Biashara ya dhahabu last season will be On June 2024

mcrounmj

JF-Expert Member
Feb 26, 2016
380
885
Nianze kwa kusema 'much respect to you all hustlers'. No matter what you're going through.... but you're the future billionaire. Hiyo ni salamu yangu kwenu watafutaji mliojipata, ambao hamjajipata na mnaamini katika kesho.

Uzi huu ni mwendelezo wa nyuzi nne zilizotangulia zikielezea mapambano yangu ya kiuchumi na namna ambavyo niliamua kujiingiza kwenye shughuli za dhahabu, mafanikio niliyoyapata na namna ambavyo niliweza kupanga mipango ya baadae. Nimeelezea historia ya maisha yangu ya huko nyuma...nikitokea familia masikini na kujikuta mhanga wa kukosa ajira baada ya kuhitimu chuo kikuu.

Yapo mengi nimeyaelezea ambayo yalinifanya niwe na ari na hamasa kubwa ya kuusaka utajiri. Lakini kubwa zaidi niliamua ku share na jamii ya jukwaa hili nikiamini, uzoefu wangu na mawazo yangu yatabadilisha mitazamo ya watu wengi namna ya kuwaza, kuamka na kuingia tena kwenye uwanja wa mapambano.... lakini mahususi nilitaka kuwasanua watu kuhusu rasilimali adhimu ambayo ni dhahabu.

Kutoka kuwa kibarua wa kuajiriwa mgodini, mpaka kufikia hatua ya kumiliki mgodi...si jambo dogo na sikuonyesha katika namna ya ujivuni bali ilikuwa kuonyesha kwamba kila kitu kinawezekana kama ukidhamilia. Guys, nikiri tu kwamba sehemu ambayo utajiri upo nje nje ni kwenye dhahabu.

Kwasababu andiko hili ni utangulizi wa sehemu ya mwisho..... Niahidi kuwa sehemu ya mwisho itakuwepo hapa jukwaani mapema juni mwaka huu 2024. Katika kipindi chote ambacho nimekuwa nikishea nanyi safari yangu ya mapambano, wapo watu ambao walihamasika na kunifata inbox. Wachache niliwajibu, na hata hao niliowajibu sikuwapa nafasi ya kuonana nao. Hii ilikuwa ni sababu yangu mahususi na mara kadhaa niliandika hapa kwamba napendelea niendelee kubakia kichakani kwa masirahi yangu binafsi. Hivyo sasa kwa sababu pale ambapo ilikuwa tamaa yangu kufikia is already done... The last season will reveal my cover, nitakuwa tayari kuwasiliana na yeyote na kumkaribisha nyumbani kwangu kama atataka kuja kujifunza.

Lakini pia kwa opposers na wakatisha tamaa... Nikiri tu kuwa ninyi ni watu mhimu mno kwenye jukwaa hili hata jamii kwa ujumla. Ninyi hamkubali katika juhudi za watu na mpo kutabili kuwa hawafiki popote. Nakumbuka uzi wangu wa kwanza nilipoonyesha kuwa mtaji wangu umekua maradufu kutoka million tatu mpaka kumi ndani ya miezi sita, mlitabili kuwa 'vina muda basi'. Lakini ilivyo ajabu nimekuwa nikiyatumia maneno yenu kupanda juu zaidi. Pia wapo ambao walihisi uzi huu ni namna ya kwenda kuwapiga watu pesa... yaani utapeli, haya naomba niliyemtapeli ajitokeze!

Kwa kumalizia niseme tu kuwa.... for whatever you're doing, do it in high spirit. Focus, consistency and determination will brought you into success. Amini kwenye unachokifanya, kifanye kwa ufasaha na na uwe na nidhamu ya matumizi.
Guys meet you at the top 'cheers'
 
Nianze kwa kusema 'much respect to you all hustlers'. No matter what you're going through.... but you're the future billionaire. Hiyo ni salamu yangu kwenu watafutaji mliojipata, ambao hamjajipata na mnaamini katika kesho.

Uzi huu ni mwendelezo wa nyuzi nne zilizotangulia zikielezea mapambano yangu ya kiuchumi na namna ambavyo niliamua kujiingiza kwenye shughuli za dhahabu, mafanikio niliyoyapata na namna ambavyo niliweza kupanga mipango ya baadae. Nimeelezea historia ya maisha yangu ya huko nyuma...nikitokea familia masikini na kujikuta mhanga wa kukosa ajira baada ya kuhitimu chuo kikuu.

Yapo mengi nimeyaelezea ambayo yalinifanya niwe na ari na hamasa kubwa ya kuusaka utajiri. Lakini kubwa zaidi niliamua ku share na jamii ya jukwaa hili nikiamini, uzoefu wangu na mawazo yangu yatabadilisha mitazamo ya watu wengi namna ya kuwaza, kuamka na kuingia tena kwenye uwanja wa mapambano.... lakini mahususi nilitaka kuwasanua watu kuhusu rasilimali adhimu ambayo ni dhahabu.

Kutoka kuwa kibarua wa kuajiriwa mgodini, mpaka kufikia hatua ya kumiliki mgodi...si jambo dogo na sikuonyesha katika namna ya ujivuni bali ilikuwa kuonyesha kwamba kila kitu kinawezekana kama ukidhamilia. Guys, nikiri tu kwamba sehemu ambayo utajiri upo nje nje ni kwenye dhahabu.

Kwasababu andiko hili ni utangulizi wa sehemu ya mwisho..... Niahidi kuwa sehemu ya mwisho itakuwepo hapa jukwaani mapema juni mwaka huu 2024. Katika kipindi chote ambacho nimekuwa nikishea nanyi safari yangu ya mapambano, wapo watu ambao walihamasika na kunifata inbox. Wachache niliwajibu, na hata hao niliowajibu sikuwapa nafasi ya kuonana nao. Hii ilikuwa ni sababu yangu mahususi na mara kadhaa niliandika hapa kwamba napendelea niendelee kubakia kichakani kwa masirahi yangu binafsi. Hivyo sasa kwa sababu pale ambapo ilikuwa tamaa yangu kufikia is already done... The last season will reveal my cover, nitakuwa tayari kuwasiliana na yeyote na kumkaribisha nyumbani kwangu kama atataka kuja kujifunza.

Lakini pia kwa opposers na wakatisha tamaa... Nikiri tu kuwa ninyi ni watu mhimu mno kwenye jukwaa hili hata jamii kwa ujumla. Ninyi hamkubali katika juhudi za watu na mpo kutabili kuwa hawafiki popote. Nakumbuka uzi wangu wa kwanza nilipoonyesha kuwa mtaji wangu umekua maradufu kutoka million tatu mpaka kumi ndani ya miezi sita, mlitabili kuwa 'vina muda basi'. Lakini ilivyo ajabu nimekuwa nikiyatumia maneno yenu kupanda juu zaidi. Pia wapo ambao walihisi uzi huu ni namna ya kwenda kuwapiga watu pesa... yaani utapeli, haya naomba niliyemtapeli ajitokeze!

Kwa kumalizia niseme tu kuwa.... for whatever you're doing, do it in high spirit. Focus, consistency and determination will brought you into success. Amini kwenye unachokifanya, kifanye kwa ufasaha na na uwe na nidhamu ya matumizi.
Guys meet you at the top 'cheers'
Will brought you???? Heeeh.... Ya wapi hii?
 
Dhahabu kama dhahabu....hainaga masihara,inakuchapa adi unachanganikiwa kama hv
 
Unasikiliza kauli za huyo mjinga ? Huyo hata mgodini kwenyewe hajawahi kufika
Najua mkuu I was just kidding with him
Biashara ya dhahabu ina faida kubwa sana na haitaisha duniani
Mimi nimejiwekea kama akiba bank nilikuwa nanunua na kuweka
Humu Kuna kila aina ya watu unaenda nao hivyo hivyo na unachagua wa kupata ushauri maana kuna wengi wanachangia tu mradi ila utakuta hajui lolote kuhusu jambo ila atakupa ushauri usiokuwa na uhalisia
 
Najua mkuu I was just kidding with him
Biashara ya dhahabu ina faida kubwa sana na haitaisha duniani
Mimi nimejiwekea kama akiba bank nilikuwa nanunua na kuweka
Humu Kuna kila aina ya watu unaenda nao hivyo hivyo na unachagua wa kupata ushauri maana kuna wengi wanachangia tu mradi ila utakuta hajui lolote kuhusu jambo ila atakupa ushauri usiokuwa na uhalisia
Kweli mkuu.... Mfano huyo anayefananisha uchimbaji na kubeti, ni vitu viwili tofauti ni kama mbingu na ardhi. Kubeti imeegemea kwenye bahati, ila madini yapo kwenye fact na reality. Million 50 huwezi kuiwekeza sehemu ambayo hujapima na kujua uwingi wa dhahabu wa sehemu husika. Yaani kuna maabara ambazo hutumia vifaa vya kisasa kukupa tathimini kabla hujaanza kuchimba. Kama hujui kitu bora unyamaze kuliko kupotosha.
 
Dhahabu kama dhahabu....hainaga masihara,inakuchapa adi unachanganikiwa kama hv
Siyo kweli mkuu. Kuna namna ulikosea ndiyo maana ilikuchapa adi ukachanganyikiwa. Pengine uliingia kama kwenye kilee kilimo cha Whatsapp. Kila kitu kinahitaji utulivu wa akili na kuendelea kujifunza huku una practice. Ili upate matokeo yenye tija kwenye kila utakachoanza kukifanya kwa mara ya kwanza.... Usikurupuke, anza kidogokidogo huku ukijifunza.
 
Back
Top Bottom