Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,891
- 155,884
Iron Dome ni mfumo wa ulinzi wa kisasa wa anga ambao ni bora na mathubuti kwa dunia ya leo uliotengenezwa na Israel kwa msaada kiasi kutoka Marekani kwa lengo la kulinda dhidi ya makombora yaliyofyatuliwa kutoka kwenye maeneo ya adui.
Mfumo huu ulianza kutumika rasmi mwaka 2011 na umekuwa sehemu muhimu ya ulinzi wa Israel dhidi ya vitisho vya makombora.
Iron Dome inafanya kazi o njia ifuatayo:
Kuchunguza: Mfumo huu una vituo vya radar vilivyosambazwa kote nchini Israel. Vituo hivi vinachunguza anga kwa kutambua makombora yanayotoka upande gani wa adui. Mara tu kombora linapogundulika, taarifa zote kuhusu harakati za mwelekeo hupitishwa katika kituo cha udhibiti wa mfumo.
Uchambuzi: Kituo cha udhibiti wa mfumo hufanya uchambuzi wa mwelekeo na harakati za kombora, ikiwa ni pamoja na kujua ni tishio la moja kwa moja kwenda maeneo ya raia au lah, hivyo mfumo huu unaweza kutambua kama kombola limaelekea maeneo yenye watu au yasiyo na watu. Kwa kuzingatia taarifa hizi, uamuzi wa ikiwa kuangusha kombora hilo au lah hufanywa. Kama haliendi kwenye makazi ya watu basi mfumo huo uachana na kombora hilo.
Kutungua: Ikiwa uamuzi wa kuangusha kombora unafanywa, mfumo wa Iron Dome unatumia makombora ya kudungua angani ambayo yanasafirishwa kwa kasi na kurushwa kuelekea uelekeo wa kombora la adui. Makombora haya yana teknolojia ya kipekee inayowezesha kuyagundua na kuyashambulia makombora ya adui hewani. Mfumo huu ukigundua kombora lenye tishio kwa raia au maeneo ya watu, mara moja utuma makombora ambayo yataenda kugongana na kombora la Adui angani na kisha kulipuka huko huko angani.
Kugundua mabaki: Baada ya makombora ya Iron Dome kudungua kombora la adui, mfumo huu unafuatilia vipande vilivyosalia vya kombora hilo na kuhakikisha kuwa hayana uwezo wa kuleta madhara.
Mfumo wa Iron Dome umethibitisha ufanisi wake katika kulinda maisha na mali za raia wa Israel dhidi ya vitisho vya makombora kutoka kwa makundi kama Hamas na Hezbollah. Hata hivyo, ni mfumo unaogharimu sana na hutumia rasilimali nyingi kwa kila kombora lililolengwa.
IRON DOME utumika kupambana na kutungua makombora ya umbali mfupi yani short range missiles. Huku kwa makombora ya masafa ya kati na masafa marefu (medium range and long range missiles) mfumo mwingine wa kujilinda ujulikanao kama ARROW SYSTEM hutumika kutungua na kuyaharibu makombora ya adui yakiwa angani. Hivyo mifumo hii miwili usaidia kulinda makazi ya watu dhidi ya mashambulizi ya makombora.
Mfumo huu ulianza kutumika rasmi mwaka 2011 na umekuwa sehemu muhimu ya ulinzi wa Israel dhidi ya vitisho vya makombora.
Iron Dome inafanya kazi o njia ifuatayo:
Kuchunguza: Mfumo huu una vituo vya radar vilivyosambazwa kote nchini Israel. Vituo hivi vinachunguza anga kwa kutambua makombora yanayotoka upande gani wa adui. Mara tu kombora linapogundulika, taarifa zote kuhusu harakati za mwelekeo hupitishwa katika kituo cha udhibiti wa mfumo.
Uchambuzi: Kituo cha udhibiti wa mfumo hufanya uchambuzi wa mwelekeo na harakati za kombora, ikiwa ni pamoja na kujua ni tishio la moja kwa moja kwenda maeneo ya raia au lah, hivyo mfumo huu unaweza kutambua kama kombola limaelekea maeneo yenye watu au yasiyo na watu. Kwa kuzingatia taarifa hizi, uamuzi wa ikiwa kuangusha kombora hilo au lah hufanywa. Kama haliendi kwenye makazi ya watu basi mfumo huo uachana na kombora hilo.
Kutungua: Ikiwa uamuzi wa kuangusha kombora unafanywa, mfumo wa Iron Dome unatumia makombora ya kudungua angani ambayo yanasafirishwa kwa kasi na kurushwa kuelekea uelekeo wa kombora la adui. Makombora haya yana teknolojia ya kipekee inayowezesha kuyagundua na kuyashambulia makombora ya adui hewani. Mfumo huu ukigundua kombora lenye tishio kwa raia au maeneo ya watu, mara moja utuma makombora ambayo yataenda kugongana na kombora la Adui angani na kisha kulipuka huko huko angani.
Kugundua mabaki: Baada ya makombora ya Iron Dome kudungua kombora la adui, mfumo huu unafuatilia vipande vilivyosalia vya kombora hilo na kuhakikisha kuwa hayana uwezo wa kuleta madhara.
Mfumo wa Iron Dome umethibitisha ufanisi wake katika kulinda maisha na mali za raia wa Israel dhidi ya vitisho vya makombora kutoka kwa makundi kama Hamas na Hezbollah. Hata hivyo, ni mfumo unaogharimu sana na hutumia rasilimali nyingi kwa kila kombora lililolengwa.
IRON DOME utumika kupambana na kutungua makombora ya umbali mfupi yani short range missiles. Huku kwa makombora ya masafa ya kati na masafa marefu (medium range and long range missiles) mfumo mwingine wa kujilinda ujulikanao kama ARROW SYSTEM hutumika kutungua na kuyaharibu makombora ya adui yakiwa angani. Hivyo mifumo hii miwili usaidia kulinda makazi ya watu dhidi ya mashambulizi ya makombora.