Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu (Mb), ameongoza kikao cha Tume ya Utumishi wa Bunge kilichofanyika siku ya leo tarehe 24 Machi, 2026 katika Ofisi ya Bunge, Jijini Dodoma.
Katika kikao hicho, Wajumbe wa Tume walipokea na kujadili Taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mfuko wa Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.
Pia Zungu amekagua ukumbi wa Bunge ambao umefanyiwa maboresho ya kuwekewa mfumo wa kisasa wa sauti ikiwa ni maandalizi kabla ya kuanza kwa Mkutano wa 3 wa Bunge la 13 ambao mahususi kwaajili kujadili na kupitisha Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ambao utaanza Machi 31, 2026.
Katika kikao hicho, Wajumbe wa Tume walipokea na kujadili Taarifa ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mfuko wa Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.