Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,494
- 21,269
Tuseme tu ukweli, couple ya Haji Manara na ZaiyLissa ni couple inayokuwa kwa kasi sana na wakiendelea hivi hivi huenda ndio ikawa couple yenye mvuto zaidi hapa nchini.
Zai na Haji wanapendezana sana sana tena sana yani, na ili couple yao izidi kunoga wanatakiwa waishi hivi hivi bila ndoa.
Haji na Zai wamekutana wote waluwalu /mapepe, Zai bado anajitafuta na anapenda yale maisha ya gharama maana akijicheki kajina kanakua na hana mia nyekundu kuendana na umaarufu unaoendelea kukua kila kukicha Sasa kuwa na mtu kama Haji ni mtu sahihi sana kwake kwa kipindi hiki maana Haji ni hodari mno wa kuhonga na ni mpenda starehe sana ,ila tu ni limbukeni mkubwa wa mapenzi.
Kwa hiyo muunganiko wa hawa wawili utakuwa na nguvu na utavutia ila tu usifikr mpaka hatua ya ndoa.