu, wasiokurupuka na wanaopenda majaridiano na sio vinginevyo...VITA NI HATUA YA MWISHO KABISAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Huyu Mmasai hapo ndipo ninapompendea katika maamuzi magumu. Huwa haumi maneno.


yaani wamalawi wakiamua kucheza na jina la huyu bwana kama tulivyo kuwa tunacheza na jina la iddi amini dada katika psycological warfare tutaumia vibaya, sioni busara kila kiongozi kuongea anyopenda katika kipindi hiki. ukumbuke vita hii inahusu raslimali persee, acheni kabisa ujinga wenu.
 
Kwa mara ya kwanza nakubaliana na Lowassa katika tamko thabiti na lisilo la kumung'unya maneno.
Tunatumaini ndugu zetu wa Malawi watatuelewa vizuri katika hili.
Wakato mwingine si vibaya kutunisha misuli jirani anapoleta chokochoko.
Nashukuru Mungu mpango wa reserve army wa JKT nao unaanza karibuni.

Jamani naomba musishushe ufahamu unaotakiwa kuwa JF. Kabla ya kumusifu huyu mtu hebu kwanza someni kazi na madaraka ya Bunge. Baada ya hapo ndo mutoe sifa.

Kwa matamko yake ya aina hii mimi kwangu nasema ni upuuzi kwa mbunge wa siku nyingi kugeuka kufanya kazi ya Amiri jeshi mkuu. Hana sababu yoyte ya kuzungumza uchafu wake kama huu. Kazi yake ni mbunge basi! Hata kama ana malengo yake mengine hatutegemei display za aina hii.

Tatizo la Lowasa kila wakati anataka sifa zimuendee. Kila wakati anaona kazidiwa na wengine.

Ni aibu ktk JF kuanza kusifu mtu wa aina hii. Naona tunajisahau na kuanza ushabiki. Bunge gani ktk nchi litatangaza vita na kutisha nchi nyingine?

Eti naye anataka kuwa Rais. Basi, asubiri mpaka muda huo ukifika ndo atoe hayo. Kama miguu itakubali kusimama majukwaani maana sasa naona ni hotuba za kwenye sofa.
 
lowasa anatangaza vita kama nani? amiri jeshi mkuu? halmashauri ya ccm? ukweli ni kuwa yeye ndo yuko tayari kwa vita, pamoja na akina fredy lowasa, rostam aziz, na mafisadi wenzake wanaofaidi raslimali za taifa hili peke yao. hakuna kijana wa tanzania atakayenenda kumwaga damu yake malawi halafu mafuta yakipatikana ziwani kule akina lowasa waanze na mikataba ya o ya ki-richimond!!!! hakuna! afadhali wamalawe wafaidi hayo mafuta kwa kuwa wale pia ni wenzetu, lakini si akina rostam na lowasaa , NOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hili ni Tamko zuri na linatia Moyo japonapata shida kuamini kama kweli tutapigana (pale itakapobidi kupigana) na Malawi coz ninashawishika kuwa kuko na kitu zaidi ya Malawi..So utayari wa jeshi letu uangalie kilicho nyuma ya Malawi na si kuiangalia Malawi kama Malawi. Jambo jingine ni kuwa, nilitegemea kusikia kauli ya rais ambaye ni Amir Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania katika sakata hili na si kusikia kauli ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje na Usala Mh. Lowassa japo hata hivyo siipingi kauli yake...
 
“Ikibidi kuingia vitani jeshi letu liko vizuri sana na kama ilivyo ahadi yao (JWTZ), wako tayari kulinda mipaka ya nchi yetu hadi tone la mwisho. Tunasali sana tusifike hapo,” - alisema Lowassa..

Hivi Amiri Jeshi MKUU yupo Likizo, au?
 
Acha nidhamu za woga. JWTZ wenyewe wana hamu ya kupigana.

Lakini vita siyo kitu cha kushangilia hata kidogo. Inaweza kutuathiri sana. Kwangu mimi naona ni mapema sana kuanza kufikiria hili la kupigana. Juhudi za kidiplomasia zingetumika kwanza kutatua huu mgogoro.

naunga mkono hoja.ila wakitukanyaga hatuna budi kuwasukuma
 
mbona sijaona pahala wamalawi wamesema hawataki hao uliowataja wanufaike na ziwa Nyasa?can you back up you claims?suluhisho la mgogoro ni lipi?huu mgogoro ulivyo,mwenye kuwa juu ni mwenye influnce at the time being,kama mama Clinton yuko nao,wala msijisumbue,kamateni mafisadi kwanza,nchi itarudi kwenye msitari,"umma" utalinda nchi.Kuna pahala panshinda nguvu ya umma?jeshi lipo lakini hata recruiting inafanyika kwenye umma wa wananchi,na sapoti ya vita pia.Hatuna nguvu za "big nations" kujiamulia bila sapoti kubwa ya wananchi.Halafu matatizo tuliyonayo ni makubwa kiasi kwamba kupostpone hii issue ni more relevant.

pointless
 
"Mimi nashangaa chain of command yetu iko wapi. Lowassa yeye ni nani kuzungumza kwa niaba ya JWTZ? Kamanda in Chief yuko wapi? Yaani Tanzania yetu imeshaparaganyika kiasi kwamba yeyote tu anaweza kuzungumza kwa niaba yake? Suala la vita au kuwa tayari kwa jeshi letu ni kamanda in chief peke yake anayeweza kulizungumzia. When was the last time you saw Lowassa inspecting a guard of honour?"

KWELI TUNA SHIDA KUBWA YA KUPAMBANUA NA KUTAFSIRI MAMBO!!! lOWASA KAONGEA VIZURI SANA-NA HUWA HAPA NDIPO NAMKUBALI. HATAFUNI MANENO NA ANAJIAMINI-(MOJA YA SIFA KUBWA YA KIONGOZI). KATIKA HILI LOWASA HAJAZUNGUMZIA VITA HATA KIDOGO. ALIJARIBU KUELEZA HALI ILIVYO-NA KAMA KIONGOZI KUWAONDOLEA WATANZANIA WOGA NA KUWAJENGEA CONFIDENCE NA JESHI LAO. HUYU NDIYO KIONGOZI-RESPONSIVE- SIO DHAIFU. LOWASA SIMSAPOTI KIUFISADA (PAMOJA NA KUWA HAKUNA UDHIBITISHO PASIPO SHAKA ULIOTOLEWA IKIACHA SPECULATIONS). IN MY VIEW-IS THE ONLY PERSON WHO CAN STAND THE COMPETITION AGAINST CHADEMA CANDIDATE- HAKUNA MWINGINE NINAEMUONA CCM. TUKIMPA URAISI ATAFANYA WOUNDERS-(I AM OPTIMISTIC ABOUT THIS) KUONYESHA YOTE YALIYOSEMWA YALIKUWA (SIASA ZA MAJI TAKA) NA KWAMBA TULICHELEWA KUMKABIDHI RU HILI.
 
Ni bora kabisa tuingie vitani maana hata wanajeshi wamekaa muda mrefu idle na hata vifaa vya kijeshi ambavyo vimenunuliwa muda mrefu tanzania imekuwa inashindwa pa kuvijaribia mpaka hata mabomu mengine yana-expire na kujilipukia ovyo! Safi sana maana hata baadhi ya wanajeshi wanashinda kwenye virabu vya gongo pale kigogo sambusa - kunduchi kwa ajili ya kukosa kazi ya kufanya!

Waitu muikalege!
 
Mimi nashangaa chain of command yetu iko wapi. Lowassa yeye ni nani kuzungumza kwa niaba ya JWTZ? Kamanda in Chief yuko wapi? Yaani Tanzania yetu imeshaparaganyika kiasi kwamba yeyote tu anaweza kuzungumza kwa niaba yake? Suala la vita au kuwa tayari kwa jeshi letu ni kamanda in chief peke yake anayeweza kulizungumzia. When was the last time you saw Lowassa inspecting a guard of honour?

Inashangaza sana'sijui wakati nyerere na iddi amin yangetokea haya ya kila mtu kutoa tamko ingekuwaje'hivi lakini kamanda in chief yuko nchini au kesha safiri?ovyo kabisa
 
I advice all my collegueTanzanians to distance ourselves from such provocative and irritating statements leaders of the Lowasa type and others.Still I believe that the confict can be sorted out through a diplomatic approach on both sides.

We should refrain from this mindset of Lowasa and his fellows who are after cheap politics and Iam sure they do these in order to cover and divert us from the current National agenda about their sabotage to the economy of this Nation.
 
Kutokana na chokochoko waziletazo nchi jirani ya Malawi na kupitia kauli za viongozi wetu Mh.Membe wakati anawasilisha Budget yake na Mh. Lowasa kupitia kikao cha siri cha Kamati yake sasa wakati umefika wa kulipia matumizi ya jina hilo la Makamanda.
Ikitupasa kuingia vitani basi nashauri wale wote wajigambao kuwa makamanda,wazalendo wa kweli na wapigania haki ni wakati wao kusonga front kama chambo ili wakainusuru Mipaka ya Nchi yetu.
Kazi kwenu kombania ya Green Guard, Blue guard na Wazee wa gwanda.

Umewasahau Red Guard mkuu
 
Kwa siasa za nchi yetu, isije iikawa kuna kundi mojawapo la CCM limeamua kushirikiana na Malawi ili vita ianze na JK apinduliwe huku au aonekane kuwa hawezi kuendesha vita kama amiri jeshi mkuu.
Kulikuwa na habari kuwa Mwamunyange hamheshimu Amiri jeshi mkuu.

Tushabikie vita ila nahisi watanzania tutaumia zaidi kwa hili.

Ukizingatia kuwa hata huko jeshini hao wakubwa wananuka rushwa kuanzania kwa Abdulrahman Shimbo na ile kashfa ya matrekta.
 
Back
Top Bottom