Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 943
Mbunge Angelina Malembeka: Vazi la Rais Samia Linatosha Kuwa Vazi la Taifa
Mbunge Angelina Malembeka amesema kwa mtazamo wake mavazi anayovaa Rais Samia Suluhu Hassan yanatosha kuwa vazi la Taifa kwani yana stara, ustaarabu, heshima na unadhifu.
Angelina ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akichangia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii na Kamati ya kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo.
Amesema katika kulitafuta vazi la Taifa kinachotakiwa kuzingatiwa ni kuhakikisha linapatikana vazi lenye stara, ustaarabu, heshima, linaloonesha unadhifu na linaloweza kuvaliwa na yeyote.