mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,966
Kwanza nianze kwa kusema sina hatimiliki na mtandao huu,na hivyo sina mamlaka ya kuanzisha ushindani wa aina yoyote ndani ya jukwaa hili na majukwaa mengine.
Baadhi yetu ni vijana wadogo ndio tunaelekea kuitwa baba. Haina ubishi kuwa baba ni kiungo kikubwa katika familia,ni kichwa,wengine huenda mbali na kusema kuwa baba ni rais na mama pengine ndiye Makamu wa rais. Kwa sifa zote hizi bado ipo changamoto ya kumjua baba bora.
Katika uzi huu ningependa tujadili kwa hoja ni kwa jinsi gani unavyomfahamu baba bora.Baba huyu aweza kuwa wewe mwenyewe,baba yako anayeishi au ambaye ametangulia mbele ya haki.
Kuna mambo wewe kama baba,au babako mzazi umeyafanya,anayafanya au aliwahi kuyafanya,na mpaka sasa umekuwa msingi mkubwa na mweongozo wa maisha yako.
Mfano mimi baba yangu ni mtu mwenye kujiamini na kujigamba kupita kiasi,lakini mimi nimechukua tabia ya kujiamini na kuona ndo inanifaa. Babu yangu ambaye ni baba wa baba yangu alikuwa ni mtu mpole na msikivu tabia hii pia nimeinyaka.
Je wewe kama baba ukoje, babako yukoje au alikuwaje?
Karibuni.
Baadhi yetu ni vijana wadogo ndio tunaelekea kuitwa baba. Haina ubishi kuwa baba ni kiungo kikubwa katika familia,ni kichwa,wengine huenda mbali na kusema kuwa baba ni rais na mama pengine ndiye Makamu wa rais. Kwa sifa zote hizi bado ipo changamoto ya kumjua baba bora.
Katika uzi huu ningependa tujadili kwa hoja ni kwa jinsi gani unavyomfahamu baba bora.Baba huyu aweza kuwa wewe mwenyewe,baba yako anayeishi au ambaye ametangulia mbele ya haki.
Kuna mambo wewe kama baba,au babako mzazi umeyafanya,anayafanya au aliwahi kuyafanya,na mpaka sasa umekuwa msingi mkubwa na mweongozo wa maisha yako.
Mfano mimi baba yangu ni mtu mwenye kujiamini na kujigamba kupita kiasi,lakini mimi nimechukua tabia ya kujiamini na kuona ndo inanifaa. Babu yangu ambaye ni baba wa baba yangu alikuwa ni mtu mpole na msikivu tabia hii pia nimeinyaka.
Je wewe kama baba ukoje, babako yukoje au alikuwaje?
Karibuni.