Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Kwema Wakuu!
Vijana wa siku hizi wamechanganyikiwa mno. Hata vitu vidogovidogo kama maana ya maneno au dhana hawajui. Mathalani, Neno "Ndoa".
Kuishi na mwanamke au mwanaume kiunyumba kwa lengo la kuunda familia ndio tafsiri sahihi ya Ndoa. Ndoa ni makubaliano ya mwanaume na mwanamke kuishi pamoja katika kuunda familia. Hiyo ni ndoa. Nature inatambua hivyo.
Ndoa haihitaji ruhusa ya Wazazi, sijui taasisi ya dini gani huko, sijui serikali. Yaani serikali inaweza isiwepo lakini ndoa ikawepo, wazazi wanaweza wasiwepo lakini ndoa ikawepo, taasisi za dini zinaweza zisiwepo lakini Ndoa ikawepo. Hiyo tosha inatakiwa ikuonyeshe kuwa Maamuzi na makubaliano ya wawili(me na ke) ndio independent Factor. Hizo zingine ni dependent Factors.
Wengi hufikiri kuwa Ndoa ni kuchukua mwenza kumpeleka kwa wazazi, sijui kutoa mahari, sijui kwenda msikitini sijui Kanisani au serikalini ati huko ndio kufunga Ndoa. Jambo ambalo sio sahihi.
Wewe ukishaishi na Mwanamke au mwanaume pamoja, kwa lengo la kushiriki kuunda familia na kampani katika maisha hiyo tayari ni NDOA.
Haupo kwenye kundi la watu wanaokataa Ndoa.
Sheria za ndoa, mila na taratibu za kiutamaduni zilizowekwa kwenye ndoa zipo kwaajili ya kuzuia Uonevu, dhulma na uminywaji wa haki miongoni mwa wanandoa ambao tayari wamekwisha kuoana hata bila kuhusisha wazazi, taasisi za Dini, na serikali.
Wazazi, Taasisi za dini na serikali hazina haki ya kuingilia mambo ya familia yako isipokuwa tuu ikiwa kuna uhalifu, dhulma inafanyika.
Kisiasa na kiutawala Ndoa ni smallest Unit ya Mamlaka na Utawala. Ni kama Seli ya mwili kwa kiumbe hai.
Kuipinga Ndoa kwa viumbe wenye utashi haitawezekana kwa sababu itatafsiriwa kama Kupinga Mamlaka za kisiasa za juu kama Serikali.
Huwezi ongoza taifa ambalo robo tatu ya Watu ni wakataa Ndoa. Hiyo haiwezekaniki. Ni kama kuongoza taifa la mashetani ambalo mara kwa mara mapinduzi, tamaa mbaya, uchafu utakuwa ndio mila na desturi.
Ndoa ni familia, familia ndio msingi mkuu wa taifa na Dunia.
Wapinga ndoa wanahaki ikiwa watakuwa ni éxceptional na wachache. Lakini kupiga kampeni Watu wakatae Ndoa ni sawa na kupiga kampeni Duniani kusiwe na serikali yaani Watu waishi vyovyote watakavyo. Yaani Tanzania serikali ifutwe, Kenya na Dunia nzima kusiwe na serikali. Unafikiri nini kitatokea?
Moja ya mambo yanayowatofautisha binadamu na wanyama wengine ni pamoja na Ndoa.
Kama mwanadamu akipinga ndoa atazidi kufanana na wanyama wengine kama Mbwa, Paka, na wanyama wengine wasio na mfumo wa kifamilia. Na hii itafanya mwanadamu asitawalike na tabia zingine chafu na mbaya zitazidi kuibuka.
Unazaa watoto kama Mbwa alafu hujui wanaishije, wanalelewaje, lakini ndani ya ndoa lazima ujue wanaishije na wanalelewaje kwa sababu nawe utakuwa mhusika wa kujenga kizazi chako.
Kutuma pesa sio Malezi. Huwezi sema umemlea mtoto kisa ulikuwa unatuma pesa. Malezi yanahusu ushiriki wa moja kwa moja kwa mzazi kwa mtoto wake.
Mtoto akikaa kwa Bibi au kwa Mamaake au kwa Babaake alafu wewe ukawa unatuma pesa za matumizi. Haiwezi kutajwa kuwa Mtoto huyo Ulimlea.
Kuishi na mtoto ndio kumlea mtoto na hakuna tafsiri zaidi ya hiyo.
Kutuma matumizi ya mtoto haiwezi kutafsiriwa kama kufanya malezi.
Vijana, kampeni ya Kukataa ndoa haiwezi kuwa kwa mtu mwenye utimamu wa Akili. Ni aidha kuna athari za kisaikolojia au Historia mbaya kwa mtu husika.
Utapeli kwenye mapenzi upo.
Ubinafsi kwenye mapenzi na ndoa upo.
Unyanyasaji na ukatili kwenye ndoa unaweza kuwepo.
Lakini nani mwenye wajibu wa kupambana kukabiliana na mambo hayo kama sio wewe?
Jukumu lako kama mwanaume au mwanamke ni kusimamisha serikali yako(familia yako). Jukumu lako kama mwanadamu ni kutawala. Utawala unaanzia kwenye kizazi chako kisha mazingira na jamii.
Yaani upo serikalini ati unakataa serikali kisa ati kuna Waasi, sijui magaidi, sijui Watu wanaotaka kukupindua, sijui wala rushwa na wanaokuhujumu. Wewe utakuwa na akili kweli.
Kama mtawala(mfano wa Mungu) ni jukumu lako kupambana na kuhakikisha kizazi chako kinakuwa bora na kizazi bora hutoka kwenye familia BORA (mke na mume) na sio nje ya hapo.
Muhimu, unapaswa uwe makini katika kuchagua mwenza wa maisha ambaye utaenda kuanzisha nayè familia(serikali yenu).
Dhamiri ya kile kinachokufanya uchague mke au mume na vigezo ulivyoviweka ndio vitaamua serikali yako(familià yako) itakavyokuwa.
Ndoa na mapenzi sio Pesa. Hilo liweke Akili kabisa. Ukishaingiza mtazamo kuwa ndoa au mahusiano ni pesa jua kabisa wewe ni Tapeli na mbinafsi kabla hata ya huyo mwenza unayemtafuta.
Kwenye utawala au mamlaka pesa hutafutwa. Lakini uaminifu, upendo, haki uadilifu, umoja, kujitoa ndio misingi ya Utawala ikiwemo familia.
Acha Nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Vijana wa siku hizi wamechanganyikiwa mno. Hata vitu vidogovidogo kama maana ya maneno au dhana hawajui. Mathalani, Neno "Ndoa".
Kuishi na mwanamke au mwanaume kiunyumba kwa lengo la kuunda familia ndio tafsiri sahihi ya Ndoa. Ndoa ni makubaliano ya mwanaume na mwanamke kuishi pamoja katika kuunda familia. Hiyo ni ndoa. Nature inatambua hivyo.
Ndoa haihitaji ruhusa ya Wazazi, sijui taasisi ya dini gani huko, sijui serikali. Yaani serikali inaweza isiwepo lakini ndoa ikawepo, wazazi wanaweza wasiwepo lakini ndoa ikawepo, taasisi za dini zinaweza zisiwepo lakini Ndoa ikawepo. Hiyo tosha inatakiwa ikuonyeshe kuwa Maamuzi na makubaliano ya wawili(me na ke) ndio independent Factor. Hizo zingine ni dependent Factors.
Wengi hufikiri kuwa Ndoa ni kuchukua mwenza kumpeleka kwa wazazi, sijui kutoa mahari, sijui kwenda msikitini sijui Kanisani au serikalini ati huko ndio kufunga Ndoa. Jambo ambalo sio sahihi.
Wewe ukishaishi na Mwanamke au mwanaume pamoja, kwa lengo la kushiriki kuunda familia na kampani katika maisha hiyo tayari ni NDOA.
Haupo kwenye kundi la watu wanaokataa Ndoa.
Sheria za ndoa, mila na taratibu za kiutamaduni zilizowekwa kwenye ndoa zipo kwaajili ya kuzuia Uonevu, dhulma na uminywaji wa haki miongoni mwa wanandoa ambao tayari wamekwisha kuoana hata bila kuhusisha wazazi, taasisi za Dini, na serikali.
Wazazi, Taasisi za dini na serikali hazina haki ya kuingilia mambo ya familia yako isipokuwa tuu ikiwa kuna uhalifu, dhulma inafanyika.
Kisiasa na kiutawala Ndoa ni smallest Unit ya Mamlaka na Utawala. Ni kama Seli ya mwili kwa kiumbe hai.
Kuipinga Ndoa kwa viumbe wenye utashi haitawezekana kwa sababu itatafsiriwa kama Kupinga Mamlaka za kisiasa za juu kama Serikali.
Huwezi ongoza taifa ambalo robo tatu ya Watu ni wakataa Ndoa. Hiyo haiwezekaniki. Ni kama kuongoza taifa la mashetani ambalo mara kwa mara mapinduzi, tamaa mbaya, uchafu utakuwa ndio mila na desturi.
Ndoa ni familia, familia ndio msingi mkuu wa taifa na Dunia.
Wapinga ndoa wanahaki ikiwa watakuwa ni éxceptional na wachache. Lakini kupiga kampeni Watu wakatae Ndoa ni sawa na kupiga kampeni Duniani kusiwe na serikali yaani Watu waishi vyovyote watakavyo. Yaani Tanzania serikali ifutwe, Kenya na Dunia nzima kusiwe na serikali. Unafikiri nini kitatokea?
Moja ya mambo yanayowatofautisha binadamu na wanyama wengine ni pamoja na Ndoa.
Kama mwanadamu akipinga ndoa atazidi kufanana na wanyama wengine kama Mbwa, Paka, na wanyama wengine wasio na mfumo wa kifamilia. Na hii itafanya mwanadamu asitawalike na tabia zingine chafu na mbaya zitazidi kuibuka.
Unazaa watoto kama Mbwa alafu hujui wanaishije, wanalelewaje, lakini ndani ya ndoa lazima ujue wanaishije na wanalelewaje kwa sababu nawe utakuwa mhusika wa kujenga kizazi chako.
Kutuma pesa sio Malezi. Huwezi sema umemlea mtoto kisa ulikuwa unatuma pesa. Malezi yanahusu ushiriki wa moja kwa moja kwa mzazi kwa mtoto wake.
Mtoto akikaa kwa Bibi au kwa Mamaake au kwa Babaake alafu wewe ukawa unatuma pesa za matumizi. Haiwezi kutajwa kuwa Mtoto huyo Ulimlea.
Kuishi na mtoto ndio kumlea mtoto na hakuna tafsiri zaidi ya hiyo.
Kutuma matumizi ya mtoto haiwezi kutafsiriwa kama kufanya malezi.
Vijana, kampeni ya Kukataa ndoa haiwezi kuwa kwa mtu mwenye utimamu wa Akili. Ni aidha kuna athari za kisaikolojia au Historia mbaya kwa mtu husika.
Utapeli kwenye mapenzi upo.
Ubinafsi kwenye mapenzi na ndoa upo.
Unyanyasaji na ukatili kwenye ndoa unaweza kuwepo.
Lakini nani mwenye wajibu wa kupambana kukabiliana na mambo hayo kama sio wewe?
Jukumu lako kama mwanaume au mwanamke ni kusimamisha serikali yako(familia yako). Jukumu lako kama mwanadamu ni kutawala. Utawala unaanzia kwenye kizazi chako kisha mazingira na jamii.
Yaani upo serikalini ati unakataa serikali kisa ati kuna Waasi, sijui magaidi, sijui Watu wanaotaka kukupindua, sijui wala rushwa na wanaokuhujumu. Wewe utakuwa na akili kweli.
Kama mtawala(mfano wa Mungu) ni jukumu lako kupambana na kuhakikisha kizazi chako kinakuwa bora na kizazi bora hutoka kwenye familia BORA (mke na mume) na sio nje ya hapo.
Muhimu, unapaswa uwe makini katika kuchagua mwenza wa maisha ambaye utaenda kuanzisha nayè familia(serikali yenu).
Dhamiri ya kile kinachokufanya uchague mke au mume na vigezo ulivyoviweka ndio vitaamua serikali yako(familià yako) itakavyokuwa.
Ndoa na mapenzi sio Pesa. Hilo liweke Akili kabisa. Ukishaingiza mtazamo kuwa ndoa au mahusiano ni pesa jua kabisa wewe ni Tapeli na mbinafsi kabla hata ya huyo mwenza unayemtafuta.
Kwenye utawala au mamlaka pesa hutafutwa. Lakini uaminifu, upendo, haki uadilifu, umoja, kujitoa ndio misingi ya Utawala ikiwemo familia.
Acha Nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam