Elections 2010 Kyela elections!

Status
Not open for further replies.

Katabazi

JF-Expert Member
Feb 18, 2007
353
19
Wana JF,
Nilibahatika kushuhudia uchaguzi wa Kyela.
Nilichogundua
1.Hata uwe na pesa kiasi gani-huwezi kuwaridhisha wana Kyela, jamaa wanapenda pesa kuliko wachaga, wanavuta kwa kila mtaka kura, siku ya mwisho hawakulala mpaka kunakucha.
2.Nilipowauliza kwanini wanampendelea yupi:
1-Dr. wanampenda tuuuuu kwa sababu pamoja na kuwa hakuleta cha maana lakini aliiweka Kyela kwenye ramani ya TZ na kikubwa wana amini alileta daraja 1. hivyo ana kila haki ya kurudi. Na yeye anasema ana uzoefu kwa hiyo wengine wasipewe.Pamoja na mengine alikuja na wapambe wa nguvu na anasema anaomba ridhaa ya wananchi kusudi aanze kazi ya kuwahudumia.
2. George Mwakalinga-huyu wanaamini pamoja na kushiriki kimaendeleo kuwaletea radio ya jamii-Kyela FM,kujenga ghorofa na kuchangia miradi mingi ya maendeleo-mashuleni etc,wanasema wanampenda lakini asubiri mpaka siku Dr. akichoka ndio watampa

3.Palikuwa na dada mmoja anaitwa Rhoda-huyu alinifurahisha kwa ushujaa wake akitegema angepewa kura kwa sababu ni dada.lakini inaelekea wanyakyusa hawathamini kina dada wala kule, gender haipo-alizunguka kila sehemu peke yake na hakutoa rushwa sana lakini aliambuliwa % ndogo sana
4.Palikuwa na m sure mmoja anaitwa Elias-huyu alikuja na gari za nguvu kama za ma waziri, pesa(anazo) na alizimwaga sana lakini kama wenzake yeye alituhumiwa kuwa anajua sana mapenzi ingawa niliona kama ni mfanya biashara mkubwa,matokeo akavuta sana kura kijijini kwao tu.
Maajabu niliyoona
a)inadaiwa kuna kundi linaitwa Task Force , wanadai hili ni la Mbunge aliyepo-lilikuwa zaidi ya sungu sungu, likilinda wengine wasiende kwenye maeneo fulani kuhonga au kuleta fujo sehemu ambazo walikuwa hawana uhakika kama mbunge wao angepita.

b)Inadaiwa pia kuwa Mbunge aliyepo na watu wake ndio walileta kadi feki ambazo wagombea wengine walizibaini na ikaleta mtafaruku lakini baadae ikasemekana zitumike,kwa hiyo sehemu zingine zilizutumika na sehemu zingine hazikutumika.
c)Takukuru walifanya kazi chini ya viwango-wakizifuatilia gari za wagombea tu na kuzi sachi wakitafuta rushwa za pesa au vitenge nk.
d)Inasemekana sasa watu hawagombei nafasi ya kwanza kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa mbunge aliyepo akafutwa, kwa hiyo sasa ni hongo kusudi mtu apate nafasi ya 2 kusudi lolote likitokea basi aangukiwe yeye.
e)La kusikitishisha kama ni kweli-nafasi za udiwani nyingi zimechukuliwa na watu ambao sio tu kuwa hawana elimu lakini hawana pia uwezo wa kuiletea Kyela maendeleo.
f)Vyama vingine kwa Kyela ni kama havipo,hivyo nguvu ya nani awe mbunge inategemea NEC ya CCM
h)La mwisho inasemekana ni jambo ambalo si la siri kuwa Mh.mbunge na RC na viongozi wengi hawaelewani, nikajiuliza kwa hali hii patakuwa na maendeleo Kyela?
Na nilipowaangalia wagombea wote ni kama wana nguvu(Kipesa) hawa wote kama waliyokuwa wakijinadi nayo wangechangia mawazo na pesa wakazimwaga kwa pamoja -loooh Kyela ingekuwa mbali, lakini naona pale kila atakayeondoka ndio itakuwa mwisho(Kwa maoni yangu)
Mengi tuliyoyatategemea kuwa kutakuwa na pesa za nguvu kutoka kwa mafisadi hazikuonekana na kiujumla amani ilikuwepo.
 
Hon Katabazi

You can put as much lipstick on a pig as you like, but it still Mwakyembe knows how to deal with Fisadis. Welcome back, again.
 
Mkuu,

Nashukuru kwa hii habari ambayo imejaa mengi ambayo nimekuwa nikiandika leo hii. Wengine walisema nina majungu ila wewe umeiweka vizuri sana na kuwa NEUTRAL.

Hao Task Force nimewasikia habari zao. Wametembeza UBABE wa waziwazi na kibaya ni kuwa vyombo vya DOLA viliwaangalia tu wakitesa na utemi wao. Nashindwa kuamini kama kweli Kyela wamechagua au mtu kawachagulia.

Maadamu wao wenyewe wanakiri kuwa Mwakalinga kawaletea vitu vingi vya maendeleo na Mwakyembe hakuleta ila tu kasaidia Kuwafanya kuwa MAARUFU Tanzania, basi nawarudisha kwenye wimbo wa Marehemu Maneti na Mwalimu wangu Msasa pale Mazengo alishawahi kuutumia katika mfano kama huu akisema "....... Najuta umaarufu umeniponza............ amejenga nyumba kwao, mimi kwangu midabwada".

Mkataa pema................. Kila la kheri wana Kyela na umaarufu wenu.

Mwakalinga nilikuambia hamia Sikonge, ukakataa. Watani zako tungeliheshimu kazi yako.

Mwanamtama, naona hii ya Lipstick umeipenda sana tangu nikushushie juzi, heheheeee :)
 
Pig will remains pig bro! Do I need to say more....... hata kura buku moja imekuwa ngumu! Shame
 
Ila si wamemchagua wampendae?? sasa kama Mwakalinga alishafanya maendeleo kyela sasa wa nini kuwa Mbunge bora mwakyembe sasa ndio afanye mambo huyo Mwakalinga mwache apumzike maana angeleta jeuri kuwa ametusaidia sana kwaiyo anarudisha hela yake tungekwisha
 
Mh. Mwanamtama, unalolisema si uongo. Niliwauliza wapambe wa Mwakyembe na wapinzani wake, la ajabu wengine hata ufisadi hawajui-ahaaaahaaaaaaa. Lakini wasomi wengi -they wish angekata 50% ya nguvu za kupinga uifisadi akawasaidia waliomchagua au angekuwa kwenye uhusiano mzuri na watoa vyeo akapewa cheo kama Mh. Makamba akarudi bungeni na kumaliza kazi ya kupigana na mafisadi (kama alivyo specialise)na kazi ya kuwahudumia wanachi wa Kyela akawaachia wasio na nguvu za kupambana na mafisadi.
Doooh nilisahau jamaa wanakula gongo kuleeeee si mchezo na police haiwezi kuwafuata,kuna sehemu unakwenda mpaka 75 Km or more. Sijui kama wilaya zingine TZ zilipata bahati kama ya Kyela RC,DC,RPC,FFU,waandishi original na kama sisi,researchers,wapelelezi original na walioletwa na baadhi ya wagombea etc wote walikuwa Kyela.
BTHW kwa mahesabu yangu ya karibu ili uwe Mbunge unahitaji sio chini ya 150M-sijui watu wanapataga nini huko na kama sio fisadi kama ndio kuosha au kusafisha itabidi uzidishe nguvu,maana jamaa wanasema mkono mupu haulambwi.
 
heh he he he... lipustiki katika pigi...lol
Mbona muanzilishi wa hii mada pointi zake ni zile zile za watu wa ile kambi ya kifisadi, ambazo tumekuwa tukizisikia kila siku?
Eti hakuna alilofanya zaidi ya daraja, na hakukuwa na fweza za ufisadi !! Tushazoea, wakati ule si mlisema mlikuwa mbugani kuangalia mafisi wakati rada ziliwaona kule kwa EL ??

Tuliwaambia hamkusikia, fweza za ufisadi ni za wizi na zina nuksi ! Kula wamezila, na kura hawakumpa huyo pandikizi.

Unafikiri wana kyela ni wajinga kiasi hicho, wafe njaa lakini wampe kura eti kwa sababu tu Prof. alileta umaarufu Kyela..... WTF !!
 
Mwakalinga oyeeeeeee.....
Hii ndiyo Kyela yetu.
Unaleta siasa za ughaibuni huku.
Sokapo apa gwa setano ugwe seee.
 
Mwakalinga hakufanya hayo ili agombee. Miradi yake tayari inarudisha hela. Li mradi la HASARA ambalo kafanya hadi leo ni Kyela FM. Anaombea tu liwe linajiendesha lenyewe na kwenye uongozi kajitoa kabisa. Imebaki chini ya watu wengine na Halmashauri ya Wilaya ya Kyela. Ila iko hoi kifedha hata sehemu za majengo haina na kaamua tu kuendelea kuikumbatia kwa kuiweka hapo kwake kwenye KBS.

Kama ulifikiri alitegemea hela yake kurudi, basi utaumia sana kuona jamaa ndiyo kwanza ataongeza miradi na huenda asigombee tena ili wenye WIVU mjinyonge. Muishi salama na mbunge wenu maarufu....... :)

Wee wa Lipstic wewe baki tu nazo. Naona tangu usikie hilo neno, umelipenda sana loohh :)
Siyo siri utabaki kuwa nguruwe hata ukipata watu wanaotaka kukusaidia kwa dhati. Wewe unataka kuwa maarufu. Maendeleo SUCK.
 
The truth is that guy (Mwakyembe) is a Hero....a true Solder for his people and all Tanzanians at large...in fact he doesn't deserve to be in those thieves party.....he has CHADEMA blood flowing in his veins....one day he will realize the truth and turn back his mind, mission n vision to CHADEMA.....All the best Mwakyembe and keep speaking for us....
 
Kata Bazi

Wananchi si wajinga siku zinavyokwenda elimu ya uraia inaongezeka! WanaKyela wamefanya uchaguzi sahihi...unajua huwa nashangaa mnaposema mbunge alete maendeleo kwa kusaidia wananchi waliomchagua! Leta mwongozo hapo. Nadhani kazi kubwa ya Mbunge ni kuwawakilisha wapiga kura bungeni. Kusema Mbunge hajajenga bara bara na madaraja huo ni uvivu wa kufikiri, lazima Mbunge na ashirikiane na serikali kuweka kwenye budget na kuingiza kwenye mipango ya Maendeleo.

Mwafrika alikuwa akiuliza wale jamaa wa George, wana sera gani jimboni, Kipi Harrison hakukifanya? badala yake walikuwa wakija na matusi na kejeli. JF si wapiga kura ila wanatoa mtazamo kwa sauti kubwa, majidai na majigambo yao yamemkosesha hata kura 1000! Wananchi watamkumbuka daima Mwakyembe kushughulikia Richmond. Mtu anaulizwa sera anasema kuna radio Kyela na amewekeza Billions lol, wanakyela wanajua nguvu alizowekeza Lowassa kutoa Mwakyembe, kupitia kwa Geroge...wamekunywa na kula kwao na na kura kwa Harrison.

Lesson learned!
 
heh he he he... lipustiki katika pigi...lol
Mbona muanzilishi wa hii mada pointi zake ni zile zile za watu wa ile kambi ya kifisadi, ambazo tumekuwa tukizisikia kila siku?
Eti hakuna alilofanya zaidi ya daraja, na hakukuwa na fweza za ufisadi !! Tushazoea, wakati ule si mlisema mlikuwa mbugani kuangalia mafisi wakati rada ziliwaona kule kwa EL ??

Tuliwaambia hamkusikia, fweza za ufisadi ni za wizi na zina nuksi ! Kula wamezila, na kura hawakumpa huyo pandikizi.

Unafikiri wana kyela ni wajinga kiasi hicho, wafe njaa lakini wampe kura eti kwa sababu tu Prof. alileta umaarufu Kyela..... WTF !!

Mwanzilishi wa mada ni kambi ya Mwakalinga ... anajaribu kujifariji na kutoa part(ing) gifts AKA matusi kwa Mwakyembe ... talk about sore losers
 
Daaa, Mwakalinga anapendwa hapa JF kama SUKARI hivi.

Watu wakiona tu Kyela na Mwakalinga basi haoooooooo..................

Wakiona Mwakyembe tu basi utakuta litopic limeboa............

Lazima mkiri kuwa Mwakalinga anapendwa sana hata hapa JF ila kutokana na ushabiki na UNGURUWE, hata akiwekwa kugombea na Makamba, basi watu wa Kyela mtamchagua Makamba ili awaletee umaarufu maana yeye ni katibu wa CCM Taifa.

Tunahitaji watu wenye mwamko kama wa Kyela kwa Tanzania nzima. Kumbe Wakyela ni kama Wazambia vile. Gari zuri, tai nzuri, nguo nzuri ila hata nyumba hana na anaishi kwenye gari lake. WTF.
 
heh he he he... lipustiki katika pigi...lol
Mbona muanzilishi wa hii mada pointi zake ni zile zile za watu wa ile kambi ya kifisadi, ambazo tumekuwa tukizisikia kila siku?Eti hakuna alilofanya zaidi ya daraja, na hakukuwa na fweza za ufisadi !! Tushazoea, wakati ule si mlisema mlikuwa mbugani kuangalia mafisi wakati rada ziliwaona kule kwa EL ??

Tuliwaambia hamkusikia, fweza za ufisadi ni za wizi na zina nuksi ! Kula wamezila, na kura hawakumpa huyo pandikizi.

Unafikiri wana kyela ni wajinga kiasi hicho, wafe njaa lakini wampe kura eti kwa sababu tu Prof. alileta umaarufu Kyela..... WTF !!

Say it again.....and Again Loud
 
Ninachojua mimi ni kuwa mwakilishi wa wananchi kazi yake ni kuwawakilisha na kufikisha matatizo yao bungeni ili yafanyiwe kazi,suala la kujenga au kuleta kitu binafsi si hoja ya mtu kuchaguliwa kuwa mwakilishi hivyo wananchi wa Kyela wameona kinachowafaa kwao kwa sasa ni Mwakyembe.Mwakalinga pole na sasa ni wakati wa kuendeleza yale maendeleo unayosifiwa kwani si lazima mleta maendeleo aende bungeni,kama umaarufu nawe unao sana hapo Kyela.
 
mkuu,

nashukuru kwa hii habari ambayo imejaa mengi ambayo nimekuwa nikiandika leo hii. Wengine walisema nina majungu ila wewe umeiweka vizuri sana na kuwa neutral.

Hao task force nimewasikia habari zao. Wametembeza ubabe wa waziwazi na kibaya ni kuwa vyombo vya dola viliwaangalia tu wakitesa na utemi wao. Nashindwa kuamini kama kweli kyela wamechagua au mtu kawachagulia.

Maadamu wao wenyewe wanakiri kuwa mwakalinga kawaletea vitu vingi vya maendeleo na mwakyembe hakuleta ila tu kasaidia kuwafanya kuwa maarufu tanzania, basi nawarudisha kwenye wimbo wa marehemu maneti na mwalimu wangu msasa pale mazengo alishawahi kuutumia katika mfano kama huu akisema "....... Najuta umaarufu umeniponza............ Amejenga nyumba kwao, mimi kwangu midabwada".

Mkataa pema................. Kila la kheri wana kyela na umaarufu wenu.

Mwakalinga nilikuambia hamia sikonge, ukakataa. Watani zako tungeliheshimu kazi yako.

Mwanamtama, naona hii ya lipstick umeipenda sana tangu nikushushie juzi, heheheeee :)
kwani hiyo task force ndio ilikuwa inapiga kura za maoni?naomba mtueleze
 
Watu wa Kyela wana tabia za masikini jeuri. Labda kama wamebadilika, kwa kawaida hawastushwi na vitu ambavyo wanadhania ni vya kupita hata kama ni vizuri namna gani. Siko upande wa Mwakyembe wala Mwakalinga, ila ninawajua wana Kyela, you have to be from there to understtand their decision making mechanism, otherwise it may not make sense to you.
 
Nyie watu wa Kyela mnataka kufanya sisi wengine hatuna majimbo wala wabunge? Kila kukicha Kyela tu kwa lipi hasa? Kwanza mmetuyeyusha kwa ubishi humu na matokeo tumeyaona. Tafuteni kitu badala inayovuta macho na masikio sasa siyo kila kukicha Kyela tu. Kyela yenyewe ni chovu mno kimaendeleo ukilinganisha na Wilaya zote za Mbeya na huu ni muda muafaka wa kuwashawishi wakina Mwakalinga mpange namna ya kuindeleza na siyo kujadili politics tu. Na hii tabia ya kusema kila mwaka kuwa Wanakyela ni wagumu hawayumbishwi, sijui Abdul Jumbe alitolewa jasho; haina tija hata kidogo kwenu iwapo mbazi kuwa wachovu mbofu kabisa kila mwaka. Ni muda wa kubadilika huu. Mkajenge kwenu badala ya kung'ang'ania Mbeya mjini na Dar es Salaam. Chukua ujumbe huo wape na wenzenu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom