Hapa kuna kila dalili ya udanganyifu kwenye picha hizi. Kwanza tukio linaonekana kufanyika usiku, huku jambazi akiwa amevalishwa mawani nyeusi, kitu ambacho hakiingii akilini. pili, picha ya kwanza, akiwa na mask hakuwa amevaa miwani, ila alipotolewa mawani, anaonekana amevishwa mawani. which is which? huu ni mchezo mchafu unaofanywa na makaburu wakishirikiana na askari wetu wenye njaa kali, ambao yule mhariri aliyefunguliwa kesi aliwaambia watumie akili zao katika kutekeleza maagizo ya mabosi wao
rip? You mean like in "rest in pieces"?
tofauti ya huyu jambazi na hao makaburu wanaokwapua bila kutulipa hata hiyo 3% kwa ku-underdeclare ni nini??
Unaongea Pumba hujui Crime world wala underworld vizuri otherwise usingesema hivyo....mahali popote panaibiwa hata kuwe na ulinzi wa aina gani...ni strategy tu...watu wanaiba hela bank yoyote duniani iwe GGM? kuna problem fulani naiona hapo kama mdau alivyosema wangetesti yale maguruniti before using ingekua habari nyingine .....Uvivu tu na kuamini katika njia za mkato, wenzio wachimbe wewe ukaibe tena anaonekana ni mtu aliyekula chumvi sasa sijui nani kamdanganya kwenda kuiba sehemu yenye maximum security.
Hata kama mkimtetea lazima mjue hawa ndio wanaoumiza na kuua jamaa zetu mtaani na kuchukua mali zao, amegraduate ndio kapewa huo mchongo yaani atakuwa kashafanya mauji sana tu ndio kaingia front katika dili hilo.
Mwenye Data za kueleweka kuhusu usafirishaji wa dhahabu za wawekezaji atujuze maw\swali haya:Jaribio la kutaka kuiba kiasi kikubwa sana cha dhahabu ktk mgodi wa Geita mchana huu mida ya 11:30hrs na watu wenye silaha nzito za kivitaa limezimwa na walinzi wa mgodi (snipers & quick respond unit force wakishilikiana na makomandoo walinzi wa ndege inayosafirisha dhahabu) mpaka mida hii imethibitika watu 2 wamepoteza maisha.
Jaribio hilo limefanyika Ktk airport ya mgodini wakati dhahabu hiyo ikipakiwa ktk ka ndege special tayari kwa kusafirishwa kwenda South Africa, hadi mida hii wana Geita bado tunasikia milio ya risasi zikilindima maporini na vingora vya ambulance za mgodini zikiwabeba majeruhi wengi wao ni walinzi wa wa mgodi, polisi walitarifiwa mapema kabisa lakini bado wanajipanga namna ya kufika eneo la tukio!
Tutazidi kuajuza kadri nitavyo pata habari zaidi.
UPDATE:
Polisi wamefika eneo la tukio na kwa sasa wanawakamata wakata mbao, wachungaji na wachoma mkaa wakiwatuhumu kwa ujambazi wakati wapiga deal halisi wameisha sepa , walinzi 8 wa mgodini ( wa kitanzania) wameahidiwa 10,000 USD kila mmoja kwa kuweza kulinda mali ya mwekezaji, huku mlinzi mzungu akisafilishwa kurudi RZA kwa matibabu ( huyu jamaa amepigwa kama risasi 3 mkononi na mguuni, na huyu ndio aliyeuwa jambazi baada ya kukabiliana naye uso kwa uso).
Polisi wamekabidhiwa sub machine gun 3, mabomu ya mkono 9 ( moja lilirushwa lakini halikulipuka vizuri) magazine zaidi ya 5 zikiwa na risasi zaidi 100, bullet proof vest 2.
Polisi wanasomeshwa wakubali kuwa wao ndio waliopambana na ku uwa majambazi ili hawa jamaa wanakwepa lawama za mauaji kimtindo, Mwili wa jambazi (kipande cha jibaba lenye asili ya kisomali inaaminiki ndiye alikuwa kiongozi wa uvamizi) umepelekwa mortuary, nikifanikiwa nita upload picha ya maiti yake.
Hali ya hewa imetulia kidogo na shuguli za kumtumikia kaburu zimeanza mnamo 1330hrs, kwa ujumla kulikuwa na vitofali 34 vya dhahabu ( kila kitofali kina 24KG) vilivyo pona pona kutembea ( ila nawalaumu hawa ma intruders kwa uchoyo wao!)
KUTOKA FIKRAPEVU:
PICHA ZAIDI kwa hisani ya kanta (JF member):
Hapo jambazi ni makaburu hao jamaa walienda kuchukua mali ya nchi.
huyu jamaa ni mjeshi au? ila suala la kujiuliza kwa nini hiyo dhahabu itokee kwa kiwanja cha ndege cha hapo uwanjani na kwenda direct south africa? nani anaikagua au kuthibitisha kiwango? wanaona tabu gani kuipitishia dar?