Goli ni Goli; la Mpendazoe nalo Goli!

Kuwakosesha wapiga kura wake uwakilishi katika kipindi hiki ambacho bunge la bajeti ndio kikao muhimu sana kilichobaki, tena mwaka wa fedha wa mwisho katika tenure yake, ni usaliti. Ni kujijali maslahi binafsi kuliko ya waliomchagua. Hajaikimbia CCM huyu, kawatosa wapiga kura wake. Angekuwa mwema huyu, angewawakilisha vema wananchi amalize mkataba wake waliompa, kisha aondoke.

Ni sawa na baba kusikia vishindo nje usiku, kisha anaikimbia nyumba na kuacha mlango wazi ilhali wanaomtegemea wako ndani! Usaliti wa dhahiri.

Hao mafisadi anaowakimbia ndio aliowaachia jimbo lake la Kishapu wajivinjari watakavyo! What a shame! And you call this patriotism! Amechemsha bana!

Maslahi gani binafsi kwa kuhamia upinzani? Kuna usaliti mkubwa kuliko ule wa kusaliti nafsi yako? Kuna mijitu kibao ambayo dhamira zao zinawasuta kwa kuwa CCM lakini imeshindwa kutoka kwa sababu mbalimbali binafsi na za kimwili, hawa ndio wasaliti!!
 
MTOTO WA MFALME ANGOJE NAYEYE KUVIKWA UFALME LAKINI HANA AKILI YA HOJA KATIKA TAIFA LETU, KWAKUWA MASKINI WA TANZANIA WAMENYAMAZA NAYE ANASEMA,TANGU LINI , CHA MSINGI MABWANYENYE WATENGE PESA ZA KUNUNUA UONGOZI , ILA OMBI LETU WASIENDELEE KUKEJELI WATANZANIA KWANI NI KITU KITACHOBADILI HISTORIA YA TZ, WAKUMBUKE KIZAZI CHA MASIKINI KIMEKUBALI KUTESEKA ILI MAFISADI WAISHI SALAMA , MAISHA YAO NI HISANI YA MASIKINI SASA NAWAO WAUZE NCHI KIMYA KIMYA ,

“Cruel leaders are replaced only to have new leaders turn cruel!”
KIZAZI CHA KIFALME KINYAMAZE KIMYA KAMA WAFALME WA UINGEREZA NA SWAZILAND , WAMWACHE MPENDAZOE AWE HURU KWANI WEZI HAWANA HAKI KUMKIMBIZA MWIZI MWENZAO,
WAFALME NYAMAZENI MTESE MASIKINI IMSITOE KEJELI
 
Sometimes siasa inafurahisha sana...!Ukiona mtu ananyolewa kwa wembe bila maji halafu haguni basi huyo shujaa.....lakini kwa hali ya kawaida yale maumivu lazima ugune. Ni dhahiri CCM watasema mengi na wana haki ya kuguna
 
-Unajua sipendi kujadili watu negatively,let me spare him

Hao vijana waliotoa tamko ni wanafiki tu,hivi umaskini wa Bongo umetufanya hata kupoteza utu?Yaani hata tunaweza ku-mortgadge maisha yetu?Yaani hawana haya badala ya kuona watu kama akina CHENGE,RA kama mzigo vile wanamuona mpendazoe mzigo...

Nimesema tena sijui tupeperushe bendera zetu upside down maanake tuna janga kubwa mno,hata priorities zetu ni upside down.kupeperusha bendera zetu juu ni unafiki tu sasa
 
Hilo goli la Mpendazoe kajifunga mwenyewe. Yaani imekula kwake.

Hiyo ndio tafsiri halisi ya mzalendo/ patriot. Mtu ambaye haweki maslahi yake mbele.
Wewe unadhani hajui kuwa kwa kiasi fulani imekula kwake? Alichokusudia ni kufikisha ujumbe pia, na ninaamini "message delivered to multiple recipients", yaani kwa CCM, Fisadis na wananchi. Ila message si hiyo hiyo kwa kila recipient!!
 
Kuwakosesha wapiga kura wake uwakilishi katika kipindi hiki ambacho bunge la bajeti ndio kikao muhimu sana kilichobaki, tena mwaka wa fedha wa mwisho katika tenure yake, ni usaliti. Ni kujijali maslahi binafsi kuliko ya waliomchagua. Hajaikimbia CCM huyu, kawatosa wapiga kura wake. Angekuwa mwema huyu, angewawakilisha vema wananchi amalize mkataba wake waliompa, kisha aondoke.

wale wabunge wa kuteuliwa na wa viti maalum wanamuwakilisha nani?
 
Maslahi gani binafsi kwa kuhamia upinzani? Kuna usaliti mkubwa kuliko ule wa kusaliti nafsi yako? Kuna mijitu kibao ambayo dhamira zao zinawasuta kwa kuwa CCM lakini imeshindwa kutoka kwa sababu mbalimbali binafsi na za kimwili, hawa ndio wasaliti!!

Kuhamia upinzani si tatizo hapa, tatizo ni kilichompeleka huko na muda alipotimiza azma hiyo ya kuhama. Amelitelekeza jimbo lake, kawaacha wananchi wake bila uwakilishi ili atimize azma ya kuhamia upinzani. Hayo ndiyo maslahi binafsi ninayozungumzia: kupata uanachama mpya kwa gharama ya jimbo kukosa mbunge. Ameshindwa nini kusubiri bunge livunjwe? Nani atawawakilisha wananchi wa Kishapu katika bunge hili la bajeti?

Ni maslahi binafsi kwa sababu anaamini katika chama hicho alichohamia atapata nafasi ya kutelekeza malengo yake, ambayo ukiyapima dhidi ya maslahi ya watu wa Kishapu waliomchagua, bado hayatakidhi matarajio ya waliomtuma bungeni. Ni ubinafsi tu. Na anajua kwa nini ameshindwa kusubiri hadi bunge livunjwe, bado ni maslahi yake binafsi na si ya wapigakura wake wala ya taifa.
 
Kuhamia upinzani si tatizo hapa, tatizo ni kilichompeleka huko na muda alipotimiza azma hiyo ya kuhama. Amelitelekeza jimbo lake, kawaacha wananchi wake bila uwakilishi ili atimize azma ya kuhamia upinzani. Hayo ndiyo maslahi binafsi ninayozungumzia: kupata uanachama mpya kwa gharama ya jimbo kukosa mbunge. Ameshindwa nini kusubiri bunge livunjwe? Nani atawawakilisha wananchi wa Kishapu katika bunge hili la bajeti?

Na wale waliobakia CCM wamefanya hivyo siyo kwa maslahi binafsi? Kwani wabunge wa kuteuliwa na wale wa viti maalumu wanamuwakilisha nani? Kwani Mbunge amewekewa mipaka ya kuwakilisha kiasi kwamba akitokea mbunge wa Bariadi kufuatilia swala la Kishapu atakataliwa? Ndio maana wanaitwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano!


Ni maslahi binafsi kwa sababu anaamini katika chama hicho alichohamia atapata nafasi ya kutelekeza malengo yake, ambayo ukiyapima dhidi ya maslahi ya watu wa Kishapu waliomchagua, bado hayatakidhi matarajio ya waliomtuma bungeni. Ni ubinafsi tu. Na anajua kwa nini ameshindwa kusubiri hadi bunge livunjwe, bado ni maslahi yake binafsi na si ya wapigakura wake wala ya taifa.

Hakuna tatizo kuwa na maslahi binafsi kwani hawa wanaompinga wanafanya hivyo kwa maslahi ya nani kama siyo yao binafsi?
 
Hiyo ndio tafsiri halisi ya mzalendo/ patriot. Mtu ambaye haweki maslahi yake mbele.
Wewe unadhani hajui kuwa kwa kiasi fulani imekula kwake? Alichokusudia ni kufikisha ujumbe pia, na ninaamini "message delivered to multiple recipients", yaani kwa CCM, Fisadis na wananchi. Ila message si hiyo hiyo kwa kila recipient!!

Kumbe kuwasaliti wapiga kura wake ndio sifa? Huyu hana tofauti na ile hadithi ya Biblia ya mchungaji mbaya, ambaye alipoona mbwa mwitu wametishia kondoo wake alikimbia na kuwaacha kondoo nyikani waliwe na mbwa mwitu.

Yaani huyu anawakimbia mafisadi badala ya kupambana nao? Na anawaacha wananchi wake waliomchagua waendelee kubaki chini ya hao mafisadi? Mwoga huyu, tena mbinafsi sana, 'anakimbiza ubawa wake'!
 
huo ushauri wa kutotumia pesa kwenye kampeni akampe babake kwanza si shinyanga, mbona ana nguvu kuliko akina madaraka nyerere, william mkapa au abbas mwinyi kunani............................???!!!!!
 
wale wabunge wa kuteuliwa na wa viti maalum wanamuwakilisha nani?

Hao wa viti maalumu na wa kuteuliwa wanajielewa kuwa utii wao ni kwa mwenyekiti wao wa chama ndiye aliyewateua, so wakikimbia lindo wanakuwa wamemkomoa huyo bosi wao. Lakini mbunge wa kuchaguliwa kama Mpendazoe anapokimbia lindo kama alivyofanya anakuwa amewakomoa wananchi ambao ndio anaodai anawatetea.

Charity begins at home. Kama mtu anaweza kutelekeza wananchi wake waliomchagua kwa kisa tu cha kutaka umaarufu zaidi, ataaminika tena kweli huyo?
 
Mimi bado naona chama hiki kama moto wa kifuu hivi maana sijui kama kweli wataweza au ni presha tu za hapa na pale maana sijajua ni kitu gani. ila kama amefanya hivyo kwanini asiende CHADEMA au vyama vingine au ndio geresha na uchaguzi ukiisha atarudi CCM. Mimi naona kama vile kipo kwa ajili ya kuua nguvu ya CHADEMA
 
Nimetonywa na mzee wa siasa za bongo kuwa Kina Sitta, Lucas Seleri, Mwakyembe n.k wana card mbili mbili za CCM na chama kingine cha upinzani mambo yakienda kumbo wanahamia CCJ ama CHADEMA pia uchaguzi mwaka huu kutakuwa na vurugu kama la kule Kenya tena si la kikabila bali ni la kati ya wakristo na waisilamu..
Kauli nzito hizi mkuu, hebu tufafanulie.
 
Hao wa viti maalumu na wa kuteuliwa wanajielewa kuwa utii wao ni kwa mwenyekiti wao wa chama ndiye aliyewateua, so wakikimbia lindo wanakuwa wamemkomoa huyo bosi wao. Lakini mbunge wa kuchaguliwa kama Mpendazoe anapokimbia lindo kama alivyofanya anakuwa amewakomoa wananchi ambao ndio anaodai anawatetea.

Charity begins at home. Kama mtu anaweza kutelekeza wananchi wake waliomchagua kwa kisa tu cha kutaka umaarufu zaidi, ataaminika tena kweli huyo?

kwanini unafikiri mahali pekee pa kuwatetea wananchi ni Bungeni? Hivi unafikiri mipango yote ya maendeleo iliyokuwa ifanyike kishapu itaachwa kwa sababu hakuna Mbunge?
 
Mimi bado naona chama hiki kama moto wa kifuu hivi maana sijui kama kweli wataweza au ni presha tu za hapa na pale maana sijajua ni kitu gani. ila kama amefanya hivyo kwanini asiende CHADEMA au vyama vingine au ndio geresha na uchaguzi ukiisha atarudi CCM. Mimi naona kama vile kipo kwa ajili ya kuua nguvu ya CHADEMA

Kama Chadema itapoteza nguvu yake si kwa sababu ya CCJ, CCM au chama kingine chochote bali kwa ajili yake chenyewe.
 
Hivi wewe Mtu B

kilichokuuma zaidi ni kipi kama Mpendazoe kafulia utamsaidia nini au familia yake utaisaidiaje kati ya yeye na wewe nani anatakiwa kuumia zaidi maana toka jana ni wewe tu na Mpendazoe inavyoonekana imeku tachi sana otherwise ungekuwa umepumzika hata kidogo kwa sababu umezungumza hadi hoja zimekuishia umebaki kafulia kafulia anyway ngoja nitoke kidogo usiondoke endelea
 
Na wale waliobakia CCM wamefanya hivyo siyo kwa maslahi binafsi? Kwani wabunge wa kuteuliwa na wale wa viti maalumu wanamuwakilisha nani? Kwani Mbunge amewekewa mipaka ya kuwakilisha kiasi kwamba akitokea mbunge wa Bariadi kufuatilia swala la Kishapu atakataliwa? Ndio maana wanaitwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano!




Hakuna tatizo kuwa na maslahi binafsi kwani hawa wanaompinga wanafanya hivyo kwa maslahi ya nani kama siyo yao binafsi?

Ni kweli wanaompinga wanafanya hivyo kwa maslahi binafsi, lakini yeye ndiye aliyeonesha mfano mbaya wa kukiuka mkataba na wananchi wake na kuwaacha bila mwakilishi katika kipindi tete kama hiki.

Na la pili, nazungumzia jinsi alivyoondoka, amejipeleka mahali panapoonekana wazi kuwa hawezi kupambana tena, chama hicho hakitashiriki uchaguzi mwaka huu, so kama wananchi wake wangependa wamtume tena bungeni kwa maslahi yao, keshawanyima nafasi hiyo. Sasa kama maslahi ya wananchi ni yeye kuwa mbunge, naye ameikimbia nafasi hiyo, ni maslahi gani anayoshughulikia kama si ya kwake binafsi? Ndiyo maana nasema amejitoa katika timu inayoshiriki ligi akaenda kwenye timu ya 'mchangani'. Sisemi hiyo timu ya 'mchangani' haitakuja kushiriki ligi siku moja, but then it might be too late, the cause for which he was fighting might be lost already. Ameharibu huyu, kubalini tu. Huo uanzishwaji wa CCJ kwanza umekosea timing, walikuwa wapi 3 years ago?
 
Back
Top Bottom