Elections 2010 Kyela elections!

Status
Not open for further replies.
Demokrasi imechukua nafasi yake kyela Dr amepita kwa 88% Mwakalinga asubili next time na aendelee kuwekeza Kyela bila mbwembwe za apa na pale.Kama watu wanambeza Dr kwa ushindi huo wa kura zaidi ya 7000 kura nyingi kuliko wagombea wote apo Mbeya atakuwa ana yake.
Ila CCM ninayoijua mimi huchelewi kukuta Mwakalinga ndo akapitishwa uko NEC iyo August 14?
Kikwete kama anaitakia mema Kyela amtoe mwakipesile Kyela isonge mbele na aache fitina na roho ya korosho ya kikwele ya maadui kuwaweka eneo moja.
Long live Dr na Mwakalinga subiri 2015 bse Mwakyembe hatokuwa mbunge milele.Chonde chonde endelea kuifadhili radio kyela inasaidia sana.
 
Daaa, Mwakalinga anapendwa hapa JF kama SUKARI hivi.

Watu wakiona tu Kyela na Mwakalinga basi haoooooooo..................

Wakiona Mwakyembe tu basi utakuta litopic limeboa............

Lazima mkiri kuwa Mwakalinga anapendwa sana hata hapa JF ila kutokana na ushabiki na UNGURUWE, hata akiwekwa kugombea na Makamba, basi watu wa Kyela mtamchagua Makamba ili awaletee umaarufu maana yeye ni katibu wa CCM Taifa.

Tunahitaji watu wenye mwamko kama wa Kyela kwa Tanzania nzima. Kumbe Wakyela ni kama Wazambia vile. Gari zuri, tai nzuri, nguo nzuri ila hata nyumba hana na anaishi kwenye gari lake. WTF.

Mara nyingi mimi ninapenda sana articles zako, you had a positive points on the development of our poor country. Watu ambao nilikuwa nawaheshimu sana ni pamoja na Sikonge. Ila kwa sasa nina wasiwasi na creadibility yako.

Kwa taarifa yako, topic za Mwakyembe zinakimbiliwa na wana Jf wengi kuliko za Mwakalinga, pia Mwakyembe amafanya mengi kule Kyela, acheni mambo ya kuhadithiwa na wapambe wa mafisadi, nenda mwenyewe kajionee kyela ya sasa. Physical observation matters a lot. fanya analysis ndogo tu. Mfano mwaka 2005 wakati Dr anaingia kulikuwa na shule za sekondari ngapi? na je zilikuwa katika khali gani? Na sasa zipo ngapi na katika khali gani? Siyo unakaa hapo na kumpigia simu afande Samweli ili akupe data na wewe utoe comments zako, utakwenda na maji.
Suala la kuleta maendeleo siyo lazima uwe mbunge, kama mwakalinga ni muungwana basi aendelee kuwasaidia watu wa kyela, kwani ndiyo nyumbani kwake.
 
naona wanapiga kampeni ili mwakalinga apitishwe kwa mlango wa nyuma. hiyo miradi aliyo wekeza si ni yake binafsi? au ndio ilikuwa funga kamba ili akija kugombea apiti kirahisi? kama ghorofa la biashara au nyumba ni yake, sasa hayo maendeleo aliyo leta ni yapi ya kuwasaidia watu? labda useme ya kuona nyumba nzuri nao waige.
asante ,Mwakalinga kwa hilo.
 
Watu wa Kyela wana tabia za masikini jeuri. Labda kama wamebadilika, kwa kawaida hawastushwi na vitu ambavyo wanadhania ni vya kupita hata kama ni vizuri namna gani. Siko upande wa Mwakyembe wala Mwakalinga, ila ninawajua wana Kyela, you have to be from there to understtand their decision making mechanism, otherwise it may not make sense to you.

Wewe umesema vyema.

Katabazi kama hafanyi utani hapa, basi bado hajalielewa hili.
 
Mwana Mtama,
Naafikiana na wewe kwa % kadhaa. Mm si politician ila sioni ubaya wa kujifunza au kusikiliza.Kwa maoni yangu(labda nilikosea)nilifikiri Mbunge hata bila kutegemea pesa inayotoka bungeni angeweza kuwasaidia wananchi wake ki mawazo au kama anayo pesa akawasaidia watu wake kama anavyofanya adv.Mkono na wengine wenye pesa zao.
Lakini ungejisikiaje ungekuwa na mbunge ambaye unajua kabisa ana uwezo na anakueleza ana uwezo wa e.g kukuletea mnunuzi wa maharage yako ambayo unayo lakini hamleti kwa sababu ambazo huzijui?
Kizuri kuliko vyote kama wananchi wameridhika na uchaguzi wao hilo ndio la maana -uchaguzi ni kupanga.
La kusikitisha ni kuwa wilaya nyingi zinawatu potential na mawazo mengi, lakini anayechukua ubunge nadhani inakuwa si rahisi kushirikiana na wengine labda ina matatizo yake -wacha tuangalie tutaona nini kutoka mfumo wa ZNZ.

Kata Bazi

Wananchi si wajinga siku zinavyokwenda elimu ya uraia inaongezeka! WanaKyela wamefanya uchaguzi sahihi...unajua huwa nashangaa mnaposema mbunge alete maendeleo kwa kusaidia wananchi waliomchagua! Leta mwongozo hapo. Nadhani kazi kubwa ya Mbunge ni kuwawakilisha wapiga kura bungeni. Kusema Mbunge hajajenga bara bara na madaraja huo ni uvivu wa kufikiri, lazima Mbunge na ashirikiane na serikali kuweka kwenye budget na kuingiza kwenye mipango ya Maendeleo.

Mwafrika alikuwa akiuliza wale jamaa wa George, wana sera gani jimboni, Kipi Harrison hakukifanya? badala yake walikuwa wakija na matusi na kejeli. JF si wapiga kura ila wanatoa mtazamo kwa sauti kubwa, majidai na majigambo yao yamemkosesha hata kura 1000! Wananchi watamkumbuka daima Mwakyembe kushughulikia Richmond. Mtu anaulizwa sera anasema kuna radio Kyela na amewekeza Billions lol, wanakyela wanajua nguvu alizowekeza Lowassa kutoa Mwakyembe, kupitia kwa Geroge...wamekunywa na kula kwao na na kura kwa Harrison.

Lesson learned!
 
Demokrasi imechukua nafasi yake kyela Dr amepita kwa 88% Mwakalinga asubili next time na aendelee kuwekeza Kyela bila mbwembwe za apa na pale.Kama watu wanambeza Dr kwa ushindi huo wa kura zaidi ya 7000 kura nyingi kuliko wagombea wote apo Mbeya atakuwa ana yake.
Ila CCM ninayoijua mimi huchelewi kukuta Mwakalinga ndo akapitishwa uko NEC iyo August 14?
Kikwete kama anaitakia mema Kyela amtoe mwakipesile Kyela isonge mbele na aache fitina na roho ya korosho ya kikwele ya maadui kuwaweka eneo moja.
Long live Dr na Mwakalinga subiri 2015 bse Mwakyembe hatokuwa mbunge milele.Chonde chonde endelea kuifadhili radio kyela inasaidia sana.

Asante sana! CCM hawezi kujifanyia fitina wenyewe! WanaKyela watamfuata Dr Mwakyembe CHADEMA na jimbo litaishia zake
 
Nyie watu wa Kyela mnataka kufanya sisi wengine hatuna majimbo wala wabunge? Kila kukicha Kyela tu kwa lipi hasa? Kwanza mmetuyeyusha kwa ubishi humu na matokeo tumeyaona. Tafuteni kitu badala inayovuta macho na masikio sasa siyo kila kukicha Kyela tu. Kyela yenyewe ni chovu mno kimaendeleo ukilinganisha na Wilaya zote za Mbeya na huu ni muda muafaka wa kuwashawishi wakina Mwakalinga mpange namna ya kuindeleza na siyo kujadili politics tu. Na hii tabia ya kusema kila mwaka kuwa Wanakyela ni wagumu hawayumbishwi, sijui Abdul Jumbe alitolewa jasho; haina tija hata kidogo kwenu iwapo mbazi kuwa wachovu mbofu kabisa kila mwaka. Ni muda wa kubadilika huu. Mkajenge kwenu badala ya kung'ang'ania Mbeya mjini na Dar es Salaam. Chukua ujumbe huo wape na wenzenu

Wewew lazima unatoka Ileje.....
Kyela sasa ni halmashauri ya mji....hupewi hadhi hiyo bila kufikia vigezo kadhaa......
Kwa maana nyingine, Kyela inafanana na Njombe , Rungwe nk
Ongea kwa point siyo kukurupuka.
 
All in all,
Uwepo wa Mwakalinga kwenye uchaguzi wa mwaka huu umeleta changamoto nzuri. Bila kujali matokeo, nampongeza Mwakalinga kwa kujitosa kinyang'anyiro hiki. Nina sababu
1. Mara nyingi wanaogombea Kyela hutoka koo za Kichifu; kwa Mwakalinga na wengine kujitokeza kunavunja mwiko huo
2. Kwa kuwa kila mtu alito hoja na mawazo ya jinsi ya kuendeleza Kyela, naamini hata Dokta akipita atakuwa amecopy baddhi ya mbinu za kuleta maendeleo, badala ya kusubiri mgao toka serikali kuu. Mfano wa haya tumeyaona wilayani Karatu kwa Raisi wetu Mtarajiwa Dk Slaa!
3. Umetoa mwanya kwa wananchi kuelewa umuhimu wa kupiga kura. Kwamba hawatapiga tena kura bila kuhoji uwezo na sababu zinazowasukuma wagobea kutaka ubunge wa wilaya yao
4.Mwakalinga amekubali yaishe, na nashangaa kwanini watu bado wanadhani Mwakalinga ana Kinyongo. Huu ndio ushindani.

Kwa hiyo, vyovyote vile isemavyo, iwe Mwakalinga ametumwa, au amejituma mwenyewe, tumejifunza mengi hapa.
Pia naamini Mwakalinga atakuwa ameelewa sababu za kushindwa kwake. Mimi nimeona haya
1. Mwakalinga ameingia kwenye kampeni kipindi kibaya. Kipindi ambacho watu wengi walishaaminishwa kwamba Mwakyembe anahujumiwa. Binafsi nilijaribu kumzuia George kuvuta subira, lakini bahati mbaya wafuasi wa George walikuwa si watafiti wa siasa za kule kiasi kwamba walikuwa wana mpa George wrong information ( bila kujua). Kwa kufanya hivyo wamesaidia kuanguka kwa mtu ambaye naamini kabisa bado ni potential. Kwa kuwa wengi tuko mbali na jimbo hili, tulishindwa kupata hoja za msingi kumjenga George ili ajitose lini na kwa namna gani.
Kuna wakati ilikuwa ukiwauliza washauri wa George mantiki, mikakati, nk, jamaa walikuwa wanajibu mkato, hawakupi muda wa kufikiri, na in short wanakuambia wewe ni msaliti. Hii haifai. Kumsaidia mtu ni pamoja na kumuuliza maswali hata ya ndani kabisa ili unapotoa mchango wako uwe na hoja za kushawishi watu. Naamini safari nyingine Mwakalinga artakuja na mbinu mpya na kushinda
2. Kutokuwa karibu mara nyingi Kyela. Kwa kuwa George alikuwa na mipango ya kuingia kwenye siasa, ilikuwa ni vyema akajenga ukaribu na watu wa jamii zote na rika zote na kabila zote. Kyela si ya Wanyakusa: Kyela ni Metro sasa hivi. Sasa unapoanguka hata kijiji ulikozaliwa hilo ndilo jibu lake. Kwamba hata ndugu wanakuwa hawakuelewi ( na sio hawakupendi). Ukiwa ni mwanasiasa, basi ni lazima unywe na watu kwa level zao ili wajue wewe ni mmoja wao. Vinginevyo watakuita unaringa; na wewe utawaita wana wivu. Yote haya ndio huleta negative results.
Bila shaka hili George ameliona
3.Kuchagua kwa usahihi Campaign Mangers. Wapambe si lazima wawe ndugu. Ukiweka ndugu wengi kwenye kampeni zako ni kwamba watu hawakuelewi, maana watadhani mmekuja kutangaza uchifu tu. Na zaidi ni kwamba huwa arogant kwa watu , na wewe utashindwa kuwakemea kwaw sababu ni ndugu! Nadhani hili litarekebika baadaye, come 2010

Mwisho:
Nimesikia fununu kwamba kuna watu wanamkatisha tamaa Mwakalinga ili asirudie tena mambo ya siasa. Nakusihi usiwasikilize. Kajipange, rekebisha kasor njoo 2010. Au bado kuna vyama vingine na jaribu huko ili uzidi kuleta changamoto kwenye siasa za jimbo ambalo naamini una mapenzi nalo kabisa. Unaonaje ujaribu kwa tiketi ya CHADEMA ?

Pia, Dr Mwakyembe, umesikia yote, chagua yaliyo postive kutoka kwa Mwakalinga, Rhoda, Elias nk ili kama kweli wote lengo lenu lilikuwa moja, mlete maerndeleo Kyela.
Vunjeni makambi yanayomsaidia Lowasa na Makuwadi wake, tusemezane tuijenge Kyela
Mwaibisheni Mwakipesile , ajifunze kwamba anwahujumu Kyela, kule kwenye Masyeto yake, kwa faida ya watu ambao hawana uchungu na wala hwana mjukuu pale Kyela. Shikaneni mikono na Mwakalinga, na TUANZE UKURASA MPYA
TABIA ya upambe si tabia ya wana Kyela, stop being used, you are killing your own people and the Generation there after. After all, we die so soon, so why the Lowasas, and the Aziz want to use you guys? We are grown up buds......
 
Matokeo ya mwisho kabisaa nia haya

Dr. Mwakyembe 15,336 77%
G.Mwakalinga 1,691 9%
Elius Mwakalinga 1,407 7%
E.Mwanjala 937 5%
R.Mwamnyange 466 2%

Hapo sasa mwaonaje wana kyela?
 
Matokeo ya mwisho kabisaa nia haya

Dr. Mwakyembe 15,336 77%
G.Mwakalinga 1,691 9%
Elius Mwakalinga 1,407 7%
E.Mwanjala 937 5%
R.Mwamnyange 466 2%

Hapo sasa mwaonaje wana kyela?


Nafurahia anguko la Lowassa Kyela!
 
Matokeo ya mwisho kabisaa nia haya

Dr. Mwakyembe 15,336 77%
G.Mwakalinga 1,691 9%
Elius Mwakalinga 1,407 7%
E.Mwanjala 937 5%
R.Mwamnyange 466 2%

Hapo sasa mwaonaje wana kyela?

Kulikuwa na upinzani mkubwa sana kwenye kumtafuta mshindi wa pili, ni wazi kuwa hao wote walikuwa na nguvu sawa na yeyote kati yao angeweza kuikamata nafasi ya pili.

Hongera G. Mwakalinga kwa ushindi wa nafasi ya pili ambayo ndio hasa iliyokuwa haijulikana itakamatwa na nani.
 
Mwakalinga hakufanya hayo ili agombee. Miradi yake tayari inarudisha hela. Li mradi la HASARA ambalo kafanya hadi leo ni Kyela FM. Anaombea tu liwe linajiendesha lenyewe na kwenye uongozi kajitoa kabisa. Imebaki chini ya watu wengine na Halmashauri ya Wilaya ya Kyela. Ila iko hoi kifedha hata sehemu za majengo haina na kaamua tu kuendelea kuikumbatia kwa kuiweka hapo kwake kwenye KBS.

Kama ulifikiri alitegemea hela yake kurudi, basi utaumia sana kuona jamaa ndiyo kwanza ataongeza miradi na huenda asigombee tena ili wenye WIVU mjinyonge. Muishi salama na mbunge wenu maarufu....... :)

Wee wa Lipstic wewe baki tu nazo. Naona tangu usikie hilo neno, umelipenda sana loohh :)
Siyo siri utabaki kuwa nguruwe hata ukipata watu wanaotaka kukusaidia kwa dhati. Wewe unataka kuwa maarufu. Maendeleo SUCK.
Mzee huna hoja, Kwani hakuna cha maana unachoandika zaidi ya kujifanya msemaji wa Mwakalinga. Kwanza kabisa Kyela hakuna kitu kinachoitwa KBS. Mwakyembe kakusea nini? Mwakyembe akiwa mbunge wewe unapungukiwa nini? Unataka Mwakalinga awe mbunge ana nini kichwani? Hivi hio Redio kyela walimwambia wanahitaji redio au alijiletea tu? Endelea kuwa msemaji wa Mwakalinga huenda utaambulia laptop
 
Masaiti,
Usinihukumu bure hapa JF ndugu yangu. Nikiandika kuhusu Kyela, ninakuwa kati ya UKWELI na UTANI. Wanyakyusa ni watani wangu na hiyo huwa inanipa eneo kubwa sana la KUJIDAI kila ninapoandika.

Wanakyela wameamua kuchagua UMAARUFU, let it be.
Mara nyingi mimi ninapenda sana articles zako, you had a positive points on the development of our poor country. Watu ambao nilikuwa nawaheshimu sana ni pamoja na Sikonge. Ila kwa sasa nina wasiwasi na creadibility yako.

Kwa taarifa yako, topic za Mwakyembe zinakimbiliwa na wana Jf wengi kuliko za Mwakalinga, pia Mwakyembe amafanya mengi kule Kyela, acheni mambo ya kuhadithiwa na wapambe wa mafisadi, nenda mwenyewe kajionee kyela ya sasa. Physical observation matters a lot. fanya analysis ndogo tu. Mfano mwaka 2005 wakati Dr anaingia kulikuwa na shule za sekondari ngapi? na je zilikuwa katika khali gani? Na sasa zipo ngapi na katika khali gani? Siyo unakaa hapo na kumpigia simu afande Samweli ili akupe data na wewe utoe comments zako, utakwenda na maji.
Suala la kuleta maendeleo siyo lazima uwe mbunge, kama mwakalinga ni muungwana basi aendelee kuwasaidia watu wa kyela, kwani ndiyo nyumbani kwake.
 
Kulikuwa na upinzani mkubwa sana kwenye kumtafuta mshindi wa pili, ni wazi kuwa hao wote walikuwa na nguvu sawa na yeyote kati yao angeweza kuikamata nafasi ya pili.

Hongera G. Mwakalinga kwa ushindi wa nafasi ya pili ambayo ndio hasa iliyokuwa haijulikana itakamatwa na nani.

Mkuu nilikuwa sijagundua kumbe ukijumlisha George na Elias Mwakalinga, Mwanjala na dada Mwamunyange jumla yao ni 4501 bado wanashindwa na Dr Harrison M, labda kama wangechukua na zile kadi 10,000 hahahahahahahahaahhhh
 
Kitu gani wakati mmemshinda? Binadamu tuna tabia mbaya sana. Rafiki yako akishindwa au kufeli maisha, mtihani, uchaguzi basi unamkimbia. Mimi hilo sifanyi hata kidogo. Sihitaji kitu chochote kutoka kwa Mwakalinga. Yeye atajirudia zake UK na mie ntabaki hapa Sikonge and life goes on. Mie sijafika Kyela na yeye hajafika Sikonge. Sijapokea Pesa wala Mzigo kutoka kwake.
Kitu pekee nitachowepokea na nitaendelea kupokea ni USHAURI na nini cha kufanya kusaidia Wana Sikonge wangu hapa. Kwa Vision ya maendeleo hata Mwakyembe kakubali kuwa George yuko juu. Pia Wanakyela wanakiri hilo ila Mwakyembe kawaletea umaarufu na hilo niyo MUHIMU KWAKO. Kupanga ni kuchagua. Uamuzi wa Wanakyela uheshimiwe.

Halafu wewe hoja zako ziko wapi ili na sisi TUZIJADILI? Au unataka nikuachie JF peke yako ili Uwe inaandika na kujichambua mwenyewe kama Mr. Beans?
Mzee huna hoja, Kwani hakuna cha maana unachoandika zaidi ya kujifanya msemaji wa Mwakalinga. Kuna kitu unatafuta kwa Mwakalinga wewe!!!
 
Nyumbu,

Kila ukiandika hapa kwa kuwa NEUTRAL, wanakuita uko kambi ya Mwakalinga na unaandika KUJIPOZA. Mwakalinga akirudi hapa, kuna moto utawaka maana kuna watu wana ugomvi naye wa siku nyingi na wako tayari hata kusikia Mwakyembe kauwa watu ili ashinde. Hata kama watakuwa wameuawa ndugu zao, watafurahi tu kisa Mwakalinga kashindwa. Sintashangaa wengine walienda hadi kuloga.

Kuna mijitu ni kama Mipare vile. Iko tayari KUUZA ngo'ombe ili ashinde kesi ya KUKU.

Nilikuwa nafikiria achukue fomu za CHADEMA ingawa kwa lengo zaidi ya kusaidia na kulinda kura za Dr. Slaa huko Kyela. Sijui atakuwa na uamuzi gani kwa sasa. Akifanya hivyo basi atakuwa anasaidia zaidi Watanzania na si Kyela peke yake. Na pia hapa Umafia waliomchezea hautakuwepo tena. Ukweli halisi wa KURA utaonekana na hiyo ndiyo itakuwa Final Say. Mtu akitoa HONGO basi afahamu kesi haiendi kwa Makamba ila itakwenda MAHAKAMANI.

KATABAZ: Nakubaliana na maneno yako. Naweza kusema wazi kuwa wewe na Nyumbu kweli mlikuwa Kyela na hawa wengine wote akina Kasyabone, Malafyale, Afande Samuel na wengine wote wanaobishana hapa ni wapiga story za kijiwe na hawako KYELA. Mie nakiri kabisa wala sijafika Kyela. Ila cha kushangaza, pamoja na kuwa hawapo Kyela, wanataka Kutuaminisha habari kama vile walikuwepo. UChaguzi umeisha na Mwakyembe wenu kashinda, KUWENI WAKWELI BASI HATA SIKU MOJA.
 
Hizi kura 15,336 mhhhh!!!! Ngoja wazihakiki akina Mwakalinga maana naanza kuogopa kuwa Kyela nzima ilipiga kura na kuwa jimbo lenye wana CCM waaminifu sana. Sitashangaa wakiibua majina hadi ya akina Marehemu Mwaka............
Matokeo ya mwisho kabisaa nia haya

Dr. Mwakyembe 15,336 77%
G.Mwakalinga 1,691 9%
Elius Mwakalinga 1,407 7%
E.Mwanjala 937 5%
R.Mwamnyange 466 2%

Hapo sasa mwaonaje wana kyela?
 
Mkuu nilikuwa sijagundua kumbe ukijumlisha George na Elias Mwakalinga, Mwanjala na dada Mwamunyange jumla yao ni 4501 bado wanashindwa na Dr Harrison M

Just for a laugh!

Assume zile kadi 10,000 zilitumika.................

15336 - 10,000 = 5336. The guy still beat the combination hahaha haha hahah!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hizi kura 15,336 mhhhh!!!! Ngoja wazihakiki akina Mwakalinga maana naanza kuogopa kuwa Kyela nzima ilipiga kura na kuwa jimbo lenye wana CCM waaminifu sana. Sitashangaa wakiibua majina hadi ya akina Marehemu Mwaka............
.

hahahah.

Jamani, hivi wilaya ya kyela ndiyo inayoongoza kwa tanzania kwa kuwa na wanachama wengi wa ccm?.Yaani waliopiga kura ni 20,000? na je ambao hawakupiga ni wangapi?.

Karibu majimbo yote wanachama wa ccm waliopiga kura ni chini ya 10,000..
Hapa kazi ni kubwa kweli kweli.
 
Just for a laugh!

Assume zile kadi 10,000 zilitumika.................

15336 - 10,000 = 5336. The guy still beat the combination hahaha haha hahah!!!!!!!!!!!!!!!
.

No. was more than 10,000.
Let say 15,000.
15336-15,000= 336.jamaa angekuwa wa mwisho.
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom