Jaribio la kuiba dhahabu katika mgodi wa Geita (GGM) lazimwa

Hapa kuna kila dalili ya udanganyifu kwenye picha hizi. Kwanza tukio linaonekana kufanyika usiku, huku jambazi akiwa amevalishwa mawani nyeusi, kitu ambacho hakiingii akilini. pili, picha ya kwanza, akiwa na mask hakuwa amevaa miwani, ila alipotolewa musk, anaonekana amevishwa mawani. which is which? huu ni mchezo mchafu unaofanywa na makaburu wakishirikiana na askari wetu wenye njaa kali, ambao yule mhariri aliyefunguliwa kesi aliwaambia watumie akili zao katika kutekeleza maagizo ya mabosi wao
 
Hapa kuna kila dalili ya udanganyifu kwenye picha hizi. Kwanza tukio linaonekana kufanyika usiku, huku jambazi akiwa amevalishwa mawani nyeusi, kitu ambacho hakiingii akilini. pili, picha ya kwanza, akiwa na mask hakuwa amevaa miwani, ila alipotolewa mawani, anaonekana amevishwa mawani. which is which? huu ni mchezo mchafu unaofanywa na makaburu wakishirikiana na askari wetu wenye njaa kali, ambao yule mhariri aliyefunguliwa kesi aliwaambia watumie akili zao katika kutekeleza maagizo ya mabosi wao

walimvua kofia wakamvalisha miwani..kuficha utambuzi on th spot..unaweza kujifanya kwenda kuangalia ukakuta ni mmeo
 
Nawapa big up sana majambazi hawa....tunaitambua kazi yenu nzuri...sasa tutakua tunaongea with "evidence"...

Mungu amrehemu shujaa wetu aliefariki.
 
Uvivu tu na kuamini katika njia za mkato, wenzio wachimbe wewe ukaibe tena anaonekana ni mtu aliyekula chumvi sasa sijui nani kamdanganya kwenda kuiba sehemu yenye maximum security.

Hata kama mkimtetea lazima mjue hawa ndio wanaoumiza na kuua jamaa zetu mtaani na kuchukua mali zao, amegraduate ndio kapewa huo mchongo yaani atakuwa kashafanya mauji sana tu ndio kaingia front katika dili hilo.
 
Ahaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!, lakini imekuaje mabomu yakakataa kulipuka,kimkakakati naona tulijipanga vyema lakini tukasahau kutest magurunet, la sivyo mission ingekua kompliti ngoja tujipange upya hao jamaa hawawezi kuyatumia hayo matofali peke yao wakati mjomba angu anapelekwa mabwepande kukaa kwenye mahema wakati kumbe tunaweza kuuza tofali moja tu na kuwajengea nyumbanzuri pamoja na kuimarisha huduma za afya, walahi aluta kontinua tutarudi tena tukiwa tumekamilika eneo la tukio ni lazima kieleweke.RIP Kamanda.
 
Msichoke jaribuni tena bora muibe nyie kuliko magamba na mabwana zao makaburu
 
Uvivu tu na kuamini katika njia za mkato, wenzio wachimbe wewe ukaibe tena anaonekana ni mtu aliyekula chumvi sasa sijui nani kamdanganya kwenda kuiba sehemu yenye maximum security.

Hata kama mkimtetea lazima mjue hawa ndio wanaoumiza na kuua jamaa zetu mtaani na kuchukua mali zao, amegraduate ndio kapewa huo mchongo yaani atakuwa kashafanya mauji sana tu ndio kaingia front katika dili hilo.
Unaongea Pumba hujui Crime world wala underworld vizuri otherwise usingesema hivyo....mahali popote panaibiwa hata kuwe na ulinzi wa aina gani...ni strategy tu...watu wanaiba hela bank yoyote duniani iwe GGM? kuna problem fulani naiona hapo kama mdau alivyosema wangetesti yale maguruniti before using ingekua habari nyingine .....
 
Kuiba ni kosa kubwa sana kama ilivyo kwenye vitabu vya dini cha kusikitisha ndege imetua porini bila hata ya Serikali ya Wilaya/ Mkoa ama Serikali Kuu kuwa na taarifa na hakukuwa hata na TRA ama afisa biashara wa Wilaya kutathmini ni kiasi gani kinachoondoka na thamani yake, Rada iliyonunuliwa na Wananchi wakala ... Inafanya kazi gani? Ndege ngapi zimetua hapo tangu mradi umeanza? Tumefunguliwa macho, tuangalie kwenye soko la dunia dhahabu tani moja ni kiasi gani? La tutakuwa tunapiga mbizi tu!
 
tena hicho kiwango kinachotajwa nadhani si rasmi lazima kunauchakachuaji hapo,hivi kwa siku jamaa wawe wana safirisha mali ya zaidi ya bill 1 tambuwa pia wamekodi ndege ikimaanisha mzigo ni wa gharama,je kwa wiki ni shi ngapi itakuwa zaidi y 7xbill 1,je kwa mwezi 7xzaidi ya bill 1x4,kwa mwaka je.

ni mijipesa mkuu na hatuambulii chochote zaidi ya watu wetu kuungua kwa kemikali na kufa
 
Jaribio la kutaka kuiba kiasi kikubwa sana cha dhahabu ktk mgodi wa Geita mchana huu mida ya 11:30hrs na watu wenye silaha nzito za kivitaa limezimwa na walinzi wa mgodi (snipers & quick respond unit force wakishilikiana na makomandoo walinzi wa ndege inayosafirisha dhahabu) mpaka mida hii imethibitika watu 2 wamepoteza maisha.

Jaribio hilo limefanyika Ktk airport ya mgodini wakati dhahabu hiyo ikipakiwa ktk ka ndege special tayari kwa kusafirishwa kwenda South Africa, hadi mida hii wana Geita bado tunasikia milio ya risasi zikilindima maporini na ving’ora vya ambulance za mgodini zikiwabeba majeruhi wengi wao ni walinzi wa wa mgodi, polisi walitarifiwa mapema kabisa lakini bado wanajipanga namna ya kufika eneo la tukio!


Tutazidi kuajuza kadri nitavyo pata habari zaidi.

UPDATE:
Polisi wamefika eneo la tukio na kwa sasa wanawakamata wakata mbao, wachungaji na wachoma mkaa wakiwatuhumu kwa ‘ujambazi’ wakati wapiga deal halisi wameisha sepa , walinzi 8 wa mgodini ( wa kitanzania) wameahidiwa 10,000 USD kila mmoja kwa kuweza kulinda mali ya ’ mwekezaji’, huku mlinzi mzungu akisafilishwa kurudi RZA kwa matibabu ( huyu jamaa amepigwa kama risasi 3 mkononi na mguuni, na huyu ndio aliyeuwa jambazi baada ya kukabiliana naye uso kwa uso).

Polisi wamekabidhiwa sub machine gun 3, mabomu ya mkono 9 ( moja lilirushwa lakini halikulipuka vizuri) magazine zaidi ya 5 zikiwa na risasi zaidi 100, bullet proof vest 2.

Polisi wanasomeshwa wakubali kuwa wao ndio waliopambana na ku uwa majambazi ili hawa jamaa wanakwepa lawama za mauaji kimtindo, Mwili wa jambazi (kipande cha jibaba lenye asili ya kisomali inaaminiki ndiye alikuwa kiongozi wa uvamizi) umepelekwa mortuary, nikifanikiwa nita upload picha ya maiti yake.

Hali ya hewa imetulia kidogo na shuguli za kumtumikia kaburu zimeanza mnamo 1330hrs, kwa ujumla kulikuwa na vitofali 34 vya dhahabu ( kila kitofali kina 24KG) vilivyo pona pona kutembea ( ila nawalaumu hawa ma intruders kwa uchoyo wao!)

KUTOKA FIKRAPEVU:



PICHA ZAIDI kwa hisani ya
kanta (JF member):

jambazi-geita1.jpg

jambazi-geita2.jpg
Mwenye Data za kueleweka kuhusu usafirishaji wa dhahabu za wawekezaji atujuze maw\swali haya:
1. Dhahabu kama hii, airway bill yake hutolewa na nani? Je serikali ina record za AWB?
2. Mnunuzi wa dhahabu hii ya mwekezaji huwa anaingiza pesa kwenye account ya mwekezaji chini kutokana na invoice aliyopewa na mwuuzaji(Mwekezaji) au huondolewa tu kutumia ndege za wawekezaji?
3. Kwa nini serikali haina utaratibu wa kutengeneza government godown za dhahabu ili kuweza kuwa karibu zaidi kuangalia kiwango cha dhahabu kinachotolewa nchini kwenda huko ughaibuni?
4. Kwa nini serkali haina mpango wa kutengeneza port of exit ya dhahabu ambayo iko monitored na serikali?
Lengo ni kujua DHAHABU imenunuliwa na kampuni gani, Kiasi cha pesa kimeingia kwenye account ya mwekezaji nchini Tanzania toka nchi inayonunua dhahabu hiyo, dhahabu imetolewa government godown ,mahali alipopewa mwekezaji iihifadhi, airway bill imetolewa na shirika au kampuni ya usafirishaji kwenda kwa mnunuaji.TRA wamehakiki pesa zimeingia nchini na asilimia wamekata, pia madini nao chao wamechukua, benki zetu nazo zimepata commission za transfer na exchange rates.Serikali nayo imepata chake hata kwa kukata VAT. Je kwa utaratibu uliopo serikali ianpata kweli?
 
Hapo jambazi ni makaburu hao jamaa walienda kuchukua mali ya nchi.
 
Lazima serikali itakuwa inajua ujanja huo,ila watakuwepo TOP DOGS ambao wanaficha haya mambo, wana chao humo.
Kwani unafikiri walikuwa hawajui ndege zinatua humo kufanya nini? Wizara ya nishati na madini itakuwa inajua.
 
Hapo jambazi ni makaburu hao jamaa walienda kuchukua mali ya nchi.

walienda kuchukua mali yao halali,baada ya kuona mgawanyo hauko sawa kwa watz wote,kama kunge kuwa na kufaidika kwa watz wote wala usingewaona wakienda na mabunduki ama mabomu kutaka kuichukuwa kwa lazima
 
Hawataki kuipitisha Dsm kwani "wanapunguza gharama".

Watz wengi hawajui mambo haya but tujue kila tukio ni darasa. NI KWELI KWAMBA "MAJAMBAZI HAYA" YALIYOOKOA DHAHABU WANAYOITA YAO wana viwanja kwenye karibu migodi yao yote. Hakuna kinachopitia Dsm au TA zaidi ya ule "mchanga wa dhahabu" ambao wanafanya hivyo kutokana na uzito tu.
Eti hukohuko migodini kuna maofisa wawili wa serikali; mmoja wa TRA na mwingine wa TMA wakifanya "uwakilishi"-I'M NOT SURE IF THIS WORKS!!
-Ni kama ile ya kamati teule ya bunge iliyotakiwa kwenda kukagua malalamiko ya wanaMARA huko kwenye mgodi halafu mwekezaji/mlalamikiwa akatuma ndege yake kuwabeba.

TANZANIA ILIPATA UHURU NA BAADAE IKAURUDISHA KWA NGUVU ZOTE NA KUWAAMBIA "HATUWEZI KUJITAWALA"... Inaumiza ila Mungu tu ndiye anaweza kuwatetea waTZ.

huyu jamaa ni mjeshi au? ila suala la kujiuliza kwa nini hiyo dhahabu itokee kwa kiwanja cha ndege cha hapo uwanjani na kwenda direct south africa? nani anaikagua au kuthibitisha kiwango? wanaona tabu gani kuipitishia dar?
 
Back
Top Bottom