Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,255
- 113,669
Wow! maelezo mazuri sana NN sikujua kama unajua kiswahili hivi....ok baada ya haya how can you tell someone loves you?
Nilizaliwa Darisalama hospitali ya Ocean Road saa mbili za usiku,siku, tarehe, na mwaka kapuni. Kwa hiyo Kiswahili ni lugha yangu ya kwanza. Ni lugha mama kwangu. Na ni lugha ya asili. Siwezi kutokukijua Kiswahili ingawa sikijui chote.
Kwa raghba na uchu nilionao, nitaendelea kujifunza na kuhimiza wengine wajifunze na wakitumie zaidi katika mawasiliano yao na wenzao. Bila hivyo kina hatari ya kumezwa na hatimaye kufifia kama siyo kutoweka kabisa vinywani mwa waja kwa sababu ya huu mseto uitwao "Kiswanglish".
Kwa hiyo natoa wito kwako na kwa wengine kukitumia kila iwezekanapo bila kuchanganya na hiyo lugha ingine tuliyorithishwa na mkoloni.
Wakatabahu,
Jemedari wa Majemedari Nyani mwana wa Ngabu