masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Nimeikuta hii makala mahali, nikajisemea, wanafiki wote hata geti la mbinguni hawataliona, Makonda akiwemo.
Paulo Makonda akiwa Mkuu wa Mkoa DSM, alimtafuta mwanamke anaitwa Fatma Chikawe, akampa jina la ‘Fatma Lowassa’. Edward Lowassa alikuwa mjumbe wa kamati kuu CHADEMA.
Paulo Makonda akamuita mwanamke huyo katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mbele ya waandishi wa habari, akijitambulisha kama mtoto wa kike aliyetelekezwa na Edward Lowassa.
Edward Lowassa akagoma kupimwa DNA akisema hamtambui mwanamke huyo na anatumika kumchafua kisiasa. Edward Lowassa alisema hayo alipohojiwa na gazeti la NIPASHE 2018.
April 10, 2018, Fatma Chikawe alikuwa kati ya waliojitokeza ofisi ya Mkuu wa Mkoa - DSM kutafuta msaada wa kisheria akidai Edward Lowassa ni baba yake mzazi na hajawahi kumuona tangu kuzaliwa.
April 14, 2018, Paulo Makonda akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alisema anayo majina zaidi ya 100 ya viongozi wa serikali wakiwepo wastaafu, viongozi wa dini, na wabunge ambao walitajwa.
April 15, 2018, ikaonekana video nyingine katika mitandao ya kijamii, Fatma Chikawe akiomba radhi kwa kumdhalilisha Edward Lowassa akisema tukio hilo limechukuliwa kisiasa na anakosa amani.
Fatma Chikawe katika video hiyo iliyosambaa alinukuliwa alisema aliwahi kukutana na Fred Lowassa (mtoto mkubwa wa Edward Lowassa) na akamuahidi kumsaidia lakini amekuwa kimya.
Mtoto mkubwa wa Edward Lowassa, Fred Lowassa, alishangaa mwanamke huyo aliyejitokeza na kudai kuwa ni binti wa mwanasiasa huyo mkongwe aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
Fred Lowassa akamjibu huyo mwanamke, Fatma Chikawe, “Kwa taarifa tu sisi watu wa Monduli kwetu watoto ni baraka na neema, nimeshangaa ametukosa ukoo mzima kujitambulisha.”.
“Namwambia Paul Makonda, nimetoka naye mbali sana, nasikitika sana anavyotumia nafasi yake vibaya kwa manufaa anayoyajua. Paulo Makonda nimekulea.” Alisema Fred Lowassa
Leo Paulo Makonda nyumbani kwa Edward Lowassa, Masaki, Dar es Salaam, anasema kuna watu walimchafua Edward Lowassa na leo wanampongeza na kumsifia Lowassa. Bashite ni TAPELI wa kisiasa.
🤣🤣🤣🤣
Paulo Makonda akiwa Mkuu wa Mkoa DSM, alimtafuta mwanamke anaitwa Fatma Chikawe, akampa jina la ‘Fatma Lowassa’. Edward Lowassa alikuwa mjumbe wa kamati kuu CHADEMA.
Paulo Makonda akamuita mwanamke huyo katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mbele ya waandishi wa habari, akijitambulisha kama mtoto wa kike aliyetelekezwa na Edward Lowassa.
Edward Lowassa akagoma kupimwa DNA akisema hamtambui mwanamke huyo na anatumika kumchafua kisiasa. Edward Lowassa alisema hayo alipohojiwa na gazeti la NIPASHE 2018.
April 10, 2018, Fatma Chikawe alikuwa kati ya waliojitokeza ofisi ya Mkuu wa Mkoa - DSM kutafuta msaada wa kisheria akidai Edward Lowassa ni baba yake mzazi na hajawahi kumuona tangu kuzaliwa.
April 14, 2018, Paulo Makonda akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alisema anayo majina zaidi ya 100 ya viongozi wa serikali wakiwepo wastaafu, viongozi wa dini, na wabunge ambao walitajwa.
April 15, 2018, ikaonekana video nyingine katika mitandao ya kijamii, Fatma Chikawe akiomba radhi kwa kumdhalilisha Edward Lowassa akisema tukio hilo limechukuliwa kisiasa na anakosa amani.
Fatma Chikawe katika video hiyo iliyosambaa alinukuliwa alisema aliwahi kukutana na Fred Lowassa (mtoto mkubwa wa Edward Lowassa) na akamuahidi kumsaidia lakini amekuwa kimya.
Mtoto mkubwa wa Edward Lowassa, Fred Lowassa, alishangaa mwanamke huyo aliyejitokeza na kudai kuwa ni binti wa mwanasiasa huyo mkongwe aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
Fred Lowassa akamjibu huyo mwanamke, Fatma Chikawe, “Kwa taarifa tu sisi watu wa Monduli kwetu watoto ni baraka na neema, nimeshangaa ametukosa ukoo mzima kujitambulisha.”.
“Namwambia Paul Makonda, nimetoka naye mbali sana, nasikitika sana anavyotumia nafasi yake vibaya kwa manufaa anayoyajua. Paulo Makonda nimekulea.” Alisema Fred Lowassa
Leo Paulo Makonda nyumbani kwa Edward Lowassa, Masaki, Dar es Salaam, anasema kuna watu walimchafua Edward Lowassa na leo wanampongeza na kumsifia Lowassa. Bashite ni TAPELI wa kisiasa.
🤣🤣🤣🤣