Hadithi: Roho ya paka. (Ben R. Mtobwa)

Nyie mnaoiba ndo muache roho mbaya. Unapaswa kuwa civilised kujua kuthamini mali ya mtu. Unapotaka kutumia, jaribu kuomba kwa mwenye nacho. sio kujichukulia kama vile anayekimiliki alikupa wewe. Kuna kipindi baba mwenyewe aliingia mjini kukamata watu wa aina yenu. Na wengi waliibuka na hatia. Sasa hayupo, mnaona mtumie mpendavyo.
Anyway, sitaimaliza, natoa kidogo tu kwaajili ya kupromote kitabu.
Usiwasikilize hao nameless girl!!
 
Yan kitabu chenyewe nikunyime, kuja kwetu ndo ntakubali? na ukibahatika kuja ugali ntakunyima.
Wewe huwezi ninyima ugali, utaninyima vingine. Kwanza ntakuja na gia ya kuchukua machapisho kadhaa, then naamini utanigudumia.

Halafu najipanga nifungue book shop, vitabu vya mzee itakuwa moja ya bidhaa dukani kwangu, lzm unipende na unigudumie nikija dar
 
Wewe huwezi ninyima ugali, utaninyima vingine. Kwanza ntakuja na gia ya kuchukua machapisho kadhaa, then naamini utanigudumia.

Halafu najipanga nifungue book shop, vitabu vya mzee itakuwa moja ya bidhaa dukani kwangu, lzm unipende na unigudumie nikija dar
hahaha ndo umeanza promo ili nikukaribishe kabisa!!!
 
***

Ulikuwa usiku mrefu mno kwa Joram Kiango, usiku unaochosha na kukinaisha kupita kiasi. Kwa mtu wa vitendo kama yeye, ilikuwa kama adhabu kukesha wima, ndani ya chumba chako, kando ya kitanda chako, ukisubiri jambo ambalo halitokei.

Kucha aliyatega macho yake yakipasua kiza kuchunguza chochote ambacho kingekuwa kigeni chumbani humo. Kadhalika, masikio yake yalikuwa makini, tayari kunasa mchakacho wowote ambao angeusikia. Lakini hadi kulipopambazuka hakusikia wala kuona chochote, jambo ambalo lilimfanya ajikute akipandwa na hasira kali zaidi dhidi ya yeyote aliyekuwa akimtendea kitendo hicho, hasira ambazo kiasi zilimfanya ajione mpumbavu kwa uamuzi wake wa kuwasubiri adui hao.

Ilikuwepo haja gani ya kupoteza usiku mzima akiwa ameketi akiwasubiri badala ya kuwa mitaani akipambana nao? ‘Haiwezekani kuwa kitendo chake cha kukesha hapo bila ya kushughulika ndicho hasa walichokihitaji ili waendelee na unyama wao mitaani? Wamenifanya mpumbavu!’ aliwaza kwa uchungu na hasira. Na kwa hasira hizo alitabasamu.

Hata hivyo, hakujilaumu sana. Alijua kama siyo leo, kesho wangekuja kuhakikisha mauti yake. Na alikusudia wamkute akiwa anajua adui yake ni nani na anakusudia nini. Hivyo, asubuhi hiyo aliamua kuitumia kwa uchunguzi.

Kulipopambazuka kikamilifu, Joram akaingia bafuni kuoga. Kisha, akaliendea kabati la nguo na kutafuta moja kati ya mavazi yake ambayo humfanya asitambulike kwa urahisi wala kumtazama kwa makini. Leo alivaa kanzu nyeupe, kijikoti cheusi juu, ndala miguuni, kofia pana kichwani na miwani myeusi.

Akachukua fimbo yake ya kutembelea na kutoka nje akitumia mlango wa nyuma. Baada ya kupenya hapa na pale, aliifikia barabara kuu ambako alikodi gari lililomfikisha mjini. Huko alitafuta hoteli na kujipatia kifungua kinywa. Kutoka hapo alikwenda Mtaa wa Mkwepu kwenye duka moja ambalo wanaruhusu wapita njia kupiga simu kwa malipo. Alimwomba Mhindimwenye simu hiyo aitumie nusu saa huku akimpa shilingi elfu tano.

“Napiga hapahapa mjini zikiisha, nitaongeza,” alimwambia.

Huku akiwa na mshangao, mwenye duka huyo alipokea harakaharaka na kumpisha Joram kiti.

Polisi ni watu wanaojua sana kufumba midomo. Kujaribu kunyofoa ukweli toka katika mikono ya polisi ni kazi ngumu kama kujaribu kung’oa ulimi wa jabali. Lakini si kwa mtu kama Joram Kiango. Hadhi yake katika masuala ya mapambano ilimpatia marafiki wengi katika jeshi hilo. Aidha, alikuwa na marafiki zake wawili, watatu ambao humuuzia siri na habari mbalimbali anazohitaji, kama vile ambavyo yeye huwapa ‘tip’ wanapofuatilia masuala fulanifulani anayoyafahamu.

Akiwa na hakika kuwa mauaji ya wasichana wote wawili yalikwishagundulika na polisi, simu yake ya kwanza aliielekeza Idara ya Upelelezi ya kituo kikuu. Alikuwa na bahati ya kumpata mtu wake.

Baada ya maongezi mafupi ya mafumbo-mafumbo, Joram aliweka simu chini. Habari alizopata licha ya kuwa hazikumnufaisha sana bado zilimwongezea hasira. Mpelelezi huyo alikiri kuwa bado kuna jambo la ‘moto sana’.

Anachofahamu ni kwamba, raia watatu na askari kanzu mmoja wamekwishauawa. Ni hilo lililomsikitisha Joram Kiango. Watu zaidi wameendelea kufa wakati yeye ameketi juu ya kochi akisubiri adui ajilete. Aibu iliyoje!

Maswali yake yaliyofuata hayakupata majibu zaidi. Hivyo, Joram akakata na kupiga kwenye simu ya Kombora. “Namtaka Shoka,” aliomba.

“Hayupo”

“Yuko wapi?”

“Amehama.”


Moyo wa Joram ulidunda kwa nguvu. Hakuwa mgeni wa msamiati huo. Askari anapotamka moja kwa moja kuwa askari fulani amehama, huwa haina maana nyingine zaidi ya kufa. Yawezekana ni yeye aliyekufa kwa ajili yake? Joram alijikaza na kutaja jina la pili.

“Hayupo,” mtu wake wa tatu pia hakuwepo.

Wakati Joram akiwa ameduwaa, mtu aliyekuwa upande wa pili wa simu alimshangaza alipomwambia, “Au nikupe Inspekta Kombora mwenyewe Joram?”

“Ndi…yo… hapana. Labda hahitaji kuniona. Pengine wewe unaweza kunisaidia…”

“Najua Inspekta hana muda wa kukuona. Wala asingependa kukushirikisha. Hata hivyo, mimi nitakuibia siri. Suala hili ni zito na gumu. Watu wanaendelea kuteketea kwa ajili yako, wakati uko gizani. Mwiba hutokea ulikoingilia. Tunaweza kuonana wapi nikudokolee hicho tulichonacho?”

“Tukutane New Africa…”

“Hapana.”

“Embassy.”

“Haifa?”

“Wewe unadhani wapi panafaa?” Joram alimuuliza.

“Hapohapo ulipo. Dakika tano baadaye. Uko wapi?”

Joram akaeleza.

Kama walivyo vijana wote wa Inspekta Kombora, kijana huyu ambaye alimtokea Joram Kiango dakika saba baadaye, alikuwa mkakamavu, mtulivu na mstaarabu kiasi kwamba haikuwa rahisi kumshuku kuwa ni kachero. Lakini si kwa Joram. Alitambua mara tu alipoingia katika mgahawa huo, gazeti mkononi na kuketi kama wateja wengine, akimsubiri mhudumu ambaye aliagizwa kuleta soda. Joram aliiacha meza yake na kuhamia meza aliyoketi bwana huyo.

“Ningeomba kuwa mwenyeji wako,” alimnong’oneza.

Mgeni huyo alimtazama Joram kwa mshangao kidogo, mshangao ambao uligeuka kuwa tabasamu baada ya kumtambua, licha ya mavazi yake bandia.

“Vizuri. Nadhani tunaweza kuzungumza hapahapa. Au?”

“Siyo pabaya.”

“Kwanza, ningeomba unielewe kuwa kwa kuzungumza nawe navunja amri zote za kazi yangu. Jambo ambalo natarajia kuzungumza ni siri kubwa sana ambayo haikutakiwa kuyafikia masikio ya raia yeyote yule. Mzee Kombora ataninyonga kwa mkono wake kama atasikia kuwa nimekudokezea. Natumaini unanielewa.”

“Vizuri sana,” Joram alimjibu.

“Hata hivyo, kama nilivyoeleza awali, sioni umuhimu wa kutokukuhusisha. Hakuna asiyefahamu mchango wako katika kupambana na udhalimu hapa nchini na kote duniani. Zaidi, sioni kwa nini watu wasio na hatia waendelee kuuawa kinyama wakati wewe umestarehe. Sidhani kama wewe u mvivu kiasi hicho. Natumaini tutakuwa bega kwa bega kupambana naye. Sawa.”

Joram aliona kama anayepotezewa muda kwa maelezo yasiyo ya msingi. Alichohitaji ilikuwa ni kitu kidogo sana. Kuelewa makachero wanaelewa nini juu ya adui huyo, ili aanze harakati. Kulala ndani kulikuwa kumemchosha.

“Unaonaje ukikata mahubiri na kunieleza kile ulichopanga kunieleza. Huoni kama tunapoteza muda?” alimuuliza.

“Yote ambayo naweza kukueleza yako katika gazeti hili. Ambacho hakimo ni kwamba sasa hivi Kakakuona yuko Zanzibar.”

“Kakakuona?”

“Inaonekana humfahamu,” kachero huyo alieleza. “Huyo ndiye mbaya wako. Anaweza kuwa ni mtu hatari zaidi ya kifaru aliyejeruhiwa. Anaua huku ametulia kama anakunywa maji baridi. Kifo chake ni muhimu kitokee kabla hajatuathiri,” alimaliza akiinuka huku akiliacha gazeti lake mezani.

“Wazulu wa kale hawakuwa na neno ‘asante’ katika msamiati wao, wala samahani, mimi na wewe tunaishi katika dunia na kucheza na kifo. Hatuna tofauti yoyote na Wazulu hao. Hivyo, sina la kusema…” Joram alimwambia kachero huyo huku akijaribu kumpa mkono ambao ulipuuzwa.

“Hunijui, sikujui. Sawa?”

“Sawa,” alijibu akitabasamu. Kisha, akalichukua gazeti hilo na kuhamia hoteli nyingine ambako nako pia alichukua meza ya kando, isiyo na mtu. Baada ya kupata kinywaji chake alitoa nakala sita za kopi za maandishi yaliyoonekana kama yaliyotoka kwenye faili.

Alizisoma kwa makini. Dakika mbili baadaye alizichanachana huku akiwa tayari amezichora akilini.

‘Kakakuona!’ aliwaza kwa hasira. ‘Anamtaka nini? Ameibuka kutoka wapi? Nani anamtumia? Kwa nini? Kwa nini? Kwa nini?’ alifoka kimoyomoyo.

Maswali yalikuwa mengi na marefu. Majibu yalihitaji muda. Kuwasiliana na wenzake wa nje. Kuwasiliana na benki, kujadiliana na nyumba za wageni, kufuata nyayo zake zinakotokea, kuwalipa maajenti wa nje, wenye kompyuta ambazo zinaweka kumbukumbu za vitendo vya watu kama hao n.k. Yote hayo yalihitaji muda, kitu ambacho Joram hakuona kama kilikuwepo. Kilichohitajika ni kumuua Kakakuona kwanza, na kuuliza maswali baadaye.

Baada ya kuwaza hayo, alifanya haraka kwenda Air Tanzania ambako walimvunja moyo kwa kutokuwa na ndege ambayo ingeondoka muda huo isipokuwa “Saa kumi na mbili za jioni.”

Shingo upande, akageuza njia na kuifuata Sea Express.

Boti ambayo ingeondoka mapema zaidi ilikuwa ni ya saa tisa mchana, saa nne baadaye. Joram alikata tiketi yake. Kisha, akatafuta simu ambapo alipiga moja Zanzibar na ya pili Nairobi. Zote hazikuwa na majibu ya mara moja. Akaahidi kupiga tena usiku huo.

Muda wa kusubiri Joram aliuona mrefu kupita kiasi. Kila dakika iliyopita ilizidi kumtia wasiwasi. Mara kwa mara akilini ilimjia picha ya Nuru akiwa na uso kama ulioteketezwa kinyama kama nyuso alizoziona katika picha alizotumiwa, jambo ambalo lilizidi kumtia hasira na kumfanya atamani kuruka, apae hadi Zanzibar, mbele ya Kakakuona.

***

“Ndege yake inatua mzee.”

Kombora aliarifiwa katika simu, kutoka Uwanja wa Ndege Zanzibar.

“Vizuri,” alijibu.

“Anashuka. Abiria ni mmoja tu. Amebeba mkoba. Mavazi yake ni kama uliyoyaeleza. Haonekani kama mtu mwenye wasiwasi wowote. Sasa hivi amefika meza ya Uhamiaji. Tumkamate?”

“Nimesema msimsogelee hadi nitakapotoa amri nyingine. Ni mtu hatari kuliko mnavyoweza kufikiria nyie,” Kombora alifoka. Kisha akaongeza “Endelea kuniarifu kila tukio na wekeni makachero wengi waangalie kila hatua yake. Angalieni asifahamu kuwa anafuatwa. Sawa?”

“Sawa”

Baada ya muda, “Amekodi teksi. Anaelekea mjini. Magari yetu mawili ya teksi yanamfuata kwa uangalifu.” Na baadaye “Inaelekea kama anafahamu kuwa anafuatwa. Lakini yaelekea hajali.”

Dakika kumi baadaye Kombora aliarifiwa ghafla, “Ameshuka mzee! Amechoropoka ghafla sehemu za Darajani. Haonekani alipo. Yaelekea amejichanganya katikati ya watu na kuingia mitaa ya Mji Mkongwe. Tufanyeje?”

“Asipotee.” Kombora alinguruma “Makachero wote wafanye kazi ya kumtafuta ili awe chini ya miwani yenu kila dakika. Nataka kujua anafanya nini, anakutana na nani, na kadhalika, na bado naonya asisogelewe wala kushtuliwa. Sawa?”

“Sawa, Afande.”
 
Back
Top Bottom