Just in: UDSM wafukuzwa

Uamuzi wa wanafunzi kugoma ni uamuzi wa sahihi kabisa. Pia ninaunga mkono kwa wao kuweza kuhusisha mateso wanayopata na kero kadhaa mfano matumizi mabovu yaliyoripotiwa na mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali.

Si sahihi kwa watu kusema wanafunzi wamekosea. Dhana ya mgomo ni wao kushitaki kwa jamii kwa kero zao ambazo serikali haitaki kuzisikia.

Ifahamike kuwa toka sheria namba 9 ya mwaka 2004 itungwe serikali imekuwa ikiikiuka sheria hii makusudi kabisa. Kwa mafano sheria haisemi na wala haitoa mamalka kwa bodi ya HESLB au chombo kingine chochote kusema ni madaraja gani ya watu watasomeshwa kutokana na mkopo wa serikali. Serikali ilikaa na kuamua tu.

Sasa ndio yakaja haya mambo ya asilimia 40 ambayo ni kinyume kabisa na sheria na 9 ya mwaka 2004.

Mimi binafsi nadhani ilikuwa sahihi kwa wanafunzi kugoma. Vilevie ni makosa kwa utawala wa chuo kuwafukuza. Kanuni za chuo (by-laws) zinasema kuwa wanafunzi watatimuliwa, au chuo kufungwa iwapo tu watagoma kwa siku tatu mfululuzo. Hazikufika.

Kwa mimi ambae nimewahi kuwa Kiongozi wa wanafunzi, naanza kuona kuwa ni afadhali ya Prof. Luhanga kuliko huyu wa sasa. Nakumbuka mimi jinsi Luhanga alivyokuwa makini kumaliza migogoro ya wanafunzi. Prof wangu Mukandara nadhani has to learn kutoka aliyemtangulia. Kufukuza wanafunzi haijawahi kuwa sulhisho miaka nenda rudi. Hatujifunzi?

Nadhani katika mijadala ya kitaifa mingi tunayohitaji ni pamoja na huu wa elimu ya juu.
 
George Mason University, Virginia, USA, ada ya mwanafunzi kwa mwaka ni US $.3300. Kima cha chini cha mshahara US $ 6.50. Ikiwa mwanafunzi atafanya kazi mwaka mzima na kusave pesa zote basi anaweza kuwa na akiba ya walau US $ 10000.

Is it true kwamba kila mwanafunzi anapaswa kulipa TShs.2,000,000?? Kiwango hiki wamekipata kwa kuzingatia vigezo gani? Yaani ktk hili la kuchangia masomo, Mtanzania anashindana na mwananchi wa Marekani!!

Baada ya hapo, hebu chunguza mazingira ya elimu[academic & proffesional environment] ya GMU halafu linganisha na yale ya UDSM. Kama mwanafunzi analazimishwa kulipa Tsh 2,000,000[if that is true] halafu anasikiliza mihadhara kwa kuchungulia madirishani, au kwa kusimama kwa vile hakuna madawati, basi serikali inawaibia.

Kwa malipo ya Tshs 2,000,000[US $ 2000] wanafunzi wa UDSM walipaswa kupatiwa maktaba,lecture rooms, maabara, na karakana za kiwango cha juu zaidi ya zilizopo sasa hivi.

http://admissions.gmu.edu/common/UndergraduateTuition.asp
 
Mh. Zitto,

Katika historia ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, VC aliyekuwa makini katika kukiongoza kama an Institution of Higher Learning ni mmoja tu: Professor Mmari akisaidiwa na Professor Msuya.

Professor Luhanga alikuja kujifunza baada ya kuwa amefanya blunders nyingi sana; kinachomsaidia kwenye record ni kwa sababu alikaa pale muda mrefu sana hadi akajifunza. Aliyekuwa bomu kabisa ni Mr. Nicholaus Kuhanga ambaye alikuwa anendesha chuo kile kama shina la Chama. Sikuona uongozi wa waliomtangulia Mzee Kuhanga kama akina Mr. Ibrahimu Kaduma, Mr. Pius Msekwa na Dr. Wilbert Changula, ingawa najua kuwa mmja wao alisimamia ufungwaji wa wanachuo ambao hata mimi nilikuwa mobilized kuandamana na kuunga mkono wakati sijui huko chuo kikuu kuna nini.
 
George Mason University, Virginia, USA, ada ya mwanafunzi kwa mwaka ni US $.3300. Kima cha chini cha mshahara US $ 6.50. Ikiwa mwanafunzi atafanya kazi mwaka mzima na kusave pesa zote basi anaweza kuwa na akiba ya walau US $ 10000.

Is it true kwamba kila mwanafunzi anapaswa kulipa TShs.2,000,000?? Kiwango hiki wamekipata kwa kuzingatia vigezo gani? Yaani ktk hili la kuchangia masomo, Mtanzania anashindana na mwananchi wa Marekani!!

Baada ya hapo, hebu chunguza mazingira ya elimu[academic & proffesional environment] ya GMU halafu linganisha na yale ya UDSM. Kama mwanafunzi analazimishwa kulipa Tsh 2,000,000[if that is true] halafu anasikiliza mihadhara kwa kuchungulia madirishani, au kwa kusimama kwa vile hakuna madawati, basi serikali inawaibia.

Kwa malipo ya Tshs 2,000,000[US $ 2000] wanafunzi wa UDSM walipaswa kupatiwa maktaba,lecture rooms, maabara, na karakana za kiwango cha juu zaidi ya zilizopo sasa hivi.

http://admissions.gmu.edu/common/UndergraduateTuition.asp


Hili ndilo nililosema hapo mwanzo. Huwezi kuendesha chuo cha dar es Salaama kwa kutumia mfumo wa maisha wa marekani kwa vile mazingira yake ni tofauti kabisa. Kudai kuwa mwanafunzi wa UDSM akafanye kazi mitaania ya kumsaidia kulipia gharama za chuo ni ndoto ya alinacha.
 
wakati wa Ibrahim Kaduma "ibra kadu" kulitokea mgomo, na wanafunzi walipigwa na kufurumushwa na FFU mpaka maeneo ya Manzese[soweto.]
 
Tuwe makini sana tunapojaribu kulinganisha vyuo vya nje na vyuo vyetu. Kuna factors nyingi zinazofanya wanafunzi katika vyuo vya nje wasome na kufanya kazi wakati sisi hatuna. Mnaongelea mazingira ambayo kuna mahala ambapo kazi za suluba kwa mfano, ni nyingi kuliko wafanyakazi! Tusiwe kasuku.
 
kuna mambo ambayo yanawezekana endapo yatapangwa vizuri. Hilo la wanafunzi kufanya kazi na kusoma siyo gumu kama inavyofikiriwa. Nina uhakika wanaohusika wakikaa chini na kukuna vichwa wakiangalia mazingira yetu wanaweza kuja kabisa na mfumo ambao utawawezesha wanafunzi kujipatia kiasi kidogo pembeni na kusoma. Hii ina maana ni lazima kuwa na mabadiliko ya mfumo wa ajira.

Ukifiria sana utaona kuwa kuna kizazi cha watanzania ambao hawachangii kiuchumi kwa vile wako shule tu. Hapa nazungumzia hasa wale wa kidato cha 5-6 na wale waliovyuo vikuu. Kama kuna mwanafunzi anaweza kusoma na kufanya kazi kwanini asipewe nafasi hiyo.

Kama tunaweza kuwaiga hawa wazungu mavazi, muziki, kuzungumza n.k we better imitate them kwenye vitu vinavyowafanya wao wawe mahiri!
 
Kuiga is OK,

Tunachoongelea ni kuwa hatujaiga kutengeneza mazingira yanayowezesha hayo yote kufanyika, kwa hiyo siyo haki kwa serikali kuwafukuza watoto hawa kwa msingi huo. Tumekuwa tunaiga mambo nusunusu tu, na hasa hasa serikali inachukua yale mambo yanayoipunguzia wajibu wake kwa umma, na kukwepa yale yanayohitaji serikali kuwajibika kwa umma.
 
Si sahihi kwa watu kusema wanafunzi wamekosea. Dhana ya mgomo ni wao kushitaki kwa jamii kwa kero zao ambazo serikali haitaki kuzisikia.


Sawa kabisa. Lakini ndio nikauliza jana kwa madai ambayo vijana wetu wamekuwa wakiyatoa wanaweza kweli kupata huruma ya wananchi? Nikauliza jana kwa mfano, RTD itakapofafanua kwenye mazungumzo baada ya habari kuwa vijana wanadai kuwa 3,600 kwa siku haitoshi wanataka 6,000/siku, ndugu zetu wa Keko Magurumbasi, Manzese kwa mfuga mbwa, Kibondo, Kahororo, Gumanga, Kibiti, etc. watawahurumia au watawaona ni matapeli?

Kimsingi hapa hakuna anayepinga madai au mgomo wa vijana wetu. Mimi wasiwasi wangu siku zote imekuwa presentation. Ni rahisi kupata support/sympathy ya wananchi ukiyaweka madai kiupana. kwa mfano hapa walipaswa kuwa wanaandamana kupinga concept nzima ya wazazi kuchangishwa kulipia ghrama ya jelimu ya juu. Wangejenga hoja kuonesha kwamba wazazi wao wanabebeshwa mzigo mara tatu, baada ya kulipa kodi na kutoa michango ya kujenga mashule, vyoo vya polisi, n.k.

Naendelea pia kuwalaumu hawa vijana kwa kuchezea nafasi walioipata kuongea na JK Diamond Jubilee. Siku hiyo walipaswa wamsomeshe JK athari za sera za serikali kuhusu elimu ya juu ikiwemo hiyo ya mikopo. Badala ya kujianda vizuri kihoja, wao wakaamua kujianda kwa kupiga pasi magwanda na kofia za CCM. Badala ya kujenga hoja za kisomi, wakaishia kumuimbia JK ngonjera za CCM. Kikwete akawapa tabasamu zito wakajua wameula, kumbe wameliwa.

Matatizo ya elimu yetu ya juu ni mapana kuliko hii mikopo. Vijana wetu waliopo katika vyuo vya elimu ya juu wana nafasi kubwa sana kusaidia kubadilisha hali kwa kutumia nguvu ya hoja na hoja ya nguvu!
 
Hili ndilo nililosema hapo mwanzo. Huwezi kuendesha chuo cha dar es Salaama kwa kutumia mfumo wa maisha wa marekani kwa vile mazingira yake ni tofauti kabisa. Kudai kuwa mwanafunzi wa UDSM akafanye kazi mitaania ya kumsaidia kulipia gharama za chuo ni ndoto ya alinacha.
Hivi hizo kazi za mtaani mnazowataka hao wanafunzi wakafanye ziko wapi?Kuna watu wamemaliza masomo na wana Qualifications zao nzuri na uwezo kikazi na KAZI KUPATA SHIDA,Wachilia kazi hata kibarua na akibahatisha malipo yake ni madogo chini ya dola mia au mia ,hiyo ni kutoka asubuhi hadi jioni ,usafiri wa taabu akirudi nyumbani ni usiku ,sasa sijui kama ni mwanafunzi atahudhuria vipindi muda gani na atasoma muda gani?Bongo Hakuna kazi za masaa au shift kwa makampuni mengi ya watu binafsi.!
 
kichuguu,mwanasiasa,KNKCU,
nina tatizo na hizo fedha za field-work. kwanini wanafunzi wasilipwe na makampuni wanayokwenda kuyafanyia kazi? kwenye nchi za wenzetu field-work/internship huwa ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe kutafuta.

sina uhakika kwa Madaktari na Mafamasia, lakini kwenye field nyingine fieldwork/internship huwa hai-count towards the degree.

Mimi mgogoro wangu ni huo wa kuchangia gharama za masomo ambazo nadhani ni kubwa mno kwa Mtanzania wa kawaida.

Tatizo letu Tanzania ni kwamba viwango vya malipo ya kazi haviendani kabisa na gharama za huduma/maisha. Kama nilivyoonyesha in my previous posting, katika nchi za wenzetu, mwanafunzi anaweza kujilipia Chuo Kikuu kwa ku-serve malipo ya kazi ya kima cha chini.

Kuhusu suala la kuiga, naomba ieleweke kwamba: mwanafunzi anayesoma FULL-TIME hawezi kufanya kazi hata part-time. Ulaya na Marekani, ukiona mwanafunzi anasoma na kufanya kazi ujue huyu ni PART-TIME STUDENT. Hapa ninazungumzia Universities zinazotambulika na kuheshimika.

Kitu kingine kinachowasaidia wenzetu hasa Marekani ni mfumo wa semester system. Vilevile mwanafunzi anaruhusa ya kuchagua masomo anayoona atayamudu kulingana na mazingira yake in a particular semester.

In case mwanafunzi analazimika kufanya kazi na hatukuwa na muda mwingi wa kujisomea basi huchagua masomo rahisi kidogo. Kwenye semester ambayo anaona ana masomo magumu basi huacha kazi na ku-concentrate kwenye masomo. Hilo haliwezekani kwa mfumo wetu wa masomo UDSM.
 
kichuguu,mwanasiasa,KNKCU,
nina tatizo na hizo fedha za field-work. kwanini wanafunzi wasilipwe na makampuni wanayokwenda kuyafanyia kazi? kwenye nchi za wenzetu field-work/internship huwa ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe kutafuta. .
Mwajiri gani bongo atakubali akupe nafasi ya kufanya mafunzo kwa vitendo halafu bado akulipe na mshahara.Mara nyingi vyuo husika vinaomba sehemu fulani fulani na hasa ni serikalini na mara chache watu wanajitafutia wenyewe,Kwa mfumo wetu wa bongo ukisikia Field work basi ujue ina sehemu yake katika kufikia lengo la wewe kuwa mhitimu si swala la hiari ni lazima.Na watu wengi hupelekwa sehemu za mbali ukiwacha wachache wanaobahatika kubaki Dar au Morogoro kwa SUA.
sina uhakika kwa Madaktari na Mafamasia, lakini kwenye field nyingine fieldwork/internship huwa hai-count towards the degree..
Wanafunzi wa udaktari,wafamasia , wahandisi na wanasheria kwa Field work kwa mfumo wetu ni lazima na inachangia towards your degree.Na si hao hata vitivo vingine.Na hulipwi.Kuhusu Internship kwa Madaktari na wafamasia na wanasheria ni lazima na kwa upande wa madaktari na wafamasia ninahakika wanalipwa na internship zao ni baada ya kuhitimu.
Mimi mgogoro wangu ni huo wa kuchangia gharama za masomo ambazo nadhani ni kubwa mno kwa Mtanzania wa kawaida.

Tatizo letu Tanzania ni kwamba viwango vya malipo ya kazi haviendani kabisa na gharama za huduma/maisha. Kama nilivyoonyesha in my previous posting, katika nchi za wenzetu, mwanafunzi anaweza kujilipia Chuo Kikuu kwa ku-serve malipo ya kazi ya kima cha chini.

Kuhusu suala la kuiga, naomba ieleweke kwamba: mwanafunzi anayesoma FULL-TIME hawezi kufanya kazi hata part-time. Ulaya na Marekani, ukiona mwanafunzi anasoma na kufanya kazi ujue huyu ni PART-TIME STUDENT. Hapa ninazungumzia Universities zinazotambulika na kuheshimika.

Kitu kingine kinachowasaidia wenzetu hasa Marekani ni mfumo wa semester system. Vilevile mwanafunzi anaruhusa ya kuchagua masomo anayoona atayamudu kulingana na mazingira yake in a particular semester.

In case mwanafunzi analazimika kufanya kazi na hatukuwa na muda mwingi wa kujisomea basi huchagua masomo rahisi kidogo. Kwenye semester ambayo anaona ana masomo magumu basi huacha kazi na ku-concentrate kwenye masomo. Hilo haliwezekani kwa mfumo wetu wa masomo UDSM.
Hapa ninakubalina nawe kuanzia kwenye kuchangia mpaka kwenye kufanyakazi kwa wanafunzi wetu ni vigumu.Hii inatokana na mfumo wetu wa elimu na kwa upande mwengine ugumu wa upatikanaji wa kazi kwani Hakuna NAFASI NYINGI ZA KAZI ZINAZOTENGENEZWA na kwa wazazi kipato ni kidogo hakikidhi na kuwawezesha kuwalipia watoto wao .Nafikiri Mikopo kwa asilimia 100 ni suluhisho zuri tu kwasasa na wale waliokopa ni vyema wakarudisha.
 
kichuguu,mwanasiasa,KNKCU,
nina tatizo na hizo fedha za field-work. kwanini wanafunzi wasilipwe na makampuni wanayokwenda kuyafanyia kazi? kwenye nchi za wenzetu field-work/internship huwa ni jukumu la mwanafunzi mwenyewe kutafuta.

sina uhakika kwa Madaktari na Mafamasia, lakini kwenye field nyingine fieldwork/internship huwa hai-count towards the degree.

Mimi mgogoro wangu ni huo wa kuchangia gharama za masomo ambazo nadhani ni kubwa mno kwa Mtanzania wa kawaida.

Tatizo letu Tanzania ni kwamba viwango vya malipo ya kazi haviendani kabisa na gharama za huduma/maisha. Kama nilivyoonyesha in my previous posting, katika nchi za wenzetu, mwanafunzi anaweza kujilipia Chuo Kikuu kwa ku-serve malipo ya kazi ya kima cha chini.

Kuhusu suala la kuiga, naomba ieleweke kwamba: mwanafunzi anayesoma FULL-TIME hawezi kufanya kazi hata part-time. Ulaya na Marekani, ukiona mwanafunzi anasoma na kufanya kazi ujue huyu ni PART-TIME STUDENT. Hapa ninazungumzia Universities zinazotambulika na kuheshimika.

Kitu kingine kinachowasaidia wenzetu hasa Marekani ni mfumo wa semester system. Vilevile mwanafunzi anaruhusa ya kuchagua masomo anayoona atayamudu kulingana na mazingira yake in a particular semester.

In case mwanafunzi analazimika kufanya kazi na hatukuwa na muda mwingi wa kujisomea basi huchagua masomo rahisi kidogo. Kwenye semester ambayo anaona ana masomo magumu basi huacha kazi na ku-concentrate kwenye masomo. Hilo haliwezekani kwa mfumo wetu wa masomo UDSM.


Ndugu yangu JokaKuu, labda nikupe taarifa ya kusikitisha kuwa hata bila malipo, makampuni hukataa kuwachukua vijana wetu kwa ajili ya fieldwork! Sasa kama utataka walipe na kulipa sijui nani atawachukua hao vijana. Sitaki kuongelea hapa uwezo wenyewe wa vijana wetu, hiyo ni mada ya aina yake.

Naomba pia nitifautiane nawe kuwa wanafunzi wanaofanya kazi marekani ni wale tu wanaosoma part-time. Hii sio kweli hata kidogo, labda ni experience uliyo nayo katika vyuo ulivyopita wewe. Lakini ukweli ni kuwa katika vyuo vingi wanafunzi wawe parttime au full time wanachapa mzigo. Isipokuwa kuna limitation ya masaa ya kufanya kazi. Tena wabongo waliosoma fulltime ulaya na marekani wakikusimulia walivyokuwa wanachapa mzigo, acha kabisa! Hivi niandikapo hapa kuna wanafunzi fulltime wanaosha masufuria, wanasafisha vyoo, n.k.
 
Jamani hakuna kazi Bongo ya kumwezesha mwanafunzi kufanya na kusoma. Mnaongelea kima cha chini cha UK ambacho ni kama £5.00 kwa saa ambapo TZ ni kamaTZs 12500.00 kwa saa. Nafikiri hii ni ndoto, huku huku UK na USA wanaofanya hizo kazi ni WTZ na wanafunzi kutoka nchi masikini wakati wenyewe bado wanawarundikia pesa za kufaulu wanafunzi wao.

Haiwezekani ni lazima Serikali iweke kipaumbele katika elimu na watu walipe hiyo kodi. Mbona misamaha ya kodi inatolewa kila siku? Huu ni wakati mzuri wabunge wanakutana hebu waiweke serikali sawa kwa hili, hatuwezi kuendelea kwa namna hii - Nyie viongozi mliosoma bure wakati wa Mwalimu hebu oneni aibu.
 
Ndugu yangu JokaKuu, labda nikupe taarifa ya kusikitisha kuwa hata bila malipo, makampuni hukataa kuwachukua vijana wetu kwa ajili ya fieldwork! Sasa kama utataka walipe na kulipa sijui nani atawachukua hao vijana. Sitaki kuongelea hapa uwezo wenyewe wa vijana wetu, hiyo ni mada ya aina yake.

Naomba pia nitifautiane nawe kuwa wanafunzi wanaofanya kazi marekani ni wale tu wanaosoma part-time. Hii sio kweli hata kidogo, labda ni experience uliyo nayo katika vyuo ulivyopita wewe. Lakini ukweli ni kuwa katika vyuo vingi wanafunzi wawe parttime au full time wanachapa mzigo. Isipokuwa kuna limitation ya masaa ya kufanya kazi. Tena wabongo waliosoma fulltime ulaya na marekani wakikusimulia walivyokuwa wanachapa mzigo, acha kabisa! Hivi niandikapo hapa kuna wanafunzi fulltime wanaosha masufuria, wanasafisha vyoo, n.k.
Inategemea unasomea nini? Na vyuo vingi kwa mwaka wa kwanza kwa marekani huruhusiwi kufanyakazi kama ni mwanafunzi wa kigeni lakini kama ni Muhamiaji ni kivyakovyako utakavyoweza kujipanga.Kwa uingereza ukishapata ukipata namba tu mwendo mdundo kivyakovyako!
 
Tatizo ndugu zangu ni kuwa Tanzania hatutaki kufanya mambo ya kwanza kwanza, kila mara tunajaribu kuruka hatua halafu baadaye tunagundua kuwa hatua hizo haziwezi kufanikiwa pasipo kufanya vitu fulani kwanza! Kwa ufupi, hatuju kupanga ili kushinda, tunashindwa kupanga!!
 
Just agree with me..we aint doing enough, yet we expect the governemnt to do enough! Total illogical! Tusijenge vikwazo kwamba haiwezekani...lets try................
 
mwanasiasa,
.....oh well, kama makampuni hayataki kuchukua wanafunzi as interns then kuna tatizo kubwa la kimtizamo. kama hali ni hivyo nakiri kwamba nimekwama.

kichuguu,knkcu,dua,mwanasiasa,
mwanafunzi anaweza kufanya kazi nje ya shule kwa uamuzi wake mwenyewe. lakini wale wanaofanya kazi on-campus wanabanwa na sheria zinazolinganisha masaa ya kazi vs academic load and standing.

vilevile mazingira yetu ya kazi,usafiri, na malazi, kwa kweli ni vigumu sana kwa mwanafunzi kufanya kazi while attending higher learning institution.

uchumi wa nchi za wenzetu umechangamka sana kiasi kwamba kazi za "u-kibarua" ziko kila wakati. halafu kazi zenyewe siyo ngumu, na hata kama ni ngumu zinalipa.
 
The government should not pay or provide free university education. When university students graduate they all want to go overseas to look for greener pastures so to speak. They do not want to stay and help build or serve the country. So in effect if Tanzanian taxpayers are subsidizing the economies in other countries like Botswana, South Africa, Europe and USA where these graduates eventually end up. This is particularly true for Medical students. I know the salaries in Tanzania are low but if you stick around eventually you will end up making a good living in maybe 10 years or even less if you have your education.
 
Uchumi unaowezesha mwanafunzi asome na huku akifanya kazi kwa manufaa, ni uchumi wenye kazi nyingi a viwango vizuri vya malipo. Kazi zinazofanywa na wanafunzi kwingineko, kama za kuhudumia kwenye migahawa, kufanya usafi mabwenini, ulinzi etc., hapa kwetu zinalipa kwenye shilingi elfu 50 kwa mwezi. Ni kiasi ambacho hakitoshi kutegemewa na mwanafunzi kwa ajili ya kuchangia 40% ya gharama ya masomo yake.

Serikali imekosea sana kuwafukuza wanafunzi. Tatizo la msingi hapa ni la serikali kutotenga fedha za kutosha kwa ajili ya Elimu. Kiasi cha ziada wanachohitaji wanafunzi wetu hawa ni shilingi bilioni 50 tu. Si kiasi kikubwa kwa serikali ambayo kwa kipindi cha miezi 3 tu ya kwanza ya mwaka huu, imepoteza shilingi bilioni 978 za wananchi (Hii ni takwimu iliyotolewa na James Mbatia. Siona shida kuiamini kwani hata taarifa ya Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali inaonyesha mwelekeo huo huo).

Serikali ya Tanzania imetenga chini ya 10% ya bajeti yake ya 2006-2007 kwa ajili ya Elimu. Hii ni kukosea haki wanafunzi WOTE wa Tanzania. Kenya imetenga 27% ya bajeti yake kwa ajili ya Elimu. Majirani zetu wote wametenga sehemu kubwa zaidi kuliko sisi, ya bajeti yao kwa ajili ya Elimu.

Kwa upande mwingne, huu ukatili wa serikali wa kuwafukuza wanafunzi na kuwapa muda kidogo waondoke huenda ukawafanya watumie akili zao zaidi. Wamekuwa wakimshangilia JK bila kufikiri, kama vile mtu anavyoshangilia mpira. JK aliwaahidi kwamba hakuna mwanafunzi hata mmoja atakayeshindwa kusoma kutokana na umaskini. Uongo huo utaonekana wazi sasa.

Augustine Moshi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom