CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

Pasco,
Naona bado tatizo lako liko pale pale: unataka kulazimisha kitu ambacho hakiwezekani ile mradi tu message yako iwe sent!, Hata sisi wananchi wa vijijini unaotusemea kuwa hatuelewi haya mambo tayari tumeshatambua kuwa CUF imeshajiunga rasmi na CCM!. Hivi kuna tija gani kutaka CHADEMA lazima ishirikishe CUF kwenye uongozi wa vyama vya upinzani bungeni wakati CUF tayari wako serikalini???:bowl:

Suala la kwanini mhe. Zitto asiwe kiongozi wa upinzani bungeni nalo halina mantiki kwa sababu mhe. Zitto tayari ni makamu wa kiongozi wa upinzani bungeni. Kwanza hivi bunge lililopita wakati mhe. Zitto akishirikiana na Dr.(Ph.D) Slaa kutoa hoja nzito nzito bungeni mbona hakuwa kiongozi wa upinzani bungeni?. Mhe. Mbowe ni kiongozi wa chama na kwa bahati nzuri naye amefanikiwa kuwamo bungeni, ndio maana emeendelea kuwa kiongozi wa wabunge wake kule mjengoni. Lakini hili halimzuii Mhe Zitto ama kamanda SUGU kutoa hoja zao na kuzizimamia kisawasawa kule mjengoni.

Dr.(Ph.D) Slaa alishasema kwamba tusubiri CAHDEMA kama chama watakuja na maelezo ya kina kwa wananchi juu ya nini kilitokea wakati wa uchaguzi na nini cha kufanya huko mbeleni lakini wewe unaita ni political immaturity! . Bila shaka siku ile angeenda pale, wewe ungekuwa ni mtu wa kwanza humu jamvini kumtuhumu kwanini alihudhuria!!!

Kwakuwa umekiri mwenyewe hukufanya research ni vema ufanye research kabla ya kutoa maoni ambayo yanaweza kuleta mgawanyiko usio na msingi haswa kipindi hiki ambacho tunatakiwa kushikamana zaidi.
Asante Bantugbro, nitazingatia.
 
Pasco ana point anatakiwa point zake zichukuliwe kama anagalizo zuri kwa Chadema,

Kuhusu Analysis yake amekiri hakwenda deep ila still anona kitu ktk maneno yake.

Naumngana mkono na Slaa kuhusu hali ya upinzani sasa CUF wako na serikali Znz ni ngumu sana kuwaita wapinzani n.k
Mutu, asante sana kwa hili, nami nakubaliana nawe.
 
Superman, ni kweli sometimes huwa sisemi source ya baadhi ya thread zangu, hii inakubalika kwa kutumia msingi unaitwa 'the confidentiality of the source', unamhifadhi ili kumlinda. Moja wa hawa ma souce ni yule aliyeniambia hata kura zipigwe vipi, CCM imeshinda kwa 80%, nilishambuliwa sana, ila ilimaanisha walijipanga wajitangazie 80% walipoona imeleak, ndipo wakatangaza walichotangaza.

Hili la hoja nyepesi nalikubali,na linatokana na kiwango cha kichwa changu ni chepesi tuu, ziwezi kuja na hoja mzoto za lever ya kina Mzee Mwanakijiji, ni mpaka ni kicha cha level hiyo. Uzito wa hoja ni lever ya kichwa husika, kwa hili nakubali mimi mwepesi.

Hili la "ego" na kujinyanyua ni relative, mimi najiona niko chini usawa wa mavumbini, sijawahi kusema shughuli zangu nini, naishi wapi, maisha yangu yakoje ili tuu nisionekana najinyanyua, ukweli mimi ni mtu wa chini sana, na ni kawaida watu wa chini, kutaka kujinyanyua ili angalau waonekane wako juu, pont noted nitabaki uvunguni.
Ila la kuanzisha thread zinazofanana,hili sikubaliani nawe, kwa vile mimi huanzisha thread za aina mbili tuu, ya kwanza ni kuhusu event fulani, na wakati huo mimi huwepo hapo kwenye event phisically, hutokea nimeshapost kumbe kuna mwingine naye alianzisha kabla yangu, mfano mzuri ni juzi wakati wa matokeo ya uchaguzi, nikiwa chumba cha kutangaza matokeo nikaanzisha kumbe kuna member kaona life kwenye tv akanitangulia, thread yangu ilifungwa na niliupdate thread iliyotangulia.
Aina ya pili ya thread zangu, ni my opinion, hii huusu mawazo na mitazamo yangu binasi kama thread hii. Ila pia nitafuatilia kwa karibu to make right the wrong ones.



Superman,
Asante tena,
Amandla!
Pasco.

Tupo pamoja Mkuu.

Pamoja na JF wote tutaleta madadiliko na kuijenga Tanzania ambayo ni kubwa kuliko sisi sote.
 
Mkuu Pasco,

Ni kweli kwamba CCM imechokwa na kuna ukweli kwamba CHADEMA inahitaji kujipanga mapema kwa ajili ya 2015. Lakini naomba kutofautiana kwa kiasi fulani na hoja zako kuhusu kambi ya upinzani na pia ku-revamp CCM.

Kumuondoa Makamba na kuwaweka damu changa akina Nape, Kippi, Makamba Jr na wengineo, haiwezi kuwasaidia CCM. Tatizo ni mfumo mzima wa CCM. Hao vijana unaowasema wanaweza kuishia kwenye secretariat ya Chama lakini hawana maamuzi ya mwisho. Wenye maamuzi ya mwisho ni CC na NEC, na wenye nguvu zaidi ni CC. Ukiangalia CC imejaa hao hao wenye mawazo ya akina Makamba. Mfano mzuri ni Mama Makinda aliposema anavyoelewa yeye ni kwamba fisadi ni mwizi wa wake za watu, lakini akawa amesahau kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano lilishatumia neno hilo hilo kwa maana tofauti na aliyoisema yeye, na pia yeye mwenyewe alishatumia neno hilo hilo kwa maana ile ile tunayoifahamu sisi. Kwanini leo hii ageuke ghafla na kuanza kutupatia tafsiri ya kwenye Kamusi? Makinda anaingia kwenye CC sasa anaenda kuwa mmoja wao. Utakuwa umemtoa Makamba umemuingiza Makinda wenye mawazo yale yale ambayo yanaficha ukweli.

Ushindi wa JK haukuwa wa 60%, alipata pungufu ya hizo, na yeye anajua hilo. Hilo pekee ni jibu tosha kwa JK ambaye alisema 70% ya wapiga kura wa Tanzania ni bendera fuata upepo, na ndio maana alikuwa anatarajia kupata more than 80%, kwamba 70% ya akina bendera fuata upepo + 15 ambao wanampenda na wanamuelewa. So zile 15% ndio wangegawana Dr. Slaa, Prof Lipumba na wagombea wengine. Aibu aliyo nayo ni kubwa kuliko unayoisema wewe hasa akikumbuka hilo tusi alilotutukana watanzania.

Nije kwenye swala la Kambi ya Upinzani: Binafsi nilitamani sana vyama vya upinzani vyote vyenye wabunge ndani ya Mjengo waungane pamoja ili wawe na sauti kubwa na umoja, lakini pia nilikuwa ninasita kwa kiasi fulani hasa nikizingatia mseto wa Zanzibar. Kumbuka kwamba wabunge wa kuchaguliwa wa CUF kutoka Bara wako 2 tu, na viti Maalum nadhani kama 4 hivi, the rest wanatoka Zanzibar. Kule Zanzibar CCM na CUF wana mseto, ni rahisi sana kutumia huo mseto kuwa-influence wabunge wa CCM huku bara ili waweze kuiunga mkono CCM kwenye jambo lolote. Yaliandikwa mengi kuhusu makubaliano binafsi ya Januari Makamba na Jussa, na wao walisema yalikuwa personal, hata kama ni personal, Jussa ana influence kubwa ndani ya chama chake na ni mtu wa karibu sana Maalim Seif.

Mrema tulimsikia akimpigia debe JK wakati wa kampeni na ilihali chama chake [TLP] kilikuwa na mgombea wa nafasi hiyo. Mpaka sasa ameishaonyesha wazi kwamba yeye atakuwa pro-CCM, kwa hiyo ukimuweka kwenye kambi ya upinzani ni sawa na kuweka nyoka chumbani ambaye ana sumu maana siku yoyote anaweza kukudhuru.

Mwaka jana, Mzee Cheyo alitimliwa kwenye nafasi yake ya uwaziri baada ya kwenda kinyume na msimamo wa kambi ya upinzani. Mtu kama huyo huwezi kumtegemea, na ameishasikika mara kibao akisema JK ni safi.

NCCR Mageuzi siwezi kuwasemea, maana hao vijana wote siwafahamu, zaidi ya kujua kasheshe za uongozi wao tu.

Ili kambi ya upinzani iwe na nguvu lazima wapinzani wote wawe na agenda moja na msimamo ulio na lengo moja. Lakini ukiangalia maelezo yangu hapo juu kila chama kinaonekana kina agenda yake na hivyo it is much easy kambi hiyo kusambaratika au kwenda kuumbuana ndani ya vikao vya bunge.

Binafsi ninaweza kusema kwamba muafaka wa CCM na CUF kule Zanzibar ni chanzo kikubwa cha kutokuwa na kambi moja ya upinzani yenye nguvu. Ili kuimarisha zaidi huo muafaka, usije ukashangaa ukisikia JK ameteua mwaka CUF mmoja kwenye zile nafasi 10 ili kupunguza makali ya CUF kwenye Bunge.
Keil asante kwa hili, nimeelimika.
 
Wanabodi,


Angalizo: Pasco wa Jamii Forums ni political analyst ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya ubunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!


Is it true? Hmmmmmmmm!
 
CHADEMA ni chama cha ajabu sana. Hivi mnadhani kila mtu ana kumbukumbu fupi?
Wakati CUF wanawashirikisha kwenye uongozi wa upinzani (kwenye bunge la tisa) hamkuona kuwa wao ni "wanafiki". Leo hii nyinyi ndio mko "juu" tayari mnaona makosa ya kila mtu. Hivi vyama vyote vina kasoro isipokuwa CHADEMA??? Namuomba Mungu atujalie uhai tuone inakoelekea CHADEMA.

Kwa hiyo Slaa alikuwa anadanganya watanzania kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa, au alipanga kuiunda kwa kushirikiana na chama gani?

Fundisho: Kama CHADEMA wanangoja kiwepo chama kisicho na kasoro yoyote ndio washirikiane nacho basi ni sawa na kusema hawataki kushirikiana na chama kingine. Chama chenye kasoro duniani HAKIPO.
 
Sioni pengo la kuchangia,nimejifunza mengi katika Posts hizi chache.Ushauri wangu kwa Pasco,Tafuta muda uzungumze na Mzee Slaa,kuna mengi ya kumueleza nawe utaelimika kwa mengi kutoka kwake...Unaeleweka na Dr amekuelewa vilivyo katika Post yako...Kwa wadhifa wake majibu yake ni changamoto kwako!Kwa pamoja tunaweza tujadiliane kwa uwazi,Mafanikio na mapungufu ya Vyama vyetu.Hii ndio maana halisi ya uhuru wa kujieleza.
 
Mkuu Pasco,

Ni kweli kwamba CCM imechokwa na kuna ukweli kwamba CHADEMA inahitaji kujipanga mapema kwa ajili ya 2015. Lakini naomba kutofautiana kwa kiasi fulani na hoja zako kuhusu kambi ya upinzani na pia ku-revamp CCM.

Kumuondoa Makamba na kuwaweka damu changa akina Nape, Kippi, Makamba Jr na wengineo, haiwezi kuwasaidia CCM. Tatizo ni mfumo mzima wa CCM. Hao vijana unaowasema wanaweza kuishia kwenye secretariat ya Chama lakini hawana maamuzi ya mwisho. Wenye maamuzi ya mwisho ni CC na NEC, na wenye nguvu zaidi ni CC. Ukiangalia CC imejaa hao hao wenye mawazo ya akina Makamba. Mfano mzuri ni Mama Makinda aliposema anavyoelewa yeye ni kwamba fisadi ni mwizi wa wake za watu, lakini akawa amesahau kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano lilishatumia neno hilo hilo kwa maana tofauti na aliyoisema yeye, na pia yeye mwenyewe alishatumia neno hilo hilo kwa maana ile ile tunayoifahamu sisi. Kwanini leo hii ageuke ghafla na kuanza kutupatia tafsiri ya kwenye Kamusi? Makinda anaingia kwenye CC sasa anaenda kuwa mmoja wao. Utakuwa umemtoa Makamba umemuingiza Makinda wenye mawazo yale yale ambayo yanaficha ukweli.

Ushindi wa JK haukuwa wa 60%, alipata pungufu ya hizo, na yeye anajua hilo. Hilo pekee ni jibu tosha kwa JK ambaye alisema 70% ya wapiga kura wa Tanzania ni bendera fuata upepo, na ndio maana alikuwa anatarajia kupata more than 80%, kwamba 70% ya akina bendera fuata upepo + 15 ambao wanampenda na wanamuelewa. So zile 15% ndio wangegawana Dr. Slaa, Prof Lipumba na wagombea wengine. Aibu aliyo nayo ni kubwa kuliko unayoisema wewe hasa akikumbuka hilo tusi alilotutukana watanzania.

Nije kwenye swala la Kambi ya Upinzani: Binafsi nilitamani sana vyama vya upinzani vyote vyenye wabunge ndani ya Mjengo waungane pamoja ili wawe na sauti kubwa na umoja, lakini pia nilikuwa ninasita kwa kiasi fulani hasa nikizingatia mseto wa Zanzibar. Kumbuka kwamba wabunge wa kuchaguliwa wa CUF kutoka Bara wako 2 tu, na viti Maalum nadhani kama 4 hivi, the rest wanatoka Zanzibar. Kule Zanzibar CCM na CUF wana mseto, ni rahisi sana kutumia huo mseto kuwa-influence wabunge wa CCM huku bara ili waweze kuiunga mkono CCM kwenye jambo lolote. Yaliandikwa mengi kuhusu makubaliano binafsi ya Januari Makamba na Jussa, na wao walisema yalikuwa personal, hata kama ni personal, Jussa ana influence kubwa ndani ya chama chake na ni mtu wa karibu sana Maalim Seif.

Mrema tulimsikia akimpigia debe JK wakati wa kampeni na ilihali chama chake [TLP] kilikuwa na mgombea wa nafasi hiyo. Mpaka sasa ameishaonyesha wazi kwamba yeye atakuwa pro-CCM, kwa hiyo ukimuweka kwenye kambi ya upinzani ni sawa na kuweka nyoka chumbani ambaye ana sumu maana siku yoyote anaweza kukudhuru.

Mwaka jana, Mzee Cheyo alitimliwa kwenye nafasi yake ya uwaziri baada ya kwenda kinyume na msimamo wa kambi ya upinzani. Mtu kama huyo huwezi kumtegemea, na ameishasikika mara kibao akisema JK ni safi.

NCCR Mageuzi siwezi kuwasemea, maana hao vijana wote siwafahamu, zaidi ya kujua kasheshe za uongozi wao tu.

Ili kambi ya upinzani iwe na nguvu lazima wapinzani wote wawe na agenda moja na msimamo ulio na lengo moja. Lakini ukiangalia maelezo yangu hapo juu kila chama kinaonekana kina agenda yake na hivyo it is much easy kambi hiyo kusambaratika au kwenda kuumbuana ndani ya vikao vya bunge.

Binafsi ninaweza kusema kwamba muafaka wa CCM na CUF kule Zanzibar ni chanzo kikubwa cha kutokuwa na kambi moja ya upinzani yenye nguvu. Ili kuimarisha zaidi huo muafaka, usije ukashangaa ukisikia JK ameteua mwaka CUF mmoja kwenye zile nafasi 10 ili kupunguza makali ya CUF kwenye Bunge.
Hapa kikubwa cuf ni wabinafsi na tegemeo lao kubwa ni kupata nafasi za upendeleo (ubunge) na kikwete sasa wakionekana wamejenga umoja na chadema wanaona watazikosa hizo nafasi, cuf zanzibar si bara.
 
The Dreamer, asante kwa angalizo hilo, naadmit mistake pale niliposema wenu na wetu, hivyo nami kujionyesha ni kama Chadema flan, sorry nikosa, sina bifu yoyote na Mhe. Mbowe, who am I?. I'm nothing ila nakiri udhaifu kuwa Zitto namkubali sana mpaka kupoteza objectivity, nitajirekebisha thanks again.
Pasco
Kama kuna thread ambayo dialogue yake imenisisimua kwa kiwango cha juu basi ni hii. Nimefurahishwa zaidi na response ya Dr. W. Slaa (PhD) ambayo kwa kweli presentation yake inamthibitishia msomaji yeyote kwamba ni great thinker. Asante sana Dr., Rais wa nyoyo zetu. Asante sana kwa busara zako, kweli huu ni ushuhuda wa kwamba hukurupuki. Nawashukuru wachangiaji wengine wote na haswa Pascoe ambaye kwa comment yake niliyoi-quote amekiri mapungufu yake na kuahidi kujirekebisha. Ilikuwa conclussion nzuri mno. Thank you all. Mungu ibariki Tanzania.
Ama kweli JF ni home of great thinkers.
 
CHADEMA ni chama cha ajabu sana. Hivi mnadhani kila mtu ana kumbukumbu fupi?
Wakati CUF wanawashirikisha kwenye uongozi wa upinzani (kwenye bunge la tisa) hamkuona kuwa wao ni "wanafiki". Leo hii nyinyi ndio mko "juu" tayari mnaona makosa ya kila mtu. Hivi vyama vyote vina kasoro isipokuwa CHADEMA??? Namuomba Mungu atujalie uhai tuone inakoelekea CHADEMA.

Kwa hiyo Slaa alikuwa anadanganya watanzania kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa, au alipanga kuiunda kwa kushirikiana na chama gani?

Fundisho: Kama CHADEMA wanangoja kiwepo chama kisicho na kasoro yoyote ndio washirikiane nacho basi ni sawa na kusema hawataki kushirikiana na chama kingine. Chama chenye kasoro duniani HAKIPO.

Very True!

Lakini kuna kasoro kubwa ambazo ukiziangalia ni ngumu sana kukubaliana nazo. Tatizo la siasa za Tanzania ni za kinafiki, usoni mtu anasema hiki akienda pembeni au ukimpa kisogo anabadilika. Ndio wale ambao Makamba alikuwa anasema kwamba wanavaa njano na kijani, lakini mioyo yao iko upinzani. Same applies kwa wapinzani, hata ndani ya vyama hawaaminiani.

CUF bunge lililopita walianza peke yao kama kambi ya Upinzani, lakini baada ya muda fulani waliwakaribisha CHADEMA na UDP ili waunganishe nguvu. Bado ni mapema sana, labda kunaweza kuwa na mijadala ambayo inaendelea nyuma ya mapazia.

Lakini kumbuka kwamba Bunge lililopita kuna mwana CUF mmoja aliteuliwa na JK kuingia kwenye Bunge la JMT akiwa Mbunge mteule wa Rais na hayo yalikuwa ni matunda ya Muafaka wa Zanzibar. Swali langu ni hili, je, iwapo JK atateua tena mwana CUF mwingine kwenye Bunge la 10, atakuwa anahesabika mpinzani au mwana CCM? Je, unaweza kushirikiana na huyo mteule wa Rais kwenye kuandaa mikakati ya kwenye vikao vya wapinzani ukiwa na imani kwamba mikakati hiyo haiwezi kuvuja na kwenda CCM? Hata kama hahudhurii vikao, lakini bado ana wana CUF wenzake ambao watampa "news" na anaweza kuzitumia apendavyo. Kibaya zaidi JK hateui mwanachama wa kawaida tu, bali anateua wale ambao ni influential ili akitaka kumtumia aweze kumtumia effectively. Bunge la tisa aliteuliwa Bwana Jussa ambaye ni very influential ndani ya CUF na siasa za Zanzibar.
 
Sioni pengo la kuchangia,nimejifunza mengi katika Posts hizi chache.Ushauri wangu kwa Pasco,Tafuta muda uzungumze na Mzee Slaa,kuna mengi ya kumueleza nawe utaelimika kwa mengi kutoka kwake...Unaeleweka na Dr amekuelewa vilivyo katika Post yako...Kwa wadhifa wake majibu yake ni changamoto kwako!Kwa pamoja tunaweza tujadiliane kwa uwazi,Mafanikio na mapungufu ya Vyama vyetu.Hii ndio maana halisi ya uhuru wa kujieleza.
Mwawado, nashukuru sana, busara yako nimeipokea.
 
Wanabodi,

Nikiwa hapa Dom, nimebahatika kukutana baadhi ya wabunge wapya wa CCM na wa kambi ya upinzani, kujaribu kufahamiana, sio siri, baadhi yao hawana hata substance ya ni nini kilichowafanya washinde, na viti maalum ndio usiseme kabisa, wengi ni makapi tuu, kama sio vidumu, basi ni kwa ajili ya kutoa huduma na kibinaadamu, na hili litathibitishwa na michango yao kikao cha Januari.

Nilipoongea na wale makamanda walikata magogo kanda ya ziwa, nao ni wa kawaida tuu, hivyo nimefikia jibu moja la uhakika, CCM imechokwa baadhi ya maeneo, upinzani hata ungesimamisha jiwe, lingechaguliwa, nadhani ni moja ya sababu kuu iliyopelekea wengi hawakujitokeza waliona ni kujisumbua.

Nasisitiza CCM imechokwa, na ule ushindi wa kishindo wa toka Asilimia 80% niliyohakikishiwa na mwana CCM mwandamizi mpaka asilimia 60% ni uthibitisho tosha, Watanzania wameichoka CCM ila pia hawakuwachagua wapinzania kwa wingi zaidi, kwa sababu wapinzani hawajaonyesha wako tayari kukamata dola.

Najua kwa dhati, japo JK anafurahia ushindi kwa furaha ya machoni, lazima atakuwa na huzuni moyoni kwa kukataliwa na hiyo asilimia 20% kukataliwa ni kukataliwa tuu, kunauma. Hivyo CCM lazima watakaa na kujiuliza kulikoni, huenda wakajipanga upya na kuja kwa mbinu mpya, ila kwa vile CCM imechokwa, hata ijipange vipi, safari ya kwaheri ndio imeanza, there is nothing to stop it from failing down.

Dawa pekee ya kuitibu CCM, kuirevamp CCM completely, task nambari moja ni Makamba should go first with his old guards team. Leteni fresh blood kina January type, Kippi, Nape type and the like ambao wanaweza siasa za kisasa za dot com type.

Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tazizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msiku chama chenu bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa, Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.

Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa kwenye Usukani, Katibu Mkuu mpeni Zitto, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, ili Walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kuwapigia kura 2015.

Kitendo cha kuihodhi kambi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani, Chadema peke yenu hamuwezi!.

Nasisitiza Chadema hamjajipanga vyema na tatizo lenu kubwa ni ubinafsi wa viongozi wenu na ugonjwa wa umimi. Hakuna ubishi kuhusu uwezo wa Zitto Kabwe na Uwezo wa Freeman Mbowe katika kukata issue. Mbowe sio born leader, ni made leader, tena ameletewa uongozi kwenye kisaani cha chai. Zitto ni born leader na amepambana kufika hapo alipofika.

Kitendo cha Mbowe kuwa ndie kiongozi rasmi wa upinzani Bungeni is a waste. Mbowe hana features za promising great leader, Zitto anazo. Mbowe hana powers from withing to make things happen, Zitto is powerful from within who can make things happen, he is a force to recon with. Juzi wakati wa kampani za Marando, alimgomea kata kata Ole Sendeka kuzungumzia kisemeo cha Marando, alisimama, akagonga meza na kusema kwa sauti kubwa "we can't allow such a thing, never on earth!" Spika Makinda ndipo akakazia msimamo na Ole Sendeka kufurushwa!.

Kiongozi sahihi wa upinzani bungeni should be Zitto not Mbowe. Naibu kiongozi wa upinzani alitakiwa awe Hamad Rashid. Chief Whip Lissu is ok.

Kama CCM iko ICU na Chadema haijajipanga, spika ndio huyo mama ma over confidence na over reaction, 2015 tutegemee nini?.

Angalizo: Pasco wa Jamii Forums ni political analyst ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya ubunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!
Pasco

Asante kwa maoni yako ambayo umekiri is not scientific analysis it is just an obsevation.
Kama ni observations basi ungeyaacha yawe huru bila kuja na critical conclusions kama kutumia maneno 'umimi' 'kiongozi wenu, wetu' 'immaturity' nk. Kama ni observations tu huwezi kufikia conclusion kama uliposema
Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa

Kama tatizo la Chadema ni uongozi kwa mfano ulikuwa na maana gani uliposema Chadema inapaa, kupaa huko kunapaishwa na nani kama si uongozi imara wa Chadema chini ya Jemedari Mbowe wewe umetumia neno jemedari wenu hilo si tatizo kubwa. Lakini cha msingi nataka kukueleza hata kama jeshi lina wapiganaji wazuri na silaha nzuri huwezi kushinda vita ikiwa kiongozi ni mbovu kitu ambacho Mh. Mbowe na Chadema wame proves right.

Umemwita Dr. (PhD) Slaa ni immaturity kwa kutokwenda kusikiliza matokeo feki, sidhani hiyo ndiyo sababu iliyokufanya hadi ufikie conclusion hiyo NO nakataa kuna zaidi ya hapo. Wewe ni mwanasheria, ipo mifano mingi unaweza kujikumbusha kama Odinga Oginga wa Kenya, Morgan Tsvangirai wa Zimbabwe, Abdallh Abdallah wa Afganstan wote hao walisusia matokeo sijui nao tuwaite immature. Tusiende mbali Seif na Lipumba waliwahi kususia si matokeo tu hadi kuhudhuria bunge na kutomtambua Karume kwa kipindi kirefu utatuambiaje kwa hilo.

Kuhusu muungano wa CUF na Chadema sidhani kama wewe ambaye uko mstari wa mbele kutuletea matukio hasa ya bungeni hujui kinachoendelea Zanzibar kuwa CUF ni sehemu ya serikali. Kwa mantiki hiyo unategemea nini kitatokea ikiwa Chadema na CUF watapeleka hoja ambayo itaonekana kwenda kinyume na matakwa ya serikali, mbona hili liko wazi Pasco huhitaji kuwa na PhD kuliona.

Naku- quote
Kitendo cha Mbowe kuwa ndie kiongozi rasmi wa upinzani Bungeni is a waste. Mbowe hana features za promising great leader, Zitto anazo. Mbowe hana powers from withing to make things happen, Zitto is powerful from within who can make things happen, he is a force to recon with.
Nikisoma hiyo quotation inanipeleka kwenye mawazo ya watu wanaosali usiku na mchana utokee mpasuko ndani ya Chadema wanajaribu kujenga makundi ya kufikirika na kulazimisha yawe kweli, ila sitaki nikuhusishe na watu hao but all in all asante kwa maoni yako ambayo yatawafanya wahusika ukiwemo wewe kujiangalia zaidi.
 
Pasco

Asante kwa maoni yako ambayo umekiri is not scientific analysis it is just an obsevation.
Kama ni observations basi ungeyaacha yawe huru bila kuja na critical conclusions kama kutumia maneno 'umimi' 'kiongozi wenu, wetu' 'immaturity' nk. Kama ni observations tu huwezi kufikia conclusion kama uliposema

Kama tatizo la Chadema ni uongozi kwa mfano ulikuwa na maana gani uliposema Chadema inapaa, kupaa huko kunapaishwa na nani kama si uongozi imara wa Chadema chini ya Jemedari Mbowe wewe umetumia neno jemedari wenu hilo si tatizo kubwa. Lakini cha msingi nataka kukueleza hata kama jeshi lina wapiganaji wazuri na silaha nzuri huwezi kushinda vita ikiwa kiongozi ni mbovu kitu ambacho Mh. Mbowe na Chadema wame proves right.

Umemwita Dr. (PhD) Slaa ni immaturity kwa kutokwenda kusikiliza matokeo feki, sidhani hiyo ndiyo sababu iliyokufanya hadi ufikie conclusion hiyo NO nakataa kuna zaidi ya hapo. Wewe ni mwanasheria, ipo mifano mingi unaweza kujikumbusha kama Odinga Oginga wa Kenya, Morgan Tsvangirai wa Zimbabwe, Abdallh Abdallah wa Afganstan wote hao walisusia matokeo sijui nao tuwaite immature. Tusiende mbali Seif na Lipumba waliwahi kususia si matokeo tu hadi kuhudhuria bunge na kutomtambua Karume kwa kipindi kirefu utatuambiaje kwa hilo.

Kuhusu muungano wa CUF na Chadema sidhani kama wewe ambaye uko mstari wa mbele kutuletea matukio hasa ya bungeni hujui kinachoendelea Zanzibar kuwa CUF ni sehemu ya serikali. Kwa mantiki hiyo unategemea nini kitatokea ikiwa Chadema na CUF watapeleka hoja ambayo itaonekana kwenda kinyume na matakwa ya serikali, mbona hili liko wazi Pasco huhitaji kuwa na PhD kuliona.

Naku- quote
Nikisoma hiyo quotation inanipeleka kwenye mawazo ya watu wanaosali usiku na mchana utokee mpasuko ndani ya Chadema wanajaribu kujenga makundi ya kufikirika na kulazimisha yawe kweli, ila sitaki nikuhusishe na watu hao but all in all asante kwa maoni yako ambayo yatawafanya wahusika ukiwemo wewe kujiangalia zaidi.

Whaaw! Luteni, can I promote you to a Full General?

Your analysis is very critical, bust still very simple, brief and to the point.

Big Cheers!
 
Dr. Slaa, asante sana kwa kunijibu, kitendo tuu cha kuonyesha umenisoma, hiyo ni faraja tosha kwangu kuwa hata kama hamtayarekebisha mapungufu, my only defence ni kuwa tuliwaambia, mesej sent.

Kwa kuanzia, nakupongeza sana wewe binafsi kugombea, umeleta changamoto ambayo haijawahi kutokea.Ushindi wa hayo majimbo mliyoyatwaa ni uthibitisho wa the powers within you. For the first time in my life, nimehamasika na naweza kutupa karata yangu mahali 2015.

Pole kwa kutopata ushindi uliotarajiwa, ila amini usiamini, wewe bado ni mshindi kwenye roho za watu, na JK ni mshindi kwenye makatasi ya kura. Tunatakiwa kuwa wa shukrani kwa kidogo chochote tunachopata, wewe mwenye majimbo 5 hadi 22 na la 23 ni kesho, ulitakiwa kuonyesha appreciation kwa Watanzania waliokuamini, kitendo cha kususia kutangazwa matokeo for whataver reasons, ni political immaturity, na binafsi nilifadhaishwa sana, umepoteza the golden opportunity ya kuspeak out you mind, hata kama hatimaye utakuja kuita waandishi na kuyasema ya moyoni, never will they have the impact kama ungejitokeza pale na kusema nimekuja siyakubali matokeo kwa sababu yamechakachuliwa.

Nakubaliana na wewe kuhusu weakneses kwenye analysis yangu, infact kitu nilichokisema hapa, its only my observation. True analysis inapatikana baada ya kufanya research, nakiri sijafanya research yoyote serious zaidi ya observation tuu, ila hili jicho langu ndilo la mwananchi wa kawaida kule kijijini na sio jicho la reseacher as a member of academia.

La kambi ya upinzani, nimelisemea, if you go by the books, it is ok kwa vile nyinyi peke yenu mnaconstitute ile quoram kwa mujibu wa kanuni, don't play by the book, just play by reality, logic and moderation. Umimi wenu Chadema, haujaanza leo, msipokubali weaknesses zenu, you can not turn them ito streghths. Naomba nisiende tena kwenye personalities zaidi, tunakuomba kaa siti ya mbele, shika usukani, pangeni safu yenu vizuri, futeni dhana zote zilizojengeka dhidi yenu ziwe za kweli au za kizushi, 2015 ikulu ni yenu, maana wale milioni 12 waliojiandikisha halafu hawakupiga kura, ndio mtaji wenu wa 2015 haswa ukizingatia vijana wa shule za kata ndio watakuwa vyuoni!.

Asante tena.
Pasco,

Dr Slaa ni kama nabin kitendo chake cha kutohudhuria utangazaji wa matokeo ni sahihi kbsa,

Angesimnama mbele ya wandishi wa habari na kusema siyakubali matokeo sote wenye uchungu wa kuibiwa tungeandamana na tusigetoka pale karamji hadi kieleweke,

Cuf did it in zanzibar first five years ya karume hawakumtambua a. Karume what's wrong with dr slaa kumsusia JK????

Infact kama chadema hatakuwa wanafiki na wenye njaa kali wasusie houtuba ya jk bungeni the message will be delivered!!

Tatizo letu njaa zinatofautiana mbunge akishaambiwa kuna loan unsecured 200m from crdb na marupu rupu mengine denda nje nje, hawezi toka nje ya ukumbi wa bunge atoke ili iweje?
 
CHADEMA imefika hapo chini ya uongozi wa MBOWE na SLAA, imepata wabunge 45 chini uongozi huo huo . Jambo la msingi ni kuendelea kutoa elimu ya demokrasa ya kweli kwa wananchi ambao bado wamelala na wale wanaofikiri kuwa ccm itaendelea kutawala.
 
Nimeelimika na naelimika sana na hii thread! imenifurahisha sana! We need changes, we need togetherness ktk kulikomboa hili taifa linaloelekea pabaya! thanks to Chadema so far! Mungu ibariki Tanzania!
 
Pascal,

Kama mtanzania wakweli hakika unajua kuwa uchaguzi umechezewa, hata kama hujafanya utafiti wakina utajua kuwa rais wa Tanzania mwaka huu haja ingia ikuru alie ingia ikuru anajua ameingia kwanjia gani.

Hivyo usitegemee Dr. Slaa anaye wakirisha watanzania ata hudhuria kutangazwa au kuapishwa kwa rais asiye na ridhaa ya wengi hii maana yake angetambua sanaa iliyo fanyika kinyume na watanzania hivyo ange kuwa anamwakilisha nani? Wakati mwingine unapotumia manano makali kama political immaturity wakati una kili hujafanya utafiti ju ya jambo unalotaka kutu sadikisha hakika unakuwa unafanya makosa makubwa sana katika taifa hili.

Chadema sio watu wawili au watatu ni watu wa taifa hili wanao hitaji mabadiliko katika nchi yao wanao fuata falsafa ya nguvu yauma, hawa wengine unao wataja ni watu wetu walio jitolea kutoa mwelekeo na msimamo kwaniaba yetu. Sasa angesogea eneo la sanaa mimi ninge kubali kuwa ananiwakilisha? Dr. Slaa anaakili sana na amejiandaa kuongoza watu hivyo nilazia ajue watu wanamwelekeo gani ...

Viatu alivyovaa Dr. Slaa leo ukimpa Makamba mtaona kitakachotokea
 
Kwanza kwa maoni yangu watu aina ya akina PASCO ni watu wa kuwalaani kwa sababu ni wachonganishi na wazandiki, sitaki kuamini kuwa mtu kama PASCO hasomi wala hasikii vyombo vya habari kuhusu msimamo wa CHADEMA kuhusu kushirikiana na vyama vingine makini.

CHADEMA toka siku ya kwanza kimeweka wazi kuwa kinaongea na CUF kuhusu kushirikiana na baadaye CUF wakaitaarifu CHADEMA wao wameungana na TLP, NCCR-M na UDP kuunda Minority oposition ambayo kikatiba haipo. Hilo ni dhahiri kuwa ule usemi wa umakini wa CUF haupo, mimi ninafikiri kwamba tatizo la CUF ni ile hali ya sasa ya CHADEMA kuwa na wabunge wengi kuliko wao. Ikumbukwe kuwa CUF kimekuwa chama cha upinzani chenye wabunge wengi kwa muda mrefu na hivyo kuwa na uhalali wa kuunda kambi ya upinzani rasmi bungeni. Kwa hiyo inawapa shida kuwa chama kingine kimekuwa zaidi yao, na hivyo kuanza kuvirubuni vyama ambavyo navyo siyo makini sana kama TLP.

Ikumbukwe CHADEMA katika miaka yote ambayo hakijawahi kuwa na wabunge wengi hakijawahi kulalamika kuhusu kushirikiswa kwa sababu hiyo siyo lazima. Na zaidi ya yote ni kwamba ni haki ya CHADEMA kutoa kiongozi wa upinzani bungeni kwa utaratibu ambao wanaona unafaa. Pia ukubukwe CHADEMA kimekuwa kiviunga vyama vingine kwa vitendo na siyo porojo, mfano mwaka 1995 CHADEMA hakikusimasha mgombea uraisi na badala yake kikatangaza kumuunga mkono mgombea wa NCCR_ Mageuzi. Viongozi wake siyo watu wa kung'ang'ania madaraka na siyo watu wanaoamini bila wao vyama havipo. Mfano tumeona kuwa mwaka 2005 aligombea urais ni ndugu Mbowe , lakini mwaka 2010 mwenyewe Mbowe allitamka kuwa mtu anayeonekana kwa sasa anafaa kuvaa vitatu ni Dr. Slaa. Vyama vingapi vinafanya hivyo, hata hao CUF hawawezi kufanya hivyoni Prof. Lipumba na Seifu tu. Je ni kweli chama chote hicho kina watu wawili tu wenye uwezo huo?.

PASCO na watu wanaolazimisha kwamba eti ilitakiwa ZITTO ndiye awe kiongozi wa upinzani bungeni wanakosea sana na huenda hawajui historia ya CHADEMA. Ni Mbowe huyu huyu aliye letea mabadiliko makubwa ndani ya CHADEMA na mabayo matunda yake ndiyo haya watu wanayaona. CHADEMA haikuwa na msisimko huu unaouna leo kilikuwa na wazee wengi wamehodhi nafasi zote za uongozi na hivyo hawakuweza kuwa na kasi na hamasa kama unayoina leo.

CHADEMA tofauti na vyama vingine vya upinzani vimejengwa kwa falsafa na siyo kwa jina la mtu. Na ndiyo maana kimeweza kufanya mabadiliko ya uongozi kidemokrasia kuanzia EDWIN MTEI, BOB MAKANI na sasa F. MBOWE. Makati kutoka BOB MAKANI, Dr. KABOUROU na sasa Dr. Slaa. Kwa hiyo sipendi kuamini kuwa Kung'ara kwa ZITTO kuna mpa haki ya kuwaondoa viongozi wengine. Hizo ndiyo siasa za Augustine Mrema ambazo zimepeleka kuua vyama vyote ambavyo ameviongoza NCCR-M na sasa TLP.

Kitu kingine CUF wanapiga kelele wakati hata Wizara vivuli havijatangazwa ina maana wao walitaka kiongozi wa upinzani lazima atoke CUF. Umakini wa CUF upo wapi? mimi nafikiri haya mambo ya kuungana ni sawa lakini kama malengo na dira haviko sawa hakuna haja ya kuungana. Kwa sababu kwa kufanya hivyo itakuwa ni fujo kila mtu analengo lake na hiviwezi kuwa msaada kwa watanzania. Watanzania wanataka chama makini kinachokidhi mahitaji yao.

Upinzania bila CUF inawezekana, lakini kama wanataka ushirikiano siyo kwa masharti.
 
Back
Top Bottom