Kwanini watanzania wanamlaumu mwalimu Nyerere kwa kukosa elimu?


Niruhusuni nitundike haya machache kwa haraka kuhusu Kwanini watanzania wanamlaumu mwalimu nyerere kwa kukosa elimu?

Hakujatokea Rais wa Tanzania ambaye alikazania elimu, kama Mwalimu Nyerere; tusisahau Nyerere alikuwa Mwalimu!

Mtihani wa Territorial Standard Eight uliondolewa nilipokuwa Darasa la 7 (1958), wale waliokuwa Darasa la 8 wakawa wa kwanza kuandika mtihani wa National Primary School Leaving Examination.

Territorial Standard Eight ulikuwa kikwazo kikubwa kuwapata wanafunzi wa sekondari, ambazo wakati huo zilikuwa nichache sana! Manake ilikuwa mwanafunzi ashinde Daraja la Kwanza au la Pili!
Kuna uwezekano mkubwa hata kwa hao waliokuwa wakishinda Daraja la Tatu kuweza kujifunza zaidi na kushinda hata Daraja la Kwanza wafikapo sekondari!

Wakati huo huo, sekondari za serikali karibu zote zilianza na mifumo miwili. Badala ya wanafunzi 45, zilichukua wanafunzi 90 Darasa la 9!

Darasa letu la 8 lilikuwa la mwisho kabla elimu ya Shule ya Msingi kuwa miaka saba. Hii ilisaidia kuwapata wanafunzi wengi waliokuwa wamemaliza elimu ya msingi ili waweze kuendelea na sekondari mapema.

Wanafunzi wa Darasa la 7, pia, walikubaliwa kuandika mtihani wa Darasa la 8 ili washindapo waingie sekondari bila kizuizi.

Serikali iliondoa ubaguzi wa rangi ( za Wahindi na Wazungu) na dini zote (Waismailia, Wakatoliki, Wasabato, Waprotestanti, na kadhalika) katika mfumo wa elimu zote.

Nilimaliza Darasa la 9 wakati wa uhuru. Nikiwa Darasa la 9, serikali ilitoa Mtihani wa Territorial Standard Ten. Hiki kilikuwa ni kikwazo kikubwa kuwapata wanafunzi wa kuendelea na Darasa la 11! Manake ilikuwa mwanafunzi ashinde Daraja la Kwanza au la Pili!

Mwaka uliofuata karo ikaondolewa katika mashule yote nchini. Wanafunzi wa Darasa la 11 waliruhusiwa kuandika mtihani wa Darasa la 12 wa Cambridge School Certificate, Ordinary Level ili washindapo waingie Darasa la 13 bila kizuizi.

Wakati huo huo, Mwalimu Nyerere alikuwa amefanya safari nchini Amerika na Ulaya Magharibi kuomba serikali na wafadhili wengine kuisaidia Tanganyika katika mambo ya elimu: kuanzisha Chuo Kikuu hapo Lumumba Street.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu (kampasi ya kwanza) walikuwa wakila na kulala hapo Dar es Salaa Technical College, kabla ya kuanza kujenga na kuhamia kampasi ya Mlimani!
Akiwa Amerika, Nyerere alipata pia msaada wa walimu wa Peace Corps, baada ya walimu Waingereza kufunga mizigo yao kufuatia uhuru. Peace Corps walifundisha shule za msingi hadi sekondari. Wengine watakumbuka uji wa oatmeal katika shule za msingi!

Ikumbukwe kwamba tulikuwa na koleji moja tu ya Makerere, kampala, Uganda, kwa nchi zote za Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na kupokea wanafunzi kutoka Selisheli na Nyasaland (Malawi).

Lakini hiyo koleji yetu ilikuwa chini ya mbawa za London University – wanafunzi walikuwa wanapata digrii za London University.

Kila nchi (Tanganyika, Uganda na Kenya) zikaamua kuanzisha University of East Afrika (Uganga na Kilimo, Makerere; Uhandisi na Biashara, Nairobi; na Sheria na Elimu, Mlimani).

Nikiwa Darasa la 12, mwaka huo tukawa wa kwanza kuwa pre-selected kwenda Darasa la 13 kabla ya majibu kutoka Uingereza.

1964 nilijiunga na Tabora Sekondari (Wavulana). Mwaka 1965 tukawa wa kwanza kuingia Chuo Kikuu kwa Principal moja na Subsidiary moja ili kuongeza idadi ya wanafunzi wenye digrii ya kwanza.

Kwa kuwa Tanzania ilikuwa na walimu wachache, wengi wetu iliwabidi waombwe kuchukua kozi ya Ualimu (Education Option). Kwa kila mwanafunzi wa Tanzania aliyechukua masomo yasayansi alilazimishwa kuchukua hiyo Education Option!

Kudhibiti ujinga kwa elimu ya watu wazima (kisomo, elimu ya watu wazima na maendeleo vijijini) kuliiwezesha Tanzania kuinua kisomo karibu 95% (kushinda nchi zote za sub-Saharan Africa)!

Tusisahau Azimio la Musoma: waliomaliza Darasa la 12 na kufanyakazi miaka miwili waliruhusiwa kuomba kujiunga na Chuo Kikuu. Wengine walikuwa wakijiunga kupitia mtihani wa Mature Age Entry ukidhibitiwa na Elimu ya Watu Wazima ya Mlimani.

Alileta mapinduzi katika elimu: Elimu ya Kujitegemea ili taifa lijitegemee. Tukashindwa utekelezaji wake, shauri ya kasumba nyingi za kikoloni, hadi leo hii!!!!!
 
Mkuu andindile Salam,
Umekiuka kwa Makusudi au uesahau kuwa MWALIMU pia alipokea misaada???
 
Mkuu andindile Salam,
Umekiuka kwa Makusudi au uesahau kuwa MWALIMU pia alipokea misaada???

Ndugu, hakuna mahali niliposema kuwa mwalimu hakupokea misaada fuatilia thread zote zilizotuma, hutakuta mahali popote labda unamwongelea andindile mwingine
 
Mimi nadhani kuwa wale waote wanaomlaumu Nyerere kuhusu kudidimia kwa elimu Tanzania hawamtendei haki labda kwa sababu nyingine kabisa. Ingawa nakubali kuwa Nyerere anastahili kupewa lawama kwa kiasi fulani, lakini siyo kwa kiwango kinachoandikwa hapa.

Nyerere alifanya mambo mengi sana ya kuendeleza elimu Tanzania. Tuna mifano mingi inayoonyesha kuwa nchi zinazofuata mfumo wa elimu kama ule ambao Nyeyere alikuwa akitaka kujenga zimefanikiwa sana kielimu; China na Kyuba ni mifano mizuri sana kwa hilo. Kwa hiyo kutaifisha shule za msingi, kuanzisha elimu ya watu wazima na kuifanya elimu kwa jumla iwe ya bure kabisa ilikuwa ni sera nzuri sana. Kuna wataalamu wengi sana wa kitanzania katika nyanja mbalimbali waliosoma na kufaulu chini ya mfumo huo.

Tatizo la Nyerere katika maendeleo ya elimu lililetwa na mfumo wa uchumi uliopelekea watu washindwe kuishi kwa miashahara yao. Jambo hili lilichangia kuangusha elimu kwa njia kadhaa, baadhi yake zikiwa kama ifuatavyo:

(a) Watu walianza kuchukia baadhi ya kazi ambazo zilikuwa haziwaingizii mapato ya ziada kwa njia zote za halali (kama posho) na za haramu (kama rushwa). Mojawapo ka kazi zilizoathiriwa na hili ilikuwa ni ualimu. Hata waalimu wa siku nyingi walipoteza moyo wa kazi wakawa wanatumia muda wao mwingi kwa kujitafutia chochote nje ya mshahara.

(b) Hata pale ambapo waalimu waliendelea kuwa na moyo wa kufundisha, mazingira ya kufundisha yalianza kuharibika kiasi kuwa waalimu wakawa hawana vifaa vya kufundishia kama chaki, kalamu nyekundu za kusahihisha, na vitabu; na watoto pia wakawa hawana madawati ya kukalia. Yote haya yalichangia sana kupunguza kasi ya kujifunza miongoni mwa watoto.

(c) Watoto na baadhi ya wazazi hawakuona faida ya kuwaweka watoto shuleni na kufuatilia masomo huku hawaoni faida ya moja kwa moja watakayopata baada ya kumaliza shule. Kwa hiyo hata wale waliokuwa wakienda shuleni, walifanya hivyo kwa mujibu wa sheria tu lakini hawakuwa wanazingatia masomo tena, baada ya shule walikuwa wakienda kufanya biashara za kurusha.


Kwa hiyo labda mtu aseme kuwa Nyerere kwa kujenga uchumi dhaifu alisababisha elimu ishuke, lakini siyo sahihi kusema kuwa sera za Nyerere kuhusu elimu zilikuwa mbovu, No. Kumbukeni kuwa wakati tunapata Uhuru, Tanzania hatukuwa na chuo chochote cha elimu ya juu zaidi ya ile Dar-es-Salaam University College of East Africa ambacho kilikuwa ni kitivo cha sheria cha Makerere. Katika kipindi cha miaka 24 aliyokaa madarakani, Nyerere aliacha vyuo kadhaa vya elimu ya juu ambapo Chuo Kikuu cha Dar-es Salaama kikiwa ni moja ya vyuo vinavyoheshimiwa sana Afrika.
 
Kwa hiyo labda mtu aseme kuwa Nyerere kwa kujenga uchumi dhaifu alisababisha elimu ishuke, lakini siyo sahihi kusema kuwa sera za Nyerere kuhusu elimu zilikuwa mbovu,quote]
Uchumi dhaifu upi? maana kwa kumbukumbu zangu, ni wakati wa Nyerere tulianza kuona uwekezaji wa viwanda katika baadhi ya mikoa, kilimo kiliendelea kupanda, ajira ziliendelea kuongezeka. Naomba mniambie baada ya uchumi kuanza kuyumba na yeye akaamua kuachia ngazi, wale waliochukua madaraka walifanya nini kuboresha yale yaliyoachwa?
 
Kwa hiyo labda mtu aseme kuwa Nyerere kwa kujenga uchumi dhaifu alisababisha elimu ishuke, lakini siyo sahihi kusema kuwa sera za Nyerere kuhusu elimu zilikuwa mbovu,quote]
Uchumi dhaifu upi? maana kwa kumbukumbu zangu, ni wakati wa Nyerere tulianza kuona uwekezaji wa viwanda katika baadhi ya mikoa, kilimo kiliendelea kupanda, ajira ziliendelea kuongezeka. Naomba mniambie baada ya uchumi kuanza kuyumba na yeye akaamua kuachia ngazi, wale waliochukua madaraka walifanya nini kuboresha yale yaliyoachwa?

Wewe mbona unaboronga mchana. Uchumi hausiani na ujenzi wa viwanda. Unahusiana na viwanda vinafanya nini.

Tueleze viwanda vilikuwa vinaingiza kiasi gani?
 
jokaKuu,
Kuna sababu nyingi tu kwa nini Wakenya wametuzidi katika idadi ya wasomi kuanzia siku za ukoloni. Ukiangalia miaka ya 50-60 wakati Tanganyika tulijivunia kuwa na graduates watano kutoka Makerere Kenya ilikuwa na zaidi ya 20. The only way we could have caught up with Kenya is if Kenya stopped growring---but they have been growing at the same pace--while we are playing catch up. Nakumbuka 1961 Barclays bank pale Musoma ilikuwa na maafisa kutoka Kenya simply because there were no Tanganyikans to take up those positions. Hata wakati wa University of east Africa Kenyas were still ahead of us. Ingekuwa fair zaidi kama ungesema kuwa kuna wakati tulilingana katika idadi ya graduates na sasa wenzetu wametuzidi. But was there such a time?


Jasusi:

Swala la inbalance lilikuwepo. Lakini kuna kitu kimoja cha kuangalia kwa makini. Nacho ni matumizi ya resources.

Baada ya uhuru Tanzania ilitilia sana mkazo wa primary school education. Na elimu yetu ilisukwa kuwa hili nchi iwe kama jeshi. Kwa mpango wa kuwa tuwe na wapiganaji wengi (waliomaliza darasa la saba) na majenerali wachache (waliomaliza chuo kikuu).

Mpaka katika ya 80. UDSM bado ilikuwa inatoa wanafunzi wachache sana kwa mwaka. Na kama sikosehi walikuwa chini ya 1000.

Na hiyo yote ni sera ya Nyerere ya kuwa na University ya kutoa ma-general. Na ma-general wenye tunawaona sasa.
 
Mimi nadhani kuwa wale waote wanaomlaumu Nyerere kuhusu kudidimia kwa elimu Tanzania hawamtendei haki labda kwa sababu nyingine kabisa. Ingawa nakubali kuwa Nyerere anastahili kupewa lawama kwa kiasi fulani, lakini siyo kwa kiwango kinachoandikwa hapa.

Nyerere alifanya mambo mengi sana ya kuendeleza elimu Tanzania. Tuna mifano mingi inayoonyesha kuwa nchi zinazofuata mfumo wa elimu kama ule ambao Nyeyere alikuwa akitaka kujenga zimefanikiwa sana kielimu; China na Kyuba ni mifano mizuri sana kwa hilo. Kwa hiyo kutaifisha shule za msingi, kuanzisha elimu ya watu wazima na kuifanya elimu kwa jumla iwe ya bure kabisa ilikuwa ni sera nzuri sana. Kuna wataalamu wengi sana wa kitanzania katika nyanja mbalimbali waliosoma na kufaulu chini ya mfumo huo.

Tatizo la Nyerere katika maendeleo ya elimu lililetwa na mfumo wa uchumi uliopelekea watu washindwe kuishi kwa miashahara yao. Jambo hili lilichangia kuangusha elimu kwa njia kadhaa, baadhi yake zikiwa kama ifuatavyo:

(a) Watu walianza kuchukia baadhi ya kazi ambazo zilikuwa haziwaingizii mapato ya ziada kwa njia zote za halali (kama posho) na za haramu (kama rushwa). Mojawapo ka kazi zilizoathiriwa na hili ilikuwa ni ualimu. Hata waalimu wa siku nyingi walipoteza moyo wa kazi wakawa wanatumia muda wao mwingi kwa kujitafutia chochote nje ya mshahara.

(b) Hata pale ambapo waalimu waliendelea kuwa na moyo wa kufundisha, mazingira ya kufundisha yalianza kuharibika kiasi kuwa waalimu wakawa hawana vifaa vya kufundishia kama chaki, kalamu nyekundu za kusahihisha, na vitabu; na watoto pia wakawa hawana madawati ya kukalia. Yote haya yalichangia sana kupunguza kasi ya kujifunza miongoni mwa watoto.

(c) Watoto na baadhi ya wazazi hawakuona faida ya kuwaweka watoto shuleni na kufuatilia masomo huku hawaoni faida ya moja kwa moja watakayopata baada ya kumaliza shule. Kwa hiyo hata wale waliokuwa wakienda shuleni, walifanya hivyo kwa mujibu wa sheria tu lakini hawakuwa wanazingatia masomo tena, baada ya shule walikuwa wakienda kufanya biashara za kurusha.


Kwa hiyo labda mtu aseme kuwa Nyerere kwa kujenga uchumi dhaifu alisababisha elimu ishuke, lakini siyo sahihi kusema kuwa sera za Nyerere kuhusu elimu zilikuwa mbovu, No. Kumbukeni kuwa wakati tunapata Uhuru, Tanzania hatukuwa na chuo chochote cha elimu ya juu zaidi ya ile Dar-es-Salaam University College of East Africa ambacho kilikuwa ni kitivo cha sheria cha Makerere. Katika kipindi cha miaka 24 aliyokaa madarakani, Nyerere aliacha vyuo kadhaa vya elimu ya juu ambapo Chuo Kikuu cha Dar-es Salaama kikiwa ni moja ya vyuo vinavyoheshimiwa sana Afrika.

Kichuguu:

Mkuu vyuo gani kadhaa alivyoacha ??? Unataka kuongezea na chuo cha kikuu cha chama kivukoni.
 
Wewe mbona unaboronga mchana. Uchumi hausiani na ujenzi wa viwanda. Unahusiana na viwanda vinafanya nini.

Tueleze viwanda vilikuwa vinaingiza kiasi gani?

Ni sehemu ya mihimiri ya uchumi, kuingiza shilingi ngapi nalo ni la kuuliza? Mbona huulizi watanzania wangapi waliajiriwa katika hivyo viwanda? Maana nakumbuka Mbeya tulikuwa na kiwanda cha Mbeya Textile, HISOP, Kiwanda cha zana za kilimo Mbeya (ZZK), Viwanda vya kuchambua pamba na kukamua mafuta, kiwanda cha kechemsha nguzo za umeme, hivyo vichache vilipokufa uchumi wa Mbeya mjini uliyumba hata mazao ya kilimo yalikosa soko maana hakukuwa ta tabaka la wafanyakazi wengi wa kununua hizo bidhaa
 
Jasusi,

..lakini si tuna taarifa kwamba tulikuwa tunaongoza Afrika ktk kuandikisha wanafunzi shule ya msingi?

..ni kitu gani kimetufanya tushindwe kuendeleza rekodi hiyo hiyo mpaka Chuo Kikuu?

..wakati wa East Africa Univ' Faculty of Law ilikuwa Dar-Es-Salaam, sasa ukisikia Wakenya wana wanafunzi wengi zaidi wa Sheria kuliko Tanzania utasemaje?

..mimi nadhani tu-trace our educational priorities toka tujitambue kama taifa. tujifunze toka kwa wenzetu, na tusione haya kusema kuna mahali tulikosea.

Hili swali ulilouliza kuhusu sisi kujivunia kuna jibu moja tu na hakuna humu ndani atakayekwambia.

Jibu lipo kwenye mipango ya World Bank (chini ya Robert MacNamara), IMF na Nchi matajiri za kusaidia nchi masikini hili baadaye nchi hizo ziweze kujitegemea kiuchumi.

Takwimu zinaonyesha kuwa pesa za misaada hazikusaidia nchi masikini kuendelea na kujitegemea kiuchumi. Mafanikio yalitokea katika kuongezeka kwa literacy rate na kupunguza kwa child mortality.

Hivyo tukitaka kuendelea ni lazima turudi kwenye drawing board. Hili la mSwedish kusaidia bajeti ya elimu na viongozi wetu kujivunia ongezeko la wanaojua kusoma na kuandika alitufikishi popote.

Siku zote wakikata misaada namba ya wanaojua kusoma na kuandika uwa inaporomoka.

waKenya elimu yao ilikuwa ya kulipia lakini serikali Ili-pump pesa resources nyingi na ndio sababu wako mbele.
 
Ni sehemu ya mihimiri ya uchumi, kuingiza shilingi ngapi nalo ni la kuuliza? Mbona huulizi watanzania wangapi waliajiriwa katika hivyo viwanda? Maana nakumbuka Mbeya tulikuwa na kiwanda cha Mbeya Textile, HISOP, Kiwanda cha zana za kilimo Mbeya (ZZK), Viwanda vya kuchambua pamba na kukamua mafuta, kiwanda cha kechemsha nguzo za umeme, hivyo vichache vilipokufa uchumi wa Mbeya mjini uliyumba hata mazao ya kilimo yalikosa soko maana hakukuwa ta tabaka la wafanyakazi wengi wa kununua hizo bidhaa

Mbona unakuwa specialist wa kutoelewa mambo. Kwa taarifa yako, kiwanda cha zana za kilimo Mbeya (ZZK) hakikusaidia chochote kile. Wakazi wa mkoa wa Mbeya na Rukwa walikuwa ni mastadi katika kufua chuma na zana zao za kilimo zilikuwa imara kuliko zile za ZZK.

Vilevile Tanzania ni nchi iliyokuwa inategemea kilimo kwa mapato yake. Industrialization iliyofanyika ilikuja kwa expense ya serikali kusahau masuala ya kilimo. Hivyo serikali iliua sekta ya kilimo kwa mategemeo kuwa nchi itakuwa ya viwanda.

Vilevile acha kutumia neno Tabaka la wafanyakazi. Tanzania haikuwa nchi ya class struggle. Ni obssession yenu ya ujamaa mnaanza kutumia maneno ya matabaka.
 
Ndugu kila kitu kanapoanza lazima kiwe na mapungufu, through experience tungeendelea kuboresha zana zetu. Wahuzi hawakukatazwa kuendelea na uhunzi na wao wangeendelea kuboresha zana zao. Kosa langu li wapi. Pia wakulima hawawezi tu kuzalisha mazao ya kula tu lazima wapate ziada ili wauze kwa ajili ya mahitaji mengine. Na mara nyingi soko linakuwepo kwenye urban areas ambako kama kuna watu walioajiliwa ndio soko moja wapo. Iwapo watu wanaoishi mjini hawajaajiliwa bali nao wanakuwa wakulima kama yule aliye kijijini, nani atamuuzia mmwenzie bidhaa?
Hivi sasa ukiangalia miji mingi inakuwa lakini wakaazi wake wengi ni wakulima hivyo kutokuwa chachu ya soko la bidhaa za mashambani
 
Ndugu kila kitu kanapoanza lazima kiwe na mapungufu, through experience tungeendelea kuboresha zana zetu. Wahuzi hawakukatazwa kuendelea na uhunzi na wao wangeendelea kuboresha zana zao. Kosa langu li wapi. Pia wakulima hawawezi tu kuzalisha mazao ya kula tu lazima wapate ziada ili wauze kwa ajili ya mahitaji mengine. Na mara nyingi soko linakuwepo kwenye urban areas ambako kama kuna watu walioajiliwa ndio soko moja wapo. Iwapo watu wanaoishi mjini hawajaajiliwa bali nao wanakuwa wakulima kama yule aliye kijijini, nani atamuuzia mmwenzie bidhaa?
Hivi sasa ukiangalia miji mingi inakuwa lakini wakaazi wake wengi ni wakulima hivyo kutokuwa chachu ya soko la bidhaa za mashambani


Andindile:

Unazungumza vitu kutokana na ufahamu wako bila kufanya research yoyote. Kuhusu viwanda ngoja nitoe excerpt kutoka kwa moja ya wataalamu wa Bank ya Dunia William Easterly.


Capital worker in Tanzania's manufacturing sector grew at 8 percent per annual over the period 1976 to 1990, but manufacturing output per worker fell at 3.4 percent per annum over the same period.

Hivyo sentensi yako kuwa kila kitu kinapoanza ni lazima kiwe na mapungufu zina negative impacts katika maendeleo ya kiuchumi. Kwa sababu mapungufu hayo yatajionyesha katika output. Na kwa Tanzania kuwa na mapungufu kwa muda wa zaidi ya miaka 14, hapo sio kutafuta experience. Hapo ni kuwa consistency katika kuboronga.


The World Bank helped finance the Morogoro Shoe Factory in Tanzania in the 1970s. This show factory had labor, machinery, and the latest in shoe-making technology. It had everything except shoes. It never produced more than 4 percent of its installed capacity. The plan which had planned to supply the entire Tanzanian shoe market and then export three-quarters of its production shoes to Europe, never exported a single shoe. The plant was not well designed for Tanzania's climate; it had aluminum walls and no ventilation system. The production finally ceased in 1990.

Morogoro shoe factory was owned by the Tanzania goverment, a goverment that had failed at every big and small initiative since independence.

Hayo sio maneno yangu.
 
Zakumi,
Mbona unakuwa specialist wa kutoelewa mambo. Kwa taarifa yako, kiwanda cha zana za kilimo Mbeya (ZZK) hakikusaidia chochote kile. Wakazi wa mkoa wa Mbeya na Rukwa walikuwa ni mastadi katika kufua chuma na zana zao za kilimo zilikuwa imara kuliko zile za ZZK.
Duh wewe mkali sana! yaani wananchi wa Mbeya walikuwa mastadi wa kufua vyuma!.. sasa hiyo mkuu wangu imemsaidia nini mkulima wa Mara ambaye kwa fahamu zangu zijawahi kununua jembe lilotengenezwa na mwananchi wa Mbeya na Rukwa..ila nakumbuka kutumia zana za ZZK..
Nadhani muhimu tuwe na picha kubwa ya kile anachozungumzia andindile, bado Nyerere ataendelea kubeba mzigo wake wa lawama lakini tunapofikia kusema mambo ambayo hayakuweza kabisa kumsaidia mwananchi kisha wewe tena una hoji viwanda vile vilimsaidia vipi mwananchi inanipa shida mkuu wangu..nilitegemea wewe utatueleza tofauti na viwanda hivyo ktk kutusaidia wananchi iwe kwa zana au ajira..

Kweli kabisa nakubaliana na point yako ulosema kuhusu ujenzi wa elimu ya msingi tukasahau kwamba safari ya elimu haikomei darasa la saba..Binafsi naamini kabisa kwamba tatizo lilikuwa katikati pale kati ya darasa la saba kuingia sekondari lakini pamoja na hayo yote tumeona hapo nyuma ndugu yetu Genda alivyotueleza juhudi za mwalimu ktk kubadilisha mfumo wa elimu toka ule wa mkoloni... hakika zilikuwa jitihada kubwa sana, isipokuwa tu naweza kujiuliza leo kama zilikuwa na manufaa zaidi kwa wananchi walio wengi ambao safari yao ndefu ktk kupata elimu ilikomea darasa la saba..

Na kwa bahati nzuri sana siwezi kumlaumu yeye pekee kwani naelewa fika kwamba asilimia 7 ya wanafunzi kuingia sekondary iliendelea hadi kipindi cha Mkapa mwanzoni ikipanda kwa points za asilimia moja kila mwaka..Kisha hata tulipoweza kuongeza idadi ya shule za sekondary bado tulifikiwa na tatizo la fedha.. Walimu wengi sana walikuwa hawajalipwa mishahara yao toka Mwinyi alipoondoka, mashule hayana bajeti ya mwaka isipokuwa kukatiwa kidogo kinacholpatikana..Nadhani ndio sababu iliyomsukuma Mkapa na utawala wake kuanzisha karo za shule toka Primary ili shule hizi ziweze kukusanya fedha kujiendesha lakini tena tukakumbwa na tatizo la uwezo wa wananchi kulipa karo za shule wakati wenyewe pato lao la mwaka ni chini kabisa..

Mimi nadhani hatuna haja sana ya kumlaumu mwalimu ktk elimu kwani sisi wote tunaolaumu sasa hivi ngoma ndio imefikia makumi ya mwisho yaani tupo over 50, hivyo yote hii ni refrection ya machungu yetu..Hata ukienda Kenya wapo watu wengi sana wanaolaumu utawala wa Kenyatta na mfumo wa elimu nchi hiyo..
Yes, kuna wasomi wengi sana Kenya kuliko Tanzania miaka yote lakini pia kuna mbumbumbu wengi sana Kenya kuliko Tanzania miaka yote.. Sidhani kama idadi ya wasomi Kenya inafikia hata asilimia 10 ya population yao, hivyo ni nchi maskini inayoongozwa bado Kimaskini kama sisi. Nchi yoyote yenye wajinga (wasioelimika)wengi kwa asilimia kubwa kiasi hicho haiwezi kuendelea kwa kasi...na kibaya zaidi ni kwamba sisi sote tunasoma elimu ya academic ambayo imeandikwa na mkoloni kwa ajili ya kumtumikia Mkoloni.. hatupewi elimu inayolingana na mazingira yetu au hali ya Kiuchumi duniani. hatujiandai kwa lolote zaidi ya kuiga kinachofanyika Ulaya kwa mfano wakati mgumu wa kiuchumi kama huu nchi zote duniani zinatumia wakati huu kujenga misingi ya elimu, afya, miundombinu na viwanda kulingana na mahitaji ya sasa na yale ambayo yanahusiana sana na Global warming..lakini sisi tunashindwa tuanzie wapi kwani elimu yetu inakomea tu kutazama matatizo ya uchumi Ulaya..Hatufahamu tunapigwa na nini ikiwa haikusemwa kitabuni..

Tulishindwa kilimo cha umwagiliaji kiasi kwamba imekuwa ni sehemu ndogo sana ya Taifa letu inatumia kilimo hicho..Tumeshindwa kueneza maji safi nchi nzima, tumeshindwa kueneza Umeme nchi nzima, tumeshindwa kuwaelimisha watoto wetu toka vidudu hadi chuo kikuu kwa hesabu inayolingana na walioshinda hata kwa makisio tu. Tunashindwa kujenga Hospital kulingana na takwimu zinazotuwezesha kuwahudumia wananchi.. leo hii Hospital moja inategemea kuhudumia wananchi wagonjwa zaidi ya 1,000 kwa siku wakati hesabu ya madaktari haikubaliani na masaa ya kazi kuhudumia kila mgonjwa.. Kila unapotazama tumeshindwa.....tumeshindwa!..Ni aibu tupu ndugu zangu ni aibu..

Kumtafuta mchawi mmoja kati ya kundi la wanga ni uzushi mtupu kwani mchawi hawezi kutafutwa na mtu wa kawaida isipokuwa mganga.. na kwa tafsiri yangu mganga ni mchawi tu, tofauti yao ni moja tu mganga anaujua uchawi isipokuwa ha practice uchawi. Lakini inapobidi kujihami hugeuka kuwa mchwi na mara nyingi mwepesi wa kuvaa ngozi ya chui...kama yule mganga aliyedai kumshusha mchawi na Mkeka wake Kigamboni kumbe ilikuwa deal apate kuvutia soko la biashara zake..
Hii ndio hila inayotumiwa sana na viongozi wa leo hii kutafuta mchawi.. Nyerere amekuwa sababu ya kila ulozi unaoonekana wakati wanaoingia uwanjani na hirizi ni wao wenyewe..
hatuna sababu ya kuwa nyuma ktk elimu leo hii..misingi alojenga mwalimu itabakia kumbukumbu tu, hata kama ni magofu kinachotakiwa leo hii ni kujiuliza sisi wenyewe kama kweli tunaijenga nchi yetu kwa elimu inayotolewa leo au tunabomoa kwani miaka 20 ijayo watoto wetu watakuwa wakizungumzia elimu ktk utawala wa Kikwete...
 
Ndugu Zukum mi sikatai, suala la kuanzisha viwanda is one issue na suala la kuhakikisha kuwa viwanda vinafanya kazi kwa ufanisi nilingine. Hivyo kushuka kwa output sio kuwa ndio unakuwa mwisho wa kujaribu kuboresha hivyo viwanda. Kuhusu research sijui unataka nifanye research ipi maana nimekwambia viwanda viliajiri watu Mbeya mjini hiyo ni fact, hao watu walikuwa potential markert thats a fact, viwanda vimekufa thats also a fact, na kuwa watu walioajiriwa walipoteza kazi baada ya viwanda kufa hiyo nayo ni fact. Na sababu mojawapo nikukosekana kwa ufanisi kama data zako ulizozitoa zinavyoeleza. Sasa hapo ninaloongea na unaloongea tofauti ipo wapi?
 
Ndugu Zukum mi sikatai, suala la kuanzisha viwanda is one issue na suala la kuhakikisha kuwa viwanda vinafanya kazi kwa ufanisi nilingine. Hivyo kushuka kwa output sio kuwa ndio unakuwa mwisho wa kujaribu kuboresha hivyo viwanda. Kuhusu research sijui unataka nifanye research ipi maana nimekwambia viwanda viliajiri watu Mbeya mjini hiyo ni fact, hao watu walikuwa potential markert thats a fact, viwanda vimekufa thats also a fact, na kuwa watu walioajiriwa walipoteza kazi baada ya viwanda kufa hiyo nayo ni fact. Na sababu mojawapo nikukosekana kwa ufanisi kama data zako ulizozitoa zinavyoeleza. Sasa hapo ninaloongea na unaloongea tofauti ipo wapi?

Nadhani inabidi urudi kusoma posti yangu ya mwisho. Mtaalamu anasema kuwa Ongezeko la viwanda ambalo lilitokana na Tanzania kununua mitambo na utaalamu lilikuwa asilimia 8 kwa mwaka kuanzia 1976-1990.

Wakati huohuo uzalishaji kwa kila mfanyakazi ulikuwa unashuka kwa asilimia 3.4.

Wewe unazidi kutoa takwimu za watu kuajiriwa. Watu hawapewi ajira kulipwa mishahara. Wanapewa ajira kulipwa mishahara na wao kufanya kazi.

Na nikakupa mfano wa kiwanda cha viatu Morogoro.

Ninaposema fanya research leta data. Data nilizokupa ni za mchumi kutoka Benki ya Dunia.
 
Sasa tatizo lilikuwa kwa hao walioajiriwa kuhakikisha kuwa ufanisi unakuwepo au tatizo lilikuwa ni kiwanda kilicho ajiri?
 
Zakumi,

Duh wewe mkali sana! yaani wananchi wa Mbeya walikuwa mastadi wa kufua vyuma!.. sasa hiyo mkuu wangu imemsaidia nini mkulima wa Mara ambaye kwa fahamu zangu zijawahi kununua jembe lilotengenezwa na mwananchi wa Mbeya na Rukwa..ila nakumbuka kutumia zana za ZZK..
Nadhani muhimu tuwe na picha kubwa ya kile anachozungumzia andindile, bado Nyerere ataendelea kubeba mzigo wake wa lawama lakini tunapofikia kusema mambo ambayo hayakuweza kabisa kumsaidia mwananchi kisha wewe tena una hoji viwanda vile vilimsaidia vipi mwananchi inanipa shida mkuu wangu..nilitegemea wewe utatueleza tofauti na viwanda hivyo ktk kutusaidia wananchi iwe kwa zana au ajira..

Kweli kabisa nakubaliana na point yako ulosema kuhusu ujenzi wa elimu ya msingi tukasahau kwamba safari ya elimu haikomei darasa la saba..Binafsi naamini kabisa kwamba tatizo lilikuwa katikati pale kati ya darasa la saba kuingia sekondari lakini pamoja na hayo yote tumeona hapo nyuma ndugu yetu Genda alivyotueleza juhudi za mwalimu ktk kubadilisha mfumo wa elimu toka ule wa mkoloni... hakika zilikuwa jitihada kubwa sana, isipokuwa tu naweza kujiuliza leo kama zilikuwa na manufaa zaidi kwa wananchi walio wengi ambao safari yao ndefu ktk kupata elimu ilikomea darasa la saba..

Na kwa bahati nzuri sana siwezi kumlaumu yeye pekee kwani naelewa fika kwamba asilimia 7 ya wanafunzi kuingia sekondary iliendelea hadi kipindi cha Mkapa mwanzoni ikipanda kwa points za asilimia moja kila mwaka..Kisha hata tulipoweza kuongeza idadi ya shule za sekondary bado tulifikiwa na tatizo la fedha.. Walimu wengi sana walikuwa hawajalipwa mishahara yao toka Mwinyi alipoondoka, mashule hayana bajeti ya mwaka isipokuwa kukatiwa kidogo kinacholpatikana..Nadhani ndio sababu iliyomsukuma Mkapa na utawala wake kuanzisha karo za shule toka Primary ili shule hizi ziweze kukusanya fedha kujiendesha lakini tena tukakumbwa na tatizo la uwezo wa wananchi kulipa karo za shule wakati wenyewe pato lao la mwaka ni chini kabisa..

Mimi nadhani hatuna haja sana ya kumlaumu mwalimu ktk elimu kwani sisi wote tunaolaumu sasa hivi ngoma ndio imefikia makumi ya mwisho yaani tupo over 50, hivyo yote hii ni refrection ya machungu yetu..Hata ukienda Kenya wapo watu wengi sana wanaolaumu utawala wa Kenyatta na mfumo wa elimu nchi hiyo..
Yes, kuna wasomi wengi sana Kenya kuliko Tanzania miaka yote lakini pia kuna mbumbumbu wengi sana Kenya kuliko Tanzania miaka yote.. Sidhani kama idadi ya wasomi Kenya inafikia hata asilimia 10 ya population yao, hivyo ni nchi maskini inayoongozwa bado Kimaskini kama sisi. Nchi yoyote yenye wajinga (wasioelimika)wengi kwa asilimia kubwa kiasi hicho haiwezi kuendelea kwa kasi...na kibaya zaidi ni kwamba sisi sote tunasoma elimu ya academic ambayo imeandikwa na mkoloni kwa ajili ya kumtumikia Mkoloni.. hatupewi elimu inayolingana na mazingira yetu au hali ya Kiuchumi duniani. hatujiandai kwa lolote zaidi ya kuiga kinachofanyika Ulaya kwa mfano wakati mgumu wa kiuchumi kama huu nchi zote duniani zinatumia wakati huu kujenga misingi ya elimu, afya, miundombinu na viwanda kulingana na mahitaji ya sasa na yale ambayo yanahusiana sana na Global warming..lakini sisi tunashindwa tuanzie wapi kwani elimu yetu inakomea tu kutazama matatizo ya uchumi Ulaya..Hatufahamu tunapigwa na nini ikiwa haikusemwa kitabuni..

Tulishindwa kilimo cha umwagiliaji kiasi kwamba imekuwa ni sehemu ndogo sana ya Taifa letu inatumia kilimo hicho..Tumeshindwa kueneza maji safi nchi nzima, tumeshindwa kueneza Umeme nchi nzima, tumeshindwa kuwaelimisha watoto wetu toka vidudu hadi chuo kikuu kwa hesabu inayolingana na walioshinda hata kwa makisio tu. Tunashindwa kujenga Hospital kulingana na takwimu zinazotuwezesha kuwahudumia wananchi.. leo hii Hospital moja inategemea kuhudumia wananchi wagonjwa zaidi ya 1,000 kwa siku wakati hesabu ya madaktari haikubaliani na masaa ya kazi kuhudumia kila mgonjwa.. Kila unapotazama tumeshindwa.....tumeshindwa!..Ni aibu tupu ndugu zangu ni aibu..

Kumtafuta mchawi mmoja kati ya kundi la wanga ni uzushi mtupu kwani mchawi hawezi kutafutwa na mtu wa kawaida isipokuwa mganga.. na kwa tafsiri yangu mganga ni mchawi tu, tofauti yao ni moja tu mganga anaujua uchawi isipokuwa ha practice uchawi. Lakini inapobidi kujihami hugeuka kuwa mchwi na mara nyingi mwepesi wa kuvaa ngozi ya chui...kama yule mganga aliyedai kumshusha mchawi na Mkeka wake Kigamboni kumbe ilikuwa deal apate kuvutia soko la biashara zake..
Hii ndio hila inayotumiwa sana na viongozi wa leo hii kutafuta mchawi.. Nyerere amekuwa sababu ya kila ulozi unaoonekana wakati wanaoingia uwanjani na hirizi ni wao wenyewe..
hatuna sababu ya kuwa nyuma ktk elimu leo hii..misingi alojenga mwalimu itabakia kumbukumbu tu, hata kama ni magofu kinachotakiwa leo hii ni kujiuliza sisi wenyewe kama kweli tunaijenga nchi yetu kwa elimu inayotolewa leo au tunabomoa kwani miaka 20 ijayo watoto wetu watakuwa wakizungumzia elimu ktk utawala wa Kikwete...


Sielewi unataka kusema nini. Hapo juu nimetoa data kutoka kwa William Easterly. Mtaalamu wa Bank ya dunia.

Naomba usome hayo tena.

Capital worker in Tanzania's manufacturing sector grew at 8 percent per annual over the period 1976 to 1990, but manufacturing output per worker fell at 3.4 percent per annum over the same period.

The World Bank helped finance the Morogoro Shoe Factory in Tanzania in the 1970s. This show factory had labor, machinery, and the latest in shoe-making technology. It had everything except shoes. It never produced more than 4 percent of its installed capacity. The plant which had planned to supply the entire Tanzanian shoe market and then export three-quarters of its production shoes to Europe, never exported a single shoe. The plant was not well designed for Tanzania's climate; it had aluminum walls and no ventilation system. The production finally ceased in 1990.


Morogoro shoe factory was owned by the Tanzania goverment, a goverment that had failed at every big and small initiative since independence.
 
Sasa tatizo lilikuwa kwa hao walioajiriwa kuhakikisha kuwa ufanisi unakuwepo au tatizo lilikuwa ni kiwanda kilicho ajiri?

Morogoro shoe factory was owned by the Tanzania goverment, a goverment that had failed at every big and small initiative since independence. Period, end of story.
 
Morogoro shoe factory was owned by the Tanzania goverment, a goverment that had failed at every big and small initiative since independence. Period, end of story.
Yawezekana kilishindwa kupaform kwa sababu ya ufusadi si unajua Watanzania wanavyo jimirikisha miradi ya umma utadhani yao?
 
Back
Top Bottom