Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 21,839
- 38,736
Kuna mwamba mmoja mwaka 2007 alifanya utapeli wa kihistoria kwenye mkoa wa Geita
Alikua ni anafanya kazi kwenye mgodi wa GGM (Geita gold mine) siku moja alipiga deal na wenzie la kutorosha dhahabu kimagendo kutoka kwenye mgodi na kufanikiwa.
Walikua na hazina ya dhahabu kama vipande ishirini vya size tofauti tofauti.
Kabla hawajaviuza ili kugawana hela mmoja wao akaja na mpango wa kutumia dhahabu hizo kama chambo cha kuwanasia wazungu waliokua wanaharaka na kupata mgodi wa kununua mkoani humo.
Basi walichofanya ilikua ni kwenda kwenye eneo moja na kufukia dhahabu katika maeneo tofauti tofauti ya kiwanja hicho.
Baada ya kumaliza hilo zoezi wakatafta madalali wa kwenda kuongea na wazungu waliokua wanatafta mgodi mdogo wa kununua.
Deal lilikamilika na wazungu hao wakaja na machine zao ili kupima kama eneo hilo kweli lina dhahabu. Baada ya kupima majibu ya vipimo yakawa chanya Kwa wazungu.
Na wakaamua kufanya biashara na hao wauzaji. Wazungu wakalipa fedha taslimu na kukabidhiwa mgodi huo fake .
Basi usiku wa hiyo siku hao matapeli walirudi kwa kujificha na kuchimbua dhahabu zao na kutokomea kusiko julikana.
Alikua ni anafanya kazi kwenye mgodi wa GGM (Geita gold mine) siku moja alipiga deal na wenzie la kutorosha dhahabu kimagendo kutoka kwenye mgodi na kufanikiwa.
Walikua na hazina ya dhahabu kama vipande ishirini vya size tofauti tofauti.
Kabla hawajaviuza ili kugawana hela mmoja wao akaja na mpango wa kutumia dhahabu hizo kama chambo cha kuwanasia wazungu waliokua wanaharaka na kupata mgodi wa kununua mkoani humo.
Basi walichofanya ilikua ni kwenda kwenye eneo moja na kufukia dhahabu katika maeneo tofauti tofauti ya kiwanja hicho.
Baada ya kumaliza hilo zoezi wakatafta madalali wa kwenda kuongea na wazungu waliokua wanatafta mgodi mdogo wa kununua.
Deal lilikamilika na wazungu hao wakaja na machine zao ili kupima kama eneo hilo kweli lina dhahabu. Baada ya kupima majibu ya vipimo yakawa chanya Kwa wazungu.
Na wakaamua kufanya biashara na hao wauzaji. Wazungu wakalipa fedha taslimu na kukabidhiwa mgodi huo fake .
Basi usiku wa hiyo siku hao matapeli walirudi kwa kujificha na kuchimbua dhahabu zao na kutokomea kusiko julikana.