Fikra za Mwalimu: Hizi hapa.. mzikubali au mzipinge!

I said no spin zone. Mwanakijiji aliniuliza kuhusu Africa. Na nikasema maoni yangu kuwa tuache longolongo.

Na kuhusu IMF, IMF imesaidia. Bila IMF tungekuwa tunavaa viroba.

Kwa hiyo hii ndiyo solution uliyokuja nayo toka kwenye drawing board. IMF?
 
Afrika lazima ibadilike; kutoka bara ambalo linasubiri matukio nje yake yenye kusababisha mabadiliko kuelekea bara ambalo watu wake wanasimamia mabadiliko yao wao wenyewe.

Mkuu wangu, binafsi siwezi kujibu kila unalosema ila nitajaribu kuchota kidogo kidogo, Afrika haiwezi na bado haijafikia uwezo wa kuamua maamuzi yake, miaka 23 ya utawala wake Mwalimu alishindwa kulibadilisha hilo, matokeo yake yalikuwa sisi kutegemea upepo wa the Cold War, ilipokwisha tu na sisi ujeuri wetu ukaisha na yeye akajiuzulu, na kuishia kwenda kutibiwa UK, badala ya Muhimbili kila leo, sasa wasomi wa maandishi ya Mwalimu, si watataka kuja bongo kujionea the works za mkali wa intellectulism za change katika Afrika, exactly kuna nini cha kuonyesha? Leo Tanzania kuna nini cha kuonyesha ili kuthibitisha umahiri wa Mwalimu, on change katika baara la Afrika?

Ni nini kuarticulate ukweli kuwa lazima tuwe "a continent which challenges the environment and adapts it to man's need." Hakuna aliyeonesha ubaya wa fikra hii.

Hakuna aliyeonyesha ubaya wa hayo mawazo kama vile ambavyo na wewe hujaonyehsa uzuri wa hayo mawazo, Afrika tuta-challenge our environment kwa kutumia nyenzo ipi? Ni wapi mkuu umeonyesha jinsi Mwalimu, alivyofanikiwa sio tu kwenye hayo mawazo, bali kwa matendo chini ya utawala wake wa miaka 23, faida ya kunganga'ania mawazo yaliyoshindwa hasa ni nini? Maana the only evidence we have kuwa Mwalimu, alijaribu ku-challenge environment ni vijiji vya ujamaa, ambavyo sio siri kuwa hakufanikiwa hata kidogo, sasa why even discuss it, yes ni maneno mazito sana na ya kutisha as far as wasomi they go, lakini sisi wananchi na taifa, bado tunaendela kusubiri World Bank na IMF watakachoamua, kwa sababu pamoja na maneno yote hayo, Mwalimu hakutoa mfano hata how to go about it,

Luther, alijitoa kwenye Catholic Church, akatoa sababu zake nyingi za kujitoa kuwa ni pamoja na kuamini kuwa, then kanisa lile lilikuwa linahubiri ujamaa au umasikini na kwamba Mungu was not down with, akatoa mawazo yake mapya ambayo alisema ndio hasa mawazo ya Mungu kwa bin-adam, kwamba Mungu hajawahi kutaka bin-adam awe masikini, na ndio hasa moja ya chanzo cha Capitalism, now haya ndio mawazo ya change na environment na man's needs, lakini sasa haya ya Mwalimu, maneno tuuu

I mean unless kuna something sielewi mkuu, lakini ninaaamini at this time and moment wa-Afrika tunahitaji matendo maana maneno tumesema ya kutosha!
 
Kuhusu suala la Afrika kubadilika unakubali fikra hizo au zinamakosa mahali?

Hizo fikra zina makosa makubwa mengi sana, pamoja na sababu nyingi moja ni kwamba Afrika haiwezi kubadilika for the sake ya kubadilika tu, lazima kuwe na muongozo, muongozo hakuna, mfano hakuna, sasa tutabadilika kwa mfano gani na kwa njia gani?

Fikra hizi haziwezi kudumu, maana ni unrealistic kwa maoni yangu!
 
.... sasa wasomi wa maandishi ya Mwalimu, si watataka kuja bongo kujionea the works za mkali wa intellectulism za change katika Afrika, exactly kuna nini cha kuonyesha? Leo Tanzania kuna nini cha kuonyesha ili kuthibitisha umahiri wa Mwalimu, on change katika baara la Afrika?



.....

Mkuu FMES.

Ina maana unamaanisha haya unayosema kuwa hakuna chochote cha kuonyesha aliyofanya Nyerere?

1. Hakuna watu waliosoma bure wakati wa Nyerere?
2. Hakuna hospitali zilizojengwa na serikali?
3. Hakuna majengo ya serikali yaliyojengwa?
4. Hakuna barabara hata moja iliyojengwa?
5. Hakuna eneo hata moja lilipatiwa umeme?
6. Hakuna watu wazima waliosomeshwa na wakajua kusoma?
7. Una maanisha hakuna chochote kabisa kilichofanyika?

Jamani wakati mwingine tujaribu kuwa fair. Ni kweli kuwa sera za mwalimu zilishindwa kufanya kazi kwa kiwango fulani lakini si kweli kuwa hakuna chochote ambacho hakufanya kabisa......

Hao watu wanaokuja Afrika leo, je hawaoni kuwa Nyerere aliacha kuchimba madini kwa vizazi vijavyo tofauti na Mobutu ambaye yeye na familia yake walifaidika na madini karibu yote ya Zaire na kuwaachia wanazaire ya leo makorongo na mabonde matupu?

Serikali zinajenga juu ya serikali, Nyerere aliwaomba kina Mwinyi na Mkapa kuacha mabaya aliyofanya na kuchukua mazuri. Je nini kimefanyika kuanzia mwalimu astaafu? Katika hili je bado wa kulaumiwa ni mwalimu?
 
Tunapozungumzia kuzingatia misingi ya utawala wa sheria, kuwa na maadili n.k tunachosema ni kuwa vitu hivyo havipo sasa na tunataka tubadilike. Hivyo tunakubaliana na Mwalimu kuwa we need to change our "attitudes and practices to accord with the objectives." Kuna ubaya gani katika ukweli huu mwingine kuwa kama kweli tunataka kufikia malengo yetu hatuna budi kubadilika? Hakuna aliyeonesha hadi hivi sasa.

1. Kabla ya kushauri kubadilika kisheria, Mwalimu alipaswa kusema wazi kwa nini baada ya miaka 23 ya uhuru under utawala wake hatuheshimu sheria, maana wewe mwenyewe unasema kuwa vitu kama sheria havipo sasa swali linapaswa kuwa why? yaani chanzo chake ni nini wakati mtoa mawazo yako ya change alikuwa rais mwenye uwezo wote wa kuweka mawazo yake hayo ambayo sasa unayaita kuwa ni superior na tunahitaji kuyarudia?

Halafu ulipaswa kueleza madhara ya kutokuwa na hivyo vitu kama sheria kwa karibu muda wote huo, mpaka hiyo change itakapokuja, ni nini madahara yake? Na how far yame-reach kwenye jamii na how long hiyo change itachukua kuweza kufagia the effect baada ya kuishi bila sheria, mpaka siku ya change ya mawazo ya Mwalimu itakapofika?

Labda alipaswa kusema kuwa yeye kwanza alipaswa kubadilika ili awe mfano kwetu, maana maneno tu alishindwa kuyatfsiri kwa vitendo.
 
1. Kabla ya kushauri kubadilika kisheria, Mwalimu alipaswa kusema wazi kwa nini baada ya miaka 23 ya uhuru under utawala wake hatuheshimu sheria, maana wewe mwenyewe unasema kuwa vitu kama sheria havipo sasa swali linapaswa kuwa why? yaani chanzo chake ni nini wakati mtoa mawazo yako ya change alikuwa rais mwenye uwezo wote wa kuweka mawazo yake hayo ambayo sasa unayaita kuwa ni superior na tunahitaji kuyarudia?

Halafu ulipaswa kueleza madhara ya kutokuwa na hivyo vitu kama sheria kwa karibu muda wote huo, mpaka hiyo change itakapokuja, ni nini madahara yake? Na how far yame-reach kwenye jamii na how long hiyo change itachukua kuweza kufagia the effect baada ya kuishi bila sheria, mpaka siku ya change ya mawazo ya Mwalimu itakapofika?

Labda alipaswa kusema kuwa yeye kwanza alipaswa kubadilika ili awe mfano kwetu, maana maneno tu alishindwa kuyatfsiri kwa vitendo.

Wakati mwingine twende kwa mifano jamani. Ni nini kinachofanyika leo ambacho ni mwendelezo wa sera za utendaji za Nyerere. Nikiona kwa haraka, yafuatayo yamefanyika kinyume cha utashi wa Nyerere:

1. Kuuza mashirika ya umma
2. Kuruhusu makampuni ya kigeni kumiliki njia kuu za uchumi
3. Kuuza migodi ya madini kwa wageni huku wazawa wakinyanganywa
4. Kuruhusu viongozi kuwa na biashara binafsi

Na mengineyo mengi ambayo ni kinyume na sera za Nyerere. Sasa haya mawazo ya kuwa inabidi sumu ya Nyerere itoke ndio tuendelee yana msingi upi?
 
mungu akubaliki msee FMES, maana huyu bwana MKJJ mie hata sielewi motive(s) yake ni nini!!?? inatisha namna hii, yaani mjuvi kama huyu aweza kuwa bwiga namna hii, sasa hao wakina bwana kabwela huko main street wapoje sijui!? nyerere alikuwa na miaka 23 ya kutengeneza legacy yake......... he failed and failed miserably, yaani hata 'F' hakupata!! full stop.

Jamani sidhani kama kutumia lugha za ubwiga kutasaidia chochote kwenye huu mjadala. Yaani ina maana mtu anayejaribu kuona huo upande mzuri wa Nyerere ni bwiga?
 
Labda niulize swali la haraka haraka kidogo wakati mjadala huu ukiendelea. Je ikiamuliwa kuwa Nyerere alishindwa kabisa na wale wote wanaomtetea ni mabwiga. Na pia je ikiamuliwa kuwa Nyerere afutwe kabisa kwenye historia cha Tanzania maana yeye ndiye chanzo cha matatizo yote ya watanzania na waafrika wengine kama wamalawi, wazaire, wazambia, wasumbiji ambao wana matatizo kama ya Tanzania leo. Je Tanzania itafaidika nini? Je kutakuwa na mabadiliko yoyote ukichukulia kuwa viongozi wa ccm kina Kikwete na wenzao hawafuati sera au chochote alichosema na kufanya Nyerere kwa sasa?
 
KIONGOZI ANAPIMWA KWA HIBA; NYERERE HAJAACHA HIBA

Azimio la Arusha: Limechanwa! Tuna Azimio la Zanzibar.

Mfumo wa Chama Kimoja: Falsafa za kuhodhi siasa zilitupiliwa mbali 1992

Siasa za Ujamaa: Zilitoswa kabla hata hajaacha madaraka

Sera za Kujitegemea:
aaaaaah… Tanzania haijawahi kujitegemea. Hakuwa mkweli hapa!

Elimu ya Bure:
Siku hizi unalipia elimu

Uzembe na Uzururaji:
Hakuna sheria za Kangaruu kama hizo siku hizi

Maadili ya Viongozi:
Yeye mwenyewe alisema wananuka rushwa

Azimio la Iringa: Hakuna anaeongelea 'Siasa ni Kilimo' siku hizi. Tafadhali bwana!

Vijiji Vya Ujamaa: Kuna cha kusema hapa?

Heshima ya Nchi kwa Misimamo Mikali:
Siasa yetu inaandikwa na wahisani

Umiliki wa Njia Kuu za Uchumi:
Tumeuza kila kampuni

Suti za Kichina:
Zaidi ya Malecela na Kingunge hakuna anae taka upuuzi wa Kichina!


Muungano: hapa kaacha hiba

Umoja wa Kitaifa:
na hapa kaacha hiba
 
KIONGOZI ANAPIMWA KWA HIBA; NYERERE HAJAACHA HIBA

Azimio la Arusha: Limechanwa! Tuna Azimio la Zanzibar.

Mfumo wa Chama Kimoja: Falsafa za kuhodhi siasa zilitupiliwa mbali 1992

Siasa za Ujamaa: Zilitoswa kabla hata hajaacha madaraka

Sera za Kujitegemea:
aaaaaah… Tanzania haijawahi kujitegemea. Hakuwa mkweli hapa!

Elimu ya Bure:
Siku hizi unalipia elimu

Uzembe na Uzururaji:
Hakuna sheria za Kangaruu kama hizo siku hizi

Maadili ya Viongozi:
Yeye mwenyewe alisema wananuka rushwa

Azimio la Iringa: Hakuna anaeongelea 'Siasa ni Kilimo' siku hizi. Tafadhali bwana!

Vijiji Vya Ujamaa: Kuna cha kusema hapa?

Heshima ya Nchi kwa Misimamo Mikali:
Siasa yetu inaandikwa na wahisani

Umiliki wa Njia Kuu za Uchumi:
Tumeuza kila kampuni

Suti za Kichina:
Zaidi ya Malecela na Kingunge hakuna anae taka upuuzi wa Kichina!


Muungano: hapa kaacha hiba

Umoja wa Kitaifa:
na hapa kaacha hiba


Huu ni uthibitisho kuwa hakuna chochote cha Nyerere kinachoendelea kwenye maisha ya watanzania. Sasa kama ni kweli, hizi lawama na vilio vya kila siku kuwa nyerere hivi na vile ni za nini?
 
Ina maana unamaanisha haya unayosema kuwa hakuna chochote cha kuonyesha aliyofanya Nyerere?

1. Hakuna watu waliosoma bure wakati wa Nyerere?
2. Hakuna hospitali zilizojengwa na serikali?
3. Hakuna majengo ya serikali yaliyojengwa?
4. Hakuna barabara hata moja iliyojengwa?
5. Hakuna eneo hata moja lilipatiwa umeme?
6. Hakuna watu wazima waliosomeshwa na wakajua kusoma?
7. Una maanisha hakuna chochote kabisa kilichofanyika?

Jamani wakati mwingine tujaribu kuwa fair. Ni kweli kuwa sera za mwalimu zilishindwa kufanya kazi kwa kiwango fulani lakini si kweli kuwa hakuna chochote ambacho hakufanya kabisa......

Mkuu wangu MWK,

Heshima mbele, mimi sio intellectual, ninakubali kuwa kuna mazuri aliyoyafanya Mwalimu, ambayo mpaka leo yanaweza kuhesabiwa, lakini tatizo ni kwa yale ambayo hakuyafanya kwa sababu ya mapungufu ya kibin-adam, huku akiendelea kuimba nyimbo za change ambazo hata yeye mwenyewe hakuweza kuzifanya kwenye miaka 23 ya utawala wake, sasa tutegemee nini kwa wananfunzi wake wanaotawala miaka 10 tu per term?

Kuna ambayo hujayataja ambayo ni ya muhimu zaidi kama something to show kuhusu uzuri wa Mwalimu, lakini otherwise uliyoyataja hata Mwinyi, Mkapa, na Muungwana sasa wameyafanya, maana mengi ya hayo uliyoyasema yanategemea sana bureaucratic sysytem ya serikali, kuliko uamuzi wa rais.

Hao watu wanaokuja Afrika leo, je hawaoni kuwa Nyerere aliacha kuchimba madini kwa vizazi vijavyo tofauti na Mobutu ambaye yeye na familia yake walifaidika na madini karibu yote ya Zaire na kuwaachia wanazaire ya leo makorongo na mabonde matupu?

Mobuttu, kama Mwalimu, walitegemea kutawala kwa kutumia upepo wa the Cold War, Mwalimu hakuwa mroho wa mali, Mobuttu alikuwa, lakini Zaire mkuu wangu kama hujafika, kuna barabara, hospitali, shule na the rest, lakini sio kwa idadi kama yetu bongo. Mwalimu aliacha kuchimba madini? mbona kulikuwa na kiwanda cha almasi Mwadui, na kiwanda cha kusafishia almasi Iringa? au?

Serikali zinajenga juu ya serikali, Nyerere aliwaomba kina Mwinyi na Mkapa kuacha mabaya aliyofanya na kuchukua mazuri. Je nini kimefanyika kuanzia mwalimu astaafu? Katika hili je bado wa kulaumiwa ni mwalimu?

Hakusema wazi mabaya aliyoyafanya, na nimemuomba sana Mwanakijiji aweke hizo hotuba ambazo Mwalimu alisema wazi mabaya yake huko magereza, sijawahi kuzisikia ningependa kuzisikia, ili tuweze kuwakaba Mkapa, Mwinyi na Muungwana, kwa nini hawakusikiliza, maana huenda wao wanaendeleza mabaya walioachiwa na yeye bingwa Mwalimu, bila ya kujua kuwa ni mabaya,

However, you are right kuwa matatizo yetu tuliyonayo sasa ni yetu wenyewe, ila tu hata Mwalimu, hakuwa na majibu ya matatizo yetu, na mengi yeye ni chanzo, sasa kama ni change yeye kwanza ndiye aliyepaswa kubadilika kwanza, ili tufuate mfano wake.

Otherwise, una strong argument mkuu!
 
Kwa sababu hakuna mawazo yake yaliyo salimika, Nyerere hakuacha hiba.

Mara nyingi hutupi wazo zuri, unatupa baya. Kama nilivyoziorodhesha, nyimbo zake zote zimetupwa!

Tukimpima kwa aliyo yaacha, Nyerere anatia huruma.
 
what i understand here is people are not trying to dirtify Mwalimu Nyerere's record ! Oh no ! for that, no one should hesitate to stand up for the teacher !

Uongo utajulikana, na kama kuna mtu ana nia ya kuchafua rekodi ya mwalimu, jamani hamtaweza ! His records are clear, lakini hakuwa mtakatifu !

So, endeleeni na debate wazee, lakini record zake ni halali na anapswa kupongezwa !

Wengine wanatumia kuchafua records za nyerere kama getaway yao ya kile ambacho we are yet to see/hear ! Wanajua kama itakubalika Nyerere hakuwa chochote, then wanaweza wakasema viongozi wote waliotoka upande wa nyerere, nao ni hivyo hivyo ! This wont happen guys !
GETAWAY FAILED !
 
Labda niulize swali la haraka haraka kidogo wakati mjadala huu ukiendelea. Je ikiamuliwa kuwa Nyerere alishindwa kabisa na wale wote wanaomtetea ni mabwiga. Na pia je ikiamuliwa kuwa Nyerere afutwe kabisa kwenye historia cha Tanzania maana yeye ndiye chanzo cha matatizo yote ya watanzania na waafrika wengine kama wamalawi, wazaire, wazambia, wasumbiji ambao wana matatizo kama ya Tanzania leo. Je Tanzania itafaidika nini? Je kutakuwa na mabadiliko yoyote ukichukulia kuwa viongozi wa ccm kina Kikwete na wenzao hawafuati sera au chochote alichosema na kufanya Nyerere kwa sasa?


Ni viongozi wachache sana duniani wenye bahati ya kupata nafasi na kujenga nchi kwe kutumia sera wanazotaka.

Dunia ina mabadiliko mengi na kiongozi akiwa madarakani inabidia aachane na sera zake na kufuata reality ya dunia. Na viongozi wengi wanaofanikiwa ni wale wenye kufuata reality ya dunia kuliko sera.

Wanaong'ang'ania sera siku zote wanaawacha watu wao masikini (Nyerere, Mugabe, Kaunda you name them). Na hii ipo mpaka kwenye nchi zilizoendelea. Chukua Bush alivyoingia madarakani, ameng'ang'ania sera za Iraq na mambo hayanyooki.
 
Mkuu wangu MWK,

Heshima mbele, mimi sio intellectual, ninakubali kuwa kuna mazuri aliyoyafanya Mwalimu, ambayo mpaka leo yanaweza kuhesabiwa, lakini tatizo ni kwa yale ambayo hakuyafanya kwa sababu ya mapungufu ya kibin-adam, huku akiendelea kuimba nyimbo za change ambazo hata yeye mwenyewe hakuweza kuzifanya kwenye miaka 23 ya utawala wake, sasa tutegemee nini kwa wananfunzi wake wanaotawala miaka 10 tu per term?

Hapa ndipo inabidi tuwabane hawa ambao tunao sasa hivi ili wasifanye tena makosa yaliyofanywa na Nyerere. Tukijaribu kurudi nyuma ili kutafuta mchawi wakati wengine tunao hapa hapa basi inakuwa vigumu sasa.

Katika hili nakubaliana nawe pia.

Kuna ambayo hujayataja ambayo ni ya muhimu zaidi kama something to show kuhusu uzuri wa Mwalimu, lakini otherwise uliyoyataja hata Mwinyi, Mkapa, na Muungwana sasa wameyafanya, maana mengi ya hayo uliyoyasema yanategemea sana bureaucratic sysytem ya serikali, kuliko uamuzi wa rais.

Mobuttu, kama Mwalimu, walitegemea kutawala kwa kutumia upepo wa the Cold War, Mwalimu hakuwa mroho wa mali, Mobuttu alikuwa, lakini Zaire mkuu wangu kama hujafika, kuna barabara, hospitali, shule na the rest, lakini sio kwa idadi kama yetu bongo. Mwalimu aliacha kuchimba madini? mbona kulikuwa na kiwanda cha almasi Mwadui, na kiwanda cha kusafishia almasi Iringa? au?

Hapa ndipo mkuu huwa unapata heshima kwenye mjadala kama huu. Kukubaliana kuwa kuna mema na mazuri yaliyofanywa na Nyerere. Mimi sipendi wale wanaosema mabaya tu kama vile hakuna mazuri yaliyofanyika. Na pia sipendi wale wanaosema mazuri tu kama vile hakuna mabaya yaliyofanyika. Nadhani huu mjadala umewekwa hapa ili yote mabaya na mazuri yawekwe kisha mazuri yachukuliwe na mabaya yaachwe au sio?

Hakusema wazi mabaya aliyoyafanya, na nimemuomba sana Mwanakijiji aweke hizo hotuba ambazo Mwalimu alisema wazi mabaya yake huko magereza, sijawahi kuzisikia ningependa kuzisikia, ili tuweze kuwakaba Mkapa, Mwinyi na Muungwana, kwa nini hawakusikiliza, maana huenda wao wanaendeleza mabaya walioachiwa na yeye bingwa Mwalimu, bila ya kujua kuwa ni mabaya,

However, you are right kuwa matatizo yetu tuliyonayo sasa ni yetu wenyewe, ila tu hata Mwalimu, hakuwa na majibu ya matatizo yetu, na mengi yeye ni chanzo, sasa kama ni change yeye kwanza ndiye aliyepaswa kubadilika kwanza, ili tufuate mfano wake.

Otherwise, una strong argument mkuu!

Kwa hiyo mkuu unasema kuwa ukishasikia mabaya ya Nyerere basi ndio utakuwa tayari kuwabana kina Mkapa na Kikwete. Kama sio basi hutakuwa na sababu nyingine yoyote ya kuwabana ili wao wasirudie mabaya ya Nyerere.

Binafsi sidhani kama Mkapa na Kikwete wanafuata hata chembe ya kile alichofanya Nyerere. Wao wana dunia yao wenyewe ambayo wao wameamua kuifuata. Hata ukiweka bango kubwa kabisa pale Manzese kuwa mwalimu Nyerere alikuwa ni shetani mkubwa, bado Mkapa na Kikwete watafanya kile wanachoona wao.

Uzuri ni kuwa hoja za mazuri na mabaya ya Nyerere zinawekwa hapa. Nyerere alikuwa binadamu na alikuwa na mapungufu yake. Wale ambao wanataka kusema kuwa Nyerere alipumbaza watanzania wote ndio wanataka kumfanya Nyerere kuwa ni Mungu. Yaani kuwa kila mtu kuanzia Mtwara hadi Moshi alipumbazwa na Nyerere?

Hii ni ajabu sana. Zaidi sana nakubaliana na mengi unayosema katika mjadala huu. Hoja zako hazina matusi au lugha ya kejeli. Huu ni mfano mzuri sana unaweka hapa mkuu.
 
Na mengineyo mengi ambayo ni kinyume na sera za Nyerere. Sasa haya mawazo ya kuwa inabidi sumu ya Nyerere itoke ndio tuendelee yana msingi upi?

Mkuu wangu MWK,

Ninasema hivi tena kutoka kwenye damu na mifupa yangu ya mwili, kwamba kiongozi wa kutusaidia wa-Tanzania, ni yule tu atakaye yaacha yote tuliyoyapitia huko nyuma, na kuanza upya na fresh ideas, na hasa atakayesema wazi tena hadaharani kuwa mawazo ya Mwalimu mengi yalishindwa, hatutayarudia tena, na akaweza kukubaliwa na wananchi, ujue huyo ndio mkombozi hasa wa taifa letu,

Wa-Tanzania ni lazima tuwe macho sana na viongozi kama Mwalimu na Mwanakijiji, ambao ni wengi sana Tanzania, toka tupate uhuru, wameshikilia intelectualism na elimu ambayo mwisho wake ni mikogo tu kwa wasomi wengine na viongozi wasiosoma, lakini in-applicable kwa maisha ya wananchi wa kawaida ambao ndio hasa taifa letu, hawa watafikia ku-change hata the un-changeable, watasema maneno magumu ya darasani kujaribu kuweka sera kwa taifa, ambazo kila mtekelezaji atashindwa, kama Mwalimu alivyokuwa, maana it always give them an-edege ya kusema kuwa mmekosea kwa sababu mmefanya vingine na nilivyosema, mimi nilisema kii-intellectualism, nyinyi mmefanya kirahisi sana haiwezi kuwa hivyo mlivyofanya, yes mara ngapi Mwalimu alikuwa akimtupia lawama Kawawa, kuwa hakumuelewa kwenye utekelezaji wa mawazo yake ya change, kwa mfano change ya maduka ya ushirika,

Wakuu mengi yamesemwa kuhusu Marehemu Sokoine, ukweli ni kwamba all the man did ilikuwa kujaribu kutafuta change ya kufuata utawala wa kuheshimu sheria, off course kuna hitilafu nyingi sana zinazojadilika on njia alizojaribu kuzitumia kutekeleza, lakini nia ilikuwa njema sana na somehow aliweza kupata our nation's attention of what he was trying to do in only six months, lakini miaka 23 ya Mwalimu, we had no idea alikuwa anasema au anajaribu kufanya nini?

Mwalimu was the greatest ever, lakini muda wake uliisha, sasa tusonge mbele na mapya.

Na hawa viongozi waliokutana huko Butiama, na kuamua kuwa turudi kwenye mawazo ya Mwalimu, tuwaangalie vizuri sana hawa, ninasema hivyo kwa sababu ninajua kuwa sio wote walioshirki kwenye hayo maamuzi, au waliokubaliana nayo.

Ahsante wakuu!
 
ama kweli watanzania ni sawa na gari bovu !

Hata mema/mazuri yote aliyofanya nyerere leo hii wanataka kujifanya wameyasahau ? nyinyi mmezaliwa lini ? acheni kuzuga bana !

pp12b.jpg


political_africa2.jpg
 
........kutofautiana kimawazo sijambo baya....ili mradi iwe katika kujenga na si kubomoa.........watu tunatofautiana pia ktk perceptions kulingana na wakati.....

Kwenye hili mkuu you are right, maana sidhani hata siku moja hapa kuna aliyewahi kukulazimisha kuwa na mawazo tofauti na unayotaka kuwa hapa JF, I never did sasa sielewi what is this labda ufafanue exactly unasema nini?

Idea za Mwl JKN alizoweka Mwanakiji ndio kinachojadiliwa hapa and nothing less......kama uliona nimekuwa off (kwa mtizamo wako)....fine.......however hainizuii kuonyesha niliyoyaandika

Again, sijawahi kukuzuia mkuu, nilichosema ni kushitushwa na mifano yako ambayo kwangu ilikuwa ni out of the topic, niliyotoa ni hoja, lakini haikuwa kukuzuia kama unavyosema, kumbuka kuwa na wewe humzuii mtu hapa kuonyesha exaclty mifano kama yako mkuu.

ya kwamba pamoja na kuwa ideas za JKN hazikufanikiwa.....haimaanishi kuwa zilikuwa mbaya......na baadhi ya watu wamejaribu kulinganisha na yanayotokea sasa na idea alizokuwa nazo JKN (they were out of ishu as well)......na ndio maana nikaweka ulichokisoma........

Ohh yah mkuu, kama ulivyoweka nilichokisoma, na mimi ndivyo nilivyoweka ulichosoma, and we can do some more too kwani kuna anayezuiwa?, wala hakuna tatizo in the spirit ya kujadili hoja za MMJ

....other stories are out of context.......
tuendelee kujadili ideas za JKN

Hii ya mwisho, ndio hasa iliyokuwa point yangu toka mwanzo, lakini ukitaka we can go there kwenye out of context, kwa sababu tu kuna watu waliojadili mada ya MMJ, wakiwa nje ya context kwa hiyo imekupa na wewe hiyo haki, ila nafikiri unasahau kuwa inampa haki kila mtu hapa kwenda nje ya context, that was my point, lakini mkuu be my guest anytime!

Ila ninarudia never expected from you, lakini nimekupata vizuri tena sana mkuu.

Ahsante Mkuu!
 
nafikiri mkibonyeza hii link, huu mjadala sidhani kama utaendelea tena ! MSIKILIZE MWALIMU ! nimecheka sana kwa kweli wazee !

http://video.google.com/videoplay?docid=-8461113793469084009

anakiri awamu yake ilifanya mema na mambo ya kijinga, lakini viongozi wa tanzania, msifanye ya kijinga na kuyapuuzia yale mema ! sasa hapa nadhani kuna kundi la watu wanapush the envelope kwa kuongelea mabaya tu, which is not bad....sasa wale ambao ni NEGATIVE ENVELOPE PUSHERS (NEP)kazi mnayo hapo !
 

Kwa hiyo unatupa hotuba ya Nyerere akijitetea na kushutumu wengine halafu unadhani huo ni ushahidi kwamba hakuharibu. La hasha!

Basi kila haramia anaepanda kwenye kizimba akisema sikuiba, basi hakimu amuachie.
 
Back
Top Bottom