Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Najua mengi yatachangiwa humu kuhusu tamko hilo la LOWASA. wengine watasema ni shujaa, wengine watasema ni zaidi ya Serikali, wapo watakaomponda kuwa anatapatapa, lakini ukweli ubaki pale pale kuwa VITA siyo jambo ka kukimbilia hata kidogo na hakuna haja ya kulishabikia kisias, Cha msingi tu, tuombe mambo yaishe salama. Wazee wetu, watoto wetu, akina mama wajawazito kupitia maombi yao watatutafuna na hakika wote tunaoshabikia tukifikiri ni njia mojawapo ya kujipatia umaarufu kisiasa tujiulize kama tunafanya hivyo ili iweje?Kama Kuna chama cha siasa au mwanasiasa anaona hii ni njia ya kujipatia umaarufu kwa kusema, Serikali inaogopa au CCM ni waoga na serikali yao, huyo hafai hata siku moja kujiita rais wa Tanzania. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
 
Kikwete sijui kalogwa yaani utawala wake umeharibu nchi kuanzia migomo watu kuuawa bila sababu uwizi serikalini na sasa hivi tunakaribia kwenda vitani. Hivi ni laana gani hii tumeachiwa?
 
"...Nia ya kuwapiga tunayo, sababu ya kuwapiga tunayo, na uwezo wa kuwapiga tunao. Nataka dunia ituelewe hivyo..."
 
TUPO TAYARI KUINGIA VITANI NA MALAWI

Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, imekutana mchana wa jana na kutafakari hali ya mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na Malawi.

Kwanza juzi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, mheshimiwa Bernard Membe, alielezea vizuri msimamo wa Serikali kuhusu jambo hili...

 
Kiongozi makini hawezi ku speculate vita wakati diplomatic means hazijawa exhausted.

Worse still, anaji contradict kwa ku refer to diplomatic options, baada ya kupiga mbiu za vita.

Na wabongo wanamshangilia.
 
watu wa lowassa mmepata pa kutokea,eti kauli ya lowassa!hivi ni ya lowassa ama ya kamati anayoingoza?nahitaji ufafanuzi zaidi

Tena ni ujinga kujaribu kushabikia uchochezi. Huyu bwana alikuwa kapania kuivuruga bajeti ya Foreign, alipowekewa mitego akafyata lakini akaona atokee hapa kwenye swala la Malawi na kutaka kutuingiza katika panic isiyo na sababu. Na hii ni kwa sababu yeye hatoki karibu na mpaka wa Malawi wala hana maslahi ya kibiashara kule kusini. Hatuwezi kukubali watu ambao ni irresponsible kama hawa watuinguze vitani pale ambapo mazungumzo yataleta tunachokihitaji. Hivi ni raha gani kuumiza wananchi wetu na wale wa nchi nyingine kwa kitu kinachoweza kumalizwa kwenye board room? Sisi hatuna nchi nyingine ya kukimbilia na familia zetu, wala hatujanunua nyumba london.

Mwalimu alipoiingiza nchi yetu vitani, uchokozi wa Amin ulikuwa umevuka mpaka na juhudi zote za kidiplomasia zilikuwa zimeshindwa. Amin alivamia nchi yetu kijeshi na tulikuwa na haki ya kujilinda na kumfukuza kutoka katika mipaka yetu, siyo hizi motives za kisiasa ambazo unajiuliza nchi hii ikiwaka moto yeye atamuongoza nani. For once nakubaliana na Mzee Mwanakijiji kwamba kama huyu ndiye watu wanayemfikiria kuwa Amiri jeshi Mkuu wa majeshi yetu basi nchi hii haitakuwa kwenye mikono salama. Recklessness kama hii aliifanya Bush na mpaka leo Marekani wanalipa gharama za mindless attacks on perceived enemies. Ona Palestine na Israel walipigana kwa miongo mingi kwa ajili ya mipaka na maeneo lakini baada ya kugundua kwamba vita si suluhisho, sasa kila upande unasisitiza haja ya mazungumzo. Tuiache nchi sasa ijikite katika kujikwamua na umaskini wa watu wetu kuliko huu uchochezi wa mtu anayetafuta pa kutokea baada ya milango ya kisiasa kufungwa. Angejikita kwenye matibabu yake kwanza.
 
sisi wa tz tusijifariji na kauli za viongozi wasiotazama mbele.mkumbuke kuwa vita haina macho na kifo hakichagui sura wala kabila.mkumbuke kuwa watakufa watu wa Malawi na watanzania pia na pengine hao viongozi mnaowashabikia kwa kauli zao za kuhalalisha vita hawatokuwa wahanga ktk hili.ni jamaa zetu,ndugu zetu wakiwemo na wanajeshi wetu watakao poteza maisha kwa jambo ambalo zinaweza kutumika njia za kidiplomasia kutatua mgogoro huo kuliko hivyo ambavyo wengi wanataka itokee.kwa taarifa sidhani kama jeshi letu lina vifaa bora na vya kisasa vya kivita kama vile vya Gaddaff lakini aliishia kung'olewa madarakani na kile nachoweza kusema genge la wahuni likisaidiwa na mercenary.kumbe msije mkaanza kuidharau Malawi na mbwebwe zisizokuwa na tija kwani nahofia msijeangukia pua kwa umahiri wa jeshi tusiokuwa nao ila tu kwa porojo nyingi za mdomoni tu.Niishie kwa kusema tu kuwa ni heri kuwa mjinga wa kutumia maneno ya busara kwa kutatua migogoro kuliko kuwa mpumbavu wa kutofikiri kwa kutumia nguvu na uhodari usokuwa na tija kwa kupambana na matatizo kwani kuna mafundisho mengi yanayoashiria kuwa mabavu si chochote ktk harakati za kutuliza migogoro mahala popote duniani.Nani kakwambia Iraq,Pakistan,Congo,syria,Afghanistan na kwingineko mabavu yameweza?Na ikumbukwe kwamba kuwa na kichwa kikubwa si sababu tosha ya kumfanya mtu awe na uwezo wa kufikiri kuliko mwingine awaye yeyote.Mfano mzuri tunauona kwa Israeli ni moja ya nchi ndogo kuliko mataifa yamzungukayo ambayo kimsingi yanatamani kuitokomeza lakini uwezo na nguvu kwayo ni kikwazo dhidi ya nchi hiyo ndogo.Vivyo hivyo hata sisi twaweza kutumia vigezo vya kuiona malawi ni nchi ndogo sana na hivyo kudhani ni rahisi kushinda vita hii ya kimasirahi ktk kulinda eneo lake.Ndugu zangu ktk hili hakuna vita ndogo kamwe!!! Napita tu!!
 
Mbona Sitta kama kiongozi wa serikali bungeni aliongea haya haya juzi juzi hapa tena akiwa kama kiongozi wa kwanza wa kitaifa kuongea maneno haya (kabla ya Membe na huyu sasa EL kuongea).. hii imekaa kishabiki shabiki. tuwe makini na huu ushabiki wa kisiasa kwenye mambo yenye maslahi makubwa ya taifa zima.
 
kitalolo,

Wengi wanaoshabikia kauli ya kichochezi ya Lowassa ni wale ambao wamezaliwa katika miongo mitatu hii na ambao hawajui ni kwa kiasi gani vita hugharimu. Hawakumbuki miaka 18 ya kujifunga mikanda, hatimaye ikageuka kuwa miongo 18. Lowassa atafute mtaji mwingine wa kisiasa, hili litamalizwa kwa diplomasia mahiri tuliyonayo.

Chifu nakubaliana kabisa na wewe na kitalolo.

Nashangaa watu wenye uelewa kufurahia kuingia katika vita kipindi ambacho taifa lipo katika dimbwi la umaskini wa kupindukia. Kila nyanja ya huduma za jamii ipo tenge na ovyo;sasa hizo pesa za kupigana zitatoka wapi? Na itakuwa busara kutumia pesa hivyo,wakati raia tunakula vumbi? Kama athari za vita ya Uganda hadi leo zinaonekana kwenye uchumi,hizi zitakazokuja,itakuwaje?

Pili,hapa tunapaswa kutumia busara na utashi katika suala hili. Kama kuna uwezekano wa kuwepo mafuta hapo ziwani,hivi haiwezi ikawa ni chokochoko inayochokolewa na mataifa ya kaskazini? Je,hawatamani kuona tunatoana ngeu na kuchinjana huku wao wakinufaika kwa kutuuzia silaha,kisha watapeana tenda za ukarabati baada ya vita;huku wakijipenyeza taratibu katika kunywa mafuta hayo?

Kwa mtazamo wangu,taifa kwa sasa halina haja ya kufikiria vita;litumie njia zote za kidiplomasia. Linapoanza kujidai na uwezo wa kijeshi,kuna mataifa yasiyo na mapenzi mema na Afrika,tayari yanajiandaa kutoa supoti ya kijeshi kwa upande wa pili,na hapo naamini kila mtu anaelewa nini kitafuatia. Tafadhali tujifunze yaliyotokea Liberia na Sierra Leone na suala la Blood Diamonds.

Siungi mkono hilo tamko,siungi mkono vita.
Naunga mkono njia za mapatano kwa amani.
 
Last edited by a moderator:
Baaada Wa heshimiwa Lowassa na Mbembe kutoa onyo kali kwa Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka, je ni nini msimamo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa SUK kuhusu mgogoro huu? Pili mchango wa Vikosi vya Zanzibar vita vya Kagera.
 
On a serious note, why do we have to start fighting with Malawi? Have we deployed all diplomatic channels and failed?
 
lowassa ni jembe hana uwoga wa kizamani kama naniiii ambae ndio kaka mkuu lakini amekaaa kimya tu nchi inachukuliwa

Rais mwenye utashi na mbobevu wa diplomasia hakurupuki na kutoa alarmist statements ambazo zitaleta taharuki kwa watu wake ambao bado wana kumbukumbu ya vita vya msumbiji na hujuma za makaburu. Kama hao walioko kaskazini hawajui madhara ya vita waende kule kusini au kagera watajua kwamba wimbo wa vita siyo wa kuulilia. Rais makini hakimbilii kutoa tangazo la vita wakti hakuna pre-conditions za vita. Tumwache huyu mpiga porojo aendelee na kuununua umaarufu usiomstahili.
 
Kiongozi makini hawezi ku speculate vita wakati diplomatic means hazijawa exhausted.

Worse still, anaji contradict kwa ku refer to diplomatic options, baada ya kupiga mbiu za vita.

Na wabongo wanamshangilia.

Wengine watasema majadiliano ya kidiplomasia yameshafanyika tangu zamani na hayajazaa matunda.

Lakini maswali kwao ni, majadiliano hayo yalifika katika kiwango kipi? Nini kilikwamisha majadiliano hayo kuzaa matunda? Haya ndiyo baadhi ya maswali ya kujiuliza na kuwa ndiyo msingi wa kuanzia katika kutafuta njia nyingine za kidiplomasia.
 
EL ana-take advantage kwenye mfumo wenye uongozi ulio dhaifu from top to bottom, otherwise tamko lake hakupaswa kulitoa at this stage and minute.

tumeambiwa juzi tu hapa kuwa kulikuwa na delegation kutoka serikali ya malawi iliyohudhuria moja ya vikao vya bunge. jamani, kweli mtu anakuja harmlessly hadi chumbani kwako kukusalimia au kuongea na wewe kistaarabu lakini wewe unatoka huko nje unatangaza vita naye? ni sahihi kweli?

mwalimu nyerere (rip) alitangaza vita na amini, lakini hii ilikuwa ni baada ya kufanya necessary but failed "due diligence" kupitia AU (OAU wakati ule).
tusichanganye mambo na kilichotokea wakati ule. yes, mwalimu alikuwa mbabe.... lakini the old man knew what to do when and where!

Sina hakika kama unajua unachoongea. Udhaifu wa uongozi ni kutoa tamko la onyo pale bungezi na kusisitiza kwamba njia za kidiplomasia zitumike kumaliza tatizo? Serikali haiwezi kujishughulisha na mtu aliyeonyesha udahifu wa hali ya juu wa kutojua mipaka ya madaraka na kukurupuka kutoa broadsides zisizo na tija. Watanzania wenye akili sasa wameshajua tunayemzungumzia ana utashi wa namna gani na malengo hake ni yapi. Tunamsubiri aende Diamond Jubilee akatoe amri kwa majeshi yetu kuanza harakati za kivita halafu tuone kama hata kuna sisimizi atakayemtii. Tunapojadili hoja hii tukumbuke kwamba mtoa hoja ni msanii mbobevu kwa vitendo na taaluma. Hapa anaigiza mwenzenu!
 
Ataenda kupigana yeye na wanae...sisi tuko huku pori tunawaangalia tu!!!

Najua wengine mtasema sina uzalendo/sina uchungu na mengi mengineyo...but swali litabaki, ni nani atakeyefadika na vita??!!!

Je, ni mimi na wewe tunaohangaika na keybord kutoa mawazo yetu juu ya jambo ambalo hatima yake halitokuwa na faida yoyote yenye kuonekana si kwako wala kwangu wala kwa vitegemezi vyangu na vyako???.

.....give me a break...we need peace not war...mapema 1980s baada ya kumng'oa nduli, tuliambiwa kufunga mikanda kwa 18 months kabla hali haijarudi na kuwa nzuri...hesabu ni miaka mingapi sasa??? hali imezidi kudorora kutoka nafuu kuwa mbaya zaidi.

By the way...Edo, wanae na wadokozi wenzie, watafaidika b'se pengine kutatakiwa na manunuzi ya silaha ili kuingia vitani kikamilifu...bila shaka yeye kwa nafasi yake, atashiriki kwenye mchakato wa manunuzi na kama ilivyokuwa kwa Richmond...atatengeneza faranga za kutosha na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kupata kula come 2015 kupitia chama cha magamba.

Ujumbe wangu ni kuwa...we need peace not war....magamba wafanye wawezavyo kuepuka vita.
 
Na Wakala wa BAE yuko kwenye kundi hilo hilo na atawaunganisha kwenye mchakato wa silaha za kupigania.
 
Kabla ya Watanzania kuingia vita juu ya Rasilimali ya Ziwa Nyasa hatuna budi kujiuliza rasilimali ziliopo nchini tumefaidika nazo vipi. Say "NO TO WAR DOWN WITH MAFISADi"
 
hayo ni maoni yako.kama ingekua hivyo wasingeenda kulinda amani nchi za watu.
na kama wangeenda basi wangeharibu nchi ikapata aibu..
NB. japo mie si afande,wakianzisha na-join..navyopenda hizo move!!
nataka kitu 'live',lowasa lianzishe..dhaifu hawezi

nimeipenda hiyo NB yako. ha ha haaaa!!! duh!unanikumbusha enzi zile za kuchonganisha wenzio wapigane halafu wewe unakaa pembeni kufaidi kutazama watu wanavyovurumishiana masumbwi.
 
Back
Top Bottom