Goli ni Goli; la Mpendazoe nalo Goli!

GOLI NI GOLI HATA LA MPENDAZOE NALO GOLI!



Na. M. M. Mwanakijiji


Kwenye kandakanda kuna magoli yanaudhi sana na yanakera. Kuna magoli ambayo mtu unakubali tu kuwa goli hilo “halina utata” na mnajitahidi kurudisha majibu.

Lakini, wakati mwingine magoli mengine yanamfanya mtu usikie donge kooni, presha ipande na kushuka na hata kuna mengine yanaweza kufanya timu nzima muende kumzonga mwamuzi kwani goli lililokubaliwa linaonekana kama limependelewa.

Bahati mbaya goli ni goli liwe la kuudhi au kukera lakini alimradi limekubaliwa basi wakati wengine wanasikia machungu wajue kabisa ipo timu nyingine inashangilia hata kama na wao wanaona kwa kweli lile goli lilikuwa baya.

Mbunge wa Kishapu Mhe. Fred Mpendazoe kawafunga bao CCM tena bao la kuudhi, kukera, kupandisha hasira na kwa kila kipimo bao ambalo CCM ile ya zamani isingeweza kufungwa kijinga hivi. Bao alilowafunga naweza kulilinganisha na bao la “tobo” au linakaribiana na bao la kipa “kupigwa kanzu”! Mwingine anaweza kusema “kapigwa kanzu halafu akapigwa tobo”.

Kujiondoa kwa Mpendazoe kutoka Chama cha Mapinduzi kwa sababu yeyote ile kwa namna aliyotoka kunatufanya tusubiri kwa hamu maelezo ya CCM ya kutufafanulia kwanini goli hili siyo goli.Chama cha Mapinduzi bila ya shaka ambacho kina wasomi na watu waliobobea katika propaganda ya uzugaji kwa maneno kinakaribiwa na wakati mgumu wa kuelezea kujiondoa kwa Mpendazoe na bila ya shaka wanachama wengine huko mbeleni.

ref_cornerkick_shadowgram.gif
Goli kamfunga nani...?

kama ndio analogous yako...basi ni very low..!!!

Real change haiwezi kuletwa kwa Zima moto....!!!

Wale wote walioleta Mabadiliko walikuwa wameweka "Milestone" za Kufikia ktk Mabadiliko....!!! sio hawa "Materialist na Ma-oppurtunist"....!!!
 
Goli kamfunga nani...?

kama ndio analogous yako...basi ni very low..!!!


Real change haiwezi kuletwa kwa Zima moto....!!!

Wale wote walioleta Mabadiliko walikuwa wameweka "Milestone" za Kufikia ktk Mabadiliko....!!! sio hawa "Materialist na Ma-oppurtunist"....!!!

- Mkuu chuma heshima yako sana ndugu yangu, na with all due respect hakukuwa na sababu ya kejeli kwa analysis ya member mwenzako, wewe ni kuweka analysis yako tuachie sisi wengine tuamue ya nani ni bora kati yako na Mkulu Mwanakijiji.

- Mpira wanaoufaidi vizuri sana ni watazamaji, sio wachezaji na ndugu yangu heshima ni kitu cha bure sana, the CCJ's subject ndio hasa mustakabali na masilahi ya taifa either yapo au hayapo!

Respect.


FMEs!
 
Naamini akina Mpendazoe wengine bado wapo CCM, wanasubiri wavute masurufu yao kisha ndo watimke. Mpendazoe ameonyesha ujasiri wa hali ya juu kwa kutanguliza maslahi ya Taifa kuliko yake peke yake. Tusubiri Mh. Seleli, kadai ahami ng'o CCM lakini najua hiyo ni lugha ya wanasiasa tu. Jina lake likipigwa chini kwenye kura ya maoni au kuondolewa na vikao husika nina hakika atachomoka tu.
 
ref_cornerkick_shadowgram.gif


Mwanakijiji una vijembe ndugu yangu ha ha!Yani ngoma iwekwe kati,saafi sana nimeikubali,halafu inarelate sana na wabongo na hivyo message sent,bao ni bao tu,hata la kisigino,refarii kwa heshima na taadhima anaelekeza ngoma kati!sikujua unapenda soka neways,coz sijawahi kukuona kwenye jukwaa la michezo......Chandimu uliupiga mkuu?Ha ha!
 
Goli kamfunga nani...?

kama ndio analogous yako...basi ni very low..!!!

Real change haiwezi kuletwa kwa Zima moto....!!!

Wale wote walioleta Mabadiliko walikuwa wameweka "Milestone" za Kufikia ktk Mabadiliko....!!! sio hawa "Materialist na Ma-oppurtunist"....!!!

hujawaona waliofungwa wanavyojaribu kufafanua kwa jinsi gani siyo "goli"?
 
ref_cornerkick_shadowgram.gif


Mwanakijiji una vijembe ndugu yangu ha ha!Yani ngoma iwekwe kati,saafi sana nimeikubali,halafu inarelate sana na wabongo na hivyo message sent,bao ni bao tu,hata la kisigino,refarii kwa heshima na taadhima anaelekeza ngoma kati!sikujua unapenda soka neways,coz sijawahi kukuona kwenye jukwaa la michezo......Chandimu uliupiga mkuu?Ha ha!

wenzako wanaonifahamu tangu enzi hizo wananitambua kwa jina la "nyanda"... mtu aliyeweka rekodi ya "kufuta penati" hadi kuambiwa "ameazimwa"...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom