Elections 2010 Kikwete aahidi usafiri wa treni Dar

Watanzania tumekuwa wepesi mno kurithika na Ahadi zisizotekelezeka za hawa viongozi wetu wasio makini.

Mwezi July/2010 nilibahatika kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Pili wa "Tanzanian Diaspora in Ameica (DICOTA) uliofanyika Jijini Minneapolis - Minnesota,Pamoja na mambo mengine kulikuwa na Mada iliyozungumzia kirefu kuhusu Tatizo hili la Usafiri katika Jiji la Dar-Es-Salaam ,Athari zake Kiuchumi na namna ya kupunguza na hatimaye kuondoa kabisa tatizo hilo,Mada hiyo iliyokuwa na ushawishi mkubwa iliendeshwa na Pro.L.Meekisho (professor of Mechanical Engineering,Portland State University) na Prof.Primus Mtenga (Civil Engineering,Florida A&M University).Katika Majadiliano ya kuona kiini cha cha tatizo na namna gani serikali kwa kutumia mipango ya muda mfupi na mrefu kuondoa Tatizo hilo ilibidi Katibu Mkuu ofisi ya Rais Bwana Philemon Luhanjo kutolea maelezo.Katika maelezo ya Katibu Mkuu ambaye pia ni Msaidizi wa kwanza wa Rais na Katibu wa Baraza la Mawaziri,alisema njia za muda za kutatua Tatizo hilo ni pamoja na kufunga baadhi ya barabara wakati wa kazi na kufikiri kuzuia Private Public Transport kama Dalala na Bajaji kuingia Mjini.

Baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo walionyesha kutoridhishwa na njia hizo. Mapendekezo ya prof.Meekisho ilikuwa ni pamoja na kuhamisha baadhi ya huduma nyingine za mawizara na kuzipeleka katika miji midogo ya Kibaha,Bagamoyo na Kisarawe,hali hiyo itakuza Miji hiyo ya karibu kwa kuongeza Ajira,kuboresha hali ya maisha ya watu na kuboresha Miundombinu....Utatuzi wa Muda wa hali hiyo Jijini Prof alipendekeza kuwepo na usafiri wa Treni kwa kutumia Reli ya kati na Tazara ambazo kwa sasa zote hazitumiki ipasavyo. 1);Tazara itasaidia kupunguza Mlundikano wa watu wa Gombo la Mboto,Tabata,Temeke,Tandika na Uwanja wa Ndege,Kukiwepo na utaratibu Mzuri Reli ya Tazara inayoishia Kurasini itapunguza sana Mlundikano wa magari kwa njia za Uhuru,Kilwa na Nyerere. 2);Reli ya kati pia itatumika ktk mpango huo,Reli hiyo itaunganisha Jiji na maeneo mengi,kwa sababu kuna sehemu Reli hiyo imepelekwa kwenye Viwanda vya Urafiki (zamani) na saruji Wazo,kwa maana hiyo ikikarabatiwa vyema itasaidia idadi kubwa ya watu wa Ubungo,Kawe,Mwenge,Kimara na Magomeni na kwa hali hiyo itapunguza mlundikano wa magari ktk barabara za Morogoro,Ali Hassan Mwinyi,na Bagamoyo na kwa ziada kuwepo na Usafiri rahisi wa majini kutoka Ferry mpaka Jangwani Beach,ambao utatoa huduma kwa watu wa Jangwani Beach,Mbezi,Masaki na hatimaye Oysterbay.

Kwa maelezo ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais ni kwamba World Bank wapo tayari kutoa pesa,wanachoihitaji wao ni mipango makini ya kuondoka Mlundikano huo ambao mahali pa dk 30 inachukua masaa 3 - 4 kwa muda wa asubuhi na bada ya masaa ya kazi.
Katibu Luhanjo alisisitiza wazi kuwa tusiwasikilize sana wanasiasa kwa madai kwamba kipindi hichi cha Uchaguzi Ndugu zetu wanasiasa wanasema chochote wanachoona kitawapa kura....alisema hayo baada ya kuambiwa kuwa "Waziri Membe ameahidi Serikali itaamua suala la Dualcitizen kabla ya November".Bwana Luhanjo alidai kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi,na hiyo Novemba aliyoisema Mh.Membe ni Wakati ambao Rais Mteuliwa atakuwa anaunda Serikali yake,Bw.Luhanjo alisema msitegemee suala la Dual Citizenship kujadiliwa na Baraza la Mawaziri mwaka huu,kwa sababu sio priority kwa wakati huu baada ya uchaguzi.

Sasa Tunapaswa kuangalia maneno ya Bwana Kikwete ktk wakati huu karibu na Uchaguzi,Hii miradi ya magari ya kutumia mawese (mafuta nafuu),na flyovers za fire,Chang'ombe,Magomeni na Ubungo ni maneno ya kutafutia Kura!
 
katika kipindi cha miaka mitano ijayo, serikali inategema kujenga barabara itakayounganisha Dar es Salaama na visiwa vya Zanzibar na Pemba. Kutakuwa na barabara ya kwenda mwezini kutokea Dodoma!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Naona jamaa wanauliza ati njia ni wapi? Reli kuanzia Central Police katikati ya jiji mpaka Ubungo ipo siku nyingi tu. Ni namna ya kuanza kuitumia. Siyo kwamba itajengwa mpya.
Reli kama ile matreni ya kisasa hayawezi kupita..

Wait a minute, kweli sasa naanza kuamini kwamba mitanzania unaeza kuishawishi na ikakubali kwamba kuna chocolate kwene kila box!
 
Rais Jakaya Kikwete amesisitiza kuwa serikali itajenga barabara za juu kwenye makutano ya njia na kuruhusu treni kusafirisha abiria katika jiji la Dar es Salaam ili kumaliza msongamano wa magari.
Kadhalika, serikali imesema itajenga barabara za zege kwa thamani ya Sh. trilioni 7.3 kwa ajili ya kupitisha magari yaendayo kasi kwa lengo la kukabiliana na msongamano wa magari.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam alipozindua awamu ya kwanza ya ujenzi wa barabara za zege yenye urefu wa kilomita 20.9 kuanzia Kivukoni hadi Kimara.
Alisema barabara za juu zitajengwa katika maeneo ya makutano ya Tazara, Ubungo, Chang'ombe, Kamata, Magomeni na Faya.


Aliongeza kuwa Jiji la Dar es Salaam kila siku linapokea watu 50 wanaokuja kuishi na kuongeza kuwa bila kuweka mipango ya kumaliza msongamano baadaye hali itakuwa mbaya zaidi.
Kwa upande wa barabara za kawaida zinazotarajiwa kujengwa ni Morocco -Tegeta, Tankibovu - Goba, Tegeta - Mbezi Shamba kupitia Goba na Bandari hadi Gerezani.
Aliitaka sekta binafsi kujitokeza na kununua magari yaendayo kasi ili yatumike kusafirisha abiria kupitia barabara mpya za zege zitakazojengwa.


Aliwataka Wakandarasi watakaopewa kazi ya ujenzi wa barabara hizo kuhakikisha wanazijenga kwa kiwango cha hali ya juu badala ya kulipua kazi.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi yaendayo haraka (DART), Cosmas Takule, alisema awamu ya kwanza ya ujenzi huo itagharimu zaidi ya Sh. bilioni 200.

CHANZO: NIPASHE
 
Tatizo kubwa hapa si wingi wa magari au ufinyu wa barabara. Tatizo ni kurundika huduma zote muhimu mahali pamoja na kufanya watu wengi waelekee upande mmoja kwa wakati mmoja. Jawabu ni kuendeleza sehemu nyingine za jiji na kubana ujenzi katikati ya jiji. Kitu kingine ambacho kingeweza kusaidia ni kwa mashirika na vyombo vya serikali kuwa na flexible times za kuanza kufanya kazi. Si lazima wote wafungue ofisi kati ya saa moja na mbili asubuhi. Hii biashara ya treni haitasaidia sana hasa kwa kutumia treni tulizkuwa nazo. Hii ni kutokana na ongezeko la pollution kuakosababishwa na frequency ya hizo treni, maana ili ifanye kazi ni lazima hizo treni zipishane si zaidi ya saa moja, na matreni yenyewe ya dizeli! Na hii frequency bila shaka itaongeza mlundikano kwenye railway crossings. Tusipende majibu mepesi kwa maswali magumu.

Amandla.....
 
... Kitu kingine ambacho kingeweza kusaidia ni kwa mashirika na vyombo vya serikali kuwa na flexible times za kuanza kufanya kazi. Si lazima wote wafungue ofisi kati ya saa moja na mbili asubuhi.
.
Kaka, naomba tusaidie mfano wa mji duniani ambapo mashirika na serikali zinafungua ofisi saa tisa alasiri au saa sita usiku.
 
Zimeongezeka ahadi mbili jana:

(1) Kujenga bandari mpya Tanga

(2) Kujenga reli toka Tanga hadi Musoma.

Hasa huyu waziri Mkumbwa anatoa ahadi mpya kila leo. Naona wameangalia mji wa Tanga ulivyodorora wakaona wasiposema kitu hawatapata kura.

Maneno yawe machache, vitendo ndio viwe vingi!
 
Kaka, naomba tusaidie mfano wa mji duniani ambapo mashirika na serikali zinafungua ofisi saa tisa alasiri au saa sita usiku.

Aliyesema nani ofisi zifunguliwe saa tisa alasiri au saa sita usiku? Huu si ndio ubishi usio na maana? Nchi nyingi duniani, hasa za magharibi, ( mfano wa nchi zinazofanya hivi sikutolei. Amini unachotaka.) zina flexible time, mathlani, mtu anaruhusiwa kuingia kazini muda wowote kabla ya saa 3 asubuhi ili mradi afanye masaa anayopaswa kufanya kwa siku. Mashirika mengine binafsi yanaruhusu mfanyakazi kujipangia muda atakaoanza kazi ili mradi anatimiza muda anaopaswa kufanya na bila kuathiri utendaji. Ni wazi kuwa flexibility hii inategemea vile vile aina ya kazi ambayo mtu anafanya. Sasa kama unataka kuleta ubishi, kwa ajili ya kubisha tu, hiyo ni juu yako.

Amandla......
 
Mkuu huwezi kuamini, kuna ramani ya jiji inaonyesha hizo njia lakini kote kulishauzwa na kuna nyumba juu yake.

Ni kweli kwenye master plan ipo haswaa...kulikuwa na route ya UBUNGO - CHUO KIKUU - CHANGANYIKENI- MBEZI-SALSALA- TEGETA- WAZO HILL..kuna jamaa wa reli waliniambia kuwa walifanya utafiti wakagundua kuwa route yote hiyo watu wameshajenga nyumba juu yake...LAZIMA SERIKALI IZIBOMOE ...ili kuweza kulink mfumo wa reli Dar na maeneo ya viwanda TEGETA na bagamoyo..napendekeza kabla JK hajamaliza term yake aendeshe hilo zowezi...na kati ya ahadi rahisi kutekelezeka ni hii...mwanzoni mwa miaka ya 2000 walipitishaga behewa za abiria kama wiki ..nadhani walikuwa wanatafiti..mainly ile line ni kwa ajili ya viwanda...lakini ili kuondoa kero na ahadi itabidi kufanya yafuatayo:-
1]kujenga vituo vya hizo treni .....na mechanism ya ticketing
2]kuikarabati reli yenyewe
3]kujenga bridge kwenye road/rail crossing ie mabibo/relini tbt/relini/buguruni/ilala/kamata/pugu road etc ili kuondoa uwezekano wa ajali na misongamano..mfano wa bridge ya reli ni kama ile pale kabla ya shoprite kamata au pale BP ambapo reli zimepita kwa chini ...la sivyo we will experience accidents daily....
2]in the later stage ni lazima kuwe na parallel line ili kuweka uwezekano wa kupishana route badala ya mfumo utakaoanza amabao utakuwa kama wa basi la kijiji yaani treni ikiondoka ubungo hadi ifike posta ndio irudi.....

Tukiwa na mfumo wa treni kwa mtandao ambao tunao hapa dar tutakuwa na uwezo wa kuwa na route zifuataza
1] ubungo-mabibo-relini-relini-vingunguti-buguruni-kamata-posta\
2]pugu-mbagala-vingunguti-buguruni-pugu rd -temeke [near national stadium

hizi route kwa kuanzia zinatosha kusaidiana na route ya DART Ya mbezi kimara-ubungo-manzese-to feri...

la kuzingatia ni lazima kwa treni na DART watumie mfumo wa tiketi za msimu ...kama smart card ...na wahamasishe wanafunzi wote wapewe na wazazi ,wafanyakazi maofisini na wananchi wengine.....kama wakiweka mfumo kwa TT ndio wanaokusanya pesa basi miradi hiyo itajeuka miradi ya watu......
 
Hizi ni nyongeza tu ya ngonjera nyingi tutakazozisikia wakati tukielekea uchaguzi wa mwezi octoba
 
...Huu si ndio ubishi usio na maana? ... mfano wa nchi zinazofanya hivi sikutolei. Amini unachotaka.... Sasa kama unataka kuleta ubishi, kwa ajili ya kubisha tu, hiyo ni juu yako.

Unaulizwa swali unawaka kaka, nilichobisha hapo nini?

Watu wetu hata ambao ungewaona wana upeo ukichimba kidogo unakuta hawajazaoa mijadala ya dhati, unadhani ni ubishi. Mtu kauliza kitu unasema swali bishi, mara "sikwambii mji, nifikirie unavyotaka," ya nini yote hayo?

Na mtu akitofautiana haina maana mbishi. Mara nyingi mtu anaongea kutokana na ufarisi wake yeye, anavyoona yeye, na watu wanatofautiana fesheni ya kudahili, kuna wengine ni "ndio bwana, ahsante," wengine wanadai vigezo, mifano, n.k., si ubishi. Tuelewane. Kama "ubishi" ufuatao:

Dar-es-Salaam, sijui mji uliko, Dar-es-Salaam, biashara za wahindi mjini na Wapemba Kariakoo hukuti mtu kazini kabla ya saa nne. Serikalini, ofisi haijai na kazi haikolei kabla ya saa tatu, tatu unusu, uzoefu wangu mimi, nilikopita mimi. Hawapo saa moja, saa moja hadi saa tatu ni chapati, vocha na Shigongo, hawa hawabanwi, wangeweza kuja saa nne.

Na katika hali ya maadili finyu ya kazi kama hayo, ukimpa mtu unyumbufu wa kumwambia ajijie anavyotaka almuradi zitinge saa 8, huyu atajichukulia livu, kumbuka msimamizi wake nae yale yale. Ndio mazingira ya kwetu kwa kiasi kikubwa. Kwa hiyo unaweza ukatatua foleni, ukaparaganyisha uchumi.

Magharibi huko naamini zipo ratiba za aina uliyosema, japo sijabahatika kukutana na mtu anasema kazini kwake, manamba ama mtaalam, anaambiwa jijie unavyotaka almuradi usiathiri utendaji na gonga saa 8. Inawezekana ni kwa vile ni kitu nadra kupindukia, kilichooneka kinapelea ufanisi.
 
Unaulizwa swali unawaka kaka, nilichobisha hapo nini?

Watu wetu hata ambao ungewaona wana upeo ukichimba kidogo unakuta hawajazaoa mijadala ya dhati, unadhani ni ubishi. Mtu kauliza kitu unasema swali bishi, mara "sikwambii mji, nifikirie unavyotaka," ya nini yote hayo?

Na mtu akitofautiana haina maana mbishi. Mara nyingi mtu anaongea kutokana na ufarisi wake yeye, anavyoona yeye, na watu wanatofautiana fesheni ya kudahili, kuna wengine ni "ndio bwana, ahsante," wengine wanadai vigezo, mifano, n.k., si ubishi. Tuelewane. Kama "ubishi" ufuatao:

Dar-es-Salaam, sijui mji uliko, Dar-es-Salaam, biashara za wahindi mjini na Wapemba Kariakoo hukuti mtu kazini kabla ya saa nne. Serikalini, ofisi haijai na kazi haikolei kabla ya saa tatu, tatu unusu, uzoefu wangu mimi, nilikopita mimi. Hawapo saa moja, saa moja hadi saa tatu ni chapati, vocha na Shigongo, hawa hawabanwi, wangeweza kuja saa nne.

Na katika hali ya maadili finyu ya kazi kama hayo, ukimpa mtu unyumbufu wa kumwambia ajijie anavyotaka almuradi zitinge saa 8, huyu atajichukulia livu, kumbuka msimamizi wake nae yale yale. Ndio mazingira ya kwetu kwa kiasi kikubwa. Kwa hiyo unaweza ukatatua foleni, ukaparaganyisha uchumi.

Magharibi huko naamini zipo ratiba za aina uliyosema, japo sijabahatika kukutana na mtu anasema kazini kwake, manamba ama mtaalam, anaambiwa jijie unavyotaka almuradi usiathiri utendaji na gonga saa 8. Inawezekana ni kwa vile ni kitu nadra kupindukia, kilichooneka kinapelea ufanisi.

Mjadala si kumpachikia mwenzako kitu ambacho hajasema. Kufanya hivyo ni ubishi. Ungeuliza wapi wana flexible time bila kuongeza hiyo kejeli ya saa unazojua wewe, ningekujibu.

Mjadala ni hiyo hoja uliyoileta ya kuwa kutokana na tabia na mwenendo wa utendaji kazi wetu hata ukiwapa watu flexibility haitasaidia kitu maana hata sasa hivi ndiyo wakati wanaoingia kazini. Lakini hauoni kuwa unajipinga maana foleni inabanana kati ya 1 asubuhi mpaka saa 2 na jioni kuanzia saa 10 hadi saa moja. Hii kwangu mimi inaashiria kuwa inatokana na watu wengi kutaka kuingia kazini. Ofisi za serikali miaka nenda rudi zinafunguliwa kati ya saa 1 na nusu na saa mbili. Wengi wa wafanya kazi wanafika katika muda huu. Sasa kwa vile mada hii inazungumzia msongamano wa magari, wanachofanya wanapofika kazini haituhusu. Tunachozungumzia hapa ni namna ya kuhakikisha kuwa wanafika kazini katika wakati muafaka bila kutumia muda mwingi njiani. Kama watasogoa, wanauza vitumbua, wanauza vocha, wanasoma magazeti, wanaenda kula chipsi na chapati n.k. hayo ni masuala mengine. Tunachotaka ni kuwa wasiwe barabarani wakati huo, period.

Hao wafanyabiashara unaowazungumzia nao wanachangia katika msongamano. Maduka katikati ya mji yanafunguliwa saa ambazo watu wanatakiwa kuwa maofisini. Maduka mengi yanafungwa ifikapo saa 12 jioni na hivyo kuchangia katika msongamano.

Magharibi kuna watu wanafanyia kazi nyumbani na wameajiriwa na mashirika makubwa. Upande wa akademia, watafiti wengine wanafanyia kazi nyumbani na cha msingi ni kuwa watimize muda unaotakiwa, hakuna anayewauliza walianza kazi saa ngapi na walimaliza saa ngapi. Ni kuaminiana tu.

Amandla........
 
Mkwele kwa kujilipua tuu hajambo,ivi speech zake huwa zaandaliwa au huwa anajisikia tuu kuongeaaaaaaaaaa.
Wapinzani kusanyeni ahadi hasa za kati ya 2005 mpaka 2010 mtakuta ni vituko tupu.
 
hata sijaisoma hiyo thread kwani najua ni yale yale .....ahadi nyingi sana ananikumbusha kitabu cha kusadikika..
 


Katika hatua hiyo Rais Kikwete alizindua awamu ya kwanza ya ujenzi wa Miundombinu ya Mradi wa Mabasi yaendayo kasi (DART) katika jiji la Dar es Salaam ambao utanatarajiwa kukamilika mwaka 2012.

Ujenzi huo unaoanzia eneo la feri na kuishia Kimara ambapo aliwataka wamiliki wa mabasi hayo makubwa kutumia gesi asilia ili kuondokana na uharibifu wa mazingira.

Mradi huo unaotekelezwa katika awamu sita, umefadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) hadi kukamilika kwake utagharimu kiasi cha sh trilioni 7.3.


Source: Tanzania Daima




Hawa wanauhakika ni 7.3 Trl Shillings? Mbona sources nyingine zinasema tulipokea mkopo wa 190 Million USD kutoka World Bank? They need to do research before typing such news on paper.

Tazama hapa:

http://www-wds.worldbank.org/extern...ginal/510210PROP0P10121September015102009.doc

http://www.tanzaniainvest.com/tanza...a-transport-prepares-project-in-dar-es-salaam
 
tumpe nafasi JK atekele ahadi zake, tutampima akimaliza muda wake, tusiwe negative sana jana

ahadi ni deni, tutamda
 
Back
Top Bottom