kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,686
Vitambulisho vya Taifa
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), imetangaza kuanza kwa zoezi la uchukuaji alama za vidole na upigaji picha kwa watu wote waliojaza fomu za kuomba vitambulisho vya taifa, litakaloazaJumatatu ijayo.
Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati kutoka NIDA, ThomasWilliam, ilisema kuwa zoezi hilo litaanza kwa kanda na litaanzia Wilaya ya Temeke.
Alisema zoezi hilo litakalodumu kwa wiki moja katika wilaya ya Temeke, litaanzia katika maeneo ya Kimbiji, Simbamnazi, Kigamboni, Vijibweni, Mjimwema, Somangila, Kisarawe II na Tungi.
Alisema mitaa itakayoanza na zoezi hilo ni ya Mgeni Nani, Mtoni Kijichi na Misheni iliyopo katika Kata ya Kijichi.
William alisema baada ya kumaliza kwa Wilaya ya Temeke, zoezi hilo litaendelea katika Wilaya ya Ilala na kumalizia Wilaya ya Kinondoni.
CHANZO: NIPASHE