kasyabone tall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2009
- 254
- 59
Hivi vazi la taifa limekwenda wapi?
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi alikaririwa na vyombo vya habari kukemea matumizi ya suti kwa watumishi wa serikali kwa maelezo kuwa, zina gharama kubwa huku Watanzania wengi wakiwa maskini wa kutupwa.
Kauli hiyo ya mheshimiwa Pinda, imekuja wakati akiwa katika mkakati wa kupunguza matumizi ya serikali kwa kuanzia na ununuzi wa magari ya kifahari na kisha kushukia kwenye suti zinazovaliwa na watumishi wa serikali bila kujali mazingira husika.
Kutolewa kwa wazo hilo la Waziri Mkuu kumetukumbusha wazo la vazi la kitaifa ambalo lilipewa kipaumbele na serikali ya awamu ya tatu hata kukaundwa tume ya kufuatilia suala hilo ambalo mpaka sasa halijatiliwa umuhimu unaostahili.
Suala la vazi la kitaifa ni muhimu sana kujenga utaifa na kutambulika kwa haraka kwa raia wa Tanzania hata wanapokuwa nje ya nchi na pia kutangaza utamaduni wetu nje ya mipaka yetu.
Tunapokosa vazi la taifa pia tunakosa utambulisho wa taifa letu na raia wake na linapokosekana kama ilivyo sasa, kila mtu anajitumbukiza kwenye mavazi yanayompendezesha yeye na mengine kama yanayomkera waziri mkuu.
Tunashauri wahusika wa suala la vazi la kitaifa kuliangalia upya suala hilo, ili nguvu za viongozi wetu zinazotumika katika kukemea masuala kama ya suti zielekezwe kwenye masuala ya msingi ya maendeleo ya taifa letu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi alikaririwa na vyombo vya habari kukemea matumizi ya suti kwa watumishi wa serikali kwa maelezo kuwa, zina gharama kubwa huku Watanzania wengi wakiwa maskini wa kutupwa.
Kauli hiyo ya mheshimiwa Pinda, imekuja wakati akiwa katika mkakati wa kupunguza matumizi ya serikali kwa kuanzia na ununuzi wa magari ya kifahari na kisha kushukia kwenye suti zinazovaliwa na watumishi wa serikali bila kujali mazingira husika.
Kutolewa kwa wazo hilo la Waziri Mkuu kumetukumbusha wazo la vazi la kitaifa ambalo lilipewa kipaumbele na serikali ya awamu ya tatu hata kukaundwa tume ya kufuatilia suala hilo ambalo mpaka sasa halijatiliwa umuhimu unaostahili.
Suala la vazi la kitaifa ni muhimu sana kujenga utaifa na kutambulika kwa haraka kwa raia wa Tanzania hata wanapokuwa nje ya nchi na pia kutangaza utamaduni wetu nje ya mipaka yetu.
Tunapokosa vazi la taifa pia tunakosa utambulisho wa taifa letu na raia wake na linapokosekana kama ilivyo sasa, kila mtu anajitumbukiza kwenye mavazi yanayompendezesha yeye na mengine kama yanayomkera waziri mkuu.
Tunashauri wahusika wa suala la vazi la kitaifa kuliangalia upya suala hilo, ili nguvu za viongozi wetu zinazotumika katika kukemea masuala kama ya suti zielekezwe kwenye masuala ya msingi ya maendeleo ya taifa letu.