Kitu kikubwa naweza nikatoa ushuhuda hata mahakamani ni kwamba ukiwa mchangiaji kwa kusaidia watu kwa namna yoyote kwenye huu uzi, uwezekano wa Mungu kusikia maombi yako ya placement unaongezeka.
Huu uzi unabaraka ndugu zangu.
Prof. Kwa macho yangu nimeshuhudia watu wameandaa party ya ghafla ili kusherehekea kuingia kwenye mzinga wa asali.
Maana TRA ni mzinga wenyewe, kwa sababu kazi ya hawa maafisa ni kucheza na nyuki moja kwa moja, na sio pipa la asali.
Japo dogo langu aliambiwa irrelevant qualifications pamoja...
Wawakilishi wa uzi mliofanya Oral za TRA, tupeni mrejesho ili tuone kama tunapongeza au tunalaumu.
Nimesikia madogo wamepokea email za kupata Kazi huko.
Hicho ndicho kimenishtua naona mauza uza ni yale yale tu. Halafu vuta picha taasisi inadili na kutafuta wafanyakazi wake tu lakini inachukua muda kiasi hiki. Je ingekuwa wanatafuta wafanyakazi wa taasisi kumi ingekuwaje!
Ila kama taasisi moja moja kama TRA nao placement wanachelesha kiasi hiki kwa mliofanya, naanza kuwa na wasiwasi ni either kinachosababisha kuchelewa kwa placement kiko nje ya mamlaka ya utumishi au ni labda huu ucheleweshaji ni wa makusudi kuna watu wanafaidika nao.
Sawa ndugu yangu umeongea kweli tupu. Masahihisho madogo ni kwamba leseni ni optional ila ni muhimu kwa ulimwengu wa sasa. Endapo hali itakuruhusu, tafadhali jaribu kuitafuta.
Pole pia kwa unayoyapitia, ila jitahidi yasikufanye kuwa mnyonge wala kutia huruma kwa sababu dunia inaukatili mwingi...
JKT tulikuwa tunaita mapuuza. Mkuu una mapuuza sana. Naomba radhi kama nitakukosea ila ni aibu msomi kukubali kukosa utambulisho wa aina yoyote ambao ni rasmi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.